Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Kwa hiyo mkuu ni heri kuwa wamefariki wakiwa wadogo kuliko kama wangalikuja kuwa wakubwa? Kwani wewe unadhani ilikuwa heri ufe lini mkuu?

Haki ipi tunastahili sisi kuihoji kwa mitazamo kama hii?
Mimi nimeongea kwa maana njema kabisa. Ya kwamba lengo la huo upasuaji lilikuwa ni kuwaepusha na kifo ambacho kingeweza kuwatokea hapo baadaye kutokana na huo muunganiko wao. Na nikatoa na huo mfano.

Kwa bahati mbaya mambo yameenda tofauti kwa hao watoto wawili. Na ifahamike dhamira ya madaktari ilikuwa ni kuokoa maisha ya hao watoto. Hivyo usinielewe tofauti. Hata mimi pia ni mzazi! Kwa hiyo nimeguswa pia.
 
Wao ma,beneru hawafi acha kuongea bila kufikilia
 
Kwamba pacha wa pili naye hatunaye? Inasikitisha. Kwani kulikuwa na haja gani ya operation hii? Kama uwezo wetu ungali hautoshi, kwa nini kujimwambafy bure juu ya maisha ya wengine? Kwanini tusingeomba usaidizi wa beberu kwenye masuala nyeti kama haya ya maisha ya watu? Kwa hakika Muhimbili tunastahili maelezo ya kina kutoka kwenu.
Itapendeza ukijifunza kuandika kwanza, unaweka kiulizo sehemu isiyotakiwa
 
wacha kuwatusi madaktari wetu.

operation kwa twins walio ungana ni ngumu na hazina ufundi wala ubingwa ni kubahatisha tu, records nyingi zinaonyesha surgery iliyo fanywa kwa twins walio ungana wengi wao wamekufa.
mifano ipo mingi sana wala hawa wa hapa tz sio wa kwanza, kuna sugery ilifanywa kwa twins wa Irani walikuwa na umri wa miaka 29 ilifanyika mwaka 2003 baada tu ya surgery walikufa chini ya madaktari bingwa wa nchi zilizo endelea.
hivyo madaktari wetu wamejitahidi sana kadiri ya ujuzi wao wote, lkn jitihada haishindi kudura za mungu.
ahsante sana angalau angelaumu mtu mwenye taaluma na uelewa tatizo mtu anaingiza mambo ya siasa kwenye taaluma za watu.Sioni makosa ya ma daktari hata chembe
 
Mkuu hata haya yanatokea kwingine.
Umesahau yule aliyewekewa moyo wa nfguruwe marekani na wakasema operation imefanikiwa halafu baada ya majuma.kadhaa akafa.
Unless vifo viwe vimetokana na uzembe ambao tunausikia mara kwa mara na kubahatisha

Kumbuka mwenye moyo wa nguruwe hakukuwa na moyo wa binadamu wa kumuwekea. Kwenye hali kama hiyo wapo waliokwisha jaribiwa na mioyo ya nyani na hata ya kutengenezwa kwa ridhaa zao mustakabala wa uwezekano wa kuishi ukiwekwa wazi.

Tuna hata haja ya kujidanganya beberu katutangulia ndiyo maana ha Ayubu aliwapandia huko kwa gharama zetu.
 
Itapendeza ukijifunza kuandika kwanza, unaweka kiulizo sehemu isiyotakiwa
Siyo kuwa ungeanza kujifunza wewe? Umemaliza sentensi bila nukta na bado unamhimiza nani kutumia alama za uandishi?

"Hii ndiyo ile mitanzania sasa kwenye ule ubora wake. Tofauti na ming'ombe zero."

Bure kabisa!
 
Siyo kuwa ungeanza kujifunza wewe? Umemaliza sentensi bila nukta na bado unamhimiza nani kutumia alama za uandishi?

"Hii ndiyo ile mitanzania sasa kwenye ule ubora wake. Tofauti na ming'ombe zero."

