Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Unataka kusema Mungu hana uwezo wa kumpa mtu ujauzito bila kufanya matusi, na ndani ya wiki moja akajifungua?
Mungu hajawahi fanya hivyo. Mwenye uwezo wa kumpa Kiumbe ujauzito ni kiumbe mwingine na Awe na vina saba sawa. Ndio maana Huwezi kuta binadamu akazaa na Mbuzi. Mbuzi atazaa na Mbuzi mwenzake na Malaika watazaa na Malaika wenzako. Na Majini watazaa na Majini wenzao

Mungu hawezi kumtafuta Mwanadamu ndio aingie ndani yake halafu Ndio azae. Wakati kitabu hicho hicho kinakumbia Alimuumba Mwanadamu wa Kwanza Kwa Udongo sasa Alishindwa Nini Kumuumba Yesu kwa Udongo
 
Qur'an imekanusha propaganda za biblia na kusema injil ilichakachuliwa ndio maan unaona contradictions nyingi ,Qur'an imekataa yesu hajafa wala hajasulibiwa ,imekataa si mungu na bla bla kibao
Leta ushahidi kwamba Koran imekataa Yesu kusulubiwa
 
Kuna Mambo Yapo Ulimwenguni ukiyatafakari kwa Kina hayaingii Akilini ndugu waafrika wenzangu

Kuna Historia katika Vitabu kwamba Mungu alimtoa Mwanae Ili aje Kuikomboa Dunia katika Dhambi (ambazo zipo mpaka Leo)

Ukiangalia kwa Undani Historia hii ya kuzaliwa kwake inatia Shaka sana kabla ya Kujua Majibu ya kuzaliwa kwake inakuja Historia kwamba hana Baba. Kabla hujapata Majibu ya Baba ni nani Inakuja Kwamba ni Uwezo wa Mungu ndio akazaliwa. Yanakuwa Maswali juu ya Maswali

Kumbuka Yusufu na Mariam si kwamba Walikuwa ni Wachumba la hasha bali walikuwa tayari wapo Ndani (wameoana) wanaishi pamoja. Hakuna wachumba Wanaoishi pamoja kwa Utaratibu wa Kuishi. Ukichumbia wewe utakaa kwako na Huyo mchumba atakaa kwao. Kama Waliishi pamoja maana Yake waliweza Kushiriki Tendo la Ndoa yao na Ukifuatilia kwa Makini Yusuf alikuwa Pamoja na Mariam kila Sehemu hakuna Sehemu inayosema Alikuja Kumuoa mariam Ikiwa na Maana Kwamba Tayari alikuwa keshaoa maana yake ule uchumba ulio andikwa Tayari ukayeyuka

Binadamu huzaliwa Kwa Mwanaume na Mwanamke hili halina ubishi. Ila Kuna Kuja Utata wa Hapa Kwamba Yesu alizaliwa bila Mfumo maalumu wa Uzazi wa Baba na Mama ila Roho Mtakatifu kama Wanavyodai (kumbuka Hata Huko india Wapo Watu wenye Hadithi hizi hizi za Kuzaliwa bila Baba)

Sasa Hapa Unajiuliza Maswali. Mungu huyo aliyeweza Kumuumba Mwanadamu wa Kwanza Bila Kutumia mifumo ya Uzazi Inakuwaje leo aje Aanze Kumuumba Binadamu mwingine anayedaiwa ni Mwanae kwa Mifumo ya Uzazi na Akaenda kwa Mariam ambaye alikuwa teyari ana Mume(kumbuka Hapa Mungu hazai na Wala Hakuzailiwa)

Sasa Anamzaa mwanae kupitia Mariam mara Yusufu atake kumkimbia Mariam maana Kuna Siri May be Yusufu aliiona akaona Hapa Nimepigwa na Baada ya Yesu kuzaliwa Yusuf Anapotea Ghafla kwenye Maandiko na Historia yake inaishia Hapo hapo

Mungu anamtoa Mwanae. Anakuja Mnamkataa, mnampiga, mnamtesa anawahubiria mnagoma Kukubali maneno yake mnamfukuza kwenye masinagogo yake, Anaenda Kusali mlimani peke yake, anakusanya wanafunzi wake. Hao wanafunzi nao mnawakataa mnawafukuza. Hivi Mungu hapo anawaogopa Nyie kisa Nini mpak Awafanyie Haya Yote Nyie Viumbe wake

Yaani Mungu mpaka Anatoa Mtoto wake Wa Pekee ili awabembeleze nyie mmrudie Yeye na Mnakataa. Sasa Hapo Mungu Anakuwa na Ule Uwezo na Kutoshindwa Kitu kweli. Kama Kawatumia Mwanae na Mmemgomea kawatumia Manabii na Mitume mmemgomea Tena na hamtaki kumrudia. Hivi Mungu anawalemba Hivyo Ili Iweje

Si kila Mtu anayezaliwa bila Baba Yake basi Baba Yake ndio Mungu. Wachawi wanazini na Binadamu kila Siku na Wachawi hao hao ndio Binadamu wenzenu. Wanawake wanabeba Mimba zingine wasizozijua zimetoka wapi

Basi Mjue Kwamba Hapo Mwenye Enzi Mungu hayupo na Mnaozeshwa Akili zenu ndugu zangu. Kaeni Chini Mtafakari kwa Akili zenu Timamu. Mungu hawezi kufanya hayo Kwa Viumbe wake. Yeye hayupo Hivyo

[emoji3507]Mungu si Mmoja
[emoji3507]Mungu si Wengi
[emoji3507]Mungu si Baba
[emoji3507]Mungu si Mama
[emoji3507]Mungu si Kiumbe
[emoji3507]Mungu hachukii Viumbe
[emoji3507]Mungu hapendi Viumbe wake ila Ana Enzi na Viumbe wake (usijione wewe Kiumbe Mtu unapendwa na Mungu Kuliko Viumbe wake wengine aliowaumba)
[emoji3507]Mungu hakuzaa wala Kuzaliwa

Yachunguzeni maandiko Yenu mtajua kwamba si Maandiko ya kiucha Mungu ila Maandiko ya Viumbe wenye Tamaa

ASANTENI
Wewe ulitoka wapi,mama alitoka wapi,na aliyemzaa alitoka wapi?
Tuanzie hapo kwanza,
Tunajua Samsung Galaxy inatoka Korea,Toyota inatoka Japan,BMW inatoka Ujerumani,wewe ulitoka wapi?
 
