Muungano bado una shida nyingi tusidanganyane

Muungano bado una shida nyingi tusidanganyane

Siamini kama Nyerere alikuwa mjinga sana kuifuta Tanganyika yake na kuiacha hai Zanzibar, lazima alikuwa na imani fulani ambayo aidha imefeli au inaendelea kufanyakazi kuelekea kwenye lengo kuu la muungano. Lasivyo huu muungano unahojiwa na hata watoto wadogo pia.
Kila aliyehoji muundo wa huu muungano alikiona cha moto wakati wa Nyerere. Jumbe aliondolewa kwa kuhoji uhalali wa serikali mbili wakati nchi zilizoungana ni mbili.

Njelu Kasaka na kundi lake walikuwa na hoja za msingi bungeni kutaka serikali ya Tanganyika, hoja zao zilizimwa na Nyerere nje ya bunge, na waziri mkuu wakati huo Malecela akapoteza uwaziri mkuu.

Sioni nia njema aliyokuwa nayo Nyerere zaidi ya kuisaliti Tanganyika.
 
Samahani sana, lakini, wewe na mjukuu wako wote mambumbumbu.
Tueleweshe mkuu mm n mjukuu wangu. Ile T621 DTY kwenye namba ya gari "T" ni kifupi cha nini? na kwenye ile gari ya mbele yenye namba Z 293ABL "Z" ni kifupi cha nini? na je Z sio sehemu ya T?
 
Kila aliyehoji muundo wa huu muungano alikiona cha moto wakati wa Nyerere. Jumbe aliondolewa kwa kuhoji uhalali wa serikali mbili wakati nchi zilizoungana ni mbili.

Njelu Kasaka na kundi lake walikuwa na hoja za msingi bungeni kutaka serikali ya Tanganyika, hoja zao zilizimwa na Nyerere nje ya bunge, na waziri mkuu wakati huo Malecela akapoteza uwaziri mkuu.

Sioni nia njema aliyokuwa nayo Nyerere zaidi ya kuisaliti Tanganyika.
Haya tuseme Nyerere alikosea, wewe je unafanya nini sasa kuweka mambo yalivyopaswa kuwa?
 
Tueleweshe mkuu mm n mjukuu wangu. Ile T621 DTY kwenye namba ya gari "T" ni kifupi cha nini? na kwenye ile gari ya mbele yenye namba Z 293ABL "Z" ni kifupi cha nini? na je Z sio sehemu ya T?
Tazama na namba za Zanzibar zina nini, utaelewa:

1702559263558.png
 
Haya tuseme Nyerere alikosea, wewe je unafanya nini sasa kuweka mambo yalivyopaswa kuwa?
Ninachofanya ndio kama hivi kuandika nilichoandika ili hata mbumbumbu kama wewe ajue kuwa Nyerere alikosea.
 
Inaavyoelekea Tanzania Itakuwa Zanzibar Hivi Karibuni.
Hakuna Tanzania kwenye dunia hii bali iko Tanganyika na Zanzibar. Zanzibar ilikuwepo kwa karne nyingi sana, inajulikana kuliko Tanzania ya 1964 tu hapa. Kwa namna nyinginge Wazanzibar wako sahihi kuibakiza nchi yao ya kihistoria. Tanzania kwao ni jina tu la maokoto, na wanaokota kwelikweli.
 
Kama isivyowezekana kuwa Tanzania bila Tanganyika.

Naona hata warioba na timu yake sijui walijazwa nini vichwani wakaishia kuandika kwenye rasimu yao eti muungano ni kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

Hopeless kabisa.
Unaposema tanzania bara lazima useme Tanzania visiwani, lakini unapotaka kuitaja Zanzibar ni lazima pia uitaje Tanganyika. Wazee wetu wanaogopa kulitaja jina la Tanganyika kabisa, nadhani kila aliyelitaja alikiona cha mtemakuni au alipotea kabisa.
 
Zanzibar ni demu aliyeikata Tanganyika... Ila kwakuwa mwanaume ana asili ya kulazimisha Mambo ..... Basi Zanzibar imeamua kuichuna Tanganyika. Hivi kwa akili za kawaida inawezekana mtu anayetoka kwenye ki-Nchi swa na mkoa wa Tabora anaweza kuwa Rais kwenye Nchi ambayo Ina watu zaidi ya 55+m?.
 
Kwani muungano ni lazima?kama ni mzigo acheni raia wapige kura.huu ni muungano wa USA na UK
tumebebeshwa kama mzigo na ndiyo maana wanatupa misaada mingi
 
Back
Top Bottom