Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Ni sahihi, Mungu wetu tumeuona na watu wake wamemuona toka enzi na enzi. Toka Adam, Isaya, Daniel, Mikaya, Ezekieli hadi Yohana pale kisiwani patimo wameona "yule mzee wa siku nyingi" yeye aliye "mfano wa mwanadamu" ambaye kichwa chake ni Nywele safi mfano wa sufu, yeye aketiye juu ya majeruhi, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi kilicho na magurudumu ya moto na mbele yake kuna mto mkubwa wa moto na maelfu kwa maelfu wanaotumikia.

Nina ushuhuda kuhusu ufunuo huu. Mungu wetu yu jirani nasi, yu rafiki na Baba mwema kwetu. Yeye anatupenda na anatutaka nasi tumpende ili awe karibu nasi.

Nakumbuka akaniambia " Umepata Neema na Bahati katika kizazi hiki kuniona na kusikia sauti yangu"
Aisee yukoje Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo?
Mimi kumuamini inatosha sitaki kumuona Kwa macho yangu, nitamkimbia.
Sio lazima kumuona ila kama inawezekana share tufahamu zaidi.
Je ana rangi kwenye ngozi yake?
Maana aisee Kuna mafunuo sikuhizi eti Yesu ni black man , mi huwa nashangaa tu.
 
Thanks but you have not replied my questions;

  • do they use the same Bible?
  • and if they believe that Jesus stays in their heart etc than what are the current beliefs of those attending the Churches of the Catholics and Lutherans?

- Why do the preachers utilize 'oil' and charge for 'treatments'??
Walokole waanatumia biblia moja...ila katika mapokeo yao ya neno yamewekwa ndani ya mioyo yao na wanayaishi

Labda nikupe mfano hapo kwa Lutheran...

Mimi ni mlutheran hadi kipaimara nimesoma ila sasa nimeokoka ni mlokole...ishu sio dhehebu...

Siwezi kuzungumzia suala la hao Manabii na mafuta wanayotumia maana ni wapakwa mafuta ya Bwana...

Ila ninaouwezo wa kupima Roho zao nikajua huyu ni wa Bwana na huyu sio...
 
Aisee yukoje Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo?
Mimi kumuamini inatosha sitaki kumuona Kwa macho yangu, nitamkimbia.
Sio lazima kumuona ila kama inawezekana share tufahamu zaidi.
Je ana rangi kwenye ngozi yake?
Maana aisee Kuna mafunuo sikuhizi eti Yesu ni black man , mi huwa nashangaa tu.
Kimsingi, yeye anajifunua kulingana na nini anataka kukufundisha/kusema nawe. Binafsi nakiri leo nikiwa na akili timamu kuwa nimemuona si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na anajifunua kwa namna tofauti tofauti. Katika mara zote sijawahi iona sura tokana na mwanga mkali uliopo usoni mwake so sio "mzungu wala black " huwezi muangalia/uona uso wake lakini nywele za kichwa chake ni nyeupe na zinang'ara kama theluji ila zimelala kama za mzungu.(Ufunuo 1:14, Daniel 7:10)
Nimemwona kama Nuru kali(Matendo 9:3) nimemwona kama hiyo mzee wa siku, nimemwona kama mtu mrefu na mkubwa yaani Mbingu ni kiti chake na duniani ni sehemu ya kuweka miguu yake(Isaya 66:1) nimemuona akija na mawingu akiwa na malaika wengi, nimemuona akiwa amepanda farasi mweupe(Ufunuo 19:11-14)

