Mwaka 1988 Chakachaka alipiga show Makondeko Kibamba kiingilio kilikuwa 100,000


Matajiri wengi wakubwa Tanzania waliibuka kwa Mzee Mwinyi, wengine wakaja kupata pesa kwa kikwete utawala wa marais wengine pesa haikuepo, enzi za Mwinyi ndio watu walikula bata Mtu akitoa mzigo zanzibar akifika Dar anakuta watu hadi wazimbabwe wanasubiri, dili za magendo zikazaliwa kipindi hicho lakini utawala wa mwinyi ndio ulizaa hadi matapeli wakubwa hadi strong room na wazee wa bandari ilikua kwa mwinyi na mkapa kidogo,
 
Kwenye huo ukumbi kulikuwa na section inaitwa Mbinguni hall. Ni kama sehemu ya VIP hivi!
 
Hivi Wahaya walitapeliwa kipindi cha Mwinyi, na ile Bijampora mitaa ya Magomeni. Wahaya hoyeeee
 
nikuulize swali la kizushi kama wewe kweli mtoto wa mjini, Mgahawa wa chai wenye miaka mingi sana hapo dar unaujua ulipo na unaitwa jina gani na una miaka mingapi sasa?
Mi sio mtoto wa mjini🤣🤣🤣🤣🤣
Niko zangu uyole huku
 
[mention]Malila [/mention] na [mention]tbjlj [/mention] Michael Jackson hakupata kutumbuiza lakini mwaka 1992 alitembelea nchi nne za Africa kwa ziara binafsi ambapo alitembelea ivorycoast, Kenya na Tanzania na nchi nyingine nimesahau, kuja Tanzania ilikua Rais mwinyi anataka MJ aende akapige picha serengeti na mlima kilimanjaro ili wazitumie kwenda kutangaza utalii duniani huko, lakini dili haikufika mwisho na nakumbuka aliondoka Tanzania kurudi kenya ambako hakukaa akaenda london na ilikuja kufahamika baadae kua meneja wake alimpatia dili nyingine kubwa huko hivo ikaishia tu Rais mwinyi kupiga picha na MJ

 
nimegundua jamaa ni mshamba proper.
hawa ndio wale watu ambao mioyo yao imejaa chuki dhidi ya watu waliowazidi maisha.
 
Mi sio mtoto wa mjini[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Niko zangu uyole huku

Tupe story za city pub na mbeya pazuri na ueleze bata hua likoje anzia uyole, mbalizi, iyunga pale breakpoint, mafiati pale carnival, sae pub, au tueleze hata viwanja vipya vya mama john, sisi hapa ni story tu hatuna maneno na mtu
 
Kuhusu ''dala dala''. Magari yaliitwa daladala kwa sababu yalikuwa yanachaji sh. 5 ambayo ilikuwa ni ile sarafu ya pembe iliyokuwa inaitwa dala. Miaka hiyo senti 20 ilikuwa inaitwa ''mbuni'' sh 1 ikiitwa ''mwenge'' sh 5 ndiyo iliitwa ''dala''. Kuna magari yaliyokuwa yanajiibia kubeba abiria wakifika kituoni wanasema ''dala dala, dala dala''', yaani sh tano, sh tano sh tano
 
Nimeshangaa sana kijana alitaka kupotosha eti show ya Michael Jackson
 
Nimemtajia kidimbwi na matumizi yake maana najua kama yupo seriuos anaweza kwenda kuhakikisha mwenyewe kidimbwi pa kihuni flan
Huko Element mbali sana anaweza asipate acces ya kufika.
Mnabisha na wanafunzi wa shule wanajua nini? Wanadhani kama hawana fedha basi kila mtu hana! Kuna watu wanatumia siyo mchezo.
 

Uko sahihi kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…