Mwanafunzi mmoja afariki wengine hali tete wilayani Kilolo, Iringa baada ya kula futari ya msaada

Mwanafunzi mmoja afariki wengine hali tete wilayani Kilolo, Iringa baada ya kula futari ya msaada

Hii imetokea katika shule ya Sekondari Kilolo iliyopo katika Kijiji cha Luganga, kata ya Mtitu Wilaya ya Kilolo Mkoa wa Iringa.

Tukio hilo limetokea jana. Wanafunzi 7 wa kiislam waliokuwa wamefunga kwenye mfungo wa Ramadhani wamekumbana na kadhia ya kutapika na kuharisha kunakoelezwa kunatokana na Chakula cha msaada walichopewa msikitini siku ya juzi.

Tukio hili limesababisha mtoto mmoja wa kike kufariki jana huku wengine wawili wakiwa na hali mbaya na waliletwa hapa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa baada ya kusemekana kupewa chakula cha msaada kilochogawiwa juzi kwenye msikiti uliopo Kijiji cha Luganga kama msaada kwa wenzetu waliofunga toka taasisi moja ya jumuia ya kiislam.

Kati ya wanafunzi saba, mmoja alifariki. Wawili tuliwapokea hapa Hospitali wakiwa na hali mbaya na wanne wanaendelea vizuri na walibaki kule Hospitali ya Wilaya ya Kilolo

Hawa wawili nitaleta taarifa zao baada ya kufuatilia maendeleo yao ila hadi jana hali ilikiwa mbaya.

Pole kwa familia kwa kupoteza binti yao. Binti huyo alitoka Dar na kuja kusoma huku Iringa alipokutana na hiyo mauti. Mungu ampe pumziko jema binti yetu. Tunawaombea wengine hususani hawa wawili Mungu awaponye na kuwatoa katika shimo la mauti.
Epuka zawadi ya nguo kutoka kwa Mtu alie UCHI
 
Vyakula vilikuwa vimepikwa au bado?
Na kama vimepikwa vipi kuhusu uhifadhi wake?
Walikula wanafunzi Saba Tu au watu wengi?
Waliodhurika ni wanafunzi Tu au na watu wa kawaida?
 
Vyakula vilikuwa vimepikwa au bado?
Na kama vimepikwa vipi kuhusu uhifadhi wake?
Walikula wanafunzi Saba Tu au watu wengi?
Waliodhurika ni wanafunzi Tu au na watu wa kawaida?
Vimepikwa msikitini na kupelekwa shuleni. Walipewa Tambi, Viazi na Maziwa. Waliokula zaidi ya 20 kati ya hao, 7 walikuwa na hali mbaya. Huyo aliyekufa keshasafirishwa kuja dar kwa wazazi wake ambao walifika Hospitali leo. Wengine hali zao zimetangamaa
 
Ukitoka nduki kufanyia taarifa ya kusikia bila kuichakata kung'amua maswali na majibu muhimu unaweza ukajikuta unajidhalilisha mwenyewe.

Je walialikwa wanafunzi 7 pekee kula hiyo futari au walipewa wakajiandalie shuleni?

Wangapi walipewa msaada huo?

Wangapi wameripotiwa kupata kadhia hiyo zaidi ya wanafunzi hao 7?

Mtoa taarifa amehojiana na Imamu+Sheikh wa Msikiti kuhusiana huo msaada na kama kilipikwa hapo Msikitini na wengine wakala?

Umbali kutoka Msikiti hadi shuleni umekadiria?

Walianza kuugua pale pale Msikitini au walipofika shuleni?
Nilikiwa busy kidogo. Wanafunzi walienda msikitini pale kwa Shehe Ally Bakwa. Wakapewa Futari (Tambo, viazi na maziwa). Wakaenda kula shuleni umbali wa 1Km toka Msikitini hadi shuleni. Walienda wanafunzi zaidi ya 20. Hao wote waliathiriwa na hiyo futari ila 7 ndio walikiwa na halo mbaya. Kati ya saba 1 Msichana aliyetoka Dar ndio amefariki na wengine 2 wakapewa referral hadi hospital ya Rufaa Iringa.

Wengine waliobakia, wanaendelea vizuri na leo wameruhusiwa.

Kama alivyosema Fanuel Nyadwike ambaye aliwasiliana na JF, mabaki ya chakula yamechukuliwa ili kwenda kwa mkemia mkuu wa serikali kwa uchunguzi zaidi.
 
Vimepikwa msikitini na kupelekwa shuleni. Walipewa Tambi, Viazi na Maziwa. Waliokula zaidi ya 20 kati ya hao, 7 walikuwa na hali mbaya. Huyo aliyekufa keshasafirishwa kuja dar kwa wazazi wake ambao walifika Hospitali leo. Wengine hali zao zimetangamaa
Aisee...
Au labda mihogo ilikuwa na sumu?.
Mungu ampumzishe mahala pema mtoto.
 
