Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Huu nao ni ujinga.

Huwezi kuona mstari unaounganisha umasikini na kukosa elimu, ambao unakwenda moja kwa moja pia kutoka kukosa elimu mpaka imani ya Mungu.

Imani ya Mungu => Kukosa elimu => Umasikini.

Huoni uhusiano huu?
Uhusiano siuoni kwa sababu nikiangalia waarabu ambao hawana umasikini ila wanatuzidi kwenye imani ya Mungu hadi wanakuja kutupa misaada kwa msukumo wa imani ya Mungu.
 
Uhusiano siuoni kwa sababu nikiangalia waarabu ambao hawana umasikini ila wanatuzidi kwenye imani ya Mungu hadi wanakuja kutupa misaada kwa msukumo wa imani ya Mungu.
Waarabu ni special case ya utajiri wa mafuta, utajiri ambao hautumii akili, ambao hata wao wanapigwa sana kwa sababu hawakujua kuchimba mpaka hivi karibuni ndiyo wanajenga capacity.

Na hata hao waarabu wanavyozidi kuongeza elimu, imani ya Mungu inashuka, nimeweka articles tatu hapa.

Huku Africa vipi? Huoni uhusiano wa umasikini, kukosa elimu na imani ya Mungu?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Unaweza kuondoa contradictions zilizopo katika dhana ya kuwepo Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote aliyeumba ulimwengu huu ambao mabaya yanawezekana?
 
Umekuta kuna mgawo wa vitu mbali mbali, tena vinatolewa bure! Halafu unapewa uhuru wa kuchagua, ungechagua kipi?

Umeruhusiwa kuchagua kimojawapo kati ya hivi:

1. Chumvi kilo mia mbili

2. Pamba kilo mia

3. Sukari kilo themanini

4. Dhahabu safi kilo hamsini

5. Baiskeli mpya

Wewe ungechagua kipi?

Mimi nitachukua kilo hamsini za dhahabu. Kwa kilo hizo hamsini, naweza kuvipata na hivyo vyote vilivyoorodheshwa, na vingine vingi, ikiwa nitahitaji.

Ikiwa mtu amejiridhisha kuwa Mungu anayemwamini ni kila kitu, na ni zaidi ya Miungu mingine yote,ya nini kuhangaika tena na tumiungu tudogo?

Aliye na MUNGU MKUBWA hahitaji tumiungu. Mwenyezi Mungu ni kila kitu!
Unajuaje Mungu wa Biblia ndo Mungu mkubwa na sio mdogo
 
Mzungu katengeneza chanjo ya corona huku mnauombea uondoke mnadanganyana Mungu kaikoa nchi kwa corona kisa Ina dini kumbe watu kibao wanakufa na kuzikwa afu unasema we na mzungu mpo sawa kimaarifa, kamtawale basi
Ndio maana nikasema usiwe na hofu wala sitaki kuondoa uspesho na utukufu unaouona kwa wazungu, wala sitaki kuwashusha wazungu wako kuwa ni binaadamu sawa na waafrika.
 
Waarabu ni special case ya utajiri wa mafuta, utajiri ambao hautumii akili, ambao hata wao wanapigwa sana kwa sababu hawakujua kuchimba mpaka hivi karibuni ndiyo wanajenga capacity.

Na hata hao waarabu wanavyozidi kuongeza elimu, imani ya Mungu inashuka, nimeweka articles tatu hapa.

Huku Africa vipi? Huoni uhusiano wa umasikini, kukosa elimu na imani ya Mungu?

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo?

Unaweza kuondoa contradictions zilizopo katika dhana ya kuwepo Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote aliyeumba ulimwengu huu ambao mabaya yanawezekana?
Mimi nazungumzia utajiri kutokuwa na umasikini, hayo ya wamepataje utajiri ni issue nyengine point ni kwamba hawana changamoto za umasikini kwa sababu ni matajiri.

Kuna watu jinsi walivyo na umasikini hadi wanakosa muda wa kujihusisha na mambo ya Mungu, wengine wakifanikiwa kwenye maisha wanaacha habari za Mungu.

Sasa baada ya kujua kwamba elimu yenyewe unayokusudia ni ile kama waliyonayo Northern Europe sasa nipatie tena hizo links ili nisome hao waarabu waliyopata hiyo elimu jinsi wanavyoacha kuamini Mungu.
 