Kuhusu Yesu kuwamweusi wakati akiwa jinsi ya mwili au lah, Nakumbuka mwaka 2016 au 17 huku JF kulikuwa na mada kuhusu Yesu kuwa black. Nami niliiamini ile na ilinikaa moyoni. Nikamuuliza, bwana kwa jinsi ya mwili ulikuwa mweupe au mweusi? Akaniambia kuwa mweupe au mweusi haitakusaidia kitu ila kuna siku nikalala nikaona "Mkutano mkubwa wa watu wamekusanyika na Kijana mmoja mweupe/mwekundu na mwenye nywele nyeusi fupi zilizonyolewa na kuwa chini chini/ndogo zisizolala kama za wazungu ila zimesimama kama za Waafrika akiwa amesimama katikati ya kusanyiko hilo akiwa kwenye mimbari/jukwaa akihutubia. Akashuka toka kule jukwaani na kuja karibu nami na kuniita jina langu na akaniuliza, wewe una kanisa gani? Kabla ya kumjibu akaondoka ila wakati akiwa kule jukwaani/mimbari nilijua bila kuambiwa kuwa huu ndio muonekano wake alipokuwa duniani kwa jinsi ya mwili." Kwani katika ulimwengunwa Rohonkila kitu ni wazi na unaoata majibu ya moja kwa moja kwa yale uyawazayo. Kimsingi, hakuwa mnene wala mwembamba, hakuwa mrefu sana wala mfupi ni wa kati kati. Alivaa kanzu nyeupe na kujifunika kikoi/shuka cha khakhi huku amevaa sendors miguuni kwake.
 
Katika maandiko nyota zimeandikwa.

Mungu ametukataza kupiga BAO au kutafuta habari za yajayo na nyota kupitia uganga.

Anataka tumuulize na kumtegemea Yeye pekee kupitia Roho MTAKATIFU.

Niliposema nyota, nilimaanisha NAFSI. NAFSI ya mtu inaweza kufungwa kuzimu, pangoni, chooni, barabarani au chini ya kitanda nk nk,

Wakati NAFSI ya mtu imefungwa Mahali pengine, Pepo hukaa ndani ya mtu, wakati mtu halisi hayupo.

So kwenye nyota weka NAFSI mtumishi.

Amen.
Umeelezea vyema
 
Walokole waanatumia biblia moja...ila katika mapokeo yao ya neno yamewekwa ndani ya mioyo yao na wanayaishi

Labda nikupe mfano hapo kwa Lutheran...

Mimi ni mlutheran hadi kipaimara nimesoma ila sasa nimeokoka ni mlokole...ishu sio dhehebu...

Siwezi kuzungumzia suala la hao Manabii na mafuta wanayotumia maana ni wapakwa mafuta ya Bwana...

Ila ninaouwezo wa kupima Roho zao nikajua huyu ni wa Bwana na huyu sio...
Umeeleza vyema
 
Kimsingi, yeye anajifunua kulingana na nini anataka kukufundisha/kusema nawe. Binafsi nakiri leo nikiwa na akili timamu kuwa nimemuona si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na anajifunua kwa namna tofauti tofauti. Katika mara zote sijawahi iona sura tokana na mwanga mkali uliopo usoni mwake so sio "mzungu wala black " huwezi muangalia/uona uso wake lakini nywele za kichwa chake ni nyeupe na zinang'ara kama theluji ila zimelala kama za mzungu.(Ufunuo 1:14, Daniel 7:10)
Nimemwona kama Nuru kali(Matendo 9:3) nimemwona kama hiyo mzee wa siku, nimemwona kama mtu mrefu na mkubwa yaani Mbingu ni kiti chake na duniani ni sehemu ya kuweka miguu yake(Isaya 66:1) nimemuona akija na mawingu akiwa na malaika wengi, nimemuona akiwa amepanda farasi mweupe(Ufunuo 19:11-14)

Kuhusu Yesu kuwamweusi wakati akiwa jinsi ya mwili au lah, Nakumbuka mwaka 2016 au 17 huku JF kulikuwa na mada kuhusu Yesu kuwa black. Nami niliiamini ile na ilinikaa moyoni. Nikamuuliza, bwana kwa jinsi ya mwili ulikuwa mweupe au mweusi? Akaniambia kuwa mweupe au mweusi haitakusaidia kitu ila kuna siku nikalala nikaona "Mkutano mkubwa wa watu wamekusanyika na Kijana mmoja mweupe/mwekundu na mwenye nywele nyeusi fupi zilizonyolewa na kuwa chini chini/ndogo zisizolala kama za wazungu ila zimesimama kama za Waafrika akiwa amesimama katikati ya kusanyiko hilo akiwa kwenye mimbari/jukwaa akihutubia. Akashuka toka kule jukwaani na kuja karibu nami na kuniita jina langu na akaniuliza, wewe una kanisa gani? Kabla ya kumjibu akaondoka ila wakati akiwa kule jukwaani/mimbari nilijua bila kuambiwa kuwa huu ndio muonekano wake alipokuwa duniani kwa jinsi ya mwili." Kwani katika ulimwengunwa Rohonkila kitu ni wazi na unaoata majibu ya moja kwa moja kwa yale uyawazayo. Kimsingi, hakuwa mnene wala mwembamba, hakuwa mrefu sana wala mfupi ni wa kati kati. Alivaa kanzu nyeupe na kujifunika kikoi/shuka cha khakhi huku amevaa sendors miguuni kwake.
Anhaa so Yesu rangi Iko ka ya wale Middle East hivi?
 
