Muogopeni Rostam Aziz kama Corona. Spin Doctors kazini 100%

Kwa kauli hii twafa
Hapana, labda tujiuwe wenyewe kwa ujinga wetu. Lakini hao jamaa wanachohitaji ni makampuni makubwa duniani yenye hisa zao yasikose fursa za Africa.

Tanzania tunaongelea sasa hivi kujenga ma highway ya toll.


Tanzania tunaongelea sasa hivi kujenga mahospitali makubwa kuwe na utalii wa afya.

Dubai pale ilipo kama haikutafuta njia mbadala za kuzalisha utajiri wao itaanguka.

Lengo lao kuu wajijenge Congo na gateway yao iwe Tanzaniakwa huku mashariki, kwa kule maghribi tayari AD Ports imeshakamata. na DP World na AD Ports ni ndugu wa damu, hawa Dubai wale Abu dhabi. Umeona eeh?

Hakuna sehemu nyingine yoyote duniani iliyobaki na mali asili nyingi duniani isipokuwa Congo.

Wnataka wawahi japo wawepo kidogo, wao kidogo tu wakishika asilimia fulani ya biashara ya Congo inawatosha kabisa, Hawana makuu. Kinchi chao kidogo.. wanaogopa kukikuza sana zaidi ya pale kitamezwa na wahindi.
 
Nisikilize.
Hakuna anayepinga DP world kuwekeza bali tunapinga makubaliano ya awali yasiyoeleweka.

Mfano Mbarawa akiulizwa ukomo wa mkataba anajibu...Mkataba utakoma pale shughuli za uwekezaji zitakapokoma...lini?

Umewahi kuona wapi mkataba usiokuwa na ukomo kimaandishi?
 
Haiwahusu kbisa, Wamasai hawakuhamishwa Loliondo, msidanganyane, Wamasai wamehamisha ndani ya Ngorongoro Crater. Ile ni wenyewe Tanzania kwa ajili ya soko la Watalii.

Loliondo ni kitalu tu cha uwindaji, tena cha wale wafalme w Abu Dhabi, siyo hawa.

Hawa wanavyo vitalu viwili havipo kabisa huko Loliondo.
 
Hato mabilioni ya kuwahamisha mbona hayakuwepo kwenye bajeti ya wizara yoyote?
Kwanini hiyo pesa ya kuwahamisha haijasumbua kama inavyosuasua kutolewa kwenye shughuli zingine za maendeleo?

MFano pesa za kufidia watu kupisha ujenzi wa barabara huwa inachukua hadi miaka 5 lkn hii ya kuwahamisha wamasai iko mfuko wa shati?

Nchi hii tunapigwa sana kijinga...huoni kuna kitu hakipo sawa?
 
Hakuna makubaliani yasiyoeleweka, tatizo lako umejazwa ujinga wa kwanza basi hata mkataba huuoni. Jifunze "to unlearn". Futa kabisa kilicho kichwani mwako sasa hivi halafu usome ule mkataba. Utauona umetupemdelea sana Tanzania.

Usisikie ujinga wa wanasiasa wapumbavu, wao wana akili za kifungi maiko, akifanya tatizo ndiyo atengeneza pesa. Hawa watu wanaelewa, wameshalizwa sana Kenya na wanasisa na matapeli Mpaka hawana hamu napo kabisa. Hili dili la Port ya Dar lilikuwa kwanza liwe la Kenya, walipochapwa ndiyo wakaachana nao kabisa. NGoja nikuwekee ushahidi chini hapo.
 
Usitufanye wote harujui kusoma isipokuwa wewe tu.
Narudia mkata sio wote ni mbaya isipokwa unavifungu vichache wenye mitego hatari.

Mosi tenda haijatangazwa, huoni hii inatia shaka?
 
Hapo ndio una haribu.
Watufanyie kazi kwa maslahi yetu?

