Mwalimu Japhet Maganga wa CWT hafukuziki? Jibu hili hapa

Mwalimu Japhet Maganga wa CWT hafukuziki? Jibu hili hapa

Kukata mirija ya wanasiasa kuendea kufyonza mihela ya CWT ndicho kinachomponza Maganga. Ndio maana serikali inaingilia sana CWT hadi kwenye mambo ya ndan kabisa ya CWT. Majuzi wametuma polisi kuvamia mkutano wa CWT kuzuia uchaguzi baada ya kuhisi kibaraka wao huenda asipate nafasi ya kuongoza. Nchi ngumu sana hii
Uko sahihi sana Mkuu...
 
Nimeshangaa jinsi suala la Katibu Mkuu wa CWT mwalimu Japhet Maganga linavyofanyiwa siasa badala ya kuchukuliwa kama suala la kiutumishi. Kwanza sio jambo la kawaida mtumishi wa umma kufukuzwa kazi kwa mujibu sheria na jambo hilo kugeuzwa kuwa suala la umma.
rikali inaweweseka kutafuta huruma mitandaoni.

Kuna shida mahali sio bure. Let us wait and see what gona happen.
Huyo ndo mama samia anayeabudiwa na akina Lucas mwashambwa ChoiceVariable na chawa wenzao.

Hivyo ndivyo anavyotatua matatizo yake. Amri na imla
 
Ndg, tpaul na wasomaji wengine.
Mie naujua mgogoro huu wa CWT nje ndani. Kufupisha ni kwamba huu mgogoro hauwezi kuisha kamwe hadi siku Mh. Jenista Mhagama, atakapopoteza uwaziri wake.
Huyu ndiye injinia wa kuanzia uteuzi wa hawa kina maganga kwenda kuwa wakuu wa wilaya.
Katika hili hata mh. Rais Samia nakiri ni majina tu aliletewa na wala hakuwajua.

Mhagama na aliyekuwa Rais wa CWT aliyefungwa kwa matumizi mabaya ya ofisi, ambae aliwahi kuhudumu ktk chama cha walimu, na ndio kisa cha mbivu na mbichi huko CWT.

Kiufupi Mhagama na mkubwa wake flani walikuwa kwenye payroll ya CWT, hawa kina maganga waliwatoa.

Stori ni ndefu. Ipo siku nitaiandika yote.

Ogopa sana mirija ya fedha na siasa za ovyo.
Kwa hiyo kama Waziri anajipa mamlaka ya kufanya atakavyo. Tuna rais wa nini sasa?

Nikiwaambia tuna rais dhaifu mno wala sikosei. Maelezo yako yamethibitisha yenyewe
 
yeye si hodari sana, si mwamba sana, tunachoomba asijinyonge tu kwa stress, lakini Lazima ashike adabu na anyooke vizur, huu ni mwanzo tu, atapata tabu sana kwenye mafao
Mafao ya wapi sasa?

Kama hataki uteuzi wa bibi yenu huyo na kama hataki kurudi kazini huko Temeke kuendelea kula vumbi la chaki maana yake hata hayo mafao chukueni, yupo tayari na amejiandaa kwa hilo..

Unafikiri yeye ni kama wewe ambaye ili mkono uende kinywani na watoto waende chooni ni mpaka ulambe miguu ya maboss wako hapo Lumumba..?

CWT ni taasisi huru isiyofungamana moja kwa moja na serikali. Kama ameamua kufanya kazi na CWT, let him go na hao ndio watamlipa mafao yake..!
 
Nimeshangaa jinsi suala la Katibu Mkuu wa CWT mwalimu Japhet Maganga linavyofanyiwa siasa badala ya kuchukuliwa kama suala la kiutumishi. Kwanza sio jambo la kawaida mtumishi wa umma kufukuzwa kazi kwa mujibu sheria na jambo hilo kugeuzwa kuwa suala la umma.

Mwalimu Maganga kateuliwa kuwa DC amegoma kwenda kuapishwa. Ameomba aongezewe kibali cha kuendelea kutumikia CWT, serikali imegoma kumuongezea muda licha ya kwamba siku za nyuma serikali imekuwa ikimuongezea muda bila tatizo lolote. Kana kwamba hilo halitoshi, barua ya kukataliwa kuongezew muda imewekwa kwenye public domain na pia barua ya kuombwa kurudi kazini imekuwa public.

Nimebaki najiuliza: ni watumishi wangapi wamefukuzwa kimyakimya bila serikali kuutangaziia umma? Kwanini hili suala binasi linageuzwa kuwa la umma? Je, serikali hawaoni kuwa tayari wamevunja sheria kwa kuingilia faragha ya mwalimu Maganga kuhusu masuala ya kazi na kwamba anaweza kuwashtaki mahakamani wakamlipa mabilioni ya shilingi kwa kumchafua na kudhalilisha utu wake hadharani?

