Muungano wa Vyama 14 vya Siasa kuongea na vyombo vya Habari

Muungano wa Vyama 14 vya Siasa kuongea na vyombo vya Habari

"Kimsingi tumeshangazwa na viongozi wa kisiasa na moja ya chama cha siasa kupinga ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Mhe. Rais @SuluhuSamia, sidhani kama kupinga kule ni kauli ya chama, kwa tunavyofahamu tamko la chama linatokana na vikao vya chama" @BulenduDotto
... kumbe mamluki katika mwamvuli wa vyama vya siasa? Naona wanamtumikia bwana wao aliyewatuma hadi bwana kaamua kuahirisha mkutano na waandishi maana tayari alishawakilishwa na wakeze!
 
"Rais Mhe. @SuluhuSamia alipokutana na Mwenyekiti wa @ChademaTz, @TunduALissu katika kikao chao Lissu aliomba kurejeshewa passport yake na mafao, kwanini hakumwambia Rais masuala ya tume huru na katiba mpya? ili tuone wana nia njema na Taifa hili" @DoyoHassan ACD.
 
23 OCTOBER 2022
WAJUMBE 30 KUTOKA VYAMA 14 , WADAI CHADEMA WANA BAHATI SANA KTK SIASA ...


Kutafuta suluhu miongoni mwa wadau wa siasa za vyama vingi, wazungumzia wivu na choyo ya baadhi ya wanasiasa. Mgawanyo wa ruzuku, .... wakishutumu chama kikuu cha upinzani ... mgogoro wa Polisi na vyama vingi kuhusu mikutano ya hadhara sheria za vyama vingi na sheria za Polisi zinatakiwa kuhuishwa zisisuguane, CCM wanapata shilingi bilioni 2 kama ruzuku .... ripoti ya Kikosi Kazi idurufiwe na kusambazwa kwa umma ..

Wafuatao kutoka vyama 14 walikuwapo katika meza kuu kutoa tamko baada ya kikosi kazi kukabidhi ripoti kwa mheshimiwa rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania :
  1. ADA -TADEA - Zaituni Hokororo, Salehe Msumari
  2. CCK - David Majebele
  3. DP - Felix Makua, Asha Chuma
  4. UDP - Paulo Makulu
  5. UDPD - Twalib Kadege
  6. AAFP - Rashid Rai
  7. UMD - Halfani Mazrui
  8. SAU - Betha Mpata, Majaliwa P. Kyara,
  9. TLP - Richard Lyimo
  10. NRA - Mohamed Majaliwa
  11. NLD -Tozi Matangwa
  12. DEMOKRASIA MAKINI - Mohamed Abdullah
  13. ADC - Doyo Hassan Doyo
  14. ???


Source : MWANAHALISI TV

Ngoja tuone kama kuna a.mbaye atazungumzia mgombea binafsi kutokuwepo katika mapendekezo ya Tume na pia Tume ya uchqguzi kuajiri wafa yakqzi wake yenyewe kuanzia wilayani hadi Taifa.
 
"Rais Mhe. @SuluhuSamia alipokutana na Mwenyekiti wa @ChademaTz, @TunduALissu katika kikao chao Lissu aliomba kurejeshewa passport yake na mafao, kwanini hakumwambia Rais masuala ya tume huru na katiba mpya? ili tuone wana nia njema na Taifa hili" @DoyoHassan ACD.

Kwa hivyo Tundu Lissu akimwambia Rais ndio atatekeleza?. Mbona kikosi kazi kimetoa mapendekezo na bado Rais hajayakubali kasema ataenda kuyaangalia kwa jicho la tatu?.
 
Ccm acheni Sanaa hasa hizi zilizopitwa na wakati! Hivi hamfanyi tafiti za kujua aina ya wananchi mnaojing'ang'aniza kuwaongoza Wana upeo Gani wa uelewa?
Kiujumla mpo nyuma ya wakati mkidhani hii ni mwaka 1977 wa Nyerere na wananchi ni walewale!
Yaani mnahonga posho, ukumbi na agenda za kuongea Kwa watu wasio na mvuto Kisha mnataka wananchi wawaelewe! Hizo ni cheap propaganda ambazo soko lake linapatikana china TU Kwa Sasa!
Kubalini TU kuwa mmechuja na mnahitaji kutiwa rangi Kama batiki!
 
