Mwalimu atelekeza kazi baada ya malipo ya mshahara wa Tsh 34,000 kwa mwezi

Mwalimu atelekeza kazi baada ya malipo ya mshahara wa Tsh 34,000 kwa mwezi

Kumbuka huyu mwalimu alikuwa na madeni lukuki, kabla ya adhabu hiyo alikuwa na makato mengi.

Kazi ya ualimu ina laana, maana Walimu wengi wanaishi maisha magumu.
Wa zamani sio siku hizi.
Graduate anavuta sio chini ya laki 8 akiwa na masters anavuta 1.8.
Ukipata Kazi ya ualimu omba vijijini life is simple Hakuna kufatiliana baada ya Kazi piga ujasilimali.
Timiza wajibu wako wasome wasisome shauri yao na wazazi wao ukijifanya unawafatilia fatilia Ili wasome watakuroga.
Anaetaka kusoma mpe ushirikiano.
Wikiendi kuwa bize kwenye mishe zako.
 
Huyo Mwalimu ni sahihi alivyotendwa KILA Kazi Ina taratibu zake ukiacha wengine wanajaza nafasi.
Pia KILA mmoja anayo njia yake ya kutoka afanye ubarmaid kwa malengo Ili aje amiliki bar mbeleni.
 
Watanzania wengi tunapenda sana kukopakopa bila sababu maalum! Sanasana sababu ya ufahari.

Unakopa gari Harrier, mshahara hauzidi tshs 1m, unategemea nini?

Hapo ndiyo wiziwizi mpaka kwenye kahela ka chai!
 
Ni elfu thelathini na nne(34000).Mr.Ban huyu mwalimu ni graduate, ana degree kutoka UDSM.
Atunukiwe medali ya ushujaa wa kuishi kwa Sh. 1133.33 kwa mwezi na kuweza kukidhi mahitaji yake yote
 
Nimesikitishwa kupata habari kuhusu mwalimu anayefundisha shule ya sekondari Dunda iliyopo Bagamoyo mkoa wa Pwani kukimbia kazi ya ualimu baada ya kulipwa 34000 kwa mwezi.

Hii inatokana na adhabu ya kushushwa cheo na kulipwa nusu mshahara na Tume ya Utumishi wa Walimu kwa kosa la utoro kazini.

Mwalimu huyo wa kike aliishi maisha magumu sana hapo hapo shuleni ,alikosa mpaka hela ya kula ilimlazimu auze miwa na maembe aliyoyaokota hapo shuleni ili apate pesa ya kula.

Uzalendo ukamshinda baada ya mazingira magumu ya kazi aliamua kuondoka kazini bila ya taarifa kwa muajiri.

Habari nilizozipata mwalimu huyo yupo Mlandizi akifanya kazi ya kuhudumia wateja bar.

TSC mnapotoa adhabu ya kupunguza mishahara kwa walimu mzingatie iwapo kama mtuhumiwa ana mikopo benki, isitoshe adhabu ya kupunguza mshahara ni ya kikatili maana mshahara wenyewe hautoshi hapo hapo mnaupunguza.

Habari nilizozipata huyu mwalimu alikuwa na madeni benki na taasisi za fedha hapo Bagamoyo.

Kutokana na mazingira magumu ya kazi mwalimu huyo kaamua kutelekeza kazi yake.
huo mshahara mbona ni mkubwa sana kwa wenye masters na degree wasio na ajira wanaopuyanga mitaani.

Angetuliza tuu matako hapohapo.
 
Kumbuka huyu mwalimu alikuwa na madeni lukuki, kabla ya adhabu hiyo alikuwa na makato mengi.

