Mungu Yupo: Majibu kwa Wasioamini

Status
Not open for further replies.
Kwani kila swali lazima liulizwe ktk uzi huu? Na aliyekwaambia nina majibu yote nani?

kumbe hujiamni,mbona umeanza kwa risala ndefu kisha unasema huna majibu??,mbona unaweka mipaka kazika kujadili jambo hili??ama umeikariri biblia na ushakuwa mtumwa ??
 

we si mmojawapo wa wanao amini/?niwaulize akina nani tena??,kama haujadili kuhusu biblia specifically uliikuwa na maana gan kusema mungu wa biblia??,mbona unajichanganya kijana
 
Last edited by a moderator:
Umesoma mada ukaielewa wewe?

Mbona unaulizamaswali ambayo mtoa mada ametoa angalizo kuyahusu?



Wewe ni free ideas kweli?

nimeelewa sana ye ndok ajichanganya,mbona anaikana bible tena kwamba haijadili yenyewe nakat mwanzo kasema ,anamuongelea mungu wa biblia?
 

Watu hatutaki kuamini, biblia tumeitoa makosa.

Wewe unakuja kutupa mistari ya biblia!

Kuamini biblia kikondoo bila backing ndio wengine hatutaki. Biblia unavyoiona sacred wewe si kila mtu, wengine tunaweza kuiangalia na kuitoa makosa kibao tu. Kwa hiyo usitake kufanya kwamba kwa kuwa kwako wewe biblia ni sacred basi kila mtu ataiamini tu.

This is exactly why religion is so lame.

Mnapewa maneno yameandikwa na wayahudi maelfu ya miaka, wayahudi wanawapa sheria zao, mnayakumbatia kwamba ya mungu.

Watu wakitaka a scientific explanation rooted in logic, mnawaita wana kasumba za ukoloni.

Kati ya nyie mnaokariri vitabu vya wayahudi na sisi tunaouliza maswali nani ana kasumba ya ukoloni?
 
Mkuu inaonekana kama wameuogopa huu uzi
Mbona siwaoni hapa?

Do not flatter yourself.

Wewe ndiye uliyeopgopa kujibu the problem of evil.

Mpaka leo hujatoa jibu.
 
Huwa siwaelewi mnapomkana Mungu na kuleta "problem of evil". hili swali nimelijibu katika uzi huu na kama hujaelewa nitarudia. Kiranga , unaposema "problem of evil" huoni unafanya "assumption" zinazodai/zinazolazimu uwepo wa Mungu?

Ushawahi kusikia kitu kinaitwa "immanent critique" maishani mwako?

Soma zaidi hapa

Immanent critique - Wikipedia, the free encyclopedia

Kifupi, mimi kama sikubali kuna mungu, na wewe kama unasema kuna mungu, tukibishana wote kwa kusimamia pande zetu, hatutapata hata pa kuanzia.

Sasa kinachofanyika hapo, mimi naachana na position yangu ya kutokubali kwamba mungu yupo, kwa muda tu, ili kuangalia upande wako na mjadala uendelee.

Nasema, OK, tuseme mungu yupo, na ni mwenye ujuzi wote, na uwezo wote, na upendo wote. Tukubaliane kwamba hili ni kweli.

Swali linakuja tukishakubaliana hivyo.

Kama mungu yupo, na ni mwenye uwezo wote, na ni mwenye uwezo wote, na ni mwenye upendo wote.

Kwa nini karuhusu iwezekane kuzaliwa watoto vilema?

Hii ni hesabu ya ku solve for x, ambapo katika ku solve for x, unafanya let x be y, halafu jibu utakalopata la x unaweza kuli verify.

Naona somo zima la "immanent critique" limekupitia mbali.

Mtu anaposema "let's say god exists, for the sake of carrying the ergument and analysis forward" hamaanishi kusema kwamba kakubali kwamba mungu yupo.

Unatofautishaje mema na mabaya katika ulimwengu ambao hakuna Mungu?

Kuna njia nyingi tu. Unaweza kuanza kwa kusema kwamba yale yote ambayo sipendi kutendewa ni mabaya, na yale yote ambayo napenda kutendewa ni mazuri.

Hapo hujamhitaji mungu.

