Mwamba alivyojimaliza mwenyewe baada ya kugundua kuwa watoto aliezaa na mkewe sio wa kwake

Uongo, tuanzie kwa damu, siyo lazima group yako iingiane na ya baba yako.

Hosp siyo wajinga pia, hata kama walivizia DNA wasingeongea chochote kwa baba. Damu wangemtoa ingetunzwa maabara mtoto angepatiwa damu nyingine.

Unatupanga kiboya boya sie watu wazima oops
 
Hapa ndipo nilikuwa napatafuta.
 
Kasema bunduki sio bastola.
Ak 47 inatoa kwa mpigo zote ukifyatua.
Hata Smg
Sasa mzee, kati ya kujiua na smg na ile mguu wa kuku (bastola ya kawaida) unadhani mleta chai alimaanisha nini.? Haina haja ya kuumiza kichwa, hapo alimaanisha mguu wa kuku.
 
Hili ndilo jibu sahihi kwa hii chai na umemaliza kila kitu.

Kingine sidhani kama mahospitalini wako rude kiasi hicho et lete baba halisi wa mtoto. Wale wamesomea psychology na wanatambua utapeli wa mapenzi. Hawawezi kuvunja ndoa kirahisi hivyo. Ata angepima DNA wangemwambia ni mtoto wake unless awe na sababu maalumu yenye wito wa mahakama kufanya hivyo au awe anajuana na daktari tena kwa kumpa hela nyingi huku akimuahid kulinda hiyo siri ya kupima DNA bila ruhusa ya mahakama.

Sio kirahisi hivo ni jambo linaloweza kumfunga daktari ikiwemo kumfutia leseni ya udaktari.
 
Watu hawajasoma biology...huwa wananikera sana mtu ameshupaza shingo eti ukikuta mtt sio group ya damu ya mzazi sio wake...hajui mfano baba ana A positive mama ana AB,,,mtoto anaweza akatoka na group lake kabisa...
 
Risasi tano kichwani alijipigaje?
Automatically hiyo mkuu, haina ngoja ngoja wala mswalie mtume. Ukiset na kubonyeza tu basi mfululizo kama njugu vile.
 
sema story umeongeza chumvi sana ila pole kwa jamaa
Yah si unajua jambo kubwa kama hilo lazima mtu uhadithie kwa mihemko matokeo yake chumvi inazidi kidogo.
Ila kikubwa nimeeleweka mkuu.
 
Nimecheka mpka nimelia eti damu ya mtoto haikuendana na ya baba ? Mara risasi tano kichwani .

Kajamaa kaongo hadi raha alafu kama kana degree basi ni ya masomo ya sanaa maana hata mambo ya damu yanakapiga chenga sana

Wewe kajamaa 6 Pack siogopi uto tumbavu twako nitakukung'uta usituone wajinga bwana

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Storie ina walakini mwingi,kutofautiana damu na mzazi mmoja haina maana mtoto sio wako,mfano kama mzazi mmoja ana group A-/+ na mwingine O-/+,...upo uwezekano mtoto kuzaliwa na group A au O,..sasa huwez sema huyo mtoto zio wako kwa sababu ana group la damu la moja kati ya hayo mawili...kujirizisha,pima DNA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…