Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

INAENDELEA........
Basi udadisi wangu ulianzia kwa dadangu wa kuzaliwa tumbo moja,ilikua kila jioni wakati nipo mdogo miaka ya shule ya msingi,kila ikifika jioni mamangu ambae alikua mlokole alikua anawaita wamama majirani zake kusali jioni baada ya kula na wanasalia uani kwenye nyumba.Wakiwa wanasali na sisi kama watoto tunaenda kukaa chini pale tunasali nao ila sio serious,basi dadangu ananiambia angalia ukutani kuna "Malaika"wamekuja.Mimi natoa macho sioni na kumbe kuna baadhi ya wale walokole wanawaona pia ila hawasemi.Dada baadae anaenda kumsimulia mamangu na mamangu anaenda kuwasimulia waumini wenzake kua mwanangu jana kaona malaika.Basi wale wamama wakiongozwa na mama mmoja hivi anaitwa "Mama Samueli"ndio kama wamemwagiwa maji ya moto maana kesho wakija ni maombi pale uani masaa saba au sita kila jioni na kila siku nachungulia nitawaona hao malaika au sitowaona,nikaambulia patupu ila dadangu siku moja moja anawaona na kunielezea.Ndipo udadisi wangu ukaanzia hapo kutaka kujua viumbe hawa wa kiroho na jinsi walivyo na utararibu wao wa maisha na wanakaa wapi na madhumuni yao kushuka duniani kuja kukaa na walokole wanapokua wanasali.
Miaka ikaenda na nikasahau hayo mambo ila kuna vitu vikawa.Kuna siku nilikua msibani nikajiuliza sana kwanini binadamu wanakufa na wakifa wanaenda wapi,nikaanza upya udadisi wangu kuhusu ulimwengu usioonekana.Kuna wakati nilisafiri mkoani kigoma nikakutana na mzee mmoja nikamuelezea kuhusu udadisi wangu wa haya mambo ya ulimwengu usionekana.
Mosi:Akaniambia nje ya ulimwengu huu wa kawaida kuna ulimwengu mwengine na kuna jamii mbili ambazo ni jamii za watu wanaofanana na binadamu na wanaakisi mwanga wa jua na makazi yao ni anga za mbali nje kabisa na mfumo kani wa ulimwengu karibia maili trion zisizohesabika kwa hesabu za kibinadamu.Na pia jamii ya watu wanaofanana na binadamu ambao wanakaa katikati ya dunia ila wanazurura kwenye sayari zote za mfumo wa jua ila hawawezi kwenda nje ya mfumo kani wa ulimwengu sababu sio eneo lao la kiutawala.
Pili:Hizo jamii zote zina imani zao na zimeleta imani hizo kwa binadamu na kuwafundisha na nikitaka anaweza kunifundisha pia,lakini ni imani kinzani.
Tatu:Nikitaka kujua haya mambo nichague upande mmoja wa jamii zile mbili niwe mfuasi wake lakini kuna miiko na utaratibu wake wa kuzingatia katika hilo.
Akaniuliza yule mzee ""Wewe unataka kujua nini""nikamjibu kua mimi nataka kujua na kuwaona wale viumbe waliokua wanamtokea dadangu utotoni ikiwezekana niwahoji baadhi ya vitu kuhusu wao.Nakumbuka yule mzee akachekaa akaniita kwa kucheka""Mulashani""nani alikupa jina hilo na mimi nikamjibu ni babu yangu mzaa baba,akacheka akasema unajua maana yake hilo jina.Nikamjibu sijui,akasema maana yake ni mtu mpiganaji na wapiganaji waga wadadisi na wadadisi hupatwa na majanga sababu ya udadisi wao.Lakini akaniambia nitakupa njia rahisi ya wewe kuwaona hao viumbe,ila akauliza ni nani aliyekuelekeza kwangu..Nikamjibu kua wewe mzee............ ni mnajimu na una elimu ya anga nilielekezwa kwako na flani........nikamtajia jina la mtu aliyenielekeza kwake.
Akasema wewe shida yako tu ni kuwaona hao viumbe wanaokwenda kwa walokole kila mara??????Nikamjibu ndio,akaniuliza ukiwaona hautoweza kuzungumza nao sababu haujapitia njia yao kwenye ulimwengu wa ndani,kwanini usiende kwa walokole wakufundishe jinsi ya kuwaona.Nikamjibu kua shida yangu ni kuwaona na kuamini kama wapo hao viumbe.Akaniuliza tena unajua wanaitwaje,nikamjibu kwa kusema wanaitwa"Malaika au makerubi""akaniambia wanaitwa watu wa jamii ya jua na mkuu wao hana upinzani katika ulimwengu zoote saba.Nikaanza udadisi na maswali kwanini wanajihusisha na walokole.
Mzee akanijibu wanajihusisha na walokole sababu walokole wana usharika nao kupitia""Mwana wa mmliki""ambae walokole wanamwita Mungu wao na wanatumia jina lake ila hawezi kulitaja hapo sio mahali pake.Akasema wao hao watu wa jamii zenye kuakisi mwanga wa jua wana makazi yao nje kabisa ya mfumo wa sayari za ulimwengu na wana miaka sawa na mwanga wa mfumo wa sayari za ulimwengu mara trioni.Akimaanisha kua walikuepo miaka trioni kabla ya mfumo wa sayari za ulimwengu kuwepo.
Nikamuuliza vipi kuhuusu ile jamii nyingine ya wale watu alioniambia wanakaa katikati ya dunia kupitia chini ya maji,akanijibu shida yangu ni kuwajua viumbe marafiki wa walokole basi hayo mengine niachane nayo kwanza.Akaniambia tayari washajua nia yangu ya kutaka kuwaona hivyo nikwaona nijue ni kwamba wao wameamua niwaone na nisipowaona nijue ni wao wameamua nisiwaone.