Kwa mfano, mimi sipendi kuuawa, kwa hiyo hili ni baya kwangu, sipendi kufanyiwa, na sitaki kumfanyia mwingine.

Pia mimi napenda zawadi za Swiss watches, kwa hiyo hili ni jema, mtu akinifanyia nitapenda na mimi nitapenda kumpa mwingine.

Hapo tayari tushaona mema na mabaya ambayo hayamtegemei mungu.

Hebu ona hapa wanajadili "secular morality" ambayo haimuhitaji mungu

Secular morality - Wikipedia, the free encyclopedia

Kwa hiyo kufikiri hakuna wema na ubaya nje ya mungu ni makosa, ni kama samaki kufikiria hakuna dunia isiyo na maji. Just because wewe umegubikwa katika bahari ya dini inayomtegemea mungu kwa kila kitu hilo halimaanishi hakuna watu wenye moral standards bila kumtegemea mungu

Msome Albert Einstein hapa




Einstein kakusaidia hapo jinsi ya kupata moral code ambayo haimtegemei mungu.


Wewe ulitaka afanyeje? atengeneze watu ambao hawana uhuru wa kuchagua? Kama angefanya unavyotaka unafikiri angekuwa ameumba watu kwa mfano wake? Unafikiri kuna upendo bila kuchagua?

Huu uongo wa "mungu ameacha mabaya kwa kuwa anapenda uhuru wa kuchagua" nilisha u debunk.

Kama mungu anapenda kuchagua mbona hajanipa uchaguzi wa kuamua nizaliwe katika dunia ya namna gani, nchi gani, kwa wazazi gani, niwe na genes gani etc? Mbona nimejikuta nimezaliwa tu? Huyu ni mungu anayependa tuwe na uhuru wa kuchagua kweli?

Imagine mke wako ukitaka akubusu anakubusu hata kama yeye hataki. Utakwenda mtaani kifua mbele kuwa kuna upendo kati yenu?

Kama anapenda sana uchaguzi, mbona hakunipa mimi uchaguzi wa kuchagua nizaliwe au nisizaliwe?


Sasa mungu kaumba ulimwengu ambao anajua una maasi, na anajua kaumba wanadamu na udhaifu, makusudi, na kawawekea majaribu, na kajua kabisa wataasi, na kwa sababu kajua wataasi, na hawezi kukosea, hawawezi kuepuka kuasi.

Kwa maneno mengine kashawapangia kuasi.

Wakiasi atawalaumu?

Atawachoma moto kama wafanya dhambi? Wakati yeye mwenyewe ndiye aliyefanya kila jitihada kuhakikisha wanaasi?

Kaumba ulimwengu ambao uasi unawezekana, isitoshe kaweka vishawishi, isitoshe kawaumba binadamu dhaifu.

Binadamu wakiasi kosa ni la nani? Binadamu au mungu?

Kwa kuumba ulimwengu wa namna hii Mungu amedhihirisha upendo mkuu sana (Yohana 3)

Hapana.

Ukiwa software designer tu, halafu una uwezo wa kutengeneza software ya computer isiyo crash, lakini ukaamua tu kutengeneza software inferior inayocrash, unaweza kufukuzwa kazi. Hii ni standard ya kibinadamu tu.

Kwa nini mungu mwenye uwezo zaidi (mkuu) na ujuzi zaidi (mkuu) na upendo zaidi (mkuu) tumuwekee lower standards?



Simple! Kuna Magonjwa kwa sababu kuna dhambi. Kuna dhambi kwa sababu Mwanadamu aliamua kumwasi Mungu.

Uwezo wa mwanadamu kumuasi mungu mwanadamu aliutoa wapi? Mungu alipoumba ulimwengu kwa nini aliruhusu uasi uwezekanike?

Kama mungu kaumba ulimwengu na kuweka parameters zote, kwa nini aliruhusu parameters za ubaya kuwezekana?

Usiniambie kwa sababu alitaka mwanadamu awe na chaguo, kwa sababu mimi hakunipa chaguo nizaliwe au nisizaliwe, na nizaliwe wapi, vipi, niishije etc. Huyu si mungu anayependa viumbe wake wawe na chaguo


Mwanadamu alimwasi Mungu kwa sababu ya kutumia vibaya utashi wake.