Kazi ya ualimu ina laana, maana Walimu wengi wanaishi maisha magumu.
Madeni aliyatengeneza kwa kuzingatia kipo chanzo cha kipato ambacho ni mshahara kutokana na kazi yake ya ualimu kama alikosa nidhamu wangefanyeje.....TSC walimpatia adhabu ya kumshusha cheo baada ya maonyo kadhaa pia kwa kuzingatia maadili ya viongozi/watumishi wa Umma....watanzania tusiwe wanaharakati kwa kila jambo tuziache mamlaka zifanye kazi zake..

Sent from my EVA-L19 using JamiiForums mobile app
 
Ina Maana huo mshahara anakatwa zaidi ya moja ya tatu???hata kama adhabu ya makato ya nusu mshahara haiwezi kufika 34000|= kwa mfumo wa moja ya tatu!!
Taasisi za mikopo zipo nyingi na haziko integrated, mkopaji kila eneo huchukua kwa wakati wake. Kuitekeleza sheria ya kuachiwa ⅓ ya mshahara inakuwa ngumu.
 
Kuna mambo katika nchi hii yanatokea huyajui.

Nimepata kisa cha kusikitisha cha mwalimu wa shule ya sekondari Dunda iliyopo Bagamoyo, Pwani kulipwa mshahara wa elfu thelathini na nne (34,000) Tsh baada ya kupewa adhabu na Tume ya Utumishi wa Walimu TSC-Bagamoyo.

Mwalimu huyu amepewa adhabu ya kupunguziwa mshahara wake kutokana na kosa la utoro kazini.

Mwalimu huyu alijitolea sana kulitumikia Taifa hili zaidi ya miaka 20, akiwa kada wa CCM.

Mwalimu huyu aliishi maisha magumu sana kwa mshahara wa 34000 kwa mwezi hali iliyomlazimu atelekeze kazi yake bila kupenda kwani alikosa mpaka pesa ya kujikimu na maisha.

Alishinda na njaa kazini, alikosa mpaka nauli, ilimlazimu kutembea kwa miguu kutoka shule ya sekondari Dunda mpaka Kaole nyumbani kwake takribani ya km.10.

Mume wake kamtelekeza na watoto watatu, maisha ya mwalimu huyu ni magumu mno.

Mh.Rais, msaidie mwalimu huyu kwani ni kada mkubwa wa CCM wilaya ya Bagamoyo.
Hii stori ni ya kufikirika na haina hata chembe ya uhalisia. Nahisi ina lengo tu la kuwajaza watu upepo ili watokwe na mapovu!

Naomba niwe tu wa mwisho kuiamini. Maana ina maswali mengi kuliko majibu.
 
Elfu 34 tu, mbona hatari, mimi na net ya 4.6m bado haitoshi.
 
baadae atakapopata kazi nyingine serikalini kurejea kwenye utumishi ndo atajua hajui yaani. mchalato ni mgumu sanaaa. Ila hii ngozi nyeusi tuko na roho mbaya sana tunafikiria zaidi kukwamishana kuliko kusaidiana
Data base ya watumishi wa umma ni moja.
Unapotoroka kazi, kupata kazi labda ughushi kila kitu, jambo ambalo ni gumu.

Ukiona mtumishi anatoroka, elewa katamani ujasiria mali ama kazi za mashirika binafsi.
 
😂😂😂😂 mwalimu bhana😂😂😂😂😂 halafu 2025 utamkuta anabebana na masanduku ya kura za wizi ili aisaidie ccm ipate ushindi.
 
Wa zamani sio siku hizi.
Graduate anavuta sio chini ya laki 8 akiwa na masters anavuta 1.8.
Ukipata Kazi ya ualimu omba vijijini life is simple Hakuna kufatiliana baada ya Kazi piga ujasilimali.
Timiza wajibu wako wasome wasisome shauri yao na wazazi wao ukijifanya unawafatilia fatilia Ili wasome watakuroga.
Anaetaka kusoma mpe ushirikiano.
Wikiendi kuwa bize kwenye mishe zako.
Ushauri Bora kabisa huu wa mwaka
 
Back
Top Bottom