1. Pagan means mtu ambaye ana dini tofauti na zinazojulikana, sio mtu asiye na dini
2. True Scotsman fallacy, unasema kitu ambacho mtu hawezi fanya afu mtu akianza kufanya unasema hakuwa mtu fulani. Hata kanisa lenyewe halijui mkristo wa ukweli ndo maana Kuna madhehebu elfu kumi kila mtu anakuja na ukristo wake so mkristo wa ukweli hajulikani. Ni sawa na kusema wachaga wote wanapenda hela afu akitokea mchaga asiyependa hela unasema ye sio mchaga ili kusupport theory yako. Atheists wengi walikuwa wanadini wakaamua kuifatilia kusoma Biblia zaidi kuuliza maswali kuhusu historia na logic kuhusu dini Yao wakagundua ni uwongo, ndo maana hoja za atheists Zina make sense Ila watu wanaogopa kukufuru coz wametishiwa moto ambao haupo, kusingekuwa na moto na mbingu hamna mtu angeamini story za Mungu wa Biblia
Ni kweli, Mpagani si mtu asiye na dini, hata kuiabudu mizimu ni dini.

Ndiko nilikoanzia, kwenye dini ya asili. Kabla ya kuwa Mkristo, nilikuwa nikishiriki hata ibada za kipagani. Nakumbuka, nilishawahi kuhudhuria tukio ambalo kabla ya jambo lolote kufanyika, kulifanyika maombi kwanza. Maombi yalielekezwa kwa mti. Kwamba, mti ndiyo uliokuwa kama mungu.

Lakini baadaye nilikuja kugundua kuwa kuna Mungu MKUBWA kuliko mizimu ya mababu zetu. Nilipogundua hilo, niliamua kuachana na kamungu kadogoe na kumfuata MUNGU MKUU!!!

Kuwepo kwa madhehebu mengi si tatizo, muhimu tu wawe wanamwamini Kristo. Hata kukiwepo na madhehebu bilioni kumi, kama wanamwamini Kristo, wote watakuwa ni Wakristo.

Wakristo wa Kweli wanajulikana. Hata humu jukwaani, bila shaka, kuna nyuzi ambazo kwa kuzisoma tu, unajua huyo ni Mkristo au la.

Kwani wewe unashindwa kumfahamu Mkristo wa Kweli? Mbona ni rahisi tu! Hata Shetani hasumbuki kumtofautisha Mkristo wa Kweli na anayeuigiza Ukristo. Mkristo wa Kweli anafahamika, si makanisani tu, hata katika maeneo mengine. Imeandikwa, "Mtawatambua kwa matendo yao"

Hao waliogeka atheist mimi siwafahamu! Ukweli ni kuwa mtu akishaouonja utamu wa Kristo, hatatamani tena kitu kingine.
Kama kuna waliokuwa wakienda , labda makanisani lakini baadaye wakaamua kugeukia uatheist, ni kwa sababu hawajawahi kukutana na Mungu Halisi mioyoni mwao. Waliingia kwenye dini kwa kufuata mkumbo. Hawakumwamini Mungu!
 
Shetani Ashawahi kusema Mungu hayupo?, freemason Ashawahi kusema Mungu hayupo ? Shetani mwenyewe anataka watu wamjue Mungu ili wampinge. Shetani na Mungu ni story tu Kama movie zilivyokuwa na sterling na jambazi acha uwoga wa maisha Kama Mungu anapenda watu kwa Nini awachome, we unaweza mchoma mtoto wako moto, mmetishwa na makanisa ili muendelee kufata sheria zao na mtoe sadaka mwatajirishe
Kuna kitu nataka nikuambie! Una uhakika kuwa shetani hajawahi kusema kuwa Mungu hayupo?
 
Nielezee mtu kuzaliwa na cancer anakosa gani mpaka kaumwa🤣au mama ake hakuelewa biblia
Unataka nikueleze? Utanielewa? Hautaanza kuleta ubishi? Lengo lako ni kuelewa au kutafuta kupinga?

Nitakuambia! Mungu alipomwumba mwanadamu, alimwumba katika hali ya ukamilifu. Asingeweza kuugua wala kufa. Lakini kupitia anguko la Adamu, dhambi iliingia duniani. Kitu kinachoitwa Sheria ya dhambi na mauti ikaingia duniani. Warumi 8:1-2.

Hiyo ndiyo sababu mojawapo ya kuwepo kwa magonjwa.

Lakini pamoja na hayo, Mungu hajawaacha watu Wake bila ya msaada. Madhalani, kwa upande wa magonjwa, mtu anaweza kupata msaada, ama kwa njia ya kutibiwa na madaktari, au kwa kuamua kumwamini Mungu akapokea uponyaji.

Madaktari wana usemi wao usemao, "Sisi tunatibu, lakini Mungu Ndiye anayeponya". Hata madaktari wanajua kuwa Mungu ni Mponyaji.

Magonjwa hayatoki kwa Mungu! Mungu ni Mponyaji!!!
 
Mimi nazungumzia utajiri kutokuwa na umasikini, hayo ya wamepataje utajiri ni issue nyengine point ni kwamba hawana changamoto za umasikini kwa sababu ni matajiri.

