Mungu Yuko wapi?

Mungu Yuko wapi?

Nani kakupa wewe cheo cha kuamua point ni ipi?

Hujathibitisha Mungu yupo.

Hujaondoa contradictions zilizopo katika dhana ya kuwapo Mungu.

Kwa sababu Mungu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo na ondoa contradictions hizo.
Mimi ndio niliyoleta hiyo hoja ya kuhusu hao waarabu na utajiri na point yangu ni huko kuwa matajiri na wanaamini Mungu, sasa wewe unaleta habari za sijui utajiri wao ni kwa sababu ya mafuta mara sijui ni utajiri wa bahati. Point haikuwa jinsi walivyoupata utajiri bali ni huo utajiri wenyewe.

Kama ushahitimisha kwa kusema kwa uhakika kabisa kuwa hakuna Mungu, sasa kuondoa contradictions ndio kutafanya Mungu awepo?
 
Ng'ombe sio Mungu wa wahindi, hii dhana ni potovu na ya uongo, Mungu wa wahindi ni kina Krishna huko.
Huwezi separate Mungu na dini, bac utakuwa unaamini Mungu ambae hajawahi kuhusika na ulimwengu ambao ameutengeneza. It means hujui anachotaka, hujui sheria zake, hujui sifa zake. Ila huwezi ukaja kutumia zile sifa na sheria za Biblia afu ukasema huamini dini unaamini Mungu unakuwa mnafki na muongo
Usihame hame nje ya hoja. Narudia, inaanza imani ya uwepo wa MUNGU kisha inafuata dini. Hakuna unafiki wala uongo hapo zaidi ya akili yako kuona kiini cha hoja "Imani ya uwepo wa MUNGU" dini na aina za dini zinafuata baada ya hiyo imani.

Unaweza futa dini kwa kuibadili na dini nyingine ila huwezi futa imani ya uwepo wa MUNGU kwa udhaifu wa dini. Imani ya uwepo wa MUNGU itafutwa kwa kujibu maswali yaliyosababisha uwepo wa hiyo imani.

Ulimwengu ni nini?

Chanzo chake ni nini?

Hatma yake ni nini?

Kifo ni nini?

Kama huna majibu yasiyo na shaka kuhusu hayo maswali watu hawawezi fata porojo zako wakaachana na imani ya uwepo wa MUNGU just sababu unadhani una maarifa kuliko mababu walioturithisha hiyo imani.

Suala la wahindi na ng'ombe ni mfano bila kujali uhalisia wake halisi, ni jambo ambalo ulipaswa kuliona kiwepesi tu, nia haikuwa kutoa elimu sahihi ya mungu wa wahindi.
 
Mi najiuliza maswali mengi. Mungu Ni Nini, anataka Nini na Yuko wapi.

Ukifuatilia historia ya binadamu tokea tukiwa wawindaji maporini miungu ilikuwepo. Wazee walikuwa wanaongoza vijana kwa kuwaambia kuwa Mungu anataka mfanye hivi, na hio miungu ilikuwepo pangoni ambapo wazee tu wanaingia, baadae vijana wakajitoa akili kwenda wakaona wazee ni waongo na hamna kitu mule. Wagiriki wakaja na miungu yao wakasema ipo ya milima ya Olympus, Leo hii watu wamepanda milima yote ugiriki hawajaona miungu hio.

Wakaja wayahudi, wakasema Mungu yupo mawinguni. Ukifuatilia hata Yesu alipaa mawinguni, Mungu alifungua madirisha ya mbinguni kuleta mafuriko, alichungulia kutoka mawinguni kwenye mnara wa babel, etc. Waislamu nao wakaja na mbingu Saba sijui. Anyways wazungu wametengeneza ndege na rocket zimeenda mawinguni, nje ya dunia, mpaka mwezini. Sasa hivi watu wa dini wanasema yupo nje ya ulimwengu.