Akaniuliza nia yako ni kuwaona tu hakuna jingine lolote,nikamjibu ndio.Basi akasema atanielekeza nimuone mkuu wao ambae ni nyota ya mashariki wao wanajimu wanamuita hivyo.Akasema ikifika jioni twende karibia na kanisa lolote la kilokole au mkusanyiko wowote wa kilokole hasa wakiwa katika maombi yao.Yeye hawezi kusogea ila mimi naweza kuwasogelea wale walokole na wakianza kusali nifumbe macho pia ni ishara ya heshima kwa mkuu wao(Mungu wao)..Afu nitakachokiona iwe siri yangu ili nisiwashitue wale walokole wanaosali pale
Basi ile wilaya niliyokuwepo kuna makanisa mengi ya walokole hasa pale mjini,nikaona ndio kitovu cha utafiti wangu kuwatafiti walokole kisayansi nijiridhishe dukuduku zangu kuhusu matukio ya utotoni.Basi kufikia jioni tukaenda kwenye kanisa alilonielekeza tukawadadisi walokole tuwapeleleze.Mimi na akili zangu za kisayansi afu mzee wangu mnajimu na akili zake za uganga na utaalamu wa nyota na anga wanaita unajimu.Tulipokua njiani akawa ananiambia wewe kijana mdadisi ila na mimi udadisi wako umenivutia na mimi ngoja nikupeleke afu mimi nakaa mbali maana walokole nawajua na imani zao nazijua na kwa mbali tunasikia miziki ya vyombo inatoa sauti watu wanaimba kwaya maana kanisa halikua mbali sana ni kilimani tu unapandisha,mimi mbele na mzee wangu nyuma tunapandisha kilima.Cha ajabu sasa nipo njiani yule mzee wangu mnajimu tunapiga story mara nahisi ukimya ile kugeuka eeeh kanikimbia kimiujiza nimebaki peke yangu njiani.Nageuka kushoto simuoni nageuka nyuma simuoni,nageuka kulia simuoni.Lakini nilipoangalia mbele tena"""Eeeeh"""Nakutana na mtu mrefu kama wale wachezaji wa mpira wa kikapu ananitazama,na anaakisi mwanga wa jua,amevaa kanzu bwanga na miguu yake haifiki chini ila imefunikwa na ile kanzu.Uso wake ulikua wa kirafiki sababu alikua anatabasamu ila hauonekani vizuri hata nywele sababu ya kuakisi mwanga wa jua na ngozi yake kama rangi za sarafu ya mia mbili au sarafu za shilingi hamsini,kwa haraka haraka ni kama mtu wa shaba ila mrefu kuliko binadamu wa kawaida.Lakini sasa anatembea kuja barabarani nilipo,na sio kwa kutembea kule bali kuelea wimawima hewani.Hayo yote ni ndani ya nusu dakika,na mzee kashakimbia simuoni.Ile nataka nianguke kwa hofu yule mtu akapotea ila sasa mimi nipo nimeganda kama sanamu hofu yoote imetoweka limebaki bumbuwazi natoa macho tu.
Baadae kidogo ndio akili inarudi ila cha ajabu hofu sina naona kawaida tu,yule mzee wangu simuoni sijui alipoteaje bila kunitaarifu.Safari ya kwenda kanisani kwa wale walokole ikaishia hapo nikaanza kurudi chini kilimani kumtafuta mzee wangu na nilipomkosa nikarudi mpaka nyumbani kwake namkuta kakaa ananisubiri huku kanuna ila mimi nikaanza kucheka.Akaniuliza unacheka nini afu yeye akaanza kucheka ila ananicheka mimi""Wewe si mdadisi mbona ulikimbia mjukuu wangu"""nikamwambia sikukimbia ila niliganda kwa hofu na yule kiumbe alitokea na kupotea ndani ya nusu dakika.Akaniambia yule sio kiumbe bali ni wale watu wa jamii ya jua walinzi wa walokole.Akasema mpango wa kuwadadisi wale walokole tutaufanyia tukiwa mbali ila sio karibu na makanisa yao na akanitaka ninuie kua mimi shida yangu ni udadisi tu na sio kitu kingine chochote.Nikanuia pale na akaniapiza na tukapanga tutaendelea na udadisi wetu siku nyingine kwa siku ile nilichokiona kinatosha,ila sasa nikitaks kuendelea na udadisi lazima niwe msiri nisitangaze kwa watu,afu niwe nakariri maombi ya walokole maana waga wanaongea moja kwa moja na mkuu wao ambae anaitwa""Mwana wa mmliki"'ikiwezekana niombe kibali cha kufanya udadisi wangu sababu sina nia mbaya na walokole bali nachofanya ni udadisi wa kujiridhisha utafiti wangu.Cha ajabu japo yule kiumbe alikua ametokea ghafla ila sikua na uoga kabisa moyoni baada ya yeye kutoweka.Akili yangu na hamu ya udadisi kwenye ubongo wangu ikaendelea kuongezeka wakati ule nipo mkoani kigoma kwenye wilaya moja inayopakana na nchi jirani.Mzee wangu akaniambia kila alhamisi ndio siku atakazokua na nafasi kunifundisha kidogo kidogo na kunielezea kwa undani hao walokole ni watu wa aina gani na hiyo alhamisi atanieleza kwanini alinikimbia siku ile pale kilimani wakati tunaenda kuwapeleleza walokole kwenye kanisa lao
ITAENDELEA............!!!!!
 