Wewe ulitoka wapi,mama alitoka wapi,na aliyemzaa alitoka wapi?
Tuanzie hapo kwanza,
Tunajua Samsung Galaxy inatoka Korea,Toyota inatoka Japan,BMW inatoka Ujerumani,wewe ulitoka wapi?
Sasa wewe ndio unauliza Maswali. Kwanza Jua Umetoka Wapi. Mimi najua Nimetoka Wapi Chanzi cha Uhai ulionaona Umetokana Na Binadamu wa Kwanza ambao Kiuhalisia ni Fumbakasa na Mwasi mkewe. Elimu hii ipo Mwanzoni kabla ya Wakoloni na Dini hizi Kuja Afrika

Wewe una elimu ya Adam na Hawa na Watoto wao. Adam na Hawa Waliwakuta Wanadamu tayari Wapo Duniani
 
Mungu hajawahi fanya hivyo. Mwenye uwezo wa kumpa Kiumbe ujauzito ni kiumbe mwingine na Awe na vina saba sawa. Ndio maana Huwezi kuta binadamu akazaa na Mbuzi. Mbuzi atazaa na Mbuzi mwenzake na Malaika watazaa na Malaika wenzako. Na Majini watazaa na Majini wenzao

Mungu hawezi kumtafuta Mwanadamu ndio aingie ndani yake halafu Ndio azae. Wakati kitabu hicho hicho kinakumbia Alimuumba Mwanadamu wa Kwanza Kwa Udongo sasa Alishindwa Nini Kumuumba Yesu kwa Udongo
Yani Mungu Muumba vyote, hawezi na hana uwezo wa kutamka tu wewe apo uwe na mimba leo leo na ukajifungua leo leo? hata kama ni mwanaume?
 
Yani Mungu Muumba vyote, hawezi na hana uwezo wa kutamka tu wewe apo uwe na mimba leo leo na ukajifungua leo leo? hata kama ni mwanaume?
Ungejiuliza Kwanza Kwaninj Hakufanya Hayo kwa Yesu mliyemsulubisha.

Mungu keshaweka Mifumo ya uzazi
 
Mleta uzi unajichanganya sana mala huamini Mungu yupo afu unatumia mifano ya Biblia. tukuelewe vipi
 
Mungu peke ake anaweza pambana na urusi na akashinda vita?
Ndugu yangu toka Lini Mungu akapigana na Vita za Viumbe wake. Nyie piganeni wenyewe Mungu hausiki na Vita Zenu

Majini na Malaika pia Yalishapigan Huko Kwenye kugombania mamlaka hakuna Mungu aliyeingilia
 
Mleta uzi unajichanganya sana mala huamini Mungu yupo afu unatumia mifano ya Biblia. tukuelewe vipi
Kutumia Vifungu hivyo Ni ili ww unayeamini Hayo ujue Kwamba Umepotoshwa.

Kuna Mifano mingi ambayo haipo kwenye Biblia na Vifungu. Mfano ningekuambia Adam na Hawa Si Binadamu wa kwanza Ungebisha ila unajua Kaandikwa huko
 
hii ni uongo uyo mazinge wakristo munamuogopa hatariii mna anajua uongo wote uliomo kwenye biblia zenu zoooteee
Mazinge anamtafuta Mungu wa kweli amjue kiundani. Anahoji kama vile mtoa mada alivyohoji, akipata majibu ya kina kwa maswali yake anakubali kwa kuwa anakuwa amejibiwa na kuelewa. Sasa unaposema hii ni uongo bila kufafanua uongo wake ni upi unakua hujaeleweka. Ni uongo kwamba huyo videoni sio Mazinge? Ni uongo kuwa hiyo video clip imepandikizwa sauti? Ni uongo kuwa hiyo sio video clip??
 
Mazinge anamtafuta Mungu wa kweli amjue kiundani. Anahoji kama vile mtoa mada alivyohoji, akipata majibu ya kina kwa maswali yake anakubali kwa kuwa anakuwa amejibiwa na kuelewa. Sasa unaposema hii ni uongo bila kufafanua uongo wake ni upi unakua hujaeleweka. Ni uongo kwamba huyo videoni sio Mazinge? Ni uongo kuwa hiyo video clip imepandikizwa sauti? Ni uongo kuwa hiyo sio video clip??
Ivi unamjua vzr mazinge lkn? kma kabatizwa saivi anaingia msikitini au kanisani ? kumbuka kua alikua mkristo huyo alipoiona haki akaifuata
 
Ni kweli Mungu hawezi kufa wala kusinzia wala kula kma tufanyavo sisi wanadamu
Uyo yesu ety anasulubiwa huku anamuomba Mungu sasa si angejiokoa tuu

Yni ukitafakari vzr utajua kua hapa watu wamepigwa na kitu kizito sanaa
Kwanini wewe haumini Yesu aliteswa kwa ajili yako?
 
Back
Top Bottom