"Kimsingi tumeshangazwa na viongozi wa kisiasa na moja ya chama cha siasa kupinga ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Mhe. Rais @SuluhuSamia, sidhani kama kupinga kule ni kauli ya chama, kwa tunavyofahamu tamko la chama linatokana na vikao vya chama" @BulenduDotto
Tatizizo kubwa ni kudhani kuwa CHADEMA inaq hatimiliki ya nembo "upinzani". Wasiposema wao au wakipingwa basi wapingaji ni tawi la CCM. Nchi nyingi, inaposhindikana kukliondoa chama tawala madarakani, huwa vyama vyote vya upinzani vinaungani na kufanya kazi pamoja. Lakini kwa uchu wa madaraka kama ilivyo CCM, CHADEMA inataka ifanye hiyo kazi peke yake itwae uongozi.

Ni muhimu CHADEMA ijue kuwa bila kufanya kazi na vyama vingine vya siasa na kuendelea kuvibeza hivyo vyma ndiyo furaha ya CCM. Pasipo upinzani kufanya kazi pamoja na kudhani kuwa CHADEMA peke yake itatoboa, ni ndoto za mchana.

CHADEMA inazidiwa kete na CCM, maana CCM siku zote inaombea mfarakano kwenye upinzani. Katika vyama vyote CUF kilikuwa chama pekee kilichokuwa na nguvu kubwa hasa kule Zanzibar. Ilichokifanya CCM kila mtu anajuwa, sasa CUF ni karibu marehemu. CCM pia imekuwa ikiichakaza CHADEMA mdogomdogo. Migogoro mingi ndani ya CHADEMA, kama vile kuondoka/kufukuza kwa Zuberi na wengineo amao walikijenga CHADEMA haukosi mkono wa CCM. Lakini CHADEMA hili hawalioni. Wao kila kukicha ni kutaka kujiona ndiyo upinzani pekee na hivyo vyama vingine havina kitu.

Nafikiri tatizo kubwa ni uroho wa madaraka na kujitakia misifa. CHADEMA wanateka ikiwezekana washinde kura na washike nchi peke yao, maana wakiungana ukipatikana ushindi, inabidi wagawane vyeo. Ni hatari kuwategemea wanasiasa wachache na kuwaabudu kama Mungu, kudhani peke yao ndiyo wataleta mafanikio. Acheni kubeza vyama vingine. Kaeni navyo mpange mikakati ya kuiondoa CCM kwenye madaraka, lakini hii ya kufikiria CHADEMA pekee itafanikiwa ni ndoto. Sana saana mtaishia kupata ruzuku na kulipana mishahara, lakini kushika nchi hamtaweza bila kushirikiana na vyama vingine vya upinzani.
 
Leo wataongea na vyombo vya Habari.
=================
Hotuba nzima ilikuwa ni kumjibu Mnyika na CHADEMA badala ya kuzungumzia ripoti ya Kikosi Kazi.

View attachment 2395271

"Tumesikiliza taarifa ya @ChademaTz ikielezea kupinga taarifa ya kikosi kazi, tunachoweza kusema kwa sasa, CHADEMA wamejawa na ubinafsi, choyo na wivu mkubwa kuona Tanzania ikiwa kwenye maridhiano huku wao wakiwa nje ya mchakato wa kupatikana kwa maridhiano hayo" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Mhe. Rais @SuluhuSamia amesema wazi kuwa maoni sio amri kwa serikali, wapo wanaokosoa kauli hiyo, nani aliyekwambia maoni ni amri, maoni yanakuwa amri baada ya kutungiwa kanuni na sheria" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Kimsingi tumeshangazwa na viongozi wa kisiasa na moja ya chama cha siasa kupinga ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Mhe. Rais @SuluhuSamia, sidhani kama kupinga kule ni kauli ya chama, kwa tunavyofahamu tamko la chama linatokana na vikao vya chama" @BulenduDotto

"Kitendo cha chama cha siasa kupinga jambo ambalo hata hujalisoma, hujui nini kipo ndani yake, hili pekee ni tatizo kubwa. Kwani, hadi sasa taarifa iliyotolewa kwetu wananchi na wajumbe wa kikosi kazi ni muhtasari tu, unawezaje kusema ni mbaya na wananchi msiipokee" @DoyoHassan.
CHAMA CHA UPINZANI TANZANIA NI KIMOJA TU AMBACHO NI "CHADEMA" NYIE WENGINE NI MAMLUKI
 
Leo wataongea na vyombo vya Habari.
=================
Hotuba nzima ilikuwa ni kumjibu Mnyika na CHADEMA badala ya kuzungumzia ripoti ya Kikosi Kazi.

