Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Ulimwengu wa Roho kule kuna vita na majeshi ya Ulinzi na majeshi mabaya...

Ukiwa na YESU unaimani na nguvu za Rohoni basi unashinda hayo majeshi...

Ila kwa wale wasio na YESU na Imani wanashindwa...
Afu ukisema vita ujue sio hivi vita vya mabomu...Wale kule hawapatani kabisa hasa jamii za wanaotokea angani na wale wanaotokea baharini.Na wafuasi wao wa kibinadamu hawapatani kabisa.Lakini yule mungu wa walokole ni kama duara za moto zinawazunguka walokole na pia wale watu warefu wanalinda watoto wadogo wa miaka mpaka 16.Na wana uwezo wa kuzungumza na kuvichekesha vitoto vichanga.Hujawahi kuona watoto wadogo wanacheka peke yao au wanatazama sana upande mmoja??????Bas wanakua wamewaona hao watu warefu.
 
Hebu endelea mkuu!!

Nilikua mlokolet mzuri sana!nikaacha baadae!!
Rudi kua mlokole mkuu sababu hata ukifa wale watu warefu wanakuchukua,hawaachagi watu wao popote na watoto pia wakifa tu wanawachukua kwa haraka""Kama kufumba na kufumbua"""wanawapeleka nje ya pluto na mnyongeo wa sayari za ulimwengu wa jua.Mkuu wa walokole ni kama moto wa viduara duara amemzunguka kila mlokole duniani.
 
Kwa nje ni kama wanaropoka ila kwa ndani,ni kama wanazungumza na kujibizana kwa hoja na wale watu warefu..Mlokole anatoa hoja na yule mtu mrefu anajibu kwa hoja pia,ila katika hali ya urafiki na inavutia kuwatazama
Isaya 43:25-26

“Mimi, naam, mimi ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe; wala sitazikumbuka dhambi zako. Unikumbushe; na TUHOJIANE; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.”
 
Nataka kukua hao watu huwa wanawatokea walokole Tu,

Je umeshachunguza kwenye haya makanisa yetu kama Roma na KKKT je hao watu wa kuakisi Mwanga wanatokea?

Je Kwa misikitini hawa watu wanatokea?

Na kama hawatokei Je Kwa uchunguzi wako haya madhehebu mengine wakiwa ibadani nini huwa kinatokea?

Je hawa wapani wasioamini kitu chochote Je hawana ulinzi wowote ule katika ulimwengu wa nje ya mwili?

Nijibu Kwanza haya nikitulia bado nina maswali mengi,

Na ninaomba uendele kuna mengi ya kujifunza
Nguvu za Rohoni sio kuwa kanisani peke yake, yaani unatakiwa uwe na juhudi za kutaka kumtafuta MUNGU kwa bidii...

Ndio maana amesema nitafuteni kwa bidii nanyi mtaniona...

Uwe mtu wa Imani na YESU, kusali sana, Toba ya kweli, hapo ndio unaweza kuona hayo mambo ya Rohoni...


Kuna wanaosali makanisa ya walokole na hawaoni chochote...

Waislamu hawawezi kuona maana wanaimani tofauti...
 
Nataka kukua hao watu huwa wanawatokea walokole Tu,

Je umeshachunguza kwenye haya makanisa yetu kama Roma na KKKT je hao watu wa kuakisi Mwanga wanatokea?

Je Kwa misikitini hawa watu wanatokea?

Na kama hawatokei Je Kwa uchunguzi wako haya madhehebu mengine wakiwa ibadani nini huwa kinatokea?

Je hawa wapani wasioamini kitu chochote Je hawana ulinzi wowote ule katika ulimwengu wa nje ya mwili?

