Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Kama aliye wekewa moyo wa nguruwe huko kwa mabeberu Marekani hatunaye na ndiko unakokokusifia kwamba hawana majaribio, basi Madaktar wetu wamethubutu na wameweza.Lengo halikua kuua bali kuwatenganisha kila mtu aishi kivyake na aenjoi privacy yke binafsi
Mkuu wewe unatumia vizuri ubongo wako
 
Ilipangwa tu tusiwalaumu madaktari wana kazi nzito na ngumu sana!!
 
Je, walivyofanyiwa Op walikufa hapo hapo??

Je, wangeweza kuishi kwa kuungana kule kwa muda gani?

Je, waliungana nini?

Je, nini chanzo cha vifo vyao?

Je, hao Mabeberu Op zao zote hua zinafanikiwa hawajawahi kushindwa?

Je, umejuaje kama kwenye hiyo Op mabeberu hawakuwepo au kutia Muongozo?
Haaa! Leo umeamua kuja kwa staili ya maswali tupu?
 
Kwenye operesheni kama hiyo hata kwa mabeberu chance of survival huwa ni ndogo sana
Kwa beberu na kwetu wapi chance ya survival ni kubwa zaidi na kwa kiwango kipi? Kweli ukweli usisemwe kuwa bongo Nyoso?

Wapumzike kwa amani malaika hawa they deserved more kama binadamu. Ndiyo maana huwa kuna guinea pigs au siyo?
 
Uzuri walifanikiwa watenganisha na wakaishi kwa siku kadhaa
 
Ni bora basi wangebaki vilevile kama wangefariki mbeleni natural death kama wale mapacha basi ni sawa kuliko hivi ilivyotokea.
Kubaki vile ni mateso
Kumbuka wale mabinti mapacha wa Iran walikuwa wameungana kichwani, walifika umri wa miaka 22. Waliomba watenganishwe licha kuambiwa uwezekano wa kuishi ni mdogo lakini waliomba wafanyiwe. Operation ilifanyika na wote wawili walikufa
 
Wakuu hawa mapacha wakuungana(conjoined twins) matibabu yao ni magumu sana,
Tafiti zinaonesha ni asilimia 60 tu ndiyo wanafanikiwa kuishi baada ya operation yaani kama wakifanyiwa operation watu 10 kati yao wataishi watu 6 tu...
Angalia hapa
 
Kubaki vile ni mateso
Kumbuka wale mabinti mapacha wa Iran walikuwa wameungana kichwani, walifika umri wa miaka 22. Waliomba watenganishwe licha kuambiwa uwezekano wa kuishi ni mdogo lakini waliomba wafanyiwe. Operation ilifanyika na wote wawili walikufa
Sasa hapo kipi ni bora mkuu?
Kuishi wakiwa vile au kufa mapema
 
Je, walivyofanyiwa Op walikufa hapo hapo??

Je, wangeweza kuishi kwa kuungana kule kwa muda gani?

Je, waliungana nini?

Je, nini chanzo cha vifo vyao?

Je, hao Mabeberu Op zao zote hua zinafanikiwa hawajawahi kushindwa?

Je, umejuaje kama kwenye hiyo Op mabeberu hawakuwepo au kutia Muongozo?

Je, walivyofanyiwa Op walikufa hapo hapo?? --> Kwa vile walifanyiwa operation wakiwa hai, vifo vyao ni yatokanayo na operation hiyo.

Je, wangeweza kuishi kwa kuungana kule kwa muda gani? --> kwa vile walikuwa hai ni wazi wangekuwa hai leo. Hivyo ni sahihi kusema wangeishi kwingi zaidi (hata kwa saa moja zaidi) wakiwa wameungana kuliko yalivyotokea baada ya kutenganishwa.

Je, waliungana nini? --> hili waulize waliowatenganisha.

Je, nini chanzo cha vifo vyao? --> kwenye mada imeombwa tupewe maelezo ya kina kutokea hapo Mhimbili. Swali lako hili ni letu pia.

