To say something is real, You have to prove it. Otherwise if you cannot those are your thoughts, imaginations just an illusion.
Msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika.Kwani wewe kila unachokiamini umekichunguza? ingekuwa hivyo basi dunia nzima tungekuwa watafiti na wachunguzi, hakuna ambaye angeamini utafiti/uchunguzi wa mwenzake.ni imani tu inatumika
“Nimeweka uzima na kifo mbele yako, baraka na laana; nawe lazima uchague uzima ili uendelee kuwa hai.”—KUMBUKUMBU LA TORATI 30:19. (Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako)
Akili imegoma, nashangaa wenzangu mnawezaje kuamini uongo wa wazi wazi namna hii😅😅😂😂😂🙌🙌🙌 Wee utaki kuelewa tuu hizi habari ahahahahaha
Msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika.
Imani haiendani na ukweli, Imani inaendana na kutokuwa na uhakika.
Ukweli una endana na uthibitisho,Ndio maana utafiti hufanyika kutafuta ukweli wa imani fulani.
Kama huwezi kuchunguza na kukijua kitu kilicho kutengeneza wewe, Ulifahamu vipi hicho kitu kili kutengeneza?Well said sisi katika dini yetu ya uislam tumefundishwa mtu anae mchunguza mungu basi hata akili zake haziko sawa (majnun) kwa maana huwezi kuchunguzu na kikujua kitu kilichokutengeneza wewe na kukupa akili kwasababu angeweza kukuumba ukawa hata mmbu lakini kakuumba binaadam na kwa ujeuri wa binaadam et unamchunguza na kumjadili mungu. BIRA USEME MUNGU YUPO KULIKO KUSEMA HAYUPO UKAKUTANA NAE NDIO UTAJUA HAUJUI.
Kama huwezi kuchunguza na kukijua kitu kilicho kutengeneza wewe, Ulifahamu vipi hicho kitu kili kutengeneza?
Kama hicho kitu kilicho kuumba wewe haki chunguziki, uchunguzi wa kukifahamu kwamba hakichunguziki ulifanywa na nani kujua na kuthibitisha kwamba hakichunguziki?
Una elewa maana ya kuwa na uhakika?Hapana,biblia inasema imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo na ni bayana(uthibitisho) ya mambo yasiyoonekana
Una elewa maana ya kuwa na uhakika?
Ukisha kuwa na uhakika hiyo sio imani tena bali ni ukweli.
Mfano, mwanafunzi akifanya mtihani ana kuwa Hana uhakika wa marks ipi exactly ataipata, ila anakuwa na imani fulani ya marks atakayo ipata kwa vile Hana uhakika na imani yake. Tuseme labda mwanafunzi huyu ana imani ya kupata marks 80%.
Lakini akisha rudishiwa mtihani wake Anakuwa na uhakika na ukweli kwamba mtihani huu nimepata marks 80% na hiyo inakuwa siyo imani tena ya kwamba alipata marks 80% Bali ni ukweli wenye Uthibitisho.
Hata mtu akihitaji uthibitisho wa mwanafunzi huyu kupata marks 80% ataupata.
Ndio maana nakwambia hivi, Msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika.
BIBLIA KTK VITABU VYA MITHALI 4:23 NA YEREMIA 17:9 INAZUNGUMZIA JUU YA MOYO, KWAMBA, TUNAPASWA KULINDA MOYO KULIKO VITU VINGINE VYOTE KWA SABABU KWENYE MOYO NDIKO KUTOKAKO CHEMICHEMI ZA UZIMA (LAKINI KUNAWEZA TOKA CHEMICHEMI ZA MAUTI PIA).LAKINI PIA, MOYO HUWA NI MDANGANYIFU.Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.
Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!
Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.
Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!
Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?
Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.
Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.
Mchongo ukoje? Ipo hivi;
Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.
Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.
Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.
Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.
Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.
Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.
Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.
Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.
Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.
Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.
Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.
Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.
Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.
Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.
Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!
Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Ufanye makosa hapa duniani halafu uachiwe tu?Anaandika Robert Heriel,
Mtibeli.
Kuna Mungu Muumba wa mbingu na nchi halafu kuna miungu. Mungu Mkuu ambaye hajawahi kuonekana na kamwe hatokuja kuonekana Daima milele, hawezi kufanya wala kuwaza huo upuuzi wa kuchoma watu, hilo haliwezekaniki!
Miungu hii inayoabudiwa ndio inaweza kufanya hivyo, lakini yule Mungu wa miungu huo muda hana, na hawezi kufanya hivyo.
Mungu Mkuu ni Upendo, na kamwe upendo haulazimishwi. Yaani, ati Mungu aliyekuumba akulazimishe umpende (umuabudu) wakati alikuwa na uwezo wa kukuumba automatic ukawa unampenda!
Kwanza umpende (umuabudu) ili yeye apate nini? Halafu usipompende ati akuchome, wewe kosa lako lipo hapo? Yaani moyo wako haumpendi Mungu aliyekuumba, unapenda jambo jingine nini kosa lako, iko wapi haki hapo?
