Mwanamke anayechepuka ni hatari kwa uhai wa mume wake kuliko hata wauaji wa kutumia silaha

Hehehehhehe taratibu basi mama
 
Ni kumuacha tu mwanamke akianza uchepukaji hamna namna.
Unaweza kujitahidi kujua tatizo ni nini mpaka likatokea hilo ili na wewe liwe somo na ikiwezekana kusaidia ndoa isipagaranyike.
 
Mkuu nipo kwenye ndoa. Kosa la mke kuchepuka ni gumu kuvumilika kwa upande wangu na ninaomba Mwenyezi MUNGU lisitokee na likitokea nisijue.
Inakuaje pale inapotokea hivyo huku mmezaa watoto kama watatu!??
Mambo mengine Mungu na atuepushie mbali
 
Ndoa yako iko poa huku unapima watoto!! Haya bwana.

Huwezi elewa hili kwa kuwa wewe ni mwanamke, nyinyi mmepewa proof ya uhakika na mola kuwa mtoto ni wako, sisi inabidi tuwe na imani tuu, imagine that! Kitu kikubwa kama ku pass on DNA yako kwa miaka elfu na elfu ijayo eti uamini tuu maneno ya mke wako, kuwa huyu ni mwanao.

Sisemi kuwa tusiamini wenza wetu lakini, what if? Fedheha ya kuwa mume bwege ni kubwa kuliko lawama. Kwa hiyo mimi namuelewa sana Prof na kila mwanaume wa shoka lazima afanye DNA ya watoto wake, just because!
 
Pimeni tu, ila mkigundua sio wenu kuweni wapole tu mlee masna kitanda hakizai haramu. Mbona wenu huwa tunalea!! Hebu muwe na mioyo ya kupondeka.
 
Inakuaje pale inapotokea hivyo huku mmezaa watoto kama watatu!??
Mambo mengine Mungu na atuepushie mbali
Mkuu mimi nina hasira mbaya yenye kisasi na huwa inakaa muda mfupi lkn ina tabia ya kujiridiarudia. Kukaa naye ipo siku anaweza akaniudhi kwa jambo jingine halafu nikapata hasira ya kukumbuka alivochepuka nikamdhuru. Kwa usalama wangu na wake ni bora tukaachana kwa wema japo inauma kutengana but that is the price that should be paid. Mara nyingi mmoja wenu kuchepuka ndani ya ndoa ni kipimo tosha kuwa ndoa hiyo haikuwa na baraka za Mwenyezi MUNGU.
 
mke akichepuka hugeuka nyoka mwenye sumu kali kuliko kobra. Ukigundua na kuthibitisha mkeo kachepuka unatakiwa kutoa taraka siku hiyo hiyo tena usilale naye kitanda kimoja wala usile chakula chake ama maji yake atakayokuandalia. Ni ukweli mchungu.
Mumeakichepuka hata pesa yake usipokee mfungashienguo zake azikutemlangon arudi kwa mchepuko
 
Pimeni tu, ila mkigundua sio wenu kuweni wapole tu mlee masna kitanda hakizai haramu. Mbona wenu huwa tunalea!! Hebu muwe na mioyo ya kupondeka.
Kuchepuka hadi kuleta mtoto ndani ni dharau ambayo haipaswi kuvumiliwa na mwanamume yeyote
 
Pimeni tu, ila mkigundua sio wenu kuweni wapole tu mlee masna kitanda hakizai haramu. Mbona wenu huwa tunalea!! Hebu muwe na mioyo ya kupondeka.
Unaona sasa, tunarudi pale pale kwenye mitazamo tofauti, kwani unafikiri sababu ya kuzaa ni nini? Watoto sio urembo ule wa kufurahia 'how cute they are' ile in investment ya genetic material yako, kama hakuna hiyo investment basi mtoto aende huko huko alikotoka. Tujifunze kwa Simba dume anavyofanya akichukua pride, halei mbegu isiyo yake.
 
Pimeni tu, ila mkigundua sio wenu kuweni wapole tu mlee masna kitanda hakizai haramu. Mbona wenu huwa tunalea!! Hebu muwe na mioyo ya kupondeka.
Kitanda hakizai haramu na wanawake baadhi wamewasitiri waume zao kwa kuzaa nje ya ndoa.

Yawezekana mwanaume unamtosheleza mkeo kimapenzi lakini uwezo wa kumpa mimba huna.

Umekaa na ndoa miaka mitano then mke anajaribu nje mara moja tu na mimba hiyo na wewe mume hujui unajua tu Mungu ndiyo ameamua kutuondolea mtihani wa miaka mitano, kumbe ni kazi ya mchepuko hiyo.
 
Hahahaaa!
 
uchepukaji ni tabia ya mtu hausiani na upendo,ima unaletwa kwa tamaa ya maisha au ya kiisia/kimwili mke anaweza kukupenda maisha yako yotee ila tamaa ikamuacha achepuke na akafanya jambo kwa nia ua kile kilicho mpelekea tuu,ila wapo watu mapenzi unoga pale anapo kua na hamu ya kitu tuu,akisha malizana na wewe mpaka ajisikie tenaa,ila kumbuka pia mwanamke ni mtu anae taka faraja ,uwezekano unapo msononesha kwa kipindi kile kutafuta faraja ya harka ,lakini ulevi pia uwafanya baadh kina mama zetu kujiisi kujamiana kwa kipindi akiwa amelewa,je ukiwa haupo kwa kipindi mkeo kalewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…