Kwa mazingira yalivyokuwa na kwa muda uliopita toka tukio la mauaji litokee naamini Mhe. Waziri Mkuu ambaye ni mzaliwa Lindi anapotoka marehemu alishirikishwa na wananchi. Yawezekana Polisi walimdanganya kuhusu ukweli lakini kwa hiki kinachoendelea naamini kwa Nafasi yake anao uwezo wakuelekeza kuhamishwa Kwa RPC ambaye sidhani kama kwake malalamiko ya Ndugu wa marehemu akuyasikia.
Maafisa waliokamatwa ni wakuu wa vitengo na kwa taratibu za kijeshi na muundo wa Polisi maafisa ambao wapo nje na awajakamatwa ni Staff officer na RPC, waliobaki wote kwa taarifa inayosambaa wapo maabusu. Swali lakujiuliza wamekamatwa na Nani? Obviously wamekamatwa na wakubwa zaidi Yao na wakubwa hao lazima watakuwa wametoka makao makuu au wameelekezwa kutoka mikoa mingine.
Swali la pili, Hadi wanaelekezwa kwenda kuwakamata wasaidizi wa RPC huyo RPC alikuwa wapi? Naweza kutabiri kwamba alikuwepo ofisini lakini alipuuza kilio Cha walalamikaji aidha Kwa kusikia kupitia intelligence yake au kwa kufuatwa ofisini na walalamikaji.
Kama Timu imetoka nje ya Mkoa, kwanini Sasa RPC siyo mtuhumiwa angalau akarejeshwa makao makuu kuepusha kuvurigika Kwa kazi ya upelelezi? Lakini je kwa tukio lililotokea chini yake alipaswa yeye kujitokeza kwenye vyombo vya habari kulizungumzia? Ni kweli askari alijinyonga kwa tuhuma hizi na hakuna taarifa iliyotolewa hadi mwananchi walivyoandika?
Yapo maswali mengi Ila yote haya nimpongeze Mhe. Majaliwa Kwa kutimiza Wajibu wake bila kuviingilia vyombo husika. Kuiendea haki ni vyema sasa akashauri uwepo wa tume huru kuhusu suala la askari na kifo cha mfanyabiashara. Ni vigumu askari kupata kitanzi mahabusu.