Mwanangu anashindwa kutumia common sense?? Hii ni shida gani?

Mwanangu anashindwa kutumia common sense?? Hii ni shida gani?

Nina mtoto wa dada yani toka std 1 akifaulu sana ni wa pili kutoka mwisho hata form 4 ni kuungaunga hadi kamaliza, mama ake kachapa, fundisha sana yani unaweza fundisha 1+1=2 dk2 ukimuuliza tena kasahau ila sasa mpe asimamie biashara hapo hapotezi hata 100 na anajua kutengeneza faida ikabidi amsapoti na biashara tu ndipo alipo vizuri
Exactly 👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾
 
hayupo huru mbele yako, unapoongea nae hofu inamtawala zaidi, hii inaathiri hata majibu anayokupa.

Huyo mtoto wako hana tofauti na uhusiano wangu na kaka yangu, kanizi mkaka 7, alikuwa ananionea sana udogoni makonzi, vibao, vitisho, n.k. sikuweza kuwa huru nae kabisa lakini alipokuja kaka mwengine kimasomo ambae ni ndugu wa kijijini nilikuwa huru sana kwake kwenye maongezi hadi kaka yangu wa damu anashangaa mbona naongea vizuri nikiwa na kaka mwengine. nina 36 kaka yangu hadi leo inaweza kupita miezi hatujawasiliana.

Mbaya zaidi hata ukiacha ukoloni umeshamuharibu kisaikolojia, ni ngumu kumfanya awe huru mbele yako
 
Kumbe!! Kwa sentensi hii inaonyesha wazi akili karithi kwako au wewe hujamlea vizuri.

Umeshindwa kuelewa hoja yangu na kuichanganua
Chuma hainasi kwenye mbao . maana anasema amemchukua akiwa darasa la tatu. Means yeye ndiye amemshape dogo hivyo alivyo.
Kuna namna akili hazifanani na tunatofautiana namna ya kuhandle possibly ukali wa muda wote umesababisha hofu na mpaka mtoto amepoteza confidence katika kufikiri na kutenda.
 
Majibu yote ya maswali ya mtoa mada yatapatikana hapa.
Swali la kuongezea hapa je anaishi na mama wa kambo au mama yake mzazi?tatizo kubwa la mwanao kwa makisio yangu inahusiana na mambo ya saikolojia(lack of confidence).
Watu wa aina hiyo wakipataga nafasi ya kujiamini/confidence huwa wanakujaga kufanya maajabu na kila mtu anabaki mdomo wazi.
Hata mimi zamani nilikuwa naonekana hivyo mtaani kwangu na kwa jamii yangu lakini baadae nilikuja kuwaprove wrong na naweza kusema kwamba mimi ndio kijana niliyeonesha dira kwenye mtaa wangu na hakuna mwingine wa kunifananisha naye kwa mambo niliyowaonesha.
Kwa hiyo nikuondoe wasiwasi ndugu yangu,baadae atabadilika na utashangaa.
Watu wa aina hiyo huwa ni watu wa kutafakari sana kiasi kwamba akili inahama inakuwa iko mbali so wakati wewe unamuuliza swali fulani arakujibu tu ili mradi umuondolee kiwingu ili aendelee na tafakuri zake.
Ukimuuliza swali akakosea kujibu haimaanishi kwamba hajui jibu la hilo swali ila ni kwamba tu ubongo wake unakuwa bize na hataki umtoe kwenye reli.
mkuu hii shuhuda yako ni muhimu sana natumaini na wengine wamejifunza pia
 
Mtoto umebambikiwa huyo sio wako aumama yake kwao ni vilaza
Kama mzazi mtarajiwa naomba usizumngumze hivi, haya maneno yawe tu yamekutoka pasina kukusudia. Hakuna anayependa hii hali ila tukubaliana nayo kwakuwa yametokea na hamna namna.
 
Kama mzazi mtarajiwa naomba usizumngumze hivi, haya maneno yawe tu yamekutoka pasina kukusudia. Hakuna anayependa hii hali ila tukubaliana nayo kwakuwa yametokea na hamna namna.
Mimi ni mzazi😐watoto hurithi tabia na akili za wazaxo wao,eanawake wanwxaa njr yandoa sana tu sasa hapo cha ajabu kitu gani
 
Mkuu vipi watoto wako na wenyewe wana hilo tatizo?

Ebu kwanzia leo jaribu kubadili mtindo wa maisha, jitahidi unakuwa na muda wa kuwa peke yako kila siku nenda sehemu tulivu na zenye uasili kama vile uoto wa asili, beach au sehemu yeyote ile yenye utulivu kisha uweke umakini kuangalia nature mawazo mengine yote uache kufikiria jaribu kuangalia tu asili na uifurahie, utanipa majibu mkuu.

