Mwanaume unawezaje kujiua kwa ajili ya wivu wa mapenzi?

Mwanaume unawezaje kujiua kwa ajili ya wivu wa mapenzi?

Mapenzi ya siku hizi ni kujiweka mguu nje mguu ndani.
Hata ukichapwa nje we endelea na maisha yako.
Na sijawahi kuumizwa na mapenzi baada ya kukaa mguu nje mguu ndani.
 
Temea mate chini ibra87.
Mambo haya hayana kabila, dini wala rangi.
Akili yako inahamishwa na hasira kaka.
Uwiiiii

Huko ni kujiendekeza hakuna lolote. Naweza kusema ni ujinga na upumbavu mtu kujiua kisa yule mwenye K kampa mtu mwingine.
Kuna wakati wahehe wanaongoza sana kujinyonga tena bila sababu, nao utawasemaje? Ni hasira zimezidi?
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana sitaki kumiliki bunduki hata niwe na hela kiasi gani
Back to the topic.mm mtu akimwambia mpz au mke wake "eti siwezi kuishi bila ya wewe" namuangaliagaa halafu nahudhunika yaani haya mapenZi mpaka Mungu anawekwa chini binadamu mwingine anawekwa juu like seriously!!!?...huyo ndio anayekupa pumzi!?? Sasa mtu akijiua kiukweli wala sihudhuniki na hata akinusurika nikimtembelea hospital naenda na madawa mengine ayameze ili afe kabisa. Ni ujinga uliopitiliza. Linaloshangaza sasa huyu unayemuacha huku duniani ni mwezi tu anakusahau anabanjuliwa weeee mpk sugu
 
Huko ni kujiendekeza hakuna lolote. Naweza kusema ni ujinga na upumbavu mtu kujiua kisa yule mwenye K kampa mtu mwingine.
Kuna wakati wahehe wanaongoza sana kujinyonga tena bila sababu, nao utawasemaje? Ni hasira zimezidi?

We hujakutana na mwanamke aliyepikwa unyagoni..afu wengi hukumbuka muda alioupoteza hivo roho inamuuma mkuu.

Hayajakukuta
 
Kumpenda mtu ni kubaya sana, hasa mwenyewe akijua ndio loh!! Utaomba ardhi ipasuke. Asante Mungu kwa kushinda huu mtihani.
 
Kumpenda mtu ni kubaya sana, hasa mwenyewe akijua ndio loh!! Utaomba ardhi ipasuke. Asante Mungu kwa kushinda huu mtihani.

Sema wewe bwana. Hahaha Wengine tulishawahi lizwa kama mtoto na binti flani hvi, tukiwa na ndevu zetu hvi hvi. Tehe
 
Sema wewe bwana. Hahaha Wengine tulishawahi lizwa kama mtoto na binti flani hvi, tukiwa na ndevu zetu hvi hvi. Tehe

Mi nimetoka kumwagwa juzi, nikataka kuponda chupa nikaona dah!!! Sijaaga ikabidi nihairishe, ndio hvo nipo nauguza za usooo!!!
 
Mi nimetoka kumwagwa juzi, nikataka kuponda chupa nikaona dah!!! Sijaaga ikabidi nihairishe, ndio hvo nipo nauguza za usooo!!!

Time heals everything. With time u will be OK. You have a great life ahead of you.
 
Time heals everything. With time u will be OK. You have a great life ahead of you.

Hahahahahaha!!!!! Nimetania kaka nipo okey kabisa.

Na ukubwa huu niumie kuachwa loh!!! Mtu akiniacha na hesabu kama nimeanguka then nainuka najifuta vumbi nasonga mbele. Tena kwa amani kabisa.
 
Mm ndo mana nikihisi naanza kumpenda tu mwanamke taratbu naanza kujifunza kupunguza upendo..
Naanza mdogo mdogo tu kupunguza kutuma text, mpaka upendo unapungua
 
Yani hii mada inaniumiza maana nimetoka kumuona hospital kaka yangu ameponea chupuchupu kufa baada ya kujaribu kujiua kwa kujikata shingo kisa kaachwa na mwanamke..sasa sijui ni mapepo ama nini
 
Yani hii mada inaniumiza maana nimetoka kumuona hospital kaka yangu ameponea chupuchupu kufa baada ya kujaribu kujiua kwa kujikata shingo kisa kaachwa na mwanamke..sasa sijui ni mapepo ama nini

Huyo siyo wa kumchekea, mpeni dozi ya kuangalia cheaters Dstv aone mambo yalivyo kwa uhalisia wake, atajiona mjinga sana.
Mimi mtu akinifanyia ujinga, I try to reason and understand her kwa sababu Nimewahi kupenda na kupendwa na wengi tu kati yao walikuwa wapenzi wa watu, Nachukulia tu kama sehemu ya mzunguko wa life. Kwa jinsi Nilivyowahi kusumbuliwa na mapenzi, sidhani kuna cha kuniumiza katika mahusiano labda siku mama wa mwanangu anikatae kuwa siyo Baba wa mtoti wangu maana ndicho cha muhimu zaidi kwangu.
Mpenzi ni binadamu kamili anaejitegemea kihisia, kifikra na kimatendo, huwezi kumlazimisha atende kama unavyotaka au kutarajia kama yeye hajisikii kufanya hivyo na hicho ndicho unachopaswa kukumbuka kila siku.
Kingine cha muhimu kukumbuka ni kuwa maisha ni matamu sana, mtu mwingine hawezi kulinganishwa na utamu wa maisha nayoishi Mimi maana Nakutana na vitu vipya kila kukicha wakiwamo potential wapenzi wazuri zaidi, nitainjoi vipi Nikijiua kwa sababu ya kajitu kamoja tu kalikoniudhi kwa sababu ambazo hazina kichwa wala miguu? Aisee bado sana.
 
Wasaalam,

Huyu ni jamaa wa pili kumfahamu tumefanya nae kazi kwa muda baadae akaamua kupumzika leo naambiwa jamaa yako amejifumua risasi ya kichwa kwa wivu wa mapenzi, kisa kabaini mke wake anamahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi mwenzie.

Wa kwanza aliniuma sana maana umri wake na mafanikio yake ndio kwanza yalikuwa yameanza kuchanua, biashara imekubali maisha murua, huyu nae alikunywa sumu baada ya kubaini mkewe tena wenye ndoa ya miaka miwili tu anabanjuka na dereva wake wa dukani.

Bado najiuliza unawezaje kujikatisha maisha kwa wivu wa mapenzi? Hivi wanaume hatuna uvumilivu na maamuzi zaidi ya kujitoa roho?

Nimechoka kabisa.

R.I.P Bro H.

Mwombe sana Mungu yasikukute. Mapenzi ni habari nyingine kabisa sumu kuzidi bomu, mapenzi yanauwa ufahamu na kukufanya ----- kabisa..... Tumeyaona tumeyashuhudia... Omba yasikukute
 
Mwombe sana Mungu yasikukute. Mapenzi ni habari nyingine kabisa sumu kuzidi bomu, mapenzi yanauwa ufahamu na kukufanya ----- kabisa..... Tumeyaona tumeyashuhudia... Omba yasikukute
mkuu mshana nadhani nina umri wa kutosha kuwa nimeshuhudia mengi kwenye swala la mahusiano, ila swala linalo nitatiza sio kuombea kukutwa... kweli yanaweza kunikuta lakini suluhu ya jambo hili likikukuta ni kujikatisha uhai? Ebu chimbua zaidi.
 
Back
Top Bottom