Kuna watu jinsi walivyo na umasikini hadi wanakosa muda wa kujihusisha na mambo ya Mungu, wengine wakifanikiwa kwenye maisha wanaacha habari za Mungu.

Baada ya kujua elimu yenyewe unayokusudia ni ile ya kama waliyonayo Northern Europe sasa nipatie tena hizo links ili nisome hao waarabu waliyopata hiyo elimu wanavyoacha kuamini Mungu.

Utajiri mtu anaweza kupata hata kwa bahati nasibu tu.

Unapinga hilo?

Nitajie jamii ya watu walio na umasikini mpaka wamemsahau Mungu kwa umasikini wao, mimi siongelei watu mmoja mmoja, naongelea jamii za watu.
 
Mzungu katengeneza chanjo ya corona huku mnauombea uondoke mnadanganyana Mungu kaikoa nchi kwa corona kisa Ina dini kumbe watu kibao wanakufa na kuzikwa afu unasema we na mzungu mpo sawa kimaarifa, kamtawale basi
Kwani Mzungu hana dini? Unajua Tanzania hain dini lakini Marekani ina dini? Unafahamu Marekani ni Taifa la Kidini?

Pamoja na kwamba wamegundua dawa za Corona, na vitu vingine vingi, bado pia wanaamini katika Mungu.

Unafahamu kuwa Marekani inayo mpaka siku ya Kitaifa ya Maombi?

Wamarekani wenyewe wanaamini kuwa wao kuwa Super Power duniani ni kwa sababu wanamwamini Mungu. Japo siku hizi idaidi ya wanaoamini katika Mungu nchini Marekani inapungua, bado ni Taifa lenye watu wengi wanaomwamini Mungu.

Umeshawahi kuiona noti ya dola ya Marekani? Imeandikwaje?
"In God We Trust" Tusaidie tafsiri ya hiyo sentensi kwa Kiswahili, tafadhali.

Wana na kauli yao maarufu isemayo, GOD WE TRUST, BUT MONEY WE AUDIT! Ukiweza, utusaidie na hii pia tafsiri yake kwa Kiswahili.

Ujue tu kuwa Mungu hajawazuia watu kutumia akili. Ndiyo maana kawapa watu akili.

Kumwamini Mungu hakumwondolei mtu wajibu wa kuitumia akili yake panapohitajika kutumia. Mungu anataka watu Wake watumie kwa usahihi akili alizowapa ili wafanye mambo makubwa mazuri.
 
Wakristo Wana kisingizio ukiamini tu Mungu yupo na story za Yesu na ukatubu unaingia peponi, so uoga wa kwenda Motoni kwa kutoamini story za biblia
Kuamini kuwa Mungu Yupo ni jambo moja. Na watu wengi wanaliamini hilo. Hata Shetani na mapepo yote yanaamini hivyo pia, tena, wanaamini mpaka wanatetemeka.

Lakini kuamua kumwamini Mungu ni jambo jingine. Siyo kila anayeamini Mungu Yupo anamwamini Mungu. Lakini hakuna anayemwamini Mungu asiyeamini kuwa Mungu Yupo.

Suala la kumwamini Mungu si kwa ajili ya maisha ya baadaye tu, baada ya kufa , bali ni kuanzia sasa. Amwaminiye Mungu hunufaika katika maisha ya sasa na ya baadaye.
 
Kwa tafsiri ya kawaida Mungu ni uwezo mkuu usiyowezwa.
Ikiwa akili yako na imani yako haiwezi kuelewa au kujua uwepo wa Mungu ni tatizo lako binafsi. Kuleta mjadala wa Mungu pasina elimu ni sawa na kukanusha, hivyo basi ni bora ufanye juhudi ya makusudi na nia thabiti kuwaendea wale wabobezi katika masuala ya kiroho huwenda ukapata majibu ya maswali yako. Kama upo serious. Ikiwa unataka kufurahisha barza kwa kweli mada hiyo ibadilishe tafuta mada nyingine.
Na kuna watu wengi walio tayari kuwasaidia watu wenye uhitaji huo.wapo wengi, karibia kila mahali.
 
Nimefanya tafiti nimeona Mungu anayeaminiwa hawezi kuwepo coz Hana logical consistency kwenye sifa zake
Umetumia methodology gani kwenye hizo tafiti? Wewe unaweza kumtafiti Mungu?

Vipi na mtoto aliyeko tumboni naye akisema hakuna mtu kama yeye kwa vile tu hajamwona, itahesabiwa kuwa ni Kweli?

Mungu hana njaa ya wewe kujua kuwa Yupo. Usipomtambua ni hasara yako.
 
Back
Top Bottom