Museveni anaeonekana kuifahamu sana Tanzania, hii sio hatari kwa usalama?

hahahaha alikua akiitwa hivo?uncle kabila miaka hy? Safi sana
Sidhani, akiwa BONGO alikua anaitwa mzee Mtwale na sio Kabila, Kabila limekuja kujulikana akiwa Congo na hasa wakati anaendesha ile vita iliokuja kumng'oa Mobutu; kama mnakumbuka vizuri, Nyerere (akiwa mstaafu wa Bongo ) alikua ndio mtu wa kwanza kwenda Kongo/Zaire ya wakati ule na akatoa bonge moja la speach na mwelekeo wa nini Kabila afanye, alimzuia asilipe hata madeni ambayo Mobutu alikopa nje ya nchi
 
Wa mpakani hawana shida huo muingiliano ktk mipaka upo miaka na miaka hata watz wanaingia sana nchi zingine kama hao unao waona wakija tz, mfano Kenya unaingia ndani zaidi ya 200km bila wasiwasi kabisa as if uko nyumban tz
 
Kweni wewe huijui Uganda au Kenya au Rwanda

Jitahidi uijue East Africa ambayo ndo motherland yako
 
Mseven kuijua geografia ya nchi siyo mbaya. Kwa maana kakulia bongo na kasomea bongo...
Then kafanyiwa michongo ya kuingia ikulu na mwalim.
 

Nusu ya maisha yake ya ukubwani, amekulia hapa, amesoma hapa, amesoma UDSM, asingekuwa Rais kama sio Nyerere.

Kama Wengine, Kabila Senior na Junior hapo DRC. Wengine wote kusini mwa Afrika hadi huyu Rais wa sasa wa Afrika Kusini. Kambi yao ilikuwa pale Morogoro.
 
hahaha mkuu ungemueleza huyo jamaa.mie khs kabila huna chakuniambia kikawa kipya. ila atakua kajifunza kitu huyo kijana
 
DSM wadada wa kazi za ndani ni Wamalawi siku hizi.
Wana miaka mingi Sana wakifanya hivyo na kulinda mageti,warundi wao Ndio vibarua huko mashambani kigoma,wanyarwanda Ni wachunga ng'ombe huko Kagera.

Nadhani Ni specialization ya kazi
 
Ameishi Tanzania na Amesoma chuo kikuu Tanzania,kabla kurudi Uganda na kuwa Rais.
 
Museveni wakati yupo msituni kalala nyumbani be kwa babu yangu sehemu inaitwa murongo kwa muda mrefu
 
kwani hujui museveni alikuwa anafundisha chuo cha ushirika moshi wakati huo na sasa MUCO?kwa nn asiijue tz wakati ni mtoto wa tz ?fuatilieni historia za viongozi muwajue.tz ilikuwa ni kituo wa wapigania uhuru wa nchi za afrika.
 
Hiyo ya mzee Mtwale sijui, mimi namjua kama uncle Kabila Kijitonyama jirani na yard ya magari ya Hashim Rungwe tena alikuwa anakuja mara nyingi na analala hata wiki. Ile nyumba IPO hadi leo na ile familia IPO hadi kesho. Ila sijui kwanini maisha ya ile familia hayajabadilika hata baada ya uncle kuwa rais wa Congo.
 
Hopefully unajua Lt. Gen. Kainerugaba sio mtoto wa kumzaa wa Mama Janet M7.
Sikuwahi kujua kuwa Gen MK sio biological son wa Janeth.

Ila, kwa kuwa ndiye mama aliemkuta Nyumbani akiwa "wife" wa mzee anabaki kuwa na heshima ya mama kama alivyo Ridhiwani na Mama Salma.

Tafadhali tujuze mama wa Gen PK ni nani unless taarifa hizo ni classified.
 
Mwenyezi Mungu akusamehe, huenda ni makosa ya wazazi wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…