Mwananchi: Aliyemtishia Nape bastola ni miongoni mwa wanaoshikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara Mtwara

Magu na Sirro walikuwa kama pete na kidole. Magu alilifanya jeshi la polisi ndio kila kitu hapa nchini. Mungu hakika ni fundi, kwa kuondoka yule mzee mengi yanafichuka sasa. Ndiomana Samia alitaka aachie nafasi yake kipindi kile akakataliwa, akabaki amejikalia kimya tu akipelekwa pelekwa.
Mama amtoe tu Sirro kwenye ile nafasi
 
Anapaswa kujiuzuru, ana makosa mengi sana yaliyowazi mbele za macho ya raia.
 
Alivyostuka kama gari ni ya Jimmy akawa mpole?
 
Unachotetea ni watu kutishiwa maisha kwa kunyoshewa silaha za moto. Umeona uchungu habari za mwananchi kuliko matukio ya kifedhuli ?!

Mwendazake alituharibia nchi na mambo ya wasiojulikana, ambao leo wanajulikana . Ulikuwa utamaduni wa kishenzi sana
Acha kukurupuka, soma mada uelewe, Mada iliyopo ni kuhusu alie mtolea bastora waziri Nape kuwa ni mmoja wa watuhumiwa, na ikawekwa picha yake. Hizo ni habari za uongo, askari alie tuhumiwa si alie mshikia Waziri Nape silaha, ndicho nimekanusha kuwa Gazeti limedanganya. Penye ukweli tuache ukweli, si kutumia uongo kumchafua mtu. Huyo askari ana haki ya kushitaki hilo Gazeti.

Sasa weye unakuja na mambo ya Magufuli kwani hapa umeona nimeongelea Magufuli? Chuki zako na Magufuli tuache gazeti lipotoshe kuwa askari alietuhumiwa Mtwara, ati ndiye alie mtolea silaha Nape. Wewe ni waajabu saana. Fikiria, changanua kinachosemwa, na tafakari si kukurupuka na chuki zako na unaongea nje ya mada. Nadhani unamuota hata huyo ulie muongelea.
 
Kama ni kweli mwambie jamaa akitoka sero afungue kesi na adai fidia milioni 100,, mie mnigawie laki 5 tu ya consultation fee. [emoji23]
Ndugu yangu, ni kweli na ninauhakika. Hapa nishawambia nduguze wanunue gazeti hilo na walitunze. Kesi ya madai lazima.
 
Utawala wa mwendazake ulikua unafuga majambazi
 
Uwezi weka picha ya mtu katika habari isiyoendana na muhusika, tena habari yenyewe ni tuhuma. Huu ni uandishi ucharwa. Hiyo wamemzalilisha Bwana Kalanje ambaye sasa picha yake inasambaa mitandaoni na watu wanajua kuwa yeye ndo alimtolea Nape silaha. Tusubiri!
 
Ndugu yangu sipingi usemacho, ila alie mtolea Nape silaha si Gilbert kulingana na picha na video. Kama unamfahamu kweli Gilbert. KIla binadamu anamadhaifu. Sidhani kama kuna mtu ambaye hajawai tenda baya. Kosa fulani aliwezi kuwa ndiyo hukumu ya kosa jingine au kuhalalisha kosa. Hapa issue je yule alomtolea Nape silaha kweli ni Gilbert? Wakati ule zilisambaa picha za mtu anaitwa Kisasandu.
Na Gilbert wakati wa hiyo Issue hakuwepo Dar, alikuwa huko Musoma, baadae alihamishiwa Mtwara miaka mingi tu!
Ni kweli ni mshabiki kindakindaki wa Yanga!
 
akili yangu ya jicho la tatu imegoma kuamini kuwa yule askari aliyemtolea nape risasi, yupo katika orodha ya asakari waliofanya tukio la mauaji mtwara. kuna mchezo unachezwa, tutafahamu tu mbele ya safari.

hivi tarehe tatu ndio siku ambayo makonda anatakiwa kufika mahakamani?.
 
Mie nafikiri kuna haja ya haraka sana ya kuwa na kitengo kinachojitegemea ambacho kitakuwa chini ya ofisi ya rais kuchunguza makosa yanayofanya na hawa watu wetu wa vyombo vya ulinzi na usalama

Tuache siasa sasa hivi vyombo vya ulinzi na usalama havina tena imani kwa wananchi

Yaani siyo tena sehemu salama ya kupata msaada manake wanaamini kuwa wakifanya tukio watalindana manake hao hao ndo watakao unda tume

Yaani haki ya raia kuishi kwa amani yeye na mali zake siyo tena swala la msingi

Na siasa zimeteka sana majeshi yetu kwa kweli. Manake kuna baadhi ya viongozi wLidirikikusema alomtishia Nape hakuwa askari ili kulinda ugali wao na bado wako kwenye system.
 
Kwa akili ya kawaida tu mtu aliyemtolea Nape(tena akiwa waziri) alikuwa ni askari wa kawaida!?
Acheni ukasuku!
 
Kumbe ni shabiki wa Yanga? Ndio maanaaa.....
 
Hasa! Kosa kubwa lipi la gazeti la Mwananchi au polisi kutotimiza wajibu wake kwa wananchi wa kumtambua mtu aliyefanya jinai dhidi ya Nape mchana mbele ya watu wengi!
 
Aliyezoea vya kunyonga ataendelea na tabia hiyo.
Mwisho wa siku vitendo vyake alivyozoea ndio vitamuadhiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…