Mimi nimesomea shule za kimasikini sana, sasa kipindi napanda level nilijikuta nakutana na wanafunzi waliotokea shule bora na wengi walikuwa ni race tofauti na yangu sasa nilikuwa najiona si kitu ila kifupi ni kuwa niliijua siri mapema nikawa na umakini uliomakinika matokeo yake nilifanya maajabu ambayo niliwashangaza wengi hata mwenyewe nilijishangaa.
Asante kiongozi,
 
Kwa maelezo yako hapo juu. Mimi naona mtoto ndio genius wewe baba ndio kilaza maana umeshindwa kutambua kaliba ya mwanao.
Tatizo unataka kumpima uwezo wake kwenye vitu vya kawaida, uwezo wa darasani, uwezo wa kujenga hoja na takataka nyingine.
Kuna muda utafika atakuja kufanya mambo makubwa mpaka utajiona wewe ndio kilaza wazazi tunaharibu sana watoto hasa kwenye upande wa elimu kwa kulazimisha kuwa ni lazima mtoto afate mienendo yako

Kuipata hiyo div3 sio kwamba ni ufaulu mzuri lakini inatosha kukuonesha kuwa huyo sio kilaza unavyomfikiria ila umeshindwa tu kumsoma yeye ni mtu wa aina gani.
 
1715128721291.jpg
 
1.wasilisha kadi la mwanao hapa (ali score ngap alipozaliwa)
2.Malez yake mlikuw mnapga sana (alililelewa na step mother, au bibi)
3.ulimlea kisasa sana
4.lishe ni jambo la mwisho
📉📉📉
na kwann hadi amefk miak 17 huku weza jua tatzo la mwanao na ukaanz mjenga mapema
mtoto wa mwaka 1½ anaanz kuonyesh common sens katk kujinza ndan ya mazingr yake hadi kufka miak 7/10 unakuw unajua uwezo wa mwanao ndan ya mazingr ya maish na darasan yupoje.
💥🆔🚭 Au yawezekan mwanao ana mawazo mda wote
Au ana overthinking
muhusishe na michezo.sana na shughuli za kijamii
 
Tuanze na lishe unayompatia nyumbani, je ni mlo kamilii?.

Twende kwenye malezi unayompa hapo nyumbani, je ni malezi ya kumfanya aweze kujitegemeaa?

Tuelekee kwenye lugha ya mawasiliano kati yenu, je huwa unamkaripia/kumgombeza mara kwa mara?

Je, kwa wastani mwili wake upoje, je ni mnene, mkakamavu au lege lege?

Vipi anashiriki michezo yoyote shuleni kwao au hata hapo mtaani?.

Ni mwanao wangapi kuzaliwq kwenye hiyo familia yako?.

Graph yake ya makuzi kadi ya clinic ilikuwaje au ipoje kama bado upo nayo? (Ni muhimu sana kutunza hiyo kadi)

Ukimaliza hayo yote, vipi mwanao huyo ana mpenzi? Kama hana wewe kama baba yake umemsaidiaje hilo swala?. (Usishangae ni jukumu lako mshua)

Ukiona mwanao hawezi kucheka mbele yako inabidi ujitafakari upya kiongozi, kuna kitu kikubwa hakipo sawa kati yenu.

Tafakari hayo machache Mkuu mwenzetu, kila la heri.
Duh; hizi nondo mzazi anaweza kuingia mitini akautelekeza na uzi kabisa!
 
hapendi michezo anapenda kulala lala
hawezi cheza mbele yangu
Mi nimkali hasa linapokuja suala la shule
amelelewa na mama ake nimemchukua akiwa darasa la tatu
Hili ndo tatizo mkuu, moja kaja kwako na miaka mitatu huyu kaja na akili timamu itakuwa kuna vitu alilishwa yamini na mamake, hapo anakuona boya tu
 
Nina kijana wa miaka 17.
Wa kiume ni mpole na mkimya lakini hayuko smart.Tofauti na ilivo kwa watu wengi wa kimya kwa kua na akili nyingi kwa kijana wangu ni tofauti ni mkimya ila sasa akija kuongea unaweza ukajiuliza ameongea wire ukiwa connected kwene switch au Laaah.

Shuleni ni average sana si mkia maksi zake 46,67,37,50,30 kifupi alipata division 3 .
Kinachonitatiza ni uwezo wa kufikiria na kuchanganua mambo mdogo. Maswali ya kawaida ya kutumia common sense hawezi !!
Ukimuelekeza kitu cha kawaida haelewi mara moja had urudie
Ni rahisi kuchanganya vitu na kusahau.
Kifupi anashindwa kujisimamia au kupambanua vitu vya kawaida vya uelewa wa kawaida .

Alafu sometimes anachanganya vitu havihusiani
Ukimuuliza swali anajibu jibu ambalo halina uhusiano na ulichomuuliza!

MIMI MZEE WAKE NIKO VIZURI!Sijui hata karithi kwa nani haya matatizo ,,,, shulen mm nilikua smart siyo sana lakin smart kiasi cha kumlizisha mzazi yyte yule average



Nifanyaje kumsaidia
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye Bali mwana moi mbavu ni mzigo kwa mamaye MITHALI 10:1

Huyo karithi ujombani kwake!
 
Back
Top Bottom