Uwezo wa mwanadamu kutumia vibaya utashi wake umeumbwa na nani? Na kwa nini uliumbwa?

Mwanadamu alikuwa na utashi kwa sababu Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua.

Mimi mbona sikupewa uweza wa kuchagua nizaliwe au nisizaliwe? Katika tendo moja la kujamiiana kuna viini kama milioni mia mbili na nusu vinakufa ili kimoja tu kifanikiwe, kama mungu anapenda uchaguzi sana, mbona hivi vingine hajavipa uchaguzi wa kuishi?

Mungu alimuumba na uwezo wa kuchagua kwa sababu Mungu nu pendo.

Mbona mimi sijapewa uchaguzi kuamua nizaliwe au nisizaliwe? Na nizaliwe vipi? sehemu gani etc? Kama mungu kutoa uchaguzi ni upendo, sisi ambao hatujapata option kuchagua hatupendi.

Kwa hiyo "ultimately" kuna magonjwa kwa sababu kuna Mungu!

Alishindwa kuyazuia?


Unadhani kuna mahali popote ambapo ni sahihi kwa mtu kumbaka mtoto mchanga na kumkatakata vipande kisha kula nyama yake? Jibu lako lina maana gani (what does your answer imply)?

Kama si sahihi kwa nini mungu kaumba ulimwengu ambao hili linawezekana?




Hili tatizo lingine la wasioamini Mungu! Kama unaamini katika naturalism (kama ambavyo nimekusoma katika nyuzi kadhaa) kwa nini utumie "compassion, logic, ethics," vitu ambavyo havionekaniki wala kushikika?

All of those are perfectly understandable and logical memes. Einstein kakusaidia pale juu.

Compassion inaonekana pale mama anapolea mtoto na kumkuza, it is a practical concept, logic gates give you electicity and computing, unaposema logic haionekani sijui kama unajua kwamba unapotumia computer yako inatumia logic gates ambazo ziko katika circuitry za electronics ndani ya motherboard ya computer yako. Ethics ni somo la ubinadamu tu, kutumia akili ili kuwa mtu mwema.Halihitaji mungu. Einstein kakusaidia hapo juu, kwa nini unaona ni lazima kuwa na mungu ili kuwa na ethics wakati kuna watu mamilioni Asia huko hawaamini mungu lakini wana a very good ethical system?

Na pia hapa unajaribu kusema kuwa "God is morally wrong" na mimi nauliza "Under which Moral Law is God wrong?". Unapimaje ethics za Mungu na kuzithibitisha kuwa ziko chini? What are the scales?

Let's see.

If at all he exists, holding him to account.

God would violates the Hippocratic oath (he has the ability to eradicate disease but he does not).
God violates the International Criminal Court laws (he has the ability to stop all wars but chooses not to).
God violates The Universal Declaration of Human Rights (he has the ability to make all humans truly equal but he bestow on some fortunes and on some blindness from birth)
God violates The Code of Hammurabi (if a builder builds a house and the house collapses the builder is responsible, god created the earth but it is constantly crumbling down with earthquakes killing thousands)

The list goes on and on.

Apparently god violates his own laws. he forbids us to kill but he kills inordinately.




Katika ulimwengu/Dini unayoiamini ya "random and chance" kuna tatizo gani mtoto kuzaliwa kipofu?

Nani kakwambia naamini dini ya random and chance?

Katika dini yako ya "Hakuna Mungu" na hivyo hakuna "Ultimate Law" kuna tofauti gani kati ya mema na mabaya?

Ushaoneshwa hapo juu kwamba huhitaji mungu kuwa na mema na mabaya. Wewe hujaweza kutuambia kama mungu mwenye uwezo wote na ujuzi wote na upendo wote kauumba ulimwengu huu, mbona ulimwengu una maovu mengi sana?

Hitler aliona ni jambo Jema kuua wayahudi Mil 6+ na Stallin akaona ni jambo zuri tu kuua mamilioni ya Warusi.

Kwa nini mungu alimuumba Hitler na kuruhusu haya mauaji? Ina maana alishindwa kuyazuia? Kama hakushindwa kwa nini hakuyazuia? Alipendezwa nayo?

Kuna watu wanaona ni vyema wakibaka au kuua. Katika dini yenu ya hakuna Mungu, unawahukumu wana kosa? Kwa sheria ipi?