Ni walokole gani hao mkuu, maana wanaonena kwa lugha kwa sasa ni wengi na walokole wamegawanyika sana?
Haya pale wanaponena kwa lugha, ni wote hujiwa na hao watu warefu au baadhi??

Kwanini ni maskini? Watu warefu wanafaidika nini kupitia hao walokole? Kwanini wanawafanya maskini?

Mwisho kwa imani yako mtu akifa anaenda wapi??
Maswali mazuri,nitakujibu yote mkuu ucjali
 
Napata shaka kama ulimuona huyo MUNGU wa walokole...

Mbona umetumia Mnajimu? Maana Mnajimu huyo ni Mkuu wa giza...

Kumuona Mungu sio kwa kutumia mtu na nguvu za kibinadamu.

Bali ni kwa kumpokea Bwana kuwa mwokozi wa maisha yako, kuomba, kufunga, kusali...

Na hii ndio maana wapo ambao wanaenda kanisani kila siku ila hawaoni mambo ya Rohoni...

Wanajiita wakristo lakini YESU hawajui...
 
Napata shaka kama ulimuona huyo MUNGU wa walokole...

Mbona umetumia Mnajimu? Maana Mnajimu huyo ni Mkuu wa giza...

Kumuona Mungu sio kwa kutumia mtu na nguvu za kibinadamu.