Ni kweli ila ukiwawekea kwenye kitabu utawasaidia walioko nje ya hapa jf maana huu ni moja ya utafiti bora Duniani ambao utafungua akili za wanadamu

Kitabu kitauzika sana hiki
Habari za mmliki wa wamiliki na mkuu wa wakuu na mungu wa walokole haziuziki kama unavyofikiria.Lakini upo sawa ndugu yangu sababu imefikiri kama ambavyo mti mwingine yoyote angefikiri.
 
Makanisa ya Kilokole ndio yamefanya walokole wakawa wengi zaidi...

Kwanini...
Yamewafundisha watu kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wao kwa kufundisha neno kwa wingi...

Uhusiano na Mungu hauwezi kuja kirahisi bila kuwa na neno la Mungu au chakula Cha kiroho hivyo ni lazima litafitwe kwa bidii...na hayo makanisa ya Kilokole na Manabik wengi ndio wameokoa watu wengi...

Na yamefanya watu kuwa karibu na Mungu sana...ndio maana Sasa watu wanamuona Mungu
Mi nadhani aliyefanya walokole kuwa wengi ni YESU tu! Yesu peke yake!! Mwana wa Mmiliki peke yake! Yeye tu! Hakuna cha kanisa hata moja lililomfia mtu hapa duniani!

Watu wanaokolewa kwa neno la uzima! Yesu ndiye huyo neno! Hakuna cha mchungaji, nabii, mwinjiristi, mtume, mwalimu wala nani NI YESU TU! SIFA NA UTUKUFU KWA MWANAKONDOO!

Katika hili, ulokole siyo dhehebu!
 
Sijajua wapoje ila naweza sema ni kama red indian hivi. Sizijui sana hizi races mkuu ila alikuwa mweupe but sio mzungu pure kama wazungu wa sasa pia nywele hazikuwa za wazungu i.e zimelala ila zilikuwa zimesimama na fupi.
Kuhusu rangi ya ngozi yake naona inaendana na Maandiko , maana iliandikwa lazima Kristo atoke kwenye ukoo wa Daudi na rangi ya Daudi ilikuwa nyekundu

1 Samweli 16:12-13
[12]Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. BWANA akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye.
And he sent, and brought him in. Now he was ruddy, and withal of a beautiful countenance, and goodly to look to. And the LORD said, Arise, anoint him: for this is he.
[13]Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya BWANA ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.
Then Samuel took the horn of oil, and anointed him in the midst of his brethren: and the Spirit of the LORD came upon David from that day forward. So Samuel rose up, and went to Ramah.
 
Sijajua wapoje ila naweza sema ni kama red indian hivi. Sizijui sana hizi races mkuu ila alikuwa mweupe but sio mzungu pure kama wazungu wa sasa pia nywele hazikuwa za wazungu i.e zimelala ila zilikuwa zimesimama na fupi.
Watu wa Middle East ni waarabu mkuu ndo nilimaanisha, achana na Wayahudi wa Sasa walioko Israeli mi nawaona kama wazungu vile.
 