Apparently mungu naye anaona vyema, kama angeona si vyema, uwezo wa kuzuia alikuwa nao, ujuzi wa kuzuia alikuwa nao. Kwa nini hakuzuia?



Baba A akiona ni vyema kuwapa watoto chakula na Baba B akaona ni vyema watoto wake wakafa na njaa, na wote hawa ni binadamu, nani atakuwa amekosea? Kwa sheria ipi hiyo ya ubinadamu maana hawa wote ni wanadamu!

Mungu ndiye atakuwa amekosea kwa sababu yeye ndiye anayeruhusu yote, mpaka fikra za hawa watu.

Au mungu si muweza vyote?

Hujatuambia pa sheria hiyo mtunzi wake ni nani na kwa mamlaka gani aliitunga sheria hii!

Msome Einstein hapo juu.

Hujajibu kwa nini mungu mwenye uwezo wote na ujuzi wote kachia watoto wa kijerumani wachomwe moto na Hitler? Ina maana alikuwa hana uwezo wa kuwaokoa? Au alikuwa na uwezo wa kuwaokoa hakutaka tu?

Kama hakutaka tu, kweli ana upendo mkuu?


You are right na ndivyo alivyo!

Sasa imekuwaje mungu mwenye uwezo wote na ujuzi wote achinjechinje watoto na kuachia wazaliwe na vilema? Mwanadamu angefanya hivyo tungemuita monster, mbona mungu mnamuabudu baada ya uovu wote huu?


Una maana hata pale viumbe hawa wanapochagua mauti badala ya uzima Mungu awalazimishe? Mfano, wewe Kiranga leo umemkataa Mungu mbele yetu sote, halafu unatarajia kwa sababu ya upendo wake akuachie tu uende, are you kidding?

Mungu kama kaumba kila kitu kaumba mpaka uwezo wangu wa kuelewa, sasa nisipomuelewa kwa sababu yeye hajanipa uwezo wa kumuelewa atanilaumu mimi vipi?

Mimi ndiye wa kumlaumu yeye.

Suppose mungu yupo, mimi sijamwelewa, kwa sababu hajanipa uwezo wa kumuelewa, na wewe umemuelewa, kwa sababu kakupa uwezo wa kumuelewa (after all tunaokoka kwa neema tu wameimba)

Unafikiri hiyo ni just and fair?

Kwa nini mungu awape neema wengine na wengine awanyime?

Kama huyu angekuwa bosi mwanaadamu tungesema ana favoritism.

Mungu ngani huyu kila standards za kibinadamu anashindwa kuzifikia?

Hakimu anapotoa hukumu huitoa kwa upendo kwa kuwa ni haki stahili.

Mfano wako mbovu.

Hakimu hakuumba ulimwengu, ana deal na ulimwengu iliokwishaumbwa kwa mujibu wenu.

Mungu kaumba ulimwengu from scratch.

Kwa nini hakufanya mabaya yasiwezekane tangu mwanzo?

Haya Magonjwa ni haki stahili ya Mwanadamu kwa sababu ya kuukaribisha uasi (dhambi).

Na mtoto mdogo anayezaliwa leo na kufa leo kwa ugonjwa kakaribisha dhambi gani?

Huwezi kukaribisha adui halafu ukalalamikia madhara yake. Each choice have its consequence!

Mtoto mdogo anayekufa mara baada ya kuzaliwa amefanya choice gani mpaka apate consequence hiyo? Kama makosa ya wazazi wake kwa nini mungu amuue mtoto? Kwa nini asiue wazazi na kumbakisha mtoto?

Bill hajawahi kumsaidia Mungu kazi hata siku moja. kupeleka chanjo Afrika haijawahi kuwa kazi ya Mungu. Umelipata wapi hili?

Mungu kawaumba watu bila chanjo. Bill kaona mungu kachemsha, kaumba watu bila chanjo, ngoja nimsaidie kuwapa hawa watu chanjo. Anawapa.

Watu wanapata chanjo wanaishi kwa afya bora zaidi.

Utasemaje Bill Gates hajamsaidia mungu hapo?


Jibu la swali hili nimeshalijibu hapo juu...madhara ya kukaribisha adui si kazi ya Mungu kuyabeba. Ukweli hata kama unauma ndio ukweli wenyewe!