Bali ni kwa kumpokea Bwana kuwa mwokozi wa maisha yako, kuomba, kufunga, kusali...
Mungu wa walokole au mkuu wa walokole haonekani mpaka uwe kwenye njia yake kiroho,wanajimu wenyewe hawawezi kufika alipo huko nje ya kani za ulimwengu wa mfumo wa jua,ila kwa utafiti wao wanajimu wanasema yeye ni moto ndani ya roho ya moto na hakuna binadamu aliyemuona akabaki hai au kurudi duniani.Bali ule moto wa viduara unaowazunguka walokole ndio wanajimu wanaita ni pumzi za Mungu wa walokole.Na kuna nyota ya mashariki wanajimu wanamuita ""Mwana wa mmliki"""inaangaza usiku angani,wanajimu wanasema ndie kiungo kati ya walokole na mungu wao,na huyo mwana wa mmliki ndie anaodhi anga lote la mfumo wa jua na nje ya mfumo wa jua.Ndio maana wanamwita Nyota ya mashariki.Ni kiumbe wa kiroho na kiongozi wa wale watu warefu wanaoakisi mwanga wa jua.
 
Mungu wa walokole au mkuu wa walokole haonekani mpaka uwe kwenye njia yake kiroho,wanajimu wenyewe hawawezi kufika alipo huko nje ya kani za ulimwengu wa mfumo wa jua,ila kwa utafiti wao wanajimu wanasema yeye ni moto ndani ya roho ya moto na hakuna binadamu aliyemuona akabaki hai au kurudi duniani.Bali ule moto wa viduara unaowazunguka walokole ndio wanajimu wanaita ni pumzi za Mungu wa walokole.Na kuna nyota ya mashariki wanajimu wanamuita ""Mwana wa mmliki"""inaangaza usiku angani,wanajimu wanasema ndie kiungo kati ya walokole na mungu wao,na huyo mwana wa mmliki ndie anaodhi anga lote la mfumo wa jua na nje ya mfumo wa jua.Ndio maana wanamwita Nyota ya mashariki.Ni kiumbe wa kiroho na kiongozi wa wale watu warefu wanaoakisi mwanga wa jua.
Uliposema hawawezi kumsogelea ni kweli kwakuwa yeye ni moto na huwa unawaunguza...

Pia hao wakuu wa giza wanamjua YESU/MUNGU kuwa anauwezo mkubwa kuliko wao...
 
usipoteze muda, ukitaka kujua Mungu wa walokole, kawaulize wachawi. wanatujua vizuri sana na nyumba zetu huwa wanaruka hawakanyagi ng'oo. hii ni kwasababu Mungu wetu tunamwabudu katika Roho na kweli, na anakaa mioyoni mwetu, hakati kanisani au kwenye masanamu au eneo fulani kwenye nchi fulani tu.
 
Nimekuelewa Sana!

Barikiwa Sana
Kusema kweli kwa utafiti wangu nje ya mwili kuhusu hawa watu warefu nilikua nawaona wanaenda sana kwa hawa walokole wanaosalia majumbani vikundi vikundi na wengine wanakwenda kwa walokole wanaotembea barabarani,wanauza dukani,waliopo ofisini,mashambani.Walokole wana alama miilini mwao wenyewe wanaita matunda ya roho.Kuhusu makanisa wale watu warefu hawabagui popote alipo mlokole akiwaita kwa kulia wanaenda kumzunguka.
Msikitini sikuenda sababu mkufunzi wangu aliniambia nikitaka kuwadadisi wale watu warefu wapoje basi niwadadisi walokole wanaolialia,nyinyi mnaita kunena kwa lugha.Kwahiyo sikwenda misikitini au mahekalu ya wahindi au masinagogi ya wayahudi sababu nisingewakuta walengwa wangu kwenye utafiti ambao ni walokole.Lakini sehemu zinazoongoza kwa walokole ni kwenye hayo makanisa mnayaita ya kilokole na kilutheri...afu makanisa mengine yanafuatia kwa kua na mlokole mmoja mmoja
NB:Kuna makanisa mengi tu kwa nje yanaonekana ya kilokole ila wale watu warefu walikua hawaingii maana hakuna walokole ndani ila ni makanisa ya kilokole kwa muonekano wa nje.
 
Kuanzia mwaka 1997 mpaka mwaka 2019 nilikua kwenye research binafsi ya mambo yasiyoonekana kwa macho ya kawaida. Nimefanya mahojiano na watu wa fani hii,kuanzia watu wa kawaida mpaka viongozi wa fani hii katika nyanja mbalimbali.