Malengo yao yaliyojificha ni yapi?
Sikiliza kijana, wao wana malipo yao yatakayolipwa kwa huduma zao, lakini wewe hapo hapo unawakodisha sehemu ya bandari. Hapo hapo mizigo inaongezeka unalipwa kodi. Portcharges unachukuwa wewe, ambazo wao wanahakikisha mizigo inashushwa kwa haraka na wingi wao wanapata ile huduma za andarini.

. Mfano, umeleta container moja, kulitowa ndani ya meli mpaka kuliweka bandarini linapotakiwa liwekwe, kuna gharama zake za crane, labour,transport ya mule ndani. Ikipigwa hesabu hiyo ndiyo inaitwa handling charges. Sasa wao wakipewa kazi wanakwambia kila kitu tunafanya sisi badala ya kuchukuwa Dollar 100 zote wewe, chukuwa 50 na sisi 50. Na katika hiypo 50 yao, wakitengeneza faida unapata income tax. Na hapo wewe umepunguza gharama zote za administrtive costs, kazi yako ni kuweka sawa mahesanbu tu. Umekosa nini? Na vifaa vyote ambayo huna pesa ya kuweka kununuwa vya kisasa wanweka wao, kwa amakubaliano maalum.


Hebu jifunzeni kutafuta data kwenye mtatandao, uliza tu Port charges and handling charges for 20 feet container. Utapata jibu kwa bandari yoyote uitakayo. Ukiipaya jiyo piga mata m watakayoshusha kwa mwaka na kuyahudumia, ni pesa nyingi sana lakini wewe kama nchi ndiye mfaidika mkuu. Unamlolongo wa mapato kwa kila kontena nje ya bandari mpaka lifike linapokwenda.


Ni kazi ya pesa nyingi lakini nakuhakikishia peke yako, na wizi tuliokuwa nao Watanzania utaambulia ailimia 25% tu ya watakayokupa wao ukijitahidi sana. Sasa fikiria unaikosa 75% nzima kwa mapato watakaypo genereta wao wavolume ya mzigo kuomgezeka na kwa ku ennhance speed ya handling. Speed yao wewe hata ufanye nini huipati kwa sasa, labada miaka 20 ijayo. Maana wana vifaa vya kisasa.


Sasa wao mradi wanapata faida yao na nyinyti manapata yenu kwanini wwawaibie? Wangekuwa wezi wasinge ijenga nchi yao kwa biashara tu, si wangekimbiwa na kila mtu.
 
Rost tam [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mbona kaitwa kwenye mjadala Serena Hotel, kaongea sana tena kaulizwa maswali mengi sana. Tafuta Youtube utamuona, alikuwa yeye, Jenerali Ulimwengu, Lema, Zitto, na wengine wengine.


Huwa mnakurupuka sana Wtanzania. Vichwa vyenyewe vya chai ya rangi na maandazi asuhi halafu mtaweza kuyajuwa mengi yanayoendelea? Mawee.
 
Sipingi wala sikubali ilahao watu wapo sn katika kila nchi. ..I'm not sure kwa Rwanda km wapo otherwise namba 1 wao nimshirika wahuko.
Nchi za magharibi wanatumia kl mbinu na hasa fedha kufanikisha mambo yao
 
Glenn na wenzako wenye maswali bofya chini hapo, tusiharibu mada ya watu, ntajibu huko maswali yote na kuhusu chochote "General Knowledge":

 
Huyu mzee ALIKUA project ya State/kanisa kwenda upinzani kumshughulikia jk awamu ya nne!

Hakwenda kushinda urais bali check and balance KWA wanamtandao BAADA ya kushika nchi!

BILA yeye kwenda kule halo ungekua mbaya KULIKO hata jpm alivoikuta!!

BAADA ya jpm ku be nominated ndio project ikawa imeisha akarudi!!

SASA wanamtandao wameshika tena, project on!ndio MAANA kaanza kubweka like anachopewa abweke na office kubwa!!

Hakua msaliti Bali project ilikamilika!SASA amerudi tena KWA project ingine!!
 
πŸͺ“πŸͺ“πŸͺ“
 
True 😭
 
πŸͺ“πŸͺ“πŸͺ“
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…