Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Sema tu Mungu atulinde sana! Mimi huwa najiuliza kuhusu manabii unakuta wengine wamepiga tattoo baadhi ya maeneo ya mwili, na wengine jamii ya kina suguye e.t.c huwa najiuliza nguvu za kutoa unabii wanazitoa wapi...mbona kuna vijana wapo wanamuomba sana Mungu hawajapata hiyo karama ila hawa wa tattoo nabiia kavaa jeans imechanika magotini hizi za kisasa...i dont know.

Si hukumu, Mwenyez Mungu anisamehe na atupe uwezo wa kupambanua hizo roho
 
Kuna scenario moja sitakaa niisahau ilinitokea mwaka jana na kitu hivi.ila niseme tu kuwa tuwe makini sana huko kwenye makanisa ya hawa watu wanaojiita sijui nabii, mitume wenye kutabiri wanaoibuka kama uyoga sikuhizi na target zao jiji la dsm .aseeh kuna jamaa mmoja tulikua tunenda kusali mimi na wife tusipokuwepo watu hawaendi hadi akawa anamwambia wife nyie mnanyota kali sana sasa alikua anatufatilia sana kumbe jamaa ni mchawi anaetumia biblia tulikuja gundua ana nyoka na pete kama zile za waganga..

Tangu tumstukie na majirani jamaa hana hata mtu mmoja anayehudhuria tena na watu wanamtuhumu mchawi,mchonganishi, kaja kuharibu kabisa familia za watu.alitufanyia mambo ya kijinga sana na kishirikina mshenzi yule mbaya zaidi alikua anamtaka wife...mpaka leo anatufatilia na tulishatoka lile eneo hawajui tupo wapi.

Tuwe makini sana sana..sitaki tena habari za manabii Mungu ni wetu sote nikipiga magoti hata chumbani na kumwomba atanisikia ni bora nirudi kwenye u lutheran wangu
 
Yupo deep sana huyu bro sema alitukatili sana kwenye uzi wake mmoja wa "Biblia kwa jicho lingine". Ule uzi niliupenda sana na nikauprint kabisa. Ninao kwenye PC yangu. Huyu jamaa nilihisi anaweza kuwa ni yule "Askofu Sylvester Gwamanywa" wa "WAPO FM"
link plz, nime search hyo title haionekan.
 
  • Thanks
Reactions: PYD
Nilitaka kumuona ila mpaka leo siwezi,,lakini walokole waliniambia yupo kila mahali na anasikia...Niliwaamini sababu wale watu warefu wa kuakisi mwanga waga wanakuja fasta tu walokole wakianza kulia na kusali na hawataki mchezo ukiwasogelea walokole wao.

Mungu wa walokole ana nguvu Ila ana matatizo ya kusikia,waumini wake mpaka wapige mayowe ndiyo asikie
Kristo Yesu atusamehe mimi na wewe, atujaliekuisikia iliyo kweli
 
Kuna scenario moja sitakaa niisahau ilinitokea mwaka na kitu hivi.ila niseme tu kuwa tuwe makini sana huko kwenye makanisa ya hawa watu wanaojiita sijui nabii wenye kutabiri..aseeh kuna jamaa mmoja tulikua tunenda kusali mimi na wife tusipokuwepo watu hawaendi hadi akawa anamwambia wife nyie mnanyota kali sana sasa alikua anatufatilia sana kumbe jamaa ni mchawi anaetumia biblia tulikuja gundua ana nyoka na pete kama zile za waganga..

Tangu tumstukie na majirani jamaa hana hata mtu mmoja tena na watu wamtuhumu mchawi..alitufanyia mambo ya kijinga sana na kishirikina mshenzi yule mbaya zaidi alikua anamtaka wife...
Tuwe makini sana sana..sitaki tena habari za manabii Mungu ni wetu sote nikipiga magoti hata chumbani na kumwomba atanisikia ni bora nirudi kwenye u lutheran wangu
Dah bora ulishtuka mapema, yaani angempata wife basi maisha yenu yote yangesambaratika... Maana wao wametuma hasa kuharibu ndoa za wa Kristo.. Ndio maana kesi za manabii kuzini na wake za watu zinatawala Sana... They call sexual sacrifice... Hata watoto watu mabikra usithubutu kupeleka kuombea kwa Hawa jamaa.. Maana hao pia ni target. MI nashauri kabla mtu huja enda kanisani lolote hasa Yale ya kualikwa Muombe Mungu akupe kibali... Usiende tu eti aliekualika ni jirani au best friend... Ichunge sana roho yako kuliko chochote🙏
 
KWA MUJIBU WA PROPHET DAVID RICHARD,YEYE ANATOA USHUHUDA KWAMBA ALIONESHWA NA MUNGU KUMUHUSU HUYU AZAZEL.ANASEMA AZAZEL NI MALAIKA ALIYEASI NA ANA NGUVU KULIKO HATA SHETANI HIVYO MUNGU AMEMFUNGA MINYORORO NA MALAIKA WENZAKE WATATU MAANA ANGEWAACHIA TU WANGEIHARIBU DUNIA.HAWA WAMEFUNGWA ENEO LA MBALI SANA SANA LIITWALO DUDAEL.Prophet alipelekwa hadi hili eneo la dudael
We unamwamini huyo nabii wako wa mchongo find another person bro
 
Hata wewe ukitaka unaweza kuwaona...