Mambo yasiyoonekana kwa macho,watu wanaita""UCHAWI""na ni fani yenye kuchanganya kidogo sababu inajumuisha imani za dini za wanadamu na imani za dini zisizo za wanadamu. Pia inajumuisha watu ambao wanaitwa bin-adamu na inajumuisha watu wale wengine ambao hawana undugu na hawa watu wanaoitwa bin-adam.Nielezee kidogo hao watu wengine,nimewaita watu sababu wana maumbo kama binadamu ila vimo vyao vipo tofauti na wapo katika jamii mbili tofauti.

Kuna ile jamii ya wanaokaa angani ambapo bila ruhusa yao huwezi kuwafikia,na kuna ile jamii ambayo hata bila ruhusa yao unaweza kuwafikia na wanakaa chini ya bahari au mito au maziwa makubwa(Lakes).Ngoja nifafanue kidogo jamii za hawa watu.

Jamii ya watu wa angani inashuka sana duniani na sijui waga wanakuja kufanya nini ila mara nyingi wanajishugulisha na wale binadamu mnaowaita walokole,na ili uzungumze nao inategemea umekutana nao katika hali gani kwenye ulimwengu usio wazi kwa macho ya kawaida,kiasili sio waongeaji sana ila sura zao zinaakisi mwanga kwa namna ya tofauti na unaweza kujiuliza wanavaa mavazi gani, kwa mavazi wanavaa hizi nguo mnaita kanzu ila ni bwanga afu ndefu mpaka miguuni na ni nyeupe.

Jamii ile nyingine ya watu wasio na asili na binadamu ila wamefanana na binadamu kimuonekano lakini wana vimo vikubwa ni ile inayokaa chini ya bahari,maziwa(Lakes) na mito.Hii jamii wao ni wazungumzaji sana afu miili yao haiakisi mwanga na wanakuja sana duniani na unaweza kuwaona bila ridhaa yao kwa kufuata utaratibu wanaokupa wafuasi wao au wanajimu wa nyota mbao ni binadamu wa kawaida,na mavazi yao ni kanzu pia ila za rangi mbalimbali zaidi ya nyeupe.Na watu wanaojishugulisha nao sana ni wale watu ambao nyinyi binadamu mnawaita wanajimu na washirikina au wachawi ila inategemea ushirikina na uchawi wa wapi maana dunia ni kubwa kutoka bara moja mpaka lingine na ushirikina au uchawi unatofautiana.

Binadamu kuna vitu huwezi kuviona mpaka either uwe mshirika wa jamii mojawapo kati ya jamii hizo mbili nilizokutajia hapo juu.Lengo langu leo ni kuzungumzia mkuu wa jamii ile ya wale watu wa angani ambao wanapenda kushirikiana na walokole au watu wa kulia lia,maana huyo mkuu ana vitu vya tofauti kidogo ndio maana nikasema pale juu kua "Mungu wa walokole ana nguvu sana".

Katika utafiti wangu ndani ya ulimwengu usio,onekana inaonyesha kua walokole wanapendelewa sana na huyo mkuu wao,maana kuna vitu anawapa vya ziada wao hawavitumii sijui kwanini niligundua hilo huko mbele katika utafiti wangu.Nimemuita Mkuu au Mungu wa walokole sababu kila walokole wanapoanza kulialia""Kusali""wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wengine wana mabawa na wengine hawana wakitokea kwa mkuu wa walokole ama nilivyokuja kujua baadae huko huko angani wanawajia na wanawazunguka hawaondoki na lile eneo husika linakua na mwanga unaweza kupofusha macho (Ni kama mwanga wa jua au radi au shoti za umeme zile cheche) ila walokole waga hawawaoni nadhani waga wanalia(Kusali) kwa imani zaidi namaanisha meditation.

Nilisema hapo juu kua mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana nguvu sana maana wale walokole baada ya kulia kwa mkuu wao huwezi kuwasogelea katika hali ya nje ya ubinadamu au katika hali ya ushirika na jamii nyingine za kiroho zaidi ya mkuu wao na wale watu wa kuakisi mwanga.Kila mlokole anakua na yule mtu wa kuakisi mwanga na yule mtu haongei ila macho yake ni ishara tosha kua usimsogelee mlokole aliyenae.Cha ajabu wengi ya walokole hao katika hali ya ubinadamu wa kawaida hawana habari yoyote ile unawakuta sokoni au kwenye daladala au barabarani au ofisini au kwenye nyumba zao za ibada.