Mungu mwenye Upendo na muweza wa yote, anataka mtu apende anachokipenda! Kwanza yeye ndio aliyekufanya uwe hivyo ulivyo, upende unayoyapenda, achana na yale unayoyatamani na kuyachukia.
Huwezi lazimisha kupendwa bhana, na kamwe Mungu hawezi kukulazimisha umpende. Kukulazimisha haibadilishi ukweli kuwa haumpendi. Kumbuka Mungu ni Haki na Kweli.
Mchongo ukoje? Ipo hivi;
Jinsi uonavyo Ulimwengu wa nje (huu unaoonekana) ndivyo katika Ulimwengu wa ndani usioonekana, Ulimwengu wa Nafsi.
Itazame Dunia, Dunia ni moja lakini inamazingira tofauti tofauti, kuna sehemu zenye baridi kali mpaka barafu, kuna sehemu za jangwa, kuna sehemu za hali ya hewa ya kati, kuna sehemu zenye mvua nyingi, na zipo zenye mvua za Waarabu.
Kuna milimani na mabondeni, sehemu zenye maziwa, mito na bahati, sehemu yenye misitu mine, nyasi na vichaka, sehemu yenye wanyama wa aina hii sehemu nyingine hakuna.
Sasa ni uchaguzi wa mtu kutumia kile akipendacho, ukitaka kuishi kwenye baridi ni wewe, Mungu hawezi kukulazimisha uishi sehemu isiyo ya baridi wakati wewe unapenda. Haipo hiyo. Ukitaka kula chakula au wanyama fulani ni wewe mwenyewe.
Ila elewa kuwa vipo vitu ni sumu na cool vitu sio sumu. Ni wewe mwenyewe unachagua ule sumu au usile. Nasema ni wewe mwenyewe, ni kutokana na upendo wako.
Kama unavyoishi hapa Duniani kulingana na umri wako, jinsia yako, kipato na hadhi yako, mtazamo wako ndivyo nafsi yako itakavyoishi baada ya mwili wako kuondoka.
Mfano huwezi ishi Masaki, Mikocheni, Upanga wakati kipato chako na daraja lako ni kuishi kwa walalahoi huko.
Kunguru na njiwa hawawezi kaa pamoja, wanasema ndege wafananao huruka pamoja. Nenda hata wodini huko mahospitalini utaona kabisa kuwa mgonjwa wa akili hawezi lazwa wodi ya wazazi au mgonjwa aliyemahututi hawezi lazwa wodi ya wagonjwa wa meno.
Maisha ni uchaguzi wa mtu mwenyewe. Mungu kamwe hana huo muda wa kukuamulia nini chakupenda. Kuku hawezi zaa bata, kila mmoja atakaa sehemu yake. Vivyohivyo hata ukifa roho yako itaenda mahali inapopapenda, na wala hautachomwa moto.
Kama unapenda uzinzi na kuchukua wake za watu na kuua watu basi nafsi yako itaishi katika Ulimwengu wa watu wa aina yako ili mchukuliane wake na waume zenu kwa jinsi mpendavyo, ili muone utamu wa kile mnachokipenda.
Sheria siku zote sio upendo, Sheria hizi za nchi zipo kwaajili ya kudhibiti matendo ha mwili na sio nafsi. Upendo upo kwenye nafsi ya mtu wakati sheria ipo katika mwili wa mtu. Mtu anapoua akahukumiwa jela kinachoadhibiwa ni mwili wake lakini nafsi yake haiadhibiwi.
Utalipwa sawasawa na matendo ya nafsi yako, Dhamiri na utapelekwa kwenye Ulimwengu unaofanana na nafsi yako. Hiyo ndio tafsiri ya moto wa Jehanum na sio kuchomwa kama wengi walivyotafsiri au wanavyojua.
Mungu Mkuu hukupa na anatoa kitu kulingana na mtu au kiumbe husika, Ulimwengu wa wapenda haki, wapenda dhulma, wenye upendo, wenye chuki, wasema uongo na wauaji, ulimwengu wa wasema kweli na watoa uzima.
Ni wewe tuu unachagua wapi unapenda na hayo ndio yatakuwa maisha yako mpaka Mungu Mkuu atakapoona imetosha. Ukitaka kubadili vitu upendavyo ni wewe, lakini mpaka Mungu atakapoona inatosha, uende katika Ulimwengu mwingine.
Ni kama hapa Duniani, vile unavyoishi ndivyo ulivyoamua kuishi au wazazi wako walivyotaka uishi (kumbuka ulikuwa katika mwili wa wazazi wako). Hakuna kulaumiana wala hakuna wakumlaumu. Hayo ndio maisha!
Acha nipumzike sasa,
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Roboti Hawezi kumchunguza aliye mtengeneza, kwa vile yuko programmed kufuata matakwa na masharti ya mtengeneza roboti.Chukua mfano rahisi tu wa roboti na mtengeneza roboti.je roboti aweza mchunguza aliyelitengeneza?