So nikagundua trend, wanamficha, wanamweka mbali ili watu wasiweze kumfikia, why? Kwa sababu hayupo? Kwa sababu hajasema hizo sheria? Why wanamficha. Afu wanakuambia anataka uamini yupo ndo utapona usipoamini unaunguzwa. Ukiuliza nikimwona afu nikamwamini, anasema no, lazma usimwone ndo uamini. Na wanaweka kifo mwisho wa kumuani ili waweze kuendelea kutunga sheria kwa jina lake na kuweza kuendelea kutawala watu kwa sababu hamna mtu Ashawahi kurudi akasema baada ya kifo kipo hivi.

Mwanasayansi mi nauliza Mbinguni Kuna Nini. Hamna njaa hamna maumivu hamna ndoa hamna chochote zaidi ya kumuabudu Mungu. Watu kanisani na msikitini hawapendi kwenda unategemea watapenda milele ya Ibada. So wakaamua kuanzisha motoni kutishia watu kwamba wataunguzwa milele. Sasa, ukifa unaacha mwili wako hapa, wanasema una roho, roho ni Nini, hoo mawazo sijui pumzi, ukiuliza unajua kazi ya ubongo ni Nini mtu hajui, haya tufanye roho ni ka upepo kanaenda motoni ehe kanaunguaje, hakana nyama, hakana nervous system hakana ngozi, hakana pain receptors, hakana ubongo au spinal cord, maumivu unayasikiaje, na bado hatujauliza huu Moto upo wapi, walisemaga chini kisa mavolcano lakini now hawasemi Tena coz of elimu.

Tukienda kwenye sheria zenyewe sijui usivae nguo tofauti, usile shellfish, usichanganye mazao, usimwage nje, usiabudu sanamu lakini abudu kitu Cha kufikiriwa na myahudi, hivi kwa Nini mtu atengeneze nyota billion 60 na sayari trillion afu aje kujali binadamu wewe ambae ni Kama vumbi kwa huu ulimwengu unamwaga wapi. Na kwa Nini sheria hizi zinaonekana Kama sheria za kabila ya la zamani huko kwenye majangwa na haziendani na sheria za binadamu kuishi na watu vizuri. Na Wanavyosema tumuabudu siku ya Saba.

Siku zimekuja kutengenezewa baadae Sana na zimebadilika badilika Mara kwa Mara katika historia ya Mayans na Romans. Na wamechagua sun day coz ni siku ya pagans kuabudu jua. Ila yote haya tuyaache, why Mungu muweza yote anataka hela, mwisho wa siku wote mnabidi mgundue kuwa binadamu walitengeneza miungu ili kujibu maswali magumu yasiyojibika kipindi kile na ku
Mungu yuko Ulaya.
 
Usitake kuonekana mwelevu kufanya kufuru ili ufurahishe watu au kikundi fulani nakushauri usijitafutie laana kwa haya maandiko yako maana hasira ya Mungu ni kali sana tubu jiepusha na hizi kauli (acha kumfanyia kazi shetani kupotosha kondoo wa Mungu ) usipo sikia ipo siku na saa utakumbuka maandishi haya
Acha bangi mkuu.
 
Of course Biblia itasema Kuna watu hawataamini story zake, coz walioandika walijua story zao haziaminiki. Ni sawa nitengeneze thread afu niseme watu wataniponda, afu watu waniponde kweli nijiite mtabiri na mkweli. Nipe hoja sio hekaya
Ni wachache sana tunao kuelewa.
Wana mistari yao ya vitisho,utasikia ;
OLE
OLE
OLE
OLE.
 