Ingefaa kuitaja hiyo taasisi kwa manufaa ya shule zingine zisipokee msaada kutoka taasisi hiyo

Wataalamu wa sheria, je familia ya marehemu inaweza kuchukua hatua gani za kisheria dhidi ya taasisi iliyosababisha kifo hicho?
Taasisi imetoa msaada msikitini,wangeugua wote waliopewa msaada huko msikitini lakini wameugua wanafunzi tu,so lolote baya limetokea shule,nilipokua chuo,Kuna vijana wanne wakilala bweni moja,wawili waislam na wawili wakiristo, muislam mmoja akiiva Sana na mkiristo ambaye alikua akimchukia muislam mwingine ambaye alikua swala Tano,siku moja mkiristo yule akamshawishi muislam anayeiva nae wamtegee umeme kwenye maji watayomwaga chini yule muislam swala Tano,wakatega na kuondoka,yule mkiristo mwingine asiye na chuki akamshitua swala Tano kuhusu Hilo,ndiyo pona yake
 
Taarifa yake haijajitosheleza. Imekaa kishabiki. Alafu anaonekana ni mwalimu na hilo linatia wasiwasi labda kuna ushiriki wa wengine katika hilo tukio kama ni kweli.
Hapo vijana wamehujumiwa,kukomeshwa,Kuna chuki Sana taasisi za elimu
 
Unatoa taarifa kama nani? Una Mamlaka gani? Jenwengine huko msikitini waliokula hilo chakula wameugua pia?
Hili ndio swali hata mimi najiuliza
je chakula hicho walikula wanafunzi tu? yaani chakula kiliwe msikitini wale wanafunzi tu, hata hao walioleta hawakula! basi hapo kuna namna.
 
Asikia harufu ya ugaidi ngoja uchunguzi ufanyike..
 
Hivi vyakula vya ujumla ujumla pasipo umakini ni hatari sana.

Ndiyo maana watu wanakodi catering na kuletwa kikiwa tayari ,haya mambo ya kina mama mwajuma ndala ndefu kuchambua mchele na kupika ndiyo hao wanaweka sumu za mamba na kuteketeza jamii.
 
Screenshot_2024-03-17-18-52-17-796_com.instagram.android.jpg
 
Umekwenda mbali sana.Na unajieleza wewe ni nani.
Wanafunzi wa kiislamu..
kula futari..
Msikiti....
jumuiya ya kiislamu....
Mimi nina shaka huyo mtoto wewe umehusika kummaliza ili upate habari uipendayo.
Ww ulitaka aandike vipi? Kwamba ni wanaafunzi wa kikristo? Kwamba wamekula chakula kanisani? Kwamba huo msaada umetokewa na jumuiya ya wasabato?
Inferiority complex itawafanya muwe vichaa nyie watu.
 
Ww ulitaka aandike vipi? Kwamba ni wanaafunzi wa kikristo? Kwamba wamekula chakula kanisani? Kwamba huo msaada umetokewa na jumuiya ya wasabato?
Inferiority complex itawafanya muwe vichaa nyie watu.
Kilichotakiwa kuandikwa ni kuwa kuna wanafunzi wamekufa .inakisiwa walikula chakula chenye sumu.
Baada ya uchunguzi kufanyika na polisi kutoa ripoti ingefuata taarifa nyengine kuwa walidhuriwa na nini.
Yeye kwa haraka ameshajua kila kitu na hiyo ni kwa vile wanafunzi walikuwa ni waislamu na alihisi walikula futari ya msaada na kwamba ilitolewa na taasisi ya kiislamu.Ana ushahidi gani wa yote hayo.
 
Story Yako inatufundisha kwamba kila mmoja aheshimu Imani ya mwenzake ili dunia iwe sehemu salama kuishi.
Taasisi imetoa msaada msikitini,wangeugua wote waliopewa msaada huko msikitini lakini wameugua wanafunzi tu,so lolote baya limetokea shule,nilipokua chuo,Kuna vijana wanne wakilala bweni moja,wawili waislam na wawili wakiristo, muislam mmoja akiiva Sana na mkiristo ambaye alikua akimchukia muislam mwingine ambaye alikua swala Tano,siku moja mkiristo yule akamshawishi muislam anayeiva nae wamtegee umeme kwenye maji watayomwaga chini yule muislam swala Tano,wakatega na kuondoka,yule mkiristo mwingine asiye na chuki akamshitua swala Tano kuhusu Hilo,ndiyo pona yake
 
Kilichotakiwa kuandikwa ni kuwa kuna wanafunzi wamekufa .inakisiwa walikula chakula chenye sumu.
Baada ya uchunguzi kufanyika na polisi kutoa ripoti ingefuata taarifa nyengine kuwa walidhuriwa na nini.
Yeye kwa haraka ameshajua kila kitu na hiyo ni kwa vile wanafunzi walikuwa ni waislamu na alihisi walikula futari ya msaada na kwamba ilitolewa na taasisi ya kiislamu.Ana ushahidi gani wa yote hayo.
Kwan hayo yote aliyoyaandika ni kweli ama uongo?
 
Back
Top Bottom