NINAENDELEA.......!!!!
WANAJIMU NA WAGANGA :Wanajimu na waganga hawana usharika na walokole katika lolote lile.Wao ni washirika wa wale watu warefu wa baharini.Unajimu haufundishwi kwenye mikusanyiko ya kilokole sababu una makufuru na hatua zake nyingi zina ushirikiano na uganga.Wanajimu wanachukua nyota za wangu na kuzitumia kwa manufaa yao.Wanajimu wanafanya tafukuri ambayo ni laana kiroho.Wanajimu hawana utii kwa mkuu wa mamlaka aliye mkuu wa wote,bali wao wanatii uganga wako na miungu ya kwenye sayari za ndani ya mfumo ww jua wa ulimwengu.Wanajimu wanashirikiana na wale viumbe wa baharini kumuhujumu mwanadamu aliepo duniani.Wanajimu wanatafuta elimu ya anga kwa njia za uchawi wa kale wa kiarabu na kiajemi.Wanajimu hawana maombi ya kubariki bali wana maombi ya kulaani,kwani kwao laana ni sehemu ya matambiko yao.Hivyo wanajimu ndani ya ulimwengu wa kiroho sio watu wema.
WALE VIUMBE WAREFU :Kama nilivyosema pale mwanzo kua,kuna aina mbili za wale viumbe warefu
MOJA :Watu warefu wa angani wanaoakisi mwanga
MBILI :Watu warefu wa baharini wasioakisi mwanga.
WATU WAREFU WA ANGANI WANAOAKISI MWANGA :Wale watu warefu wazuri kwa muonekano,wanaoshika panga na kulinda walokole ni watu wa ajabu sababu ya tabasamu zao na upendo wao.Akikusogelea kwa karibu utatamani ulie kwa furaha maana unapata amani ya moyo iliyopitiliza.Wana upendo mkuu sababu ukiona jinsi wanavyowahudumia walokole lazima upendezwe nao.Walokole ni kama vitoto vidogo mbele ya hawa walinzi wao ""Watu warefu""..Upenda na ulinzi ndio sifa yao kuu.Wao ni moto ndani ya moto wa shaba,wana nguvu kama umeme wa radi.Kimuonekano wengine wana mabawa na wengine hawana mabawa ila wote warefu kwa vimo.
WATU WAREFU WA BAHARINI WASIOAKISI MWANGA :Hawa ni washirika wa waganga na wanajimu na wachawi.Kimuonekano ni watu wa kubadilika badilika.Hawana muonekano mzuri wa kudumu bali wanachukua sura halisi za binadamu,hasa binadamu wa bara hindi na uajemi.Hawana usharika na walokole sababu walokole wanaharibu kazi zao wanazofanya na wanajimu na wachawi.Hawana upendo wala amani ya moyo wakikusogelea,zaidi zaidi utasisimka na kuogopa.Ni washirika wa mkuu wa ulimwengu mwenye vita vya kudumu na walokole.Tusiwazungumzie sana hapa maana lengo sio kuwazungumzia wao bali Mungu wa walokole.
Kwa binadamu wa kawaida unakua na amani ukikutana na hawa watu warefu wa angani ambao ni walinzi wa walokole,maana wanalinda watoto,wanalinda wagonjwa,wanalinda walokole na wasiokua walokole na wanazuia majanga ya kutengenezwa na wale watu warefu wa baharini na washirika wao ambao ni wachawi na wanajimu na waganga na washirikina wa kibinadamu.Popote pale duniani kwenye ulimwengu wa kiroho utawaona wanaruka huko na huko.
Afu mungu wa walokole ambae ni mkuu wa mfumo wa anga kuu nje ya mfumo wa sayari za ulimwengu kaficha siri ya mfumo wa ulimwengu nje ya mfumo wa anga na sayari zote,,maana angani ni kama mfumo wa anga na sayari unaelea ila huwezi jua umejishikiza wapi.
Hesabu za kinajimu zina kikomo ila hesabu za unajimu wa nje ya mfumo wa ulimwengu hazina kikomo na zinaongozwa na mwana wa mmliki.Na ndio maaana huyo mwana wa mmliki na wale watu warefu weupe wanaishi milele toka dahari ya kwanza mpaka dahari isiyo na ukomo kwa kingereza wanaita""Eternity's""".
Walokole wanaposali ndio mda mzuri wa kua nao sababu mungu wao anashuka kwa njia kuu tatu(3)
MOJA :Kama njiwa mweupe wa dhahabu
MBILI :Kama moto wa mataji ya viduara na kukaa vichwani mwa walokole
TATU :Kama wingu za moto unafunika eneo zima.
Sasa kama walokole wakiwa wanasali na wewe upo karibu basi baraka zao kiroho zinakufikia mpaka wewe.Mungu wa walokole hana ubaguzi katika kutoa baraka kwa bunadamu,ni kama anatusubiri tumjue atubariki.Lakini pamoja na upole wake,huyu mungu wa walokole ana mzaha pale unapotaka kudhuru walokole wake na haoni hasara kukuua kwa pumzi yake ya moto.Anawapenda walokole wake kuliko kitu kingine chochote.
NITAENDELEA..... ....!!!!
Mkuu uzi huu umenipa hamasa Sana ya kusoma neno, wakati nafuatilia Habari za muonekano wa Malaika aka watu wa refu wanaoakisi mwanga Nika kutana na neno hili ambalo kiasi kikubwa linathibitisha usemayo, waebrania 1:7..na kwa Habari ya Malaika kasema, a fanya Malaika wake kuwa pepo na watumishi wake kuwa miali ya moto.. Pia Waebrania 1:13-14,je hao wote si roho watumikao, wa kitumwa kuwa huduma wale watakaourithi wokovu?
Kama unaesoma hujaokoka nakusihi kimbilia Neema hii ya wokovu Kuishi kama mwana wa mfalme... Tunapendwa sie.. Tunalidwa balaa... YESU nakushukuru kunifungua Macho ya Rohoni nikaona thamani ya Wokuvu Mkuu namna hii🙏🙏
 