Hujajibu, umebabaisha, na kubabaisha kwako kumezaa maswali zaidi. Kama mungu kaleta mabaya kutupa choice, kwa sababu anapenda sana choice, kwa nini hakunipa choice mimi niamue nizaliwe au nisizaliwe? Nizaliwe wapi, lini etc?

[/QUOTE]
Check the answer above! Huna haki ya kudai habari ya mabaya wakati unasema hakuna Mungu![/QUOTE]

Check the explanation above, including Einstein's. Huhitaji mungu kuwa na mfumo wa mabay na mazuri.

Swali hili unabadili tu namna ya kuliuliza na nimeshalijibu hapo juu!

Umebabaisha kwamba mungu anapenda choice, mbona katuleta duniani bila kutuuliza kama tunataka? Tumezaliwa bila hata kuulizwa tuchague wazazi, nchi, mwaka etc?

Huyu mungu anapenda choice kweli au mnatumia hilo conveniently tu?


Anyway hujaweka ushahidi wowote kuwa hakuna Mungu

You can't prove a negative.Kitu ambacho hakipo hakina ushahidi kwamba hakipo, kwa sababu hakipo.

Unaweza kunipa ushahidi kwamba hakuna Mchagga mwenye macho matatu anayekaa juu ya mlima Kilimanjaro?

Ukinipa ushahidi kwamba huyu hayupo na mimi nitakupa ushahidi kwamba mungu hayupo.

zaidi ya kuhoji kwa nini Mungu kama yupo alifanya A B C.

Swali ambalo hujalijibu.

Hakuna mahali umefuta point zangu na kwa ukweli umehakikisha nilichokisema kuwa ni dini yako tu inayokataa uwepo wa Mungu inakulazimisha kufika uliko.

Hakuna pahali ulipoelezea ukaeleweka kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na uoendo wote kaumba ulimwengu unaoruhusu watoto kuzaliwa na vilema vya maisha.

Si kwa sababu hakuna Mungu bali kwa sababu hutaki kukubali uwepo wake ambao pia wajua ni halisi

Sasa umekuwa kigagula unajua ninachojua just like that?

Jibu swali, kwa nini mungu hajazuia watoto kuuawa na Hitler? Alishindwa au hakutaka tu?

Kama alishindwa, je anaweza kila kitu kweli?

Kama hakutaka, je ana upendo wa juu kabisa?

Umeruka na kukimbia point zangu badala ya kuzijibu moja baada ya nyingine.

Points gani? Za kukimbia kujibu "the problem of evil"? Do not flatter yourself.

Mungu yupo, alikuweko na ataendelea kuwepo!

Kama yupo, kwa nini kaumba ulimwengu ambao uovu unawezekana wakati ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?

Huu ndio ukweli mchungu!

Ukweli mchungu ni kwamba hujajibu swali jepesi tu la "the problem of evil".
 
Owner always makes the rules. You own your home you make the rules there.
He owns all thing and makes the rules....So simple!
Bado unapiga blaa blaa tu hapa, wewe jibu swali, NI NANI ALIYEKUAMBIA (or rather, UNA UTHIBITISHO GANI) kuwa huyo mungu wako ndiye Owner wa hii dunia kiasi kwamba atukuzwe kwa kuacha a-set lolote atakalo?
 
The Bottom Line is: Absence ya Mungu ni imani kama uwepo wake,; kwa maneno mengine hakuna uthibitisho wa kutokuwepo Mungu kama ilivyo kwa uwepo wake! Eti Kaunga, hiki si ndicho ulichojifunza kutoka kwenye uzi huu, au?
 
Check the answer above! Huna haki ya kudai habari ya mabaya wakati unasema hakuna Mungu![/QUOTE]

Check the explanation above, including Einstein's. Huhitaji mungu kuwa na mfumo wa mabay na mazuri.



Umebabaisha kwamba mungu anapenda choice, mbona katuleta duniani bila kutuuliza kama tunataka? Tumezaliwa bila hata kuulizwa tuchague wazazi, nchi, mwaka etc?

Huyu mungu anapenda choice kweli au mnatumia hilo conveniently tu?




You can't prove a negative.Kitu ambacho hakipo hakina ushahidi kwamba hakipo, kwa sababu hakipo.