View attachment 2395271

"Tumesikiliza taarifa ya @ChademaTz ikielezea kupinga taarifa ya kikosi kazi, tunachoweza kusema kwa sasa, CHADEMA wamejawa na ubinafsi, choyo na wivu mkubwa kuona Tanzania ikiwa kwenye maridhiano huku wao wakiwa nje ya mchakato wa kupatikana kwa maridhiano hayo" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Mhe. Rais @SuluhuSamia amesema wazi kuwa maoni sio amri kwa serikali, wapo wanaokosoa kauli hiyo, nani aliyekwambia maoni ni amri, maoni yanakuwa amri baada ya kutungiwa kanuni na sheria" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Kimsingi tumeshangazwa na viongozi wa kisiasa na moja ya chama cha siasa kupinga ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Mhe. Rais @SuluhuSamia, sidhani kama kupinga kule ni kauli ya chama, kwa tunavyofahamu tamko la chama linatokana na vikao vya chama" @BulenduDotto

"Kitendo cha chama cha siasa kupinga jambo ambalo hata hujalisoma, hujui nini kipo ndani yake, hili pekee ni tatizo kubwa. Kwani, hadi sasa taarifa iliyotolewa kwetu wananchi na wajumbe wa kikosi kazi ni muhtasari tu, unawezaje kusema ni mbaya na wananchi msiipokee" @DoyoHassan.
Takataka hii
 
Tatizizo kubwa ni kudhani kuwa CHADEMA inaq hatimiliki ya nembo "upinzani". Wasiposema wao au wakipingwa basi wapingaji ni tawi la CCM. Nchi nyingi, inaposhindikana kukliondoa chama tawala madarakani, huwa vyama vyote vya upinzani vinaungani na kufanya kazi pamoja. Lakini kwa uchu wa madaraka kama ilivyo CCM, CHADEMA inataka ifanye hiyo kazi peke yake itwae uongozi.

Ni muhimu CHADEMA ijue kuwa bila kufanya kazi na vyama vingine vya siasa na kuendelea kuvibeza hivyo vyma ndiyo furaha ya CCM. Pasipo upinzani kufanya kazi pamoja na kudhani kuwa CHADEMA peke yake itatoboa, ni ndoto za mchana.

CHADEMA inazidiwa kete na CCM, maana CCM siku zote inaombea mfarakano kwenye upinzani. Katika vyama vyote CUF kilikuwa chama pekee kilichokuwa na nguvu kubwa hasa kule Zanzibar. Ilichokifanya CCM kila mtu anajuwa, sasa CUF ni karibu marehemu. CCM pia imekuwa ikiichakaza CHADEMA mdogomdogo. Migogoro mingi ndani ya CHADEMA, kama vile kuondoka/kufukuza kwa Zuberi na wengineo amao walikijenga CHADEMA haukosi mkono wa CCM. Lakini CHADEMA hili hawalioni. Wao kila kukicha ni kutaka kujiona ndiyo upinzani pekee na hivyo vyama vingine havina kitu.

Nafikiri tatizo kubwa ni uroho wa madaraka na kujitakia misifa. CHADEMA wanateka ikiwezekana washinde kura na washike nchi peke yao, maana wakiungana ukipatikana ushindi, inabidi wagawane vyeo. Ni hatari kuwategemea wanasiasa wachache na kuwaabudu kama Mungu, kudhani peke yao ndiyo wataleta mafanikio. Acheni kubeza vyama vingine. Kaeni navyo mpange mikakati ya kuiondoa CCM kwenye madaraka, lakini hii ya kufikiria CHADEMA pekee itafanikiwa ni ndoto. Sana saana mtaishia kupata ruzuku na kulipana mishahara, lakini kushika nchi hamtaweza bila kushirikiana na vyama vingine vya upinzani.