Mtu kukataa kuwa chawa ni utashi wake binafsi. Maganga aliona future yake haipo kwenye siasa ndio maana akaamua kugomea nafasi ya uteuzi. Kukataa uteuzi ndio iwe nongwa kiasi hiki? Acha hizo bhana. Serikali inajidhalilisha sana kwa kuendelea kukomalia jambo hili bila kufuata sheria.

Sheria za kazi zipo wazi. Mtu alitakiwa kuripoti kazini tarehe 1 lakini hadi leo tarehe 18 hajafanya hivyo na bado serikali inaweweseka mitandaoni kumtaja kama ni mtumishi wa umma wa Manispaa ya Temeke. Sheria inasema mtumishi asiporipoti kazi kwa siku 3 mfululizo bila sababu wala ruhusa kutoka kwa mwajiri anakuwa amejifuta kazi mwenyewe. Inakuwaje maganga anakuwa nje ya kituo cha kazi kwa siku 18 bado serikali inahangaika naye? Au mtu akiteuliwa kuwa DC akagoma sheria za kazi kwake zinatumika tofauti na watumishi wengine? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Ukifikiria kwa undani utagundua nia ya serikali kuwateua viongozi wakuu wa CWT kuwa wakuu wa wilaya haikuwa bahati mbaya. Watakuwa walifanya hivyo kwa nia ovu baada ya kuona hawa viongozi labda wamekuwa vikwazo kwao kujipenyeza CWT kuchota mapesa kwa ajili ya kujipanga na uchaguzi mkuu 2025 na mambo mengine ndani ya chama. Ndipo Maganga na wenzake wakashtukia ishu na kugoma. Baada ya kugoma kuondoka kupisha mwanya wa uchotaji wa hela, serikali imeamua kumkomesha kwa kutomuongezea muda wa kuendelea kubaki CWT. Hii ndio kete ya mwisho kwa serikali kupata nafasi kuingia CWT kujichotea mapesa ya bwerere.

Kwa hali ilivyo, serikali watakuwa wanatafuta sababu ya kumkomoa Maganga kwa kuwa amekuwa kikwazo kwao kutimiza kutimiza jambo lao. Na huenda kuna mahali serikali imejichanganya, hivyo Maganga anasubiri wamfukuze kazi halafu awashike pumb* washindwe kuchomoa. Bila shaka atakuwa anasubiri wautangazie umma kuwa wamemfuta kazi kisha akimbilie mahakamani kuwakamua mamilioni ya fidia. Usidhani yeye ni bwege agome kwenda kazini tangu tarehe 1 hadi leo terehe 18 lakini bado serikali inaweweseka kutafuta huruma mitandaoni.

Kuna shida mahali sio bure. Let us wait and see what gona happen.
Kwani hizo pesa za bwerere pale CWT ambazo serikali inataka Kwenda kuzichota ni za nani hasa?Maganga au serikali?maana nimeshtuka sana kwamba kumbe CWT kuna pesa za bwerere, kumbe basi ndio maana hata akina Janeth Maganga wamegomea teuzi kwa maana watakua wameondolewa kwenye mzinga wa asali ya bwerere,maana CWT ni sehemu Salama sana ya kujichotea fedha za walimu za bwerere.WALIMU KWELI FEDHA ZENU ZINATAFUNWA NA WAJANJA WACHACHE.VP HABARI YA KUAMKA KWA WALIMU,Sijui tuwaachie walimu wenyewe.
 
nadhani hata ingekua wewe katika hali ya kawaida nakuomba jambo unanipa.
Ila wewe ukija kuniomba mie nakunyima tena kwa makusudi kutokana na raha na faida ninazo pata kwenye kile ulichonipa wewe.

Kesho nikija kukuomba tena utanipa kweli? Ikiwa ndio basi wew ni binadamu wa kipekee Sana.

It is simple,
Msingi wa kazi ya ukatibu ukuu CWT ni ualimu. Na ili upate hiyo kazi ni Lazima uwe Mwalimu na unaomba ruhusa ya kuazimwa ikimaamisha hata mambo ikiharibika huko CWT uhakika wa ajira yako ya msingi uko palepale.

umeazimwa mara ya kwanza umekubaliwa, umeazimwa mara ya pili umekubaliwa, mara ya tatu umekataliwa ndio imekua nongwa?

Mtumishi wa serikali ni sharti awe mzalendo na tayari kuutumikia umma wa waTz kadiri inavyoonekana ya serikali inavyoona inafaa, sio kadiri ya tamaa na kiburi yako.
Huyo Janeth anataka Ofisi ya menejimenti ya utumishi wa umma imsikilize yy kama ilivyofanya toka barua ya kwanza ila yeye hayupo tayari kuisikiliza ofisi kuu ya Utumishi.
 
umeazimwa mara ya kwanza umekubaliwa, umeazimwa mara ya pili umekubaliwa, mara ya tatu umekataliwa ndio imekua nongwa?
Kwanini wakati huu alipokataa UCHAWA ndipo anyimwe ruhusa wakati miaka ya nyuma alikuwa anaongezewa muda bila kikwazo? Huoni kwamba kuna walakini hapo?
 