Unaweza kunipa ushahidi kwamba hakuna Mchagga mwenye macho matatu anayekaa juu ya mlima Kilimanjaro?

Ukinipa ushahidi kwamba huyu hayupo na mimi nitakupa ushahidi kwamba mungu hayupo.



Swali ambalo hujalijibu.



Hakuna pahali ulipoelezea ukaeleweka kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na uoendo wote kaumba ulimwengu unaoruhusu watoto kuzaliwa na vilema vya maisha.



Sasa umekuwa kigagula unajua ninachojua just like that?

Jibu swali, kwa nini mungu hajazuia watoto kuuawa na Hitler? Alishindwa au hakutaka tu?

Kama alishindwa, je anaweza kila kitu kweli?

Kama hakutaka, je ana upendo wa juu kabisa?



Points gani? Za kukimbia kujibu "the problem of evil"? Do not flatter yourself.



Kama yupo, kwa nini kaumba ulimwengu ambao uovu unawezekana wakati ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?



Ukweli mchungu ni kwamba hujajibu swali jepesi tu la "the problem of evil".[/QUOTE]

Dah, Kiranga umetisha. Yaani wakariri dini wote wameingia mitini na akitokea hata 1 wa kujibu hizi Arguments zako njoo unidai bia!
 
Do not flatter yourself.
Wewe ndiye uliyeopgopa kujibu the problem of evil.
Mpaka leo hujatoa jibu.
Hapa kuna tofauti kubwa

Kuna tofauti kubwa kati ya jibu na jibu unalolitaka wewe
Pia kuna tofauti kati ya jibu lisilo sahihi na jibu sahihi

Wewe umetaka jibu
Jibu umepewa lakini bado unasema hujajibiwa,hii inamaana hata jibu hulijui
Yaani hujui kama jibu ni jibu

Ni bora ungesema jibu ulilopewa sio sahihi
Hii ingemaanisha kuwa unajua jibu ni kitu gani
Tungeanza kukuhoji kama unajua kama jibu sahihi ni kitu gani
Ili tujue kama una uwezo wa kung'amua kuwa kuna jibu ambalo sio sahihi na sahihi

Lakini umeendelea kudai jibu tu
Kitendo cha wewe kupewa jibu halafu unadai hujapewa ni ishara ya kutokujua ulichouliza achilia mbali kujua kama umejibiwa

Pia inathibitisha kuwa kama huwezi kulijua jibu maana yake huwezi kujua kama ni sahihi ama la!

" Don't flatter yourself " !!!!!!
 
The Bottom Line is: Absence ya Mungu ni imani kama uwepo wake,; kwa maneno mengine hakuna uthibitisho wa kutokuwepo Mungu kama ilivyo kwa uwepo wake! Eti Kaunga, hiki si ndicho ulichojifunza kutoka kwenye uzi huu, au?

Unamuuliza Kaunga au?
Maana sikuelewi
Umeniquote mimi halafu swali umelielekeza kwingine!
 
Last edited by a moderator:

Natumia definition ya kitabu chenu. Amri kumi za mungu wenu. Anasema tusiue. Halafu yeye anafanya iwezekane mama apate mimba na mtoto afe tumboni.

Huyu mtu ni mzima kweli?

Anatuhumu kitu ambacho hata yeye mwenyewe anakitumia!
Huruma iliyoje?
 
kumbe hujiamni,mbona umeanza kwa risala ndefu kisha unasema huna majibu??,mbona unaweka mipaka kazika kujadili jambo hili??ama umeikariri biblia na ushakuwa mtumwa ??

Ni heri anayekuwa mtumwa wa biblia,kuliko mtumwa wa kutokujijua hata nafsi yake mwenyewe,kwa sababu kama
unakana uwepo wa Mungu ni sawa na kujikana uwepo wako mwenyewe,kwani hukujiumba wewe'
 
Stephano Mtangoo

Umenikumbusha Story ya mtoto wa Kimarekani ambaye Professor wao asiyeamini kuwa kuna Mungu aliwatia sumu wote kwa mafunzo yake kuwa hakuna Mungu with various supporting arguments anazozijua. Huyu Professor alikuwa na gari zuri sana.