MI KINACHONISIKITISHA

Ni kama KILA kitu kilipangwa kabla hata misingi ya ulimwengu haijakuwepo!!

Yaani hata hao wa jehanam na hao wa peponi walipangiwa kuwa fate yao itakua hivyo!!

Unafikiri huyo shetani alipoumbwa na kuwa shetani ilikua by surprise!!?

Yaani chanzo kikuu cha vyote hivi ni muumba mwenyewe hakuna Bahati mbaya wakuu!!

Uwepo wa shetani,moto,pepo vyote ni mpango KAZI hata hao watakaoingia ni mpangokazi rasmi hakuna Bahati mbaya KWA lolote itategemea yeye muumba alikuandikia nini coz hakuna anaewez and kujifanya mtakatifu wala muovu isipokua KWA Mapenzi yake yeye aliemuumba yeye na pande ZOTE mbili yaani shetani na upande wa pili!!!

Ni hayo tu!!
Nilikuwa natafuta hii comment ili nikujibu.
Ni hivi hakuna Mungu katili wa namna huyo. Leo aniumbe Kinengenengu na kunileta duniani ili aniangamize. Biblia inasema kuhusu shetani na chanzo cha dhambi ni uasi wake mwenyewe.
Ezekieli 28:13-19 In summary inasema "Mungu alimuumba Lucifer akiwa mkamilifu na mwenye kupendeza. Alimuumba maalumu kwa ajili ya sifa ila tokana na uzuri wake, kiburi kikainuka ndani yake iliyopelekea kumuasi Mungu na hivyo kuhukumiwa.
Pia Isaya 14:12-15 utaona inasema "Namna kiburi, kutamani utukufu wa Mungu na kutaka kufanana au kuwa zaidi ya Mungu ndio chanzo cha kuanguka kwa Ibilisi"
Kwa hiyo mkuu, Mungu hakuwa na mpango wa kumuumba ibilisi na mapepo(Malaika waasi) ili kuwaangamiza ila kiburi na majivuno ya shetani ndio chanzo cha hayo yote.

Kuhusu mwanadamu, Mungu hawezi kuumba mwanadamu tena kiumbe dhaifu na kukiangamiza. Biblia inasema wazi, Mungu alimuumba mwanadamu ili awe mtawala katika hii dunia. Akampa dunia ikiwa kamili apate kuishi na kutawala humo. Mungu aliumba kiumbe kinachofanana naye na kukipa mamlaka, kumuabudu, kishirikiane naye, kimuheshimu naye amuheshimu, kuwe kitoto chake naye awe Baba yake. Mungu kamwe hakumuumba mwanadamu ili amuhukumu na kumuangamiza. Huyo atakuwa Mungu wa hovyo na katili sana.

Adam alikaa bustanini katika mazingira mazuri ila alishindwa kutii. Anguko lake ndio lilileta dhambi na hukumu ya mauti. Ila tokana na upendo wake, Mungu mwenyewe akavaa mwili ili aje mkomboa Mwana wa Adam. Kwa hiyo, Mungu anatuwazi mema ila dhambi zetu ndio zimetutenga na uso wake.
 
Back
Top Bottom