Mungu anaweza kutenda dhambi?

Mungu anaweza kutenda dhambi?

1Samwel 15:3
Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng’ombe na kondoo, ngamia na punda

Kosa la Amaleki walilofanya ni ili, wakastahili kupata walichopata
Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa

Kutoka 17:8. Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu.
Torati 25:17-19
Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri;

jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu.

Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha BWANA, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.
Katika hao wa Amaleki waliohukumiwa kufa kumbuka kuna hadi watoto wanao nyonya nao wamejumuishwa

Mtoto anaye nyonya anawezaje kutenda dhambi kiasi umfanyie ukatili kama huo?
 
1Samwel 15:3
Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng’ombe na kondoo, ngamia na punda

Kosa la Amaleki walilofanya ni ili, wakastahili kupata walichopata
Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa

Kutoka 17:8. Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu.
Torati 25:17-19
Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri;

jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu.

Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha BWANA, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.
Haya maandiko yamenifundisha kitu kingine zaidi. Naamini haya ni maandiko kwenye biblia ambacho ni kitabu kitakatifu kwa wakristo! Kama ndivyo, how comes wakristo wanazuiwa kulipa kisasi wakati hapa naona kama Mungu anawa amuru Jews kulipa kisasi kwa walichotendewa na wa Amaleki?
 
Ukiangalia comments na majibu humu ni dhahiri kabisa hizi dini tumeletewa tu
 
Sasa kama yeye ndo mwandishi wa dhambi zako, kitabu anacho yeye, atajiandikaje kwa mfano? Na nani ambaye atamhukumu wakati hukumu ndo anatoa yeye?
Mungu ni dictator sio? Anagawa maumivu tu kwa wengine.
Mnasemaje Mungu roho wakati alisema "tumuumbe mtu kwa sura na mfano wetu"?
 
Dhambi ni kwenda kinyume na matakwa ya Mungu. Hence, kwake dhambi si kitu na haina maana kabisa!
i.e 1 ÷ 0 = undefined expression

Ni sawa na wewe uweke sheria kwako kuwa mwisho wa wanafamilia kuingia ndani ni saa moja, halafu wewe uingie saa tatu

Sijuwi mumenielewa!
Kwa kuwa dhambi ni tendo chukizi mbele ya Mungu. Yeye sasa ndo kashakuwa Mungu hivyo
Ukiweka sheria kwako mwisho kwa mwanafamilia yeyote kuingia ni saa3...wewe ukiingia saa4 umeivunja hiyo sheria au hujaivunja?

Bunge likipitisha muswada kuwa kosa la kubaka adhabu miaka 30, halafu mbunge akakamatwa amebaka, ...huyo mbunge amevunja sheria au hajavunja?
 
Kiwe na roho
Mkuu unanichanganya maana unanizungusha na majibu cyclical
Nmeuliza A ni nini? Ukasema A ni B nakuuliza tena Sifa za B ni nini unasema ni A.
Nauliza roho ni nini? Unasema ni nishati hai
Nkiuliza Hai ni ni nini?Unasema iwe na Roho tena?

Miti ina roho?
Majani yana roho?
 
Wakulungwa vipi?

Kuna swali huwa linanitatisha.

Kama tuliambiwa Mungu anaweza kila kitu.

Na mungu ana free will.

Je, Mungu anaweza kutenda dhambi?
Mungu ni nan dhambi ni nini tuanzie apo kwanza , coz kuna vtu kwa wengne ni okey kwa wengne sio okey
 
Ndugu zangu tunapojadili Mambo ya Mwenyezi Mungu tuwe na staha, Kuna vitu vya kufanyia mzaha lakini sio Mwenyezi Mungu. unapoleta mjadala unao muhusu Mwenyezi Mungu ni vema ukaleta mjadala wenye afya kuliko mijadala inayo mkashifu Mwenyezi Mungu. Maisha yametupiga kila mahali, badala ya kuomba rehema tunaweza kujikuta tunapata laana hivi hivi..

Mwenyezi Mungu ameleta vitabu vinne kwa wanaadamu kupitia Mitume wake ambavyo ni Taurati, Zaburi, Injili na Quran tusome hivi vitabu na tuwaulize wasomi watupe majibu pale tunapokwama. Mwenyezi Mungu hawezi na hajawahi kumdhulumu kiumbe yeyote, isipokuwa sisi viumbe ndio tunajidhulumu wenyewe nafsi zetu kwa kukataa amri zake na kuwapinga mitume wake aliowaleta na kufanyia mzaha mambo ya dini kama hivi.

QURAN 22: 3-4
' Na miongoni mwa watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu, na wanamfuata kila shetani aliye asi. Ameandikiwa kwamba anaye mfanya (shetani) kuwa rafiki, basi huyo hakika atampoteza na atamwongoza kwenye adhabu ya moto mkali. '

QURAN 22: 8-10
' Na katika watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya elimu, wala uwongofu, wala Kitabu chenye nuru. Anaye geuza shingo yake ili kupoteza watu waache njia ya Mwenyezi Mungu; duniani atapata maisha yenye dhiki, na siku ya Kiyama tutamwonjesha adhabu ya kuungua. (Ataambiwa): Hayo ni kwa sababu ya iliyo tanguliza mikono yako. Na hakika Mwenyezi Mungu sio mwenye kuwadhulumu waja wake.'
 
Swali lako ni sawa na mwanafunzi kumuuliza mwalimu hivi unaweza kufeli mtiani? Wakati huo mtiani upo kwa ajili ya mwanafunzi na mwalimu ni mtunzi na msahihishaji.

Dhambi ni uasi wa sheria. Sheria zipo kwa ajili ya binadamu. Yeye ndo anazifata au kuzivunja na mtunzi na anayehukumu ni MUNGU.
 
Back
Top Bottom