MTWARA: Basi la Shule ya King David lapata ajali, watu 10 Wamefariki na wengine 19 Wakijeruhiwa baada ya gari 'kufeli breki'

MTWARA: Basi la Shule ya King David lapata ajali, watu 10 Wamefariki na wengine 19 Wakijeruhiwa baada ya gari 'kufeli breki'

Hizi taaratibu zikianza katikati huko zinapotea.

Unakumbuka ya Lucky Vicent?
Ndio nakumbuka Dear, ile ajari ndio ilisababisha serikali itowe Amri gari ziende garage Kila mwezi na zilipelekwa kweri, naona yule Waziri alipoondoka na utaratibu ukafa
 
Ndio nakumbuka Dear, ile ajari ndio ilisababisha serikali itowe Amri gari ziende garage Kila mwezi na zilipelekwa kweri, naona yule Waziri alipoondoka na utaratibu ukafa
Ndiyo kama hivyo...
Imetokea hii Wataanza tena..baadaye Hauoni wakiendelea...
 
R.I.P Moyo unauma Maskini pole kwa wazazi maumivu yake makali mno. Majeruhi nawaombea uponaji mwema.

Magari mengi ya shule mabovu mno.
 
Njia inaelekea ni ya maporomoko kuinama,

Poleni

Ova
 
Uzembe Uzembe Uzembe Uzembe Uzembe.
Utasikia tunaanza kuisingizia bahati mbaya.
Utasikia kesho jeshi la polisi linaanza operation maalum dhidi ya haya magari.

Watoto wamekufa bila hatia bali uzembe wa mababa zao, mama zao na kaka zao.
 
Kuna taarifa kuwa basi la Shule ya King David iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani limepata ajali mbaya iliyopelekea vifo vya wanafunzi na dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa jina moja Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa mika (54-60)

Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.

Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.

======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI

Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.

Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.

Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.

UPDATES: 1130HRS

Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha

RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi

''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''

View attachment 2304245View attachment 2304246
View attachment 2304248

View attachment 2304261
Gari nyingi sana za shule ni mbovu. Na mamlaka zimekaa kimya. Naona maafa yanaweza kuongezeka. Tujiulize gari y shule inayozunguka hpo mjini inapata ajari kirahis namna hiyo.
Gari nyingi watoto wanabebana licha ya waz kulipia usafiri yaani ni Kazi kwelikweli.
 
Seat belt kwa dereva au abiria wa nyuma,
Maana kwa kawaida nchi yetu seat belt ni kwa dereva na mtu mbele


#Pole kwa wafiwa
Seat belt itoke wapi magari haya asilimia kubwa ni mabovu. Mamlaka zimafanya kaz kwa matukio.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
RPC na RTO wa huo mkoa muda huu hawapaswi kuwapo kazini.
Traffic polisi waliokuwa barabarani route zote basi lilimopita muda huu hawapaswi kuwepo shuleni.

Mmiliki wa shule anapaswa kuwa jela na shule kufungiwa kabisa maisha.

Adhabu hizi ndio zitafanya watu wazidishe umakini kwenye kazi zao.
 
Duh! taarifa mbaya sana hii...

Lakini hadi sasa najiuliza hiyo ajali imekuaje imeua watu wengi hivyo, ukitazama picha ni kama impact sio kubwa na gari imeingia kidogo tu katika korongo...
 
Duh! taarifa mbaya sana hii...

Lakini hadi sasa najiuliza hiyo ajali imekuaje imeua watu wengi hivyo, ukitazama picha ni kama impact sio kubwa na gari imeingia kidogo tu katika korongo...
Inaonekana kule upande ilipoangukia imejibamiza kwa nguvu na body likarudi huku upande wa dereva na kuwabana ukiangalia kwa makini.

Wapunzike kwa amani Marehemu wote waliotangulia kwenye ajali hiyo na maheruhi Mungu awasimamie wapate kupona haraka. [emoji17]
 
Kiwepo kitabu maalum katika Kila gari ambacho Trafic watakagua seat belts za school Bus na kusign, pia ule utaratibu kwa lazima school bus zote zipelekwe garage Kila mwezi uzingatiwe, kwa kupeleka Traffic mmoja Kila garage ili ahakikishe gari zinatengenezwa
Seatbelts zinaweza kusaidia sana. Lakini ukiangalia school buses za wenzetu huwa hazina seatbelts. Watoto wengine wadogo sana. Lakini barabarani wana sheria ambazo zinayapa magari ya wanafunzi. Mfano gari ya wanafunzi ikisimama kupakia wanafunzi, gari zingine zote zinasimama.
 
Ni uchungu kwa kweli asubuhi unamwandaa mtoto aende shule ghafla unaenda kumwangalia mochwari. Mungu awape uvumilivu wazazi wa hawa watoto jmn. Roho zao zipumzike mahali pema.
 
...Mabasi ya hizi shule kubwakubwa kila mwaka wanapoteza wanafunzi. Iko shida pahala; vyombo vya dola vifanye uchunguzi wa kina.
 
Back
Top Bottom