BIBLIA KTK VITABU VYA MITHALI 4:23 NA YEREMIA 17:9 INAZUNGUMZIA JUU YA MOYO, KWAMBA, TUNAPASWA KULINDA MOYO KULIKO VITU VINGINE VYOTE KWA SABABU KWENYE MOYO NDIKO KUTOKAKO CHEMICHEMI ZA UZIMA (LAKINI KUNAWEZA TOKA CHEMICHEMI ZA MAUTI PIA).LAKINI PIA, MOYO HUWA NI MDANGANYIFU.
MTU ANAUMBWA KTK MAENEO MATATU:
-ROHO, NAFSI, NA, MWILI.
BIBLIA HUREJEZEA NAFSI YA MTU KUWA NDIYO MOYO. ENEO LA NAFSI/MOYO NDIKO KUNA UTASHI, HISIA, NA, HAIBA YA MTU. WAINGEREZA WANATAMBULISHA MOYO/NAFSI KUWA NI PERSONALITY i.e. KWA KIBONGO, UTU WA MTU.
NDUGU HELIEL, LINDA SANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO; NA, KUMBUKA MOYO HUWA MDANGANYIFU SANA. MWENYEZI MUNGU (JEHOVAH) AMBAYE ANAJITAMBULISHA KTK BIBLIA KUWA NI MUNGU WA IBRAHIMU, NA ISAKA, NA, YAKOBO (ISRAELI) HAYUKO NAMNA MOYO/NAFSI YAKO INAVYOMCHUKULIA. NI ROHO MTAKATIFU TUU NDIYE PEKEE ANAWEZA KUMFUNULIA MTU JUU YA UUNGU WA MWENYEZI MUNGU (LAKINI KWA SEHEMU).
BIBLIA NI NENO LA MUNGU. ILIANDIKWA NA WANADAMU MBALIMBALI WALIOVUVIWA MAFUNUO NA ROHO WAKE (ROHO MTAKATIFU) WAKAIANDIKA KITABU CHA MWANZO HADI UFUNUO. MANENO YAKE NI HAKIKA NA AMINI. YAMETIWA MUHURI. KWA HALI HII HELIEL, NI HATARI SANA KUJARIBU KUBADILI, KWA NAMNA YOYOTE ILE, MAUDHUI YA BIBLIA; NI DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU; DHAMBI ISIYO SAMEHEKA KTK ULIMWENGU HATA ULE UJAO. NI HATARI SANA.
NAKUSHAURI OKOKA, YAANI, INGIA AGANO (MAKUBALIANO/ MKATABA) NA BWANA YESU KRISTO KWA KUTUBU NA KUJUTIA DHAMBI ZAKO, NA, UMKIRI KUWA AWE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO. KWA HATUA;
- UTASAMEHEWA DHAMBI ZAKO ZOTE NA HIVYO KUTAKASWA (KUWA MTAKATIFU)
-UTAPATIWA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU ATAKAYEKUFUNDISHA JUU YA BWANA YESU KRISTO NA KUKUOMBEA KWA MUNGU PIA.
-UTAPATA KIBALI CHA KUFANYIKA MTOTO WA MUNGU.
- JINA LAKO LITAFUTWA KTK KITABU CHA HUKUMU YA KWENDA KTK ADHABU YA MILELE MOTONI JEHANAMU, NA, BADALA YAKE LITASAJILIWA KTK KITABU CHA UFALME WA MBINGUNI.
NI HIVYO NDUGU YANGU HELIEL. BWANA YESU KRISTO ANAKUPENDA. ANAKUITA.
Asipothibitisha utamfanyajeSi ingilii uhuru wa mtu kuamini na wala silazimishi mtu kufuata ninacho sema.
Nachangia mada kwa kuhoji maswali ya anaye leta imani yake hapa JF.
Ni sawa kuwa na imani yako, ila unapo dai imani yako ni ya kweli lazima uthibitishe.
Na ndio maana tunahoji maswali ya uwepo wa huyo Mungu kwa vile mnaleta imani zenu hapa JF.
Mkuu kwahiyo mnaamini kwamba kwa sababu atheists wameshindwa kutoa jibu la chanzo cha ulimwengu basi automatically theists ndio wako sahihiWanao sema hakuna Mungu naomba mniambie
Ni nini chanzo cha ulimwengu,maji,hewa ardhi na viumbe hai.
Kifo ni nini.
Hafanywi kitu, lakini anapo jaribu kujenga hoja za uwepo wa huyo Mungu lazima pia aweze kujua kwamba kuna hoja pia za kutokuwepo Mungu.Asipothibitisha utamfanyaje
Kwan ni nani aliyekuambia wewe usipoamin uwepo wa Mungu ni kosa sio kosaHafanywi kitu, lakini anapo jaribu kujenga hoja za uwepo wa huyo Mungu lazima pia aweze kujua kwamba kuna hoja pia za kutokuwepo Mungu.
Vitabu vyote vya kidini ni stori za kusadikika, Fiction stories. Ndio maana hutofautiana maelezo kwenye kuelezea uwepo wa MunguReference yangu ni biblia ndugu,sijajitungia kichwani
Kuamini uwepo wa Mungu au kutokuamini uwepo wa Mungu si kosa.Kwan ni nani aliyekuambia wewe usipoamin uwepo wa Mungu ni kosa sio kosa