Je, hao Mabeberu Op zao zote hua zinafanikiwa hawajawahi kushindwa? --> beberu Wana facilities, resources, weledi, ubobezi, uzoefu nk uliopindukia kuliko mno yetu. Ndiyo maana kina Ayubu na wale raia daraja la kwanza wanakotibiwa. Huko failure rates zipo ila ni negligible na kwa hakika katu si kama kwetu.

Je, umejuaje kama kwenye hiyo Op mabeberu hawakuwepo au kutia Muongozo? --> Habari ya operation hii ilikuwa sana kwenye media. Neno kujimwambafy uliliona kwenye mada? Hatukujuzwa uwepo wao bali umwamba wetu. Hata hivyo kwanini kina Ayubu wao hawatibiwi hapa kwa usaidizi au mwongozo wa hao mabeberu?

Au wewe waonaje ndugu mjumbe?
 
Nimechelewa kukutana na huu uzi na tayari kuna comment nyingi hivyo nadhani nitakacho comment huenda Mwingine kesha elezea.

Kwanza kazi ile haikufanywa na Madaktari wa Tanzania peke yao.

Pili bila shaka wewe sio Daktari na hukubahatika kuwaona hao Watoto wanaozungumziwa hapa..mimi pia, ila kwa kuelezewa tu namna walivyokuwa huoni kuwa bado walikuwa kwenye changamoto?.

Hivi huoni kuwa kujaribu kuwasaidia mapema kuliko kuwaacha wakomae ili hali nafasi yao ya kuishi kama Binadamu wenzao wengine ilikuwa rehani?.

Na kama wangekutana na tatizo kubwa mbeleni huoni kuwa bado ingeonekana kwa nini hawakuamua angali wakiwa bado viungo havijakomaa.

Kwa maoni yangu ni bado tu ingefika mahali wangekwama na ingebaki kusubiri wapoteze maisha mmoja baada ya mwingine bila nafasi wala uwezo wa kuwasaidia kwa wakati huo...maisha yao yalikuwa 50 kwa 50 kama hata sio chini ya hapo.
Mapacha walioungana hata ulaya wapo , kuna wanaotenganishwa na kuna wanaoachwa wazeeke bila kuwagusa .
A human life is placed at very high value to take one , come with it very bold decision
Huko first class world operation kama hizi haziwei authorised na madaktari wa hopspitali moja .
 
Kwenye operesheni kama hiyo hata kwa mabeberu chance of survival huwa ni ndogo sana
Huwa hawafanyi kama chances za ku survive ni ndogo,
Hao mapacha walioungana wapo wengi tu wametenganishwa na wapo wa kutosha wanazeeka wakiwa wameungana
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Hiki ulichokiandika hakina uhalisia hata kidogo. Hao mabeberu unao waamini, kabla ya kufikia hapo walipo na wenyewe walipitia hii hatua ya kuwaamini wataalam wao!

Haikutokea tu from nowhere, wakawa ni mabingwa wa kila kitu. Hivyo wakati fulani, tukubali tu maumivu ili na sisi tufike nchi ya ahadi
Mkuu, Mm naona Tununue vifaa, tukachukue ujuzi na tuwe makini. Hatuwezi kuanza moja kwa kupita njia waliyopita wengine kwa gharama za maisha. Huwezi sema naachana na ndege za mabeberu naanza moja kutest za kwangu kwa kutoa kafara abiria.
 
Mkuu, Mm naona Tununue vifaa, tukachukue ujuzi na tuwe makini. Hatuwezi kuanza moja kwa kupita njia waliyopita wengine kwa gharama za maisha. Huwezi sema naachana na ndege za mabeberu naanza moja kutest za kwangu kwa kutoa kafara abiria.
They must understand the principle of standing on others' shoulders. Hiyo reasoning yao kwenye masuala ya uhai ni immoral, evil, na criminal.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom