Mume amfikisha mahakamani mkewe kwa kupeleka mshahara wake kanisani

Mume amfikisha mahakamani mkewe kwa kupeleka mshahara wake kanisani

Mwalimu wa shule ya Sekondari Jijini Mbeya, Julieth Kabuja (32) ameieleza Mahakama ya mwanzo Mkoani hapo kuwa ni bora ndoa yake ivunjike kuliko kumkabidhi mumewe kadi yake ya benki.

Ameyazungumza hayo mbele ya Mahakama ya mwanzo jijini hapo baada ya mumewe Charles Meshack (31) kufungua shauri la madai ya talaka akitaka kuachana na mkewe kwa kuhama dhehebu la katoliki na kuhamia la kilokole.

Aidha Meshack ambaye ni Askari Magereza amedai mkewe baada ya kuhamia katika ulokole fedha zake amekuwa akizipeleka kanisani kitendo kinachosababisha yeye kuzidiwa na majukumu ya familia.

“Naumia sana na majukumu, kodi ya nyumba nilipe mimi, ada za Watoto na chakula vyote mimi, halafu yeye mshahara wake apeleke kanisani, bora tuachane” alisema Meshack.
Hata hivyo Julieth aliiambia Mahakama kuwa yeye na mume wake wote ni wafanyakazi, lakini anashangaa anataka kumiliki kadi zote.

“Siku moja aliniamsha usiku na kuniambia nisipokubali kumkabidhi kadi yangu ya benki bora tuachane kwa kisingizio yeye alinilipia mahari hivyo mimi na kila kitu changu kipo chini yake, yaani kazi nifanye mimi halafu mshahara nimuachie huyu bwana, nipo tayari kuachika lakini siyo kuacha kadi yangu” alidai Julieth

Baada ya Hakimu Hafsa Shelimo kusikiliza pande zote mbili, aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 12, mwaka huu kwaajili ya hukumu.

Chanzo: Swahili Times
Ngoja msumeno uume pande zote mbili
1.Kama mdada anapeleka pesa kanisani basi kanisa ndio limuoe ajue kutengenisha kanisa na upendo ndani ya nyumba.Wakina mama wengi ni mateka wa dini za kilokole wakishakolea sana heshima nyumbani inashuka anatumia muda mwingi kuhudumia kanisa kuliko mume wake hata wakati mwingine anaweza kukuambia nachelewa kwenda kwa mchungaji nitakupikia nikirudi.Hili na mimi linanitesa kwa sasa nilikuwa namuachia kadi yangu lakini nimemnyang'anya kwa sasa.Wakina dada ya kaizari mpeni kaizari ya mungu mpe mungu.
2.Na wewe mwanaume acha udikteta huwezi sema mke eti uchukue kadi yake kisa umemlipia mahari mwanamke sio ATM naye ana haki yake.Ungekuwa muislam ungenielewa waislam wao mwanamme huna haki ya kuuliza mshahara au ujira wa mkeo wewe ndio una haki ya kumtunza na kumlisha hela yake ni kujipanda ili akupendezeshe wewe wewe.Mahari sio kununua mtu ni utaratibu tu wa kimila hasa za kiafrica ndio maana wazungu hawana kitu inaitwa mahari.Kumbuka wakati anatoka kwao kulikuwa na ugali hakufuata ugali kwako.Kumbuka kwao kulikuwa na mashamba hakuja kukulimia wewe
 
Kama mmeamua kuishi pamoja kama ndoa ni vizuri rasilimali za familia zikawa wazi na kutumika ipasavyo.

Ndio maana hata mume anapochepuka hupelekea kupotea Kwa rasilimali fedha za familia.

Kwa hiyo mwenza kuingilia kati ni Sawa tu
 
Kutoa sadaka na kumpa pesa mchungaji ni vitu tofauti

Hakuna muumini hutoa pesa kwa mchungaji ila hutoa sadaka kanisani.Na mchungaji hawezi jua nani katoa nini sababu sadaka huwekwa kwenye chombo cha sadaka kwenye makanisa yote yawe.ya kilokole au la

Huyo mwanaume ana hasira tu na ulokole ni fanatic.tu wa kikatoliki. Hawezi thibitisha popote kuwa pesa huyo mwanamke huwa anazipeleka kwa mchungaji

Hata wewe aliyeandika uko kwenye kundi hilo hilo.Sadaka hazipewi mkononi ikifika kipindi cha kutoa sadaka kila.mtoa sadaka huwekwa kwenye chombo cha sadaka mwisho huenda kuhesabiwa sasa pale huwezi sema hii sadaka ya fulani
Huyo mwanaume Mzushi
Hata kodi zetu zinazoliwa na hawa mafisadi hatuwapi mkononi bali tunaingiza kwenye accounts za serikali lakini mafisadi wanazifikia na kuzitafuna.

Mchungaji hakabidhiwi pesa mkononi lakini tunajua zinamfikia na anazitafuna vizuri tu. Hivyo hoja yako ni dhaifu sana
 
Hata kodi zetu zinazoliwa na hawa mafisadi hatuwapi mkononi bali tunaingiza kwenye accounts za serikali lakini mafisadi wanazifikia na kuzitafuna.

Mchungaji hakabidhiwi pesa mkononi lakini tunajua zinamfikia na anazitafuna vizuri tu. Hivyo hoja yako ni dhaifu sana
Anayetakiwa kujua pesa za sadaka zinaliwa na mchungaji ni wewe wa nje au waumini wanaotoa sadaka?
 
hakuna ndoa hapo......mume 31, mke 32...........nna hakika isiyo na uthibitisho....mke kapata mchepuko barafu.........na mmewe ni bwege.....sidhani kama alishawahi piga PULI.......
 
Hayo ni matatizo ya kifamilia mahakamani Hakuna ufumbuzi wake
 
Sababu za kikinga sana za kuacha ndoa, je sisi wenye watu wenye tabia ngumu still tunadunda miaka.
Kuna wanandoa Wana magumu yasiyovumilika lakini still wanapita.
Kama utaki changamoto oa malaika.
 
Kugombea umiliki/utawala ndio chanzo cha migogoro 90% ya ndoa. Mwanamke anataka awe sterling, mume nae hawezi kubali pokonywa sterling. KILA mmoja akiitambua mipaka yake inaishia wapi ndoa ni paradiso.
 
Huu msemo wa pesa ya mke ni ya mke na za mume ni zetu umewaharibu Sana wanawake saikolojia, wao ndio wanufaika wakuu pindi watoto wanapofanikiwa huku wanaume wakibakia kama bulldozer linatengeneza barabara ikishakamilika sio ruhusa kutumia barabara.
 
Ama kweli huyo afande kadhihirisha jeshi letu linamapungufu alitakiwa kumpiga na kitu kizito anavokuja kukumbuka miaka ishapita
 
Kuwa hakimu, jaji ni kazi ngumu, mara watu wagombanie kadi za benk, mara zumaridi ajiite Mungu na kupoteza watu, mara wanaoshindwa kuelewana kitandani hawa wote mizigo inapelekwa mahakamani dah, mara mke asiende kwa shoo ya diamond apigwe chuma aiseee
 
Mwalimu wa shule ya Sekondari Jijini Mbeya, Julieth Kabuja (32) ameieleza Mahakama ya mwanzo Mkoani hapo kuwa ni bora ndoa yake ivunjike kuliko kumkabidhi mumewe kadi yake ya benki.

Ameyazungumza hayo mbele ya Mahakama ya mwanzo jijini hapo baada ya mumewe Charles Meshack (31) kufungua shauri la madai ya talaka akitaka kuachana na mkewe kwa kuhama dhehebu la katoliki na kuhamia la kilokole.

Aidha Meshack ambaye ni Askari Magereza amedai mkewe baada ya kuhamia katika ulokole fedha zake amekuwa akizipeleka kanisani kitendo kinachosababisha yeye kuzidiwa na majukumu ya familia.

“Naumia sana na majukumu, kodi ya nyumba nilipe mimi, ada za Watoto na chakula vyote mimi, halafu yeye mshahara wake apeleke kanisani, bora tuachane” alisema Meshack.
Hata hivyo Julieth aliiambia Mahakama kuwa yeye na mume wake wote ni wafanyakazi, lakini anashangaa anataka kumiliki kadi zote.

“Siku moja aliniamsha usiku na kuniambia nisipokubali kumkabidhi kadi yangu ya benki bora tuachane kwa kisingizio yeye alinilipia mahari hivyo mimi na kila kitu changu kipo chini yake, yaani kazi nifanye mimi halafu mshahara nimuachie huyu bwana, nipo tayari kuachika lakini siyo kuacha kadi yangu” alidai Julieth

Baada ya Hakimu Hafsa Shelimo kusikiliza pande zote mbili, aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 12, mwaka huu kwaajili ya hukumu.

Chanzo: Swahili Times
sio mda risas zitarindima.kumbuka ni askar huyo
 
Mama abakie hapo hapo.
Anaitaka ATM aisee

Mwanamke kweli umkabidhi mume ATM? That is too much

Wanawake vizuri kuomba Mungu kutopata kidume kilofa kama hicho hopeless kabisa kiofisa magereza

Kinadhalilisha jeshi la magereza wanawake wenye kazi zao watakatakaa kuolewa na Askari magereza kuwa watawapokonya ATM
Ila huko kanisani wakiitaka hiyo atm kadi ataitoa kilainiiii[emoji23][emoji23]
 
Huyo mwanaume anataka pesa ya mwanamke tu

Uanaume sio kuvaa suruali na dude kama bunduki katikati ya suruali

Ni uwezo wa kuhudumia familia bila kuelekea ku force ohh nipe kadi ya benki na ATM na namba ya Siri

Watetezi wanasheria wa haki za wanawake na NGo tetea haki za wanawake siku hiyo kesi iliyotajwa jazaneni hasa kuonyesha solidarity na huyo mama. Maafisa balozi wa nje pia wawepo wa dawati la balozi wa jinsia.

Mfumo dume unahitaji kusomeshwa.

Hakimu na wewe kakamaa mwanamke mwenzio huyo. Toa hukumu ya kihistoria ambayo ita trend dunia nzima ili mwanaume yeyote Mwenye tabia kama hiyo asije tokea.
Mafeminist mna taabu ninyi si mnataka 50/50 ila kwenye majukumu ya kifamilia hapana[emoji23] halafu hakimu ahukumu kwa mujibu wa sheria au ampendelee mwanamke kwenye hukumu kisa ni mwanamke mwenzake[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom