Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

Mtwara: Maafisa Saba(7) wa Polisi wafikishwa Mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Kijana aliyekuwa akiwadai zaidi ya Tsh milioni 33.7

View attachment 2095724

JESHI la Polisi Mkoani Mtwara limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma za mauaji ya Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilayani Nachingwea Mkoani Lindi aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya Sh milioni 33.7.

Inadaiwa maafisa hao wa polisi walijipatia kiasi hicho cha pesa wakati wakimfanyia upekuzi mfanyabiashara huyo.

Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Marck Njera imesema mauaji hayo yalifanyika Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu ulitupwa kitongoji cha Majengo kijiji cha Hiari Wilayani Mtwara.

Maafisa wanaoshikiriwa ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango - Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza - Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara, Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga - Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara, Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.

Uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.

Chanzo: Habari leo
Insikitisha sana,nawapa pole wafiwa mungu awatie nguvu kwenye kipindi hiki kigumu.
 
Nimejarbu kuangalia hayo majina kwa ukaribu wake sijaona jina la kichagga....ashukuriwe Mungu aliye juu maana sipati picha kama angepatkana hata mmoja ni namna gan wachagaa wangepondwa kwa mawe huku jukwaan....sema sasa iv police ni kama wamepewa jukumu la kupora mali za watu na uhai wao..imekuwa kinyume na jukumu walilopewa
 
Kwa mazingira yalivyokuwa na kwa muda uliopita toka tukio la mauaji litokee naamini Mhe. Waziri Mkuu ambaye ni mzaliwa Lindi anapotoka marehemu alishirikishwa na wananchi. Yawezekana ...
RPC kuhusishwa kwenye ishu kama hizo ni ngumu sana, yaan ngumu sana. RPC sio mtu mdogo na mara nyingi hufatiliwa na vyombo vingine vya usalama muda wote.

Wakazi wa huko wanadai huyo RPC ndio kasimamia sana mpaka hao jamaa wamekamatwa. Embu fikiria mkuu wa upelelezi akamatwe, si kazi ndogo, maana hakujua kama na yy anapelelezwa mpaka anatiwa ndani.
 
Ishu tangu tarehe tano ni kwa vipi RPC anakosekana kuwa ndani? Jee OCD Yuki wapi? Kiufupi hao wote ni wahusika wanatakiwa kuwa ndani mahabusu na kesi yao iendeshwe mapema na haraka wanyongwe ili kuleta nidhamu kwa jeshi la polisi.
Ishu ilifanya ya SIRI sana. Hao watu wamerukwa mazee.
 
Ikithibitika kama ni kweli wameua.. wauliwe tu na wao.. tusichoshane
Kesi Iendeshwe Haraka Tuujue Ukweli
Watu Wanauwa Watu Halafu Unaona Street Wanaendesha Gari Wanajenga Haraka
 

JESHI la Polisi Mkoani Mtwara limewakamata na kuwafikisha mahakamani Maafisa wa Polisi saba kwa tuhuma za mauaji ya Mussa Hamisi Hamisi (25) mkazi wa Kijiji cha Ruponda wilayani Nachingwea Mkoani Lindi aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya Sh milioni 33.7...
Maafisa wanaoshikiriwa ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje -Mkuu wa Upelelezi wa wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango - Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza - Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara, Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga - Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara, Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
 
Ujambazi,Ujangiri na unyang'anyi ni chain inayoanzia ofisi ya waziri,rpc,rto,dc,ded,ocd na kukamilishwa na wadogo. Hapo lazima nguvu ya uma imetumika ku disclose uharifu huu au kuna makosa yamefanyika wao kwa wao na wachache tu watalipia dhambi hii hasa waliokuwa field.

Ila ukifuatilia chain hii usikute kuna Bank inahusika kutoa taarifa kuwa kuna 40M kwa mtu fulani na hao askari wakajioganaizi kwa tamaa wakaenda kumpekuwa ili tu kubeba hela za mjasiliamali korosho,maharage na mahindi
 
Ni swala la muda tu kabla naye hajapandishwa kizimbani
Hapana mkuu, kwa taarifa niliyoipata RPC alipoambiwa tu mara moja akawakamata, na ikumbukwe hao Askari wamekamatwa wiki 2 sasa hivi zinapita. Mbaya zaidi huyu mganga wa zahanati ya POLISI inasemekana alimchoma sindano ya SUMU huyo kijana na kupelekea kifo chake.
Aliyeuawa ni Ndugu wa PM hatari sana.
 
Kama kweli walihusika na.waligawana hizo pesa kila mmoja alipata millioni 5 kasoro tu!
Ni pesa kidogo sana!
Hawawezi kuwa wapumbavu kiasi hiki,kwamba wamuue mtu kwa milioni tano kila mtu.

There is something behind that amount of money.
 
Hao polisi wanazidi kuwa vibaka bila hofu yoyote kwakuwa kwa sasa ni kama wako juu ya sheria, wanafanya kazi bila kufuata sheria bali vitisho na ubabe, na hawajali lolote maana ndio wanaotumika kuweka viongozi madarakani. Utaona kabisa polisi wamekuwa na kiburi kwakuwa wana mahusiano ya kihalifu baina yao na viongozi walioko madarakani. Bila machafuko na katiba hii hawa polisi wataendelea kufanya unyama hivi bila kudhibitiwa, kwani kuna mahusiano ya kihalifu baina yao na watawala.
GT.
[emoji817][emoji3581]
 
Back
Top Bottom