Kwanini Mungu atengeneze ulimwengu mzima wenye nyota billion ili wewe Kima(primate), umuabudu, we ni Kama vumbi kwake, ye anafaidika Nini. Au ndo tunawaabudu na kuwatumika wachungaji na mnaambiwa ni Mungu. Mungu Kama ni WA yote na WA kila mahali hachagui mtu so mpaka mtu anasema katokewa na Mungu huyo ana lake anataka. Tofauti ya Musa na zumaridi ni mda tu.
Kwamba Musa na Zumaridi lao moja 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Unamuabudu kakuambia umuabudu au mwarabu/myahudi/mrumi kakuambia umuabudu ili achukue hela zako na aendeshe maisha yako na anatumia story za Mungu Kama kivuli na kukuambia usiulize maswali utaunguzwa na we unakubali ka mtoto muoga
Myunani,Mrumi,Myahudi na Mwarabu, hawa watu wana tutumia sana kutangaza vivutio vyao vya utalii huku tukilipia fedha ili tuvitangaze ndani ya majengo (kanisani na misikitini) wanaita sadaka na zaka. Ni unyonyaji wa viwango vya juu sana.
 
Usihame hame nje ya hoja. Narudia, inaanza imani ya uwepo wa MUNGU kisha inafuata dini. Hakuna unafiki wala uongo hapo zaidi ya akili yako kuona kiini cha hoja "Imani ya uwepo wa MUNGU" dini na aina za dini zinafuata baada ya hiyo imani.

Unaweza futa dini kwa kuibadili na dini nyingine ila huwezi futa imani ya uwepo wa MUNGU kwa udhaifu wa dini. Imani ya uwepo wa MUNGU itafutwa kwa kujibu maswali yaliyosababisha uwepo wa hiyo imani.

Ulimwengu ni nini?

Chanzo chake ni nini?

Hatma yake ni nini?

Kifo ni nini?

Kama huna majibu yasiyo na shaka kuhusu hayo maswali watu hawawezi fata porojo zako wakaachana na imani ya uwepo wa MUNGU just sababu unadhani una maarifa kuliko mababu walioturithisha hiyo imani.

Suala la wahindi na ng'ombe ni mfano bila kujali uhalisia wake halisi, ni jambo ambalo ulipaswa kuliona kiwepesi tu, nia haikuwa kutoa elimu sahihi ya mungu wa wahindi.
Aliyejibu hayo maswali ni nani na majibu aliyatoa wapi? Mnatishwa sana na mnatishika sana.
 
Mimi ndio niliyoleta hiyo hoja ya kuhusu hao waarabu na utajiri na point yangu ni huko kuwa matajiri na wanaamini Mungu, sasa wewe unaleta habari za sijui utajiri wao ni kwa sababu ya mafuta mara sijui ni utajiri wa bahati. Point haikuwa jinsi walivyoupata utajiri bali ni huo utajiri wenyewe.

Kama ushahitimisha kwa kusema kwa uhakika kabisa kuwa hakuna Mungu, sasa kuondoa contradictions ndio kutafanya Mungu awepo?
Sasa kama kuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kwa nini kaumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na matajiri wakubwa sana na masikini wa kutupwa, by mere chance of geography?

Huoni hiyo tu kuwa ni contradiction inayoonesha Mungu huyo hayupo?
 
Aliyejibu hayo maswali ni nani na majibu aliyatoa wapi? Mnatishwa sana na mnatishika sana.
Anatishwa nani na nini? Ni uchaguzi wa njia tu hakuna matisho. Aliyechagua kuamini uwepo wa MUNGU sababu hajui majibu ya hayo maswali anafanana na wewe unayejiamini kwa elimu unayosoma soma ya wazungu ambayo haijakupa majibu ya hayo maswali.

Tofauti yenu ni moja tu, wewe unajiamini kupita kiasi au ni muoga kupita kiasi.
 
Na
Kwanini Mungu atengeneze ulimwengu mzima wenye nyota billion ili wewe Kima(primate), umuabudu, we ni Kama vumbi kwake, ye anafaidika Nini. Au ndo tunawaabudu na kuwatumika wachungaji na mnaambiwa ni Mungu. Mungu Kama ni WA yote na WA kila mahali hachagui mtu so mpaka mtu anasema katokewa na Mungu huyo ana lake anataka. Tofauti ya Musa na zumaridi ni mda tu.
Astaghfirullah, Mussa ni Nabii wa Allah kua na heshima.

