Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Huu ni Zaidi ya Upendo ndugu zanguni Watanzania.Haijawahi kutokea hapa Nchini pengine hata ndani ya Bara zima la Afrika kwa Mwanasiasa kupendwa ,kukubalika,kuungwa mkono,kusikilizwa ,kufuatwa ,kubeba na kukusanya watu Wengi kiasi hiki Utafikiri watu wanavutwa kwa sumaku kutoka majumbani Mwao.
Embu niambieni ni Mwanasiasa yupi hapa Nchini kwenye uwezo na ushawishi wa kuwaleta pamoja watu kumsikiliza yeye kwa wingi kiasi hicho? Nani mwenye uwezo huu? Nani mwenye ubavu,nani mwenye nguvu za aina hiyo? Nani anapendwa Nchi hii kumzidi huyu Mama mwenye moyo wa upendo, ukarimu, uzalendo,unyenyekevu na upole?
Nani anaweza kuwafanya watu wengi kiasi hiki wakaacha shughuli zao kwa ajili ya kwenda kumsikiliza yeye tu? Zaidi ya Rais Samia ni Nani mwingine anaweza wafanya watu wakimbie mbio kuwahi nafasi viwanjani na kufurika mpaka kukosa nafasi ya kupita sisiminzii ili tu wamsikilize?
Rais Samia kwa hakika siyo mtu wa kawaida ,ni mtu na nusu ,ni nyota kwelikweli,ni nuru popote pawapo na giza.ni tumaini popote pawapo na kukata tamaa. Ni vipi unaweza mzuia Mama huyu kugombea Urais? Ni vipi unaweza mshinda mama huyu kushinda kwa kishindo? Utamzuia kupitia nini? Kwa njia ipi? Kwa sera zipi? Kwa kigezo kipi unaweza mzuia Mama huyu Chaguo la Mungu kurejea ikulu kwa awamu ya pili hapo Mwakani? Ni vipi unaweza kata jina la huyu Mama kwenye Urais ndani ya CCM? Nani atakuelewa? Nani atakukubalia na kunyamaza? Huoni itasababisha machafuko na vurugu Nchini?
Hivi bado hamjatambua ya kuwa huyu Mama ni Chaguo la Mungu Mwenyewe? Hamjatambua bado kuwa kainuliwa na mkono wa Mungu na hata sasa anaongoza Nchi kwa kibali cha Mungu Mwenyewe? Mnataka mpewe ishara gani mpate kuamini?muoneshwe nini na kitu gani na picha zipi mpate kuamini enyi watanzania?
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Huu ni Zaidi ya Upendo ndugu zanguni Watanzania.Haijawahi kutokea hapa Nchini pengine hata ndani ya Bara zima la Afrika kwa Mwanasiasa kupendwa ,kukubalika,kuungwa mkono,kusikilizwa ,kufuatwa ,kubeba na kukusanya watu Wengi kiasi hiki Utafikiri watu wanavutwa kwa sumaku kutoka majumbani Mwao.
Embu niambieni ni Mwanasiasa yupi hapa Nchini kwenye uwezo na ushawishi wa kuwaleta pamoja watu kumsikiliza yeye kwa wingi kiasi hicho? Nani mwenye uwezo huu? Nani mwenye ubavu,nani mwenye nguvu za aina hiyo? Nani anapendwa Nchi hii kumzidi huyu Mama mwenye moyo wa upendo, ukarimu, uzalendo,unyenyekevu na upole?
Nani anaweza kuwafanya watu wengi kiasi hiki wakaacha shughuli zao kwa ajili ya kwenda kumsikiliza yeye tu? Zaidi ya Rais Samia ni Nani mwingine anaweza wafanya watu wakimbie mbio kuwahi nafasi viwanjani na kufurika mpaka kukosa nafasi ya kupita sisiminzii ili tu wamsikilize?
Rais Samia kwa hakika siyo mtu wa kawaida ,ni mtu na nusu ,ni nyota kwelikweli,ni nuru popote pawapo na giza.ni tumaini popote pawapo na kukata tamaa. Ni vipi unaweza mzuia Mama huyu kugombea Urais? Ni vipi unaweza mshinda mama huyu kushinda kwa kishindo? Utamzuia kupitia nini? Kwa njia ipi? Kwa sera zipi? Kwa kigezo kipi unaweza mzuia Mama huyu Chaguo la Mungu kurejea ikulu kwa awamu ya pili hapo Mwakani? Ni vipi unaweza kata jina la huyu Mama kwenye Urais ndani ya CCM? Nani atakuelewa? Nani atakukubalia na kunyamaza? Huoni itasababisha machafuko na vurugu Nchini?
Hivi bado hamjatambua ya kuwa huyu Mama ni Chaguo la Mungu Mwenyewe? Hamjatambua bado kuwa kainuliwa na mkono wa Mungu na hata sasa anaongoza Nchi kwa kibali cha Mungu Mwenyewe? Mnataka mpewe ishara gani mpate kuamini?muoneshwe nini na kitu gani na picha zipi mpate kuamini enyi watanzania?
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.