Mafao ya wapi sasa?

Kama hataki uteuzi wa bibi yenu huyo na kama hataki kurudi kazini huko Temeke kuendelea kula vumbi la chaki maana yake hata hayo mafao chukueni, yupo tayari na amejiandaa kwa hilo..

Unafikiri yeye ni kama wewe ambaye ili mkono uende kinywani na watoto waende chooni ni mpaka ulambe miguu ya maboss wako hapo Lumumba..?

CWT ni taasisi huru isiyofungamana moja kwa moja na serikali. Kama ameamua kufanya kazi na CWT, let him go na hao ndio watamlipa mafao yake..!

nanaliu, si usemezane kwa polepole, fujo la nini sasa unileta huku

kwaihiyo huyo mujamaa yako, asingalikua Mwalimu, angelikua na sifa ya kua katibu mkuu wa CWT right?

ngoja nitumie na lugha hii labda utanielewa,

Msingi wa kua katibu mkuu wa CWT si ni Lazima uwe mwalimu?

na uhuru wa CWT uko upande gani au nayo ni kama chadema na ACT?
 
kweli humu Duniani kuna watu na viatu,
akiomba yeye ni sharti apewe tu eti ndio haki na hana shukran wala heshima kwa mamlaka, akiombwa yeye sasa, mabega juu hataki tena kwa mikogo kama yote,
akinyimwa sasa ilo shavu linavyofura kama chatu kameza sungura 🤓

sasa mtu kama huyu aliejaa uchoyo, tamaa na kiburi, aisee acha niishie hapo....
Huyo Janeth anataka Ofisi ya menejimenti ya utumishi wa umma imsikilize yy kama ilivyofanya toka barua ya kwanza ila yeye hayupo tayari kuisikiliza ofisi kuu ya Utumishi.
 
Mbona walimu wengi tu, kwanini wanalazimisha mwalimu asiyetaka kufundisha? Haya ni matumizi mabaya ya ofisi za umma. Kiongozi unapotumia wadhifa wako kuadhibu watu badala ya kutatua matatizo ya watu. Mwalimu humlipi mshahara, analipwa na CWT. Yeye anataka kuendelea kuwa huko, nyie hamtoi sababu ya kwanini mnataka arejee, mmegeuka miungu. Hamtaki tu, bila sababu yoyote.
Tumeambiwa aliomba kibali Utumishi,sasa mm na ww tujiulize Hv kibali huwa hakiishi ,mm naamini kibali kinaisha kulingana na muda uliopewa.JANETH hakuajiriwa CWT,waliomuajiri ndio walimpa kibali pale alipoomba kutumikia CWT,Kumbuka mwajiri mkuu ni serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na CWT sio mwajiri na kuigomea serikali iliyokupa kibali kwenda huko uliko ni kosa lingine,kama kibali kimeisha muda wake basi turudi tulipotokea ndio busara kuliko kuwa na kiburi kisicho na maana.Angeenda kutumikia CWT bila kibali kutoka Ofisi ya Utumishi kwa muda wote ambao amekuwa huko,ningewashangaa sana Utumishi kumtaka arudi kule alikokuwa ilhali hawakumuandikia kibali.Ni vema tukazingatia taratibu za Utumishi na tusi sikilize bush loyals ambao mwisho wa siku hawana cha kutusaidia.
 
Mimi nadhani serikali iko sahihi,hata sisi walimu huwa tunatumia mbinu hii,mwanafunzi anaweza kunigomea tukiwa wawili yakaisha kimya ila akinigomea darasani kukiwa na wanafunzi wanashuhudia au parade wanafunzi wote wanaona huyo lazima afukuzwe shule mbele ya parade huku wanafunzi wote wakiona ili iwe fundisho kwa wengine.

Huyo jamaa kagomea U-DC kwakuwa anapata hela nyingi za sisi walimu malofa ambazo twakatwa kila mwezi,hivyo naunga mkono huyo jamaa kushughulikiwa,ila nadhani sahihi kabisa ilikuwa ni kuishughulikia cwt ili ituachie huru walimu,can you imagine cwt wanachukua mfuko mmoja wa cement toka kwa salary yangu kila mwezi,cha kushangaza sina hata kiwanja,huku wao wakituna mashavu kama paka shume.


I hate #CWT
Mkuu huo mfuko wa sementi unaupoteza wewe mwenyewe kwa sababu ya kutojua haki zako. Hebu fanya hima umwandikie barua mwajiri wako ujitoe CWT. Hiki ni chama cha hiyari, mtu halazimishwi kujiunga au kuungwa kwa nguvu. CWT wanakata pesa zako isivyo halali na ukikomaa mahakamani watazitapika hela zote walizokukata tangu ulipoajiriwa. Hawa watu ni wahuni tu hawana lolote. Hebu soma document hii upate mwangaza kuhusu haki na wajibu wako wa kujiunga au kutojiunga na chama chochote. Pitia document hii ujielimishe.
 

Attachments

Back
Top Bottom