Chunga maneno yako,
 
Anatishwa nani na nini? Ni uchaguzi wa njia tu hakuna matisho. Aliyechagua kuamini uwepo wa MUNGU sababu hajui majibu ya hayo maswali anafanana na wewe unayejiamini kwa elimu unayosoma soma ya wazungu ambayo haijakupa majibu ya hayo maswali.

Tofauti yenu ni moja tu, wewe unajiamini kupita kiasi au ni muoga kupita kiasi.
Unamuamini mzungu ktk jina lingine eti Mungu lkn unaponda elimu aliyokupa ili ujikwamue.
Ama kweli nyani haoni kundule.
 
Unamuamini mzungu ktk jina lingine eti Mungu lkn unaponda elimu aliyokupa ili ujikwamue.
Ama kweli nyani haoni kundule.
Imani ya uwepo wa MUNGU haijaletwa na mzungu. Elimu ya hiyo imani ilikuwepo kabla mzungu hajafika Tanganyika. Dini ya biblia ndiyo iliyoletwa na mzungu.

Hakuna sehemu nimeponda elimu inayotolewa na mzungu. Mtu akisema elimu unayosoma soma ya wazungu maana yake ni kaiponda elimu ya wazungu? Kuna tatizo la kutafsiri hoja.
 
Anatishwa nani na nini? Ni uchaguzi wa njia tu hakuna matisho. Aliyechagua kuamini uwepo wa MUNGU sababu hajui majibu ya hayo maswali anafanana na wewe unayejiamini kwa elimu unayosoma soma ya wazungu ambayo haijakupa majibu ya hayo maswali.

Tofauti yenu ni moja tu, wewe unajiamini kupita kiasi au ni muoga kupita kiasi.
Unamuamini mzungu ktk jina lingine eti Mungu lkn unaponda elimu aliyokupa ili ujikwamue.
Ama kweli nyani haoni kundule.
 
Imani ya uwepo wa MUNGU haijaletwa na mzungu. Elimu ya hiyo imani ilikuwepo kabla mzungu hajafika Tanganyika. Dini ya biblia ndiyo iliyoletwa na mzungu.

Hakuna sehemu nimeponda elimu inayotolewa na mzungu. Mtu akisema elimu unayosoma soma ya wazungu maana yake ni kaiponda elimu ya wazungu? Kuna tatizo la kutafsiri hoja.
Wewe unamzungumzia Mungu wa kabla ya ujio wa dini ya biblia au wa baada ya ujio wa dini ya biblia?
 
Hivyo ni visingizio ili usikosoe dini, Mara hoo Mungu hachunguzwi, 🤣ujinga mtupu...kiumbe chenye nguvu kuliko kingetengeneza dunia isiyo na dhambi na shida, na Kama anatujali na anajua yote hamna haja ya kuumba watu afu awachome baadae, Mungu wa hivi ni wa kutungwa ili watu waogope watoe sadaka na kufata sheria za waliotunga, Mungu anajali unamwaga wapi kweli
Hizo akili zenu siwezi ziita za kijasiri kwa kumhoji Uwepo wa Mungu bali ni mawazo ya waliyokata tamaa.
Nani aliyekwambia kwamba Mungu ni kiumbe?
Nani aliyekwambia Mungu ameumba dunia isiyo na dhambi wala shida?
Kwenye utafiti wako umeshindwa hata kusoma Mathayo 13:24?
Je unajua nini maana na kusudio la sadaka?
Tatizo tunashindwa kutofautisha kati ya ukweli na uongo, haki na batili katika dini zetu, kwani kuna watu wengi wanaotumia imani za dini kwa kujinufaisha kiuchumi.
Critical thinker huwa hapingi uwepo wa Mungu bali anapinga aina ya miungu.
 
Back
Top Bottom