Muamini YESU kwa Imani, omba Toba ya kweli, omba YESU akujaze nguvu za Rohoni hapa Sasa ndio utaanza kuona
Huyo yesu mnaemtukuza ni fara tu
 
Yule nae Nabii au ndo wale wale... 😁 😁 Maana huduma yake ni ya Malaika, kutwa akisifia Malaika.. Malaika.. Wakati Hawa ni watendakazi wa bwana kwa ajili yetu.. Hatupaswi kuwapa Utukufu zaidi ya Yesu... Ila yeye sasa.... Binafsi simu amini hata kidogo....


Sio kweli,
Huruma yake, anakumbusha Wana wa Mungu aliye juu kuwa wawo ni majemedari, wasipigane vita peke yao..
“Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? ”
— Mathayo 26:53 (Biblia Takatifu

Sijawahi kumsikia akisifia malaika Ila malaika ninwatumishi wetu, wanatakiwa watuhudumie..tiwashughulishe.

Baba wa mbinguni akitaka kufanya Jambo lolote anatuma malaika..
Kwa neno la Bwana malaika poa anaweza kubadili hatma yako mf Yakobo.

... Mariam alitembelewa na malaika Gabriel kuleta habari..
... Hata ujio wa Kristo watatumwa watumishi hawa malaika kutukusanya..
(“Naye atawatumamalaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu. ”)
— Mathayo 24:31 (Biblia Takatifu)
 
Mwanzo ulipokua unasema walokole walokole sikuelewa, niakajua unaongelea makanisa ya kilokole.
Lakini kadri uzi unavyoenda nikaelewa kua watu wanatangatanga na makanisa bure tu, MUNGU yupo popote..

Wakati niko primary nilikua na imani kwelikweli, nikikumbuka enzi zile nilikua tofauto kiimani na watoto wenzangu. Nilikuwa nikimuomba MUNGU kitu kinakua.
Nakumbuka kuna siku nilipoteza kitabu cha hesabu na tulikua tunakaribia kufunga shule, na ticha alisema kama umepoteza kitabu itabidi ulipe na mimi kumwambia mshua naogopa. Basi kuna siku nilisali sana, nililia na MUNGU mno, ajabu kesho yake nilikuta kitabu kwenye begi langu wakati kilipotea kitambo sana.

Kiukweli kipindi kile nilikua na imani sana, nikisali inakua, tena vilevile au zaidi ya kile kwa njia tofauti.
Kwasasa nshakua kijana wa hovyo ila maisha ya wokovu yana raha sana aisee. Ukianza wokovu tangu utoto wako bila kupuliziwa moshi akilini alooo utapata raha maisha yako yote, utakua na stress ila MUNGU atakushangaza.
Mitihani mingi shule nimepass kimiujiza tu baada ya kusali sana.

One day Yes nitarudi kwa miguu yote miwili kwa Muumba.
 
Utafiti mzuri sana ila Kuna maeno unayachangany na yapo tofauti sana 1 Mungu au MUNGU ( bible inasema jina lake linatakiwa liamze na elufi KUBWA ayo zote ziwe kubwa)-na mungu au miungu mingine
Kwa hoja hiyo tu unaweza Kuta eti na wewe umeanzisha kanisa
Hahahahaha,
Ulichokielewa ndani ya nafsi Yako mpaka ukajua ndicho anachomaanisha ndiyo sisi wote tumekijua hicho,. Kumbuka MUNGU amekuwepo Kabla ya maandishi, Nini unawaza (inatoa maana zaidi)kuliko unatamkaje, mfano maji kwa mtoto mdogo anaita aji au mma, Sasa wewe mpe aji au mma, badala ya maji ndo utajua hujui
 
Sio kweli,
Huruma yake, anakumbusha Wana wa Mungu aliye juu kuwa wawo ni majemedari, wasipigane vita peke yao..
“Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? ”
— Mathayo 26:53 (Biblia Takatifu

Sijawahi kumsikia akisifia malaika Ila malaika ninwatumishi wetu, wanatakiwa watuhudumie..tiwashughulishe.

Baba wa mbinguni akitaka kufanya Jambo lolote anatuma malaika..
Kwa neno la Bwana malaika poa anaweza kubadili hatma yako mf Yakobo.

... Mariam alitembelewa na malaika Gabriel kuleta habari..
... Hata ujio wa Kristo watatumwa watumishi hawa malaika kutukusanya..
(“Naye atawatumamalaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu. ”)
— Mathayo 24:31 (Biblia Takatifu)
Mi sikatai uwepo wa Malaika, kukataa kwangu ni vile anawaongelea Sana kuliko kufundisha neno watu wa mjue zaidi Mungu, maana Neno la Mungu ndio uthibitisho wa mpango yote mzuri Mungu aliyoweka kwa ajili yetu.. Story za kupeleka na Malaika sijui kuzimu, Mara kaenda mbinguni Kuna magari latest version nk. Yote mwongo mbinguni hajaenda kaenda Mbingu ya Shetani.. Maana neno la Mungu halisemi asemayo yeye... Mwambie adanganye vijana wenzie wasio taka kujua neno wao binafsi... Wanataka walishwe kila kitu, manabii nk. sasa ndio wanalishwa Matango pori😁😁
 
Back
Top Bottom