Mwishoni huyu dogo akiwa na Professor kabla hajapanda gari yake yule dogo akamwambia: you know professor hii gari yako iko poa sana. Ila imejitengeneza yenyewe Tyres, Engines, Shape etc etc. Yule Professor akang'aka sana kuwa gari ilitengenezwa na Engineers makini sana aache ujinga wake.

Dogo naye akamjibu kuwa wewe ndo mjinga usiyejua kuwa Design & Engineering ya Binadamu imefanyika kwa umakini wa hali ya juu kuliko gari yako. Kama huamini kuwa gari ilijitengeneza why do u want me to believe kuwa Binadamu aliibuka tu? Professor akagwaya.

Hakika naamini Binadamu aliiumbwa na aliiumbwa na Mungu.

So, Mungu yupo!
 
Last edited by a moderator:
Ni sawa na kusema kama wewe unabisha kuwa risasi haiui na mimi nasema inaua inabidi mimi niruhusu unirarue nayo ili tuone kama inaua ama la!
Funny,isn't it?

Kwanini utoke kwenye msimamo wako?
Unataka tufanye majadiliano kutokakwenye msimamo fake,kwanini?

Kama unasema Mungu hayupo halafu ukapose kama gnostic inamaana wewe ni kigeugeu na hujui kama hujui Mungu yupo ama la!
Nasema, OK, tuseme mungu yupo, na ni mwenye ujuzi wote, na uwezo wote, na upendo wote. Tukubaliane kwamba hili ni kweli.
Kwanini "tuseme Mungu yupo"?
Kwanini tufanye majadiliano kwa kutumia assumption?
Sisi hapa atu-assume bali tunaamini yupo kama wewe UNAVYOAMINI hayupo!

Kama mungu yupo, na ni mwenye uwezo wote, na ni mwenye uwezo wote, na ni mwenye upendo wote.
Kwa nini karuhusu iwezekane kuzaliwa watoto vilema?
Haya ni maswali ambayo anatakiwa aulize mtu ambae anaamini Mungu yupo sio anae-assume Mungu yupo
Maswali yako hayana maana kwakuwa una-assume tu!
Hii ni hesabu ya ku solve for x, ambapo katika ku solve for x, unafanya let x be y, halafu jibu utakalopata la x unaweza kuli verify.
Sisi hatusemi let x be,sisi tunasema x ni ......
Wewe ndio unasema let x be ....
Huoni kuwa tuko nchi mbili tofauti?
Tutajadilije jambo ambalo hata uwepo wake hatujakubaliana?
Mtu anaposema "let's say god exists, for the sake of carrying the ergument and analysis forward" hamaanishi kusema kwamba kakubali kwamba mungu yupo.
Nimeshakujibu hii
 

Nizungumzie Kuhusu Uasi tena.
Ukisoma biblia, inaeleza wazi kutokomeza Dhambi/Uasi na Dunia kufanywa mpya isiokua na Mawaa ata kidogo!
Rejea shughuli za Hema takatifu lililokuwepo Hapa duniani likikusudia kua Mfano wa Kafara hails Yesu kuja kutufia Kama Kafara!
Katika shugghuli zile palikua na shughuli za Kila Siku na Mara moja kwa Mwaka!
Katika ile shughuli ya Mara moja kwa Mwaka kulikua baada ya shughuli anaachiwa Mbuzi wa AZAZERI,
Huyu Mbuzi alikua anabeba dhambi/Uasi zote na kwenda kufia huko nyikani; hichi Kitendo kinajulikana km kutokomeza Dhambi/Uasi.
Kwa Maana hiyo basi hizi shughuli zilikua nakala ya Yesu kuja kua Kafara halisi! Tayari Yesu alishakufa msalabani kazi iliyobaki ni Shetani kuangamizwa na Dhambi/Uasi kutokomezwa na Dunia kutengenezwa mpya bila ya kuwepo dhambi na Uasi!
Sasa wewe Uasi unaosema wewe kua waweza kutokea unaujenga kwa misingi gani?

Biblia Iko wazi na mipango ya Mungu Iko wazi yote ni Imani yako tu ndio inayokufanya useme hivyo!
Kwa mujibu wa Biblia Hapo baada ya kufanya nchi mpya kutakua hakuna Dhambi/Uasi tena!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…