Sasa ikabidi nifanye uchunguzi juu ya huyo mkuu (Mungu) wa walokole,yupoje na ni nani, wale watu wa jamii ya kuakisi mwanga wanaishi nae vipi maana wana ushirika nae.Sababu ukitoka nje ya mwili kupitia(meditation) huwezi kuwasogelea hawa watu wa jamii ya kuakisi mwanga au hao walokole.Nikajikuta napata hamu ya kuchunguza mambo ya ulimwengu usionekana na hasa jamii za wale watu warefu wa angani na walokole hasa wale wa kulialia sisi binadamu tunaita kusali ila wao walokole wanaita kunena kwa lugha,na ni lugha ambayo inawafanya wawasiliane na wale watu warefu wa kuakisi mwanga.

Udadisi wangu ulijikita katika mambo makuu matano(5)
Mosi: Kwanini walokole wana uhusiano na wale watu wa kuakisi mwanga wanaotokea kule juu kusikofikika hata ukitoka nje ya mwili na kusafiri nje ya mzunguko wa sayari za kawaida kwa maelekezo ya wanajimu wa nyota?

Pili: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao ana uhusiano wa moja kwa moja na wale watu wa kuakisi mwanga na sio ile jamii ya chini ya bahari?

Tatu: Kwanini katika jamii za nje ya mwanadamu au mtu, hasa ile jamii ya watu wa kuakisi mwanga ina nguvu sana kuliko jamii za wale watu wanaokaa chini ya bahari na wasioakisi mwanga wa jua na mwezi?

Nne: Mkuu wa walokole kwanini yeye na wale watu wa kuakisi mwanga,hawana ukaribu na Mkuu wa wale watu wa jamii inayokaa baharini na chini ya maziwa na mito(Maana nayo ina mkuu wake) na hataki wafuasi wake wa dini yake wawe na ukaribu na walokole kwa namna yoyote ile?

Tano: Kwanini mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao pamoja na nguvu zoote ila hawapi utajiri wa kibinadamu hao walokole ila ukitoka nje ya mwili hawa walokole wana nguvu sana mpaka uñashindwa kuwaelezea labda uone kwa macho.Tofauti na mkuu wa ile jamii nyingine ambayo karibia robo ya wafuasi wake wana access ya kupata mali za dunia hii tunayoishi binadamu wote.

Basi nikajikuta naanza utafiti kufuatilia nguvu za mkuu wa walokole namaanisha Mungu wao.Ni nani na yupoje na anaishi wapi..Utafiti wangu ukanipelekea kuja na kichwa cha habari hapo juu kua Mungu wa walokole ana nguvu sana maana nilishuhudia mengi kumuhusu huyu Mungu wa hawa watu wa kulialia mnawaitaga walokole.

Safari yangu ya utafiti ilinikutanisha na wazee wa kibantu,wanajimu,viongozi wa dini za wanadamu zinazoonekana na zisizoonekana na watu wa jamii zile za nje ya ulimwengu wa mwanadamu.

ITAENDELEA
Hivi mlokole ni mtu gani?
 
Uliposema hawawezi kumsogelea ni kweli kwakuwa yeye ni moto na huwa unawaunguza...

Pia hao wakuu wa giza wanamjua YESU/MUNGU kuwa anauwezo mkubwa kuliko wao...
Wanajimu wanajua uwezo wa miungu wote nje ya ubinadamu lakini mungu wa walokole""Haelezeki"ni roho yenye nguvu na kumsogelea lazima uwe katika njia yake kiroho kama wafuasi wake walokole.Wao walokole wanaita""Utakatifu""
 
Hivi mlokole ni mtu gani?
Kivipi katika ubinadamu wa nje au wa ndani???? Maana walokole wengine kwa ubinadamu wa nje ni masikini wa kutupwa au wanaishi kawaida ila kwa ubinadamu wa ndani wana tunu za moto kama mataji ya kunga'aa hv vichwani mwao na hawasogeleki ukiwa na nia mbaya.
 
Back
Top Bottom