Bure kabisa!
Kuto kuweka nukta kunamchanganya vipi msomaji? Yeye kaweka kiulizo sasa sielewi mtoto kafariki au?
 
Kwamba huko Apolo India au St Thomas London Watu hawafi?
Mungu ameweka ukomo kwenye maarifa yetu ili tutambue uwepo wake.
Hakuna anayeweza kuongeza hata sekunde ya uhai wake au wa mwingine zaidi ya ule aliopewa na Mungu.
 
ahsante sana angalau angelaumu mtu mwenye taaluma na uelewa tatizo mtu anaingiza mambo ya siasa kwenye taaluma za watu.Sioni makosa ya ma daktari hata chembe
Siasa? Siyo anayeingiza siasa ni wewe? Walikuwa wameungana wakiwa hai. Sasa wametenganishwa na wakiwa wamekufa. Hudhani kuwa kupata usaidizi kutoka kwa awaye yote kuokoa maisha ya watoto hawa ilikuwa ni busara? Au ni ubinafsi wetu ule ule uliozoeleka wenye kupitiliza?
 
Hiki ulichokiandika hakina uhalisia hata kidogo. Hao mabeberu unao waamini, kabla ya kufikia hapo walipo na wenyewe walipitia hii hatua ya kuwaamini wataalam wao!

Haikutokea tu from nowhere, wakawa ni mabingwa wa kila kitu. Hivyo wakati fulani, tukubali tu maumivu ili na sisi tufike nchi ya ahadi
Sahihi ila hakuna majaribio kwa walio hai.... Unaleta practical kwa roho ya mtu
 
Hatukutakiwa kufanya majaribio kwenye uhai wa watu Kwa kifupi walikuwa wanatafuta publicity
Mbona wale mapacha wa Mbeya walipona acheni kuingiza Siasa kwenye taaluma za watu.Naomba uelewe kuna chama cha ma daktari bingwa duniani hasa wa upasuaji.Pasuaji kama hizi zikitaka kufanyika wanapeana taarifa kuhusu uwezo na taaluma wanaofanya hivyo na WHO lazima wajue hilo ndio go ahead inatolewa
Mwaka 1986 prof Philip alifanya upasuaji kama huu Muhimbili na akafanikiwa.

Kwa taarifa yako kama hujawahi fanyiwa operation huwezi Jua kila operation ina ukubwa wake hata kupasuliwa jipu ni operation pia lakini anakufanyia ni dk mmoja tu.Na inatemea limetokea wapi.
Ikifika issue kama hii watoto kuungana pamoja inategemea wameungana sehemu gani kuna wanaoungana sehemu ambazo ukizikata hakuna madhara.

Ila ikifikia hatua wameungana kwenye viungo nyeti sana kwa mwili wana share mfano maini,figo,kichwa,tumbo issue inakuwa very complicated na ndio maana utasikia kunakuwa na wapasuaji hata 20 mabingwa kila mmoja anakuja anafanya chake anamuachia mwingine afanye yake nitakupa mfano.
Kwa upasuaji kama huo kunakuwa na bingwa wa dawa ya usingizi anakuja anafanya part yake anaondoka,anakuja bingwa wa mifumo ya hewa anafanya yake anaondoka,kunakuwa na bingwa wa damu anafanya yake anaondoka,anakuja bingwa wa moyo na mishipa ya fahamu anafanya yake anaondoka,anakuja bingwa wa maini yaani hepatologist huyu ndio main stelling kwenye operation hii maana tatizo ndio liko kwake nimekupa mfano tu hapo kwa hiyo unakuta ni jeshi kubwa mno usifikirie ni mmoja tu anakata na kumaliza operation inaweza chukua hata masaa10.

Ni vigumu hapo kusema ni nani alikosea hapo hapo ukae ukijua kuna bwana mkubwa kuliko wote hao ambaye ndio daktari bingwa wa dunia na ulimwengu mzima anaitwa MUNGU.