Nijibu Kwanza haya nikitulia bado nina maswali mengi,

Na ninaomba uendele kuna mengi ya kujifunza
Kusema kweli kwa utafiti wangu nje ya mwili kuhusu hawa watu warefu nilikua nawaona wanaenda sana kwa hawa walokole wanaosalia majumbani vikundi vikundi na wengine wanakwenda kwa walokole wanaotembea barabarani,wanauza dukani,waliopo ofisini,mashambani.Walokole wana alama miilini mwao wenyewe wanaita matunda ya roho.Kuhusu makanisa wale watu warefu hawabagui popote alipo mlokole akiwaita kwa kulia wanaenda kumzunguka.
Msikitini sikuenda sababu mkufunzi wangu aliniambia nikitaka kuwadadisi wale watu warefu wapoje basi niwadadisi walokole wanaolialia,nyinyi mnaita kunena kwa lugha.Kwahiyo sikwenda misikitini au mahekalu ya wahindi au masinagogi ya wayahudi sababu nisingewakuta walengwa wangu kwenye utafiti ambao ni walokole.Lakini sehemu zinazoongoza kwa walokole ni kwenye hayo makanisa mnayaita ya kilokole na kilutheri...afu makanisa mengine yanafuatia kwa kua na mlokole mmoja mmoja
NB:Kuna makanisa mengi tu kwa nje yanaonekana ya kilokole ila wale watu warefu walikua hawaingii maana hakuna walokole ndani ila ni makanisa ya kilokole kwa muonekano wa nje.
 
Isaya 43:25-26

“Mimi, naam, mimi ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe; wala sitazikumbuka dhambi zako. Unikumbushe; na TUHOJIANE; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.”
Mkuu wale watu warefu wanasikiliza hoja na wanajibu kwa hoja ila kiurafiki..Wao ni warefu basi wanachuchumaa kumsikiliza mlokole anaelia na wanamshika begani ila hawamzuii kusali kwa kulia mpaka amalize yeye.Hata wakiwa mia wote wanamzunguka yule mlokole kwa upendo...Hawaondoki
 
Huyo mungu wa walokole hayupo, asingekubali watu wake wauliwe 31 kule kusini mwa nigeria tena kanisani, halafu mungu huyo huyo katulia na tukio lingine la mauaji zaidi ya watu 50 na BADO kaendelea kutulia

Mungu mwenye nguvu zote alishindwa vipi kuzuia mauaji yale ya kikatili na watoto wasio na hatua?
Utajua ni stori tu
Kuna jamaa aliwahi kutoa Hilo dai

Ayubu 1: 9-11

Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?

Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.

Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”


Ayubu 2: 4

Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.


1 John 5:19 NIV

We know that we are children of God, and that the whole world is under the control of the evil one.

Yakobo 1:13 BHN

Kama mtu akijaribiwa, asiseme: “Ninajaribiwa na Mungu.” Maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu yeyote.

2 Petro 3:9 BHN

Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.

Yoshua 24:15 BHN

Kama hamtaki kumtumikia Mwenyezi-Mungu, basi chagueni leo hii ni nani mtakayemtumikia:..........Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Mwenyezi-Mungu.”
 
Wakati nipo mdogo walikua wanakuja home anawaona dadangu akiwa anasali na watu wazima ambao walikua walokole afu ananiadithia yeye na wale walokole wanawaona afu mimi siwaoni kwa macho ya kawaida kipindi hicho nikadhani wananidanganya..Sasa toka hapo nikaanza udadisi wa kuwaona,niwajue ni akina nani na wanaishi wapi na mengine mengi juu ya jamii ya hao watu wa kuakisi mwanga ambao nyie mnawaita malaika.Nitasimulia taratibu huko mbele.Na waga nawaonea wivu sana walokole na upendeleo wao kwenye ulimwengu wa nje ya mwili.
So it was a 'fairy tale' and you believed it?
 
Bufa unataka nikuunganishe na mtu aje chumbani kwako usiku saa sita kamili umuulize maswali kuhusu uchawi??? Lakini kuna masharti na viapo utavifanya.Yeye atatokea afrika ya kati ila hapo america itamchukua nusu dakika.Sema sasa ukíshakula viapo utaacha kutuadithia ndio tatizo la haya mambo.

Fanya hivyo right now. Nishaomba mara nyingi sana nirogwe ila hadi leo nadunda tu
 
Back
Top Bottom