Kweli CHADEMA ni tishio aliongea Mbowe kuhusu tozo Mwigulu akajitokeza kujibu , Sasa kaongea mnyika kidogo vyama 14 ikiwemo na CCM vimejitokeza kujibu.

Na Sasa CHADEMA imetangaza kufanya mikutano ya hadhara nchi nzima nadhani IGP lazima atoke kujibu mapigo na kutoa vitisho.
 
CDM kwa aina yao ya siasa ndio kinaifanya CCM isiweze kulala, na kwa kiasi kikubwa kinaifanya CCM izidi kutumia vyombo vya dola, maana nje ya vyombo vya ni lazima ipotee kama KANU ya Kenya. Ni Mbowe tu alizengua kwa kwenda ikulu kupoteza muda.

Mbowe alizingua Sana. Alikuwa hana Cha kupoteza umekaa rumande karibia miezi Saba bila kosa unaendaje kuongea na mama Samiah aliyekutangaza kuwa ni gaidi, tena BBC. Angeendeleza harakati Leo mambo yangekuwa tofauti. Wamemwachia mama kila kitu ataangalia kwa jicho la tatu.
 
22 October 2022

CHADEMA WAREJEA RIPOTI YA JAJI WARIOBA SIKU CHACHE BAADA YA KIKOSI KAZI KUKABIDHI MAPENDEKEZO YAKE


Source: chadema media
 
Mbowe alizingua Sana. Alikuwa hana Cha kupoteza umekaa rumande karibia miezi Saba bila kosa unaendaje kuongea na mama Samiah aliyekutangaza kuwa ni gaidi, tena BBC. Angeendeleza harakati Leo mambo yangekuwa tofauti. Wamemwachia mama kila kitu ataangalia kwa jicho la tatu.

Ndio maana huwa nasisitiza Mbowe asistaafu siasa bali apumzike kwenye nafasi ya uenyekiti. Kwa mtu wa umri na manyanyaso wanayoweza kupata viongozi wa chama kikubwa hivyo, ni vyema akapisha mwenye mwili wa kumudu shuluba, kuliko kujiangusha ndani ya 18 ukitegemea kupata penalti.
 
Leo wataongea na vyombo vya Habari.
=================
Hotuba nzima ilikuwa ni kumjibu Mnyika na CHADEMA badala ya kuzungumzia ripoti ya Kikosi Kazi.

View attachment 2395271

"Tumesikiliza taarifa ya @ChademaTz ikielezea kupinga taarifa ya kikosi kazi, tunachoweza kusema kwa sasa, CHADEMA wamejawa na ubinafsi, choyo na wivu mkubwa kuona Tanzania ikiwa kwenye maridhiano huku wao wakiwa nje ya mchakato wa kupatikana kwa maridhiano hayo" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Mhe. Rais @SuluhuSamia amesema wazi kuwa maoni sio amri kwa serikali, wapo wanaokosoa kauli hiyo, nani aliyekwambia maoni ni amri, maoni yanakuwa amri baada ya kutungiwa kanuni na sheria" @DoyoHassan, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama vya Siasa nchini

"Kimsingi tumeshangazwa na viongozi wa kisiasa na moja ya chama cha siasa kupinga ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Mhe. Rais @SuluhuSamia, sidhani kama kupinga kule ni kauli ya chama, kwa tunavyofahamu tamko la chama linatokana na vikao vya chama" @BulenduDotto

"Kitendo cha chama cha siasa kupinga jambo ambalo hata hujalisoma, hujui nini kipo ndani yake, hili pekee ni tatizo kubwa. Kwani, hadi sasa taarifa iliyotolewa kwetu wananchi na wajumbe wa kikosi kazi ni muhtasari tu, unawezaje kusema ni mbaya na wananchi msiipokee" @DoyoHassan.
Haya sasa, hawa nao wanataka wawe wanapewa RUZUKU!

Kodi za wavuja jasho wa nchi hii, kwa akili mbovu kama hizi?
 
Back
Top Bottom