Mtumishi wa Bwana89
JF-Expert Member
- Jul 23, 2018
- 3,191
- 4,220
Juzi nilipokuwa TBC niliwakumbuka sana mandojo na domokaya
RIP
RIP
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hio JF source yetu ni DJ fetty?View attachment 3066818
Mungu ailaze mahali pema peponi nafsi yake Bwana alitoa Bwana ametwaa.
===
Msanii wa Bongo fleva Mandojo amefariki dunia asubuhi ya leo August 11 2024, akiwa Jijini Dodoma.
Kwa mujibu wa habari za awali Mandojo amefariki kwa kupigwa na wananchi waliodhani kuwa ni mwizi baada ya kutokea mtafaruku kati yake na mtu ambae ndio aliemuitia mwizi.
"Nimeongea na Domokaya analia tu hawezi hata kuongea vizuri, anasema tu Mandojo, Mandojo Soggy Doggy Anter ambae nimeongea nae na kuthibitisha kutokea kwa msiba huu. Innalillahi wa inna ilayhi rajiun
Tunaendelea kufatilia taarifa zaidi
DJ FETTY
Ndio yeyeMleta Uzi hiyo picha uliyoweka ndo yeye au Mimi nawachanganya? 😥
Hao sijui wamepotelea wapiR.i.p kwake. Ivi mabaga fresh wako wapi?
🙏 Miaka yote namjua yule mwembamba ndiyo Mandojo😥😥Ndio yeye
Kuna jamani waligombana na demu wake ilikuwa 2013/2014 Tabata bima sasa mwamba ni kama aligoma kumpa kitu fulani(fedha) yule mwanamke, jamaa akaanza kuondoka ndipo yule demu akaanza kupiga kelele kuwa ni mwizi mwamba alirudi haraka na kumtandika makofi.Ifike hatua wananchi wawe wanatumia busara kumdhibiti kwanza mtu halfu wajiridhishe kama kweli ni mwizi kuliko kuanza kumshushia kipigo tu.
Tulishawahi kumuokoa mwana na hii hatari kupigwa na wananchi baada ya kugombana na demu na uyo demu kupiga kelele za mwizi wakati ni ugomvi wa kawaida tu kati yao.
Nina mshkaji wangu alishawahi kufa baada ya kupigiwa kelele za mwizi, alirudi kwake usiku amelewa sasa nyumba za kota zimefanana kinoma kufungua mlango haufunguki akapiga teke kumbe sio kwake dada wa kazi akapiga kelele za mwizi watu wakafika bila kuuliza wakapiga wakaua.
Wananchi waelimishwe kutumia busara wanaposikia makelele ya mwizi
Kweli wabongo wavivu hadi kusoma mbona taarifa ya mwandiahi imeeleza kabisa vizuriJazia nyama kidogo basi ,,, alikuwa anaumwa au ajali ???.. hivi kati ya mandojo au domokaya yupi hasa alofungua mradi wa soko ??..
Yule ni domokaya mwenyewe nilikuwa kama wewe niliwachanganya🙏 Miaka yote namjua yule mwembamba ndiyo Mandojo😥😥
Duh inabidi wananchi wapunguze hasiraNDIO NIMEKUMBUKA KISA CHANGU
Niliwahi kuitiwa mwizi maeneo ya manzese miaka mingi Sana nyuma.......japokuwa nilinusurika lakini nilivimba uso kwa kile kipigo......
Nilikuwa nachagua mtumba pamoja na wanunuzi wengine sasa ule mbanano na songombingo nikajikuta nimeugusa mkoba wa mama mmoja hivi kwa bahati mbaya......
Yule mama akaniitia mwizi kufumba na kufumbua naanza kupokea ngumi kwa kasi ya ajabu Sana....kwa bahati nzuri kuna baadhi ya waungwana wakawa wanasikia kilio changu wakanielewa.....ilikuwa nakufa pale pale.......
REST IN PEACE......MAN DOJO
John walker naye alikufa kifo kibayaHuyu jamaa sijui ni kwamba alikua na bahati mbaya au vp, Coz kuna Nyumba yake alijenga kule Mbweni ikaja kuvunjwa sikujua sababu hasa ni nini, Lakini pia jamaa alikua mpambanaji sana, Alikua na goli lake pale K.koo mtaa wa kongo, alikua anauza viatu vya wadada, na ukimkuta pale usanii na ustar anauweka pembeni anapiga kazi kweli kweli
Anyway Amepumzike kwa Amani kifo chake kinasikitisha sana, Inanikumbusha kifo cha Steve 2K aliyekufa kwa kuchomwa kisu na Producer Casto ponela, na Kifo cha john walker aliyekufa akiwa Gereji
Kwa maelezo inaonesha ni demu wake ndo kamuitia mwizi huenda baada ya kupishanaMtu kamuitia mwizi na Ukute hajaiba..kisa tu wamepishana jambo.huyo alisababisha auliwe hii damu atailipa..kama sio yeye basi wanae
Tumuachie Mungu yeye ndio anatoa adhabu stahikiDah.. Apumzike kwa amani.
Niliwahi ibiwa nikasema nikikuta mwizi anapigika sehemu simuachi, ila kwa hili nimejifunza, unaweza ua mtu wakati hana hatia..
Nawaza umekosana na mtu kariakoo akakuitia mwizi, UMEISHA.
Wanasema alikuwa na afya ya akili na walinzi wa kanisa ndio walimpigaHebu rudia ili tuelewe mkuuu
Acheni utoto na huyo mwenzio ChristopherPaul15Naona umesha anza kujichekesha chekesha tayari,niheshimu mimi babako coz ndio ninaye mla mamako.
So alikua ana changamoto ya afya ya akili..duuhh inasikitisha sanaWanasema alikuwa na afya ya akili na walinzi wa kanisa ndio walimpiga