Mwananchi: Aliyemtishia Nape bastola ni miongoni mwa wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara Mtwara

Unaenda kanisani ama msikitini?
Unajuaje kama hakutubu?
Imeandikwa Usihukumu.
km.kuna kuzimu mwendazake hatoki, mikono yake ilijaa damu ya akina saa8, Azory, Tundu Lissu na wengi
unajidanganya kuna kusamehewa
 
Huyu na mwili huu sio aliyemtolea bastola NAPE. Tangia zamani nilikuwa nakataa na hata sasa nakata huyu jamaa ni mtu wa Gym hivyo body yake ina utofauti sana na ile ya aliyemtolea bastola NAPE.
Gilbert kipindi hiko alikuwa na mwili mdogo tu kama ule na pia wanafanana urefu na yule aliyemtolea NAPE bastola, kitu nilichoona tofauti ni aina za miili yao ambapo kwa muonekano wa Gilbert mwili wake unauelekeo wa kuwa mkubwa, lkn yule wa NAPE anaonekana ni Mwembamba by nature.
 
Mkuu itoshe kusema kua Gilbert nimemjulia pale kituo cha polisi Kawe,baadae akahamia Osterbay polisi na walikua pale Diwani Athumani.

Ninachokumbuka pia mkewe nae alikua ni Askari.

Bisha na hayo.

Nimemjua kama mwananchi wa kawaida tu na hatimae tukawa marafiki kidogo na ndio maana nikakwambia kua ni shabiki mkubwa sana wa Yanga.

Sina Cha kumzulia.
 
GILBERT wa sasa ni mweupe, mwezi uliopita nilikuwa mtwara alikuwa anapiga GYM sana, na sasa amekuwa na mwili mkubwa.
 
Kaka jamaa naamini hajawahi kuwa mtu safi,mtu franga mbele, nakumbuka kama alikua na mke Askari pia.

Kwenye suala letu mtuhumiwa wetu alikuja kuachiwa na gari yake tuliyomkamata nayo na kuipeleka polisi pia akapewa,wakaanza nizungusha tu!!
Pole sana
 
GILBERT wa sasa ni mweupe, mwezi uliopita nilikuwa mtwara alikuwa anapiga GYM sana, na sasa amekuwa na mwili mkubwa.
Ahsante Mkuu,bora na wewe umekili kua jamaa mwanzo alikua black Ila kabadilika, that is life!!

Utaambiwa na wewe unapotosha
 
Magufuli alifanikiwa kugeuza jeshi la polisi kuwa genge la majambazi.

Mungu asingefanya yake,hii miaka 5 chini ya Magufuli nchi ingesambaratika sana kiusalama,uchumi nk
Inasikitisha sana maovu mengi yalifanyika wakati Mjomba Magu akiwa kwenye usukani.
Na aliposema anapigana vita ya uchumi,kumbe alitengeneza pia vikundi vya kigaidi ndani ya mikono ya sirikali.
Nakumbuka Raisi SSH aliwahi kusema kuna kesi nyingi za kubumba,na amekuwa mara kwa mara anayaweka wazi maovu yanayofanywa na polisi.

Itachukuwa miaka mingi kusafisha kabisa vyombo vya usalama.
 
Kwa nini tukuamini wewe sauti ya porini badala ya mwandishi anayejulikana wazi wa gazeti la Mwananchi?
 
Tunapo sema kwa Ujasiri kuwa Magufuli alikuwa muovu na kibaraka wa Ibilisi muwe mnaelewa na Wala hatuna ugomvi binafsi bali ni matendo yake ya kifedhuli dhidi ya Binadamu.

Kama yule mzee hayupo motoni basi hakuna Mungu tuendelee kutenda dhambi.
@mama D akiona hii atafunga siku 60
 
Kitengo kikishakuwa chini ya ofisi ya Rais hicho kitengo hakijitegemei tena.
 
Unafanya maovu makusudi ili ukatubu? Wacha kujijaza UJINGA hapa! Hata hivyo kutubu SI kusamehemwa mpaka muumba mwenyewe akusamehe.

Watu kama Hitler, Iddi Amin, Mobutu, Mussolini, Magufuli hata wakitubu, ni vigumu kusamehewa
Uko sahihi 99%
 
Huyu jamaa sijui alifanikiwa vipi kuwa katika jeshi la polisi kwa muda wote huu!

Mjasili haachi asili safari hii he's going down
Imagine nape alimfanyia vile hadharani,na hili tukio la mtwara jamaa atakua mtu wa namna gani kwa kina sie pangu pakavu!takukuru ifuatilie mali anazomiliki huyu jamaa na hakika watapata majibu jamaa ni jambazi aliekua anatumia ujambazi wake kwa kivuli cha upolisi wake
 

Kwa nini tukuamini wewe sauti ya porini badala ya mwandishi anayejulikana wazi wa gazeti la Mwananchi?
Shida yako ufatilii mambo. Kama ulifatilia toka mwanzo, alomshikia bastora Nape anaitwa Henry Kisanduku, na alitajwa na picha zake zilienea kila mahala. Pia kama unasoma maoni ya watu wengi humu utajua nini nachoongea. Swala la kujulikana si hoja. Watu wangapi wanajulikana lakini hawasemi ukweli? Pia humu kulikuwa na uzi uliletwa na mmoja wa memba ukieleza Gazeti la Mwananchi kukosea kutoa picha ya Gilbert.
Lakini sikulazimishi uamini nikisemacho. Utashi tunatofautiana. Nimeeleza nacho kifahamu, sijalazimisha mtu kuamini nacho sema. Be Blessed!
 
km.kuna kuzimu mwendazake hatoki, mikono yake ilijaa damu ya akina saa8, Azory, Tundu Lissu na wengi
unajidanganya kuna kusamehewa
We mbia wa Mungu?! Ya Mungu mengi na hatuna upeo wa kuyaelewa yote. Kaini alimuua nduguye Abeli lakini Mungu alimlinda..
 
Mbuzi kafia kwa muuza supu maaaaaaaanina!
 
Uwenda mtoa taarifa aliyemtambua ni nape mwenyewe hayo mambo ya kisanduku hata mwigulu alisema aliyemtishia nape sio askari tafakari!!😎
 
Tunapo sema kwa Ujasiri kuwa Magufuli alikuwa muovu na kibaraka wa Ibilisi muwe mnaelewa na Wala hatuna ugomvi binafsi bali ni matendo yake ya kifedhuli dhidi ya Binadamu.

Kama yule mzee hayupo motoni basi hakuna Mungu tuendelee kutenda dhambi.
Aliumiza watu wengi sana na kwa uonevu mno!
 
Nlikuwa nahisi tu huyu atakuwa mwananchi.
 
Sasa hivi huyo SSH ndio anayasema hayo?

Kwa hiyo Vice President alikuwa amekaa tu analishwa bure na serikali anasubiri Rais afe achukue madaraka ?

Na hana uwajibikaji wowote kwa matendo maovu ya Ikulu ambayo yeye alikuwa namba 2 in charge ?

Basi tukifute cheo kile kinatugharimu bila sababu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…