Naongea haya kwa ushahidi nina mdogo wangu wa kike ni dr bingwa wa upasuaji wa watoto alishiriki kutenganisha wale watoto wa Mbeya kwa mafanikio makubwa ndio alinieleza yote haya.

Hawa ma dr wanahistahili pongezi.

Nchi hii inashida moja mambo mengine watu wanaingiza siasa
 
Kwani huko majuu, wakitenganishwa hawafi!?

Mbuyu ulianza kama mchicha, na jogoo alikuwa yai.
 
Mimi hili kwa kweli nililiona toka mwanzo na nilijua haya yatatokea ukweli ni kuwa BONGO bado sana technology yetu kufanya surgery ngumu kama hizi unaweza kuwa na wataalamu ila trust me vifaaa vitakuangushaa otherwise mtaforce kufanya LOCAL na haya ndo matokeo yake... inawezekana wabongo wali assist tu ila hawa watoto hawakustahili kufanyiwa majaribio ulimwengu wa sasa sio wa kufanya majaribio na kubahatisha kama tupo miaka ya 1900 huko. IT WAS NOT RIGHT KABISAA.
 
Kwamba pacha wa pili naye hatunaye? Inasikitisha. Kwani kulikuwa na haja gani ya operation hii? Kama uwezo wetu ungali hautoshi, kwa nini kujimwambafy bure juu ya maisha ya wengine? Kwanini tusingeomba usaidizi wa beberu kwenye masuala nyeti kama haya ya maisha ya watu? Kwa hakika Muhimbili tunastahili maelezo ya kina kutoka kwenu.
Je, walivyofanyiwa Op walikufa hapo hapo??

Je, wangeweza kuishi kwa kuungana kule kwa muda gani?

Je, waliungana nini?

Je, nini chanzo cha vifo vyao?

Je, hao Mabeberu Op zao zote hua zinafanikiwa hawajawahi kushindwa?

Je, umejuaje kama kwenye hiyo Op mabeberu hawakuwepo au kutia Muongozo?
 
wacha kuwatusi madaktari wetu.

operation kwa twins walio ungana ni ngumu na hazina ufundi wala ubingwa ni kubahatisha tu, records nyingi zinaonyesha surgery iliyo fanywa kwa twins walio ungana wengi wao wamekufa.
mifano ipo mingi sana wala hawa wa hapa tz sio wa kwanza, kuna sugery ilifanywa kwa twins wa Irani walikuwa na umri wa miaka 29 ilifanyika mwaka 2003 baada tu ya surgery walikufa chini ya madaktari bingwa wa nchi zilizo endelea.
hivyo madaktari wetu wamejitahidi sana kadiri ya ujuzi wao wote, lkn jitihada haishindi kudura za mungu.
Seriously? Kumbe hua wanafanya betting kwenye maisha ya watu? Yaan unamaanisha madaktari hua wanachezesha bahati nasibu kwenye maisha ya watu, hawana uhakika na wanachokifanya si ndio?
 
Mimi nimeongea kwa maana njema kabisa. Ya kwamba lengo la huo upasuaji lilikuwa ni kuwaepusha na kifo ambacho kingeweza kuwatokea hapo baadaye kutokana na huo muunganiko wao. Na nikatoa na huo mfano.

Kwa bahati mbaya mambo yameenda tofauti kwa hao watoto wawili. Na ifahamike dhamira ya madaktari ilikuwa ni kuokoa maisha ya hao watoto. Hivyo usinielewe tofauti. Hata mimi pia ni mzazi! Kwa hiyo nimeguswa pia.

Tuko pamoja mkuu. Ila angalia kama huyu:

Mgonjwa adai fidia TMJ, Hindu Mandal

Tujifunze kutafuta usaidizi kwenye masuala nyeti kama haya. Nia au dhamira njema pekee kwa hakika haitoshi.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Back
Top Bottom