Mwandishi Ansbert Ngurumo apewa hifadhi kwa usalama wake nchini Finland

Mwandishi Ansbert Ngurumo apewa hifadhi kwa usalama wake nchini Finland

Nimekuuliza jina la huyo mtu unayesema aliletwa toka Swaziland. Andika ni nani? Acha hadithi za kutunga. Kama unatamani kwenda Ulaya na njia imekushinda, tangaza una maisha magumu. Acha ulongo eti natafutwa na wasiojulikana. Kuandika kwenye gazeti makara moja tena haina la maana ndo atafutwe.

Narudia tena nani alitetwa na serikali toka Swaziland. Kama huna jina acha kulopoka hadithi.

MTU wa Lumumba unajifanya humjui?? Muulize boss wako makonda. Halafu unajifanya unajua
 
ko unataka kunambia ni heri kufa kuliko kukimbilia kwa wazungu???!!!

sijui umesoma chuo gani??!!!

Itakuwa wanafundishwa namna ya kukimbiza mwenge huku wanaambiwa utamurika mchana😛😛
 
Nimekuuliza jina la huyo mtu unayesema aliletwa toka Swaziland. Andika ni nani? Acha hadithi za kutunga. Kama unatamani kwenda Ulaya na njia imekushinda, tangaza una maisha magumu. Acha ulongo eti natafutwa na wasiojulikana. Kuandika kwenye gazeti makara moja tena haina la maana ndo atafutwe.

Narudia tena nani alitetwa na serikali toka Swaziland. Kama huna jina acha kulopoka hadithi.

Tizama kijana wa Lumumba alivyo mvivu baada ya kutupiwa buku 7 anakuja kututapikia humu. Kwa faida ya wengine Gonga hapo

Ludovick Mwijage: The Dark Side of Nyerere's Legacy
 
Mwache akimbie kuuwa unajiona kama mwandishi wa mwananchi sio vzr. Ubaya wa kutekwa ni kuwa mtekaji anaweza asiwe na nia ya kukuua issue ikawa kukutesa tu lkn binadamu afya zinatofautiana mwingine ukimlazinisha push up dk 2 tu roho yake inatoka na kwa sababu mtekaji alifanya kwa usili ukisha kufa hana jinsi anakutumbukiza kwenye kiroba anakutupa bahari, huku mnabaki mnatafuta kama akina Ben Sanane. Tena afadhali uwindwe na Jambazi unaweza jificha kuliko kuwindwa na watu wa serikali utakufa bila kijulikana umefia wapi. Nampongeza Ngurumo kwa kusalimika, huko anaweza asiishi maisha mazuri kama nyumbani kwake lkn uhai ndo msingi kwa binadamu. Mungu anaweza kumpa uhai akarudi nchini baada ya wimbi hili la awamu ya tano kupita na maisha ya kidemokrasia yakalejea kawaida.
 
Huyu mtu huko "kukimbia" kwake ndiko kumemfanya hata huu Uzi uandikwe kumhusu; ila hana madhara yoyote; sijawahi kukutana na andiko lake lolote la maana.

Acha abadili hali ya hewa na Kula soseji.
 
Huyu ametamani kuishi nje siku nyingi sasa amepata sababu ya uwongo ya kujitengenezea.
 
Watu kwa kumsema Papa Doc. vibaya tu wamefunguliwa makesi

Nitafeli mapema kwani kuna kijana alipotea miezi 6 alipoonekana kumbe alikuwa ndani , kosa lake kaenda kuposa mke kwa mtu aliyebambikiziwa kesi ya ugaidi.
Walimwachia siku mbili baadaye kwa kueleza hii habari wamemtia adabu kwa kumfunga tena mpaka leo. Kijana hajui hata siasa ilivyokaa.

Wachilia mbali kesi za wale masheikh walioukosoa muungano kwa kutumia haki yao kikatiba na kubambikiziwa kesi za kigaidi zisizo mashiko

Ofcourse kwa kurushiwa buku saba utakuja kutapika pumba hapa, kwani hujali hayajakufika wala hakuna jamaa yako yamemfika
aaaaah Gavana Mkuuu!! labda ulitaka kumquote [HASHTAG]#Patriot[/HASHTAG] maana hajaelewa kwa nn mwandishi Ngurumo kajificha FINLAND na sio nearby shit hole country!!!!
 
Kuwa mkimbizi mnaipigia filimbi kama vile ni wa kwanza duniani.. eeeeeh

Uamuzi wake huo.. alitaka tu kwenda ulaya kuishi huko baada ya kuwa mvivu kufanya kazi kujilisha
Angeuwawa ndio ungeamini kuwa alikuwa anawindwa. Hivi ni mpaka watu wangapi wauwawe au wapotezwe ndio muuelewe ukweli. Muwe na huruma na imani,kwa vile we kila usiku upo kitandani na mwenza wako basi unadhihaki wenzio wenye maisha yaliyo hatarini. Amini nakuambia ipo siku yatakukumba, usifurahie tu yakiwa kwa mwingine. Hawa waliopotezwa na kuuawa wangekuwa jamaa zako wa karibu ungedhihaki ? Au ingekuwa ni mwenza mnaechangia kitanda ungefurahia ?
 
Kuwa mkimbizi mnaipigia filimbi kama vile ni wa kwanza duniani.. eeeeeh

Uamuzi wake huo.. alitaka tu kwenda ulaya kuishi huko baada ya kuwa mvivu kufanya kazi kujilisha
Umesema kweli, hata Ndugai alijiuguza tu makusudi ili akatembee India.
 
Wazungu wanaihitaji Tanzania zaidi ya Tanzania tunavyo wahitaji hao wazungu.
Mauzo ya London Stock Exchange mwaka jana ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka ishirini
Mauzo ya DVD London kwa mwaka ni sawa na bajeti ya Tanzania mwaka huu
Nani ana muhitaji nani?
 
Ni habari mbaya kwa nchi yetu inaendelea kuwa na hadhi mbaya ndani /nje ya mipaka yake. Maisha ya waandishi wa habari, wanasiasa na wanaharakati yamekuwa ya mashaka.

Mwanahabari Ansbert Ngurumo aliyewahi kuwa mhariri wa Magazeti ya Tanzania Daima na Mwanahalisi, amekimbilia nchini Finland na kupewa hifadhi huko, kwa muda alikuwa akisema anatishiwa kuuawa.

Habari zaidi soma=> Ansbert Ngurumo: Muda wowote naweza kufa maana natishiwa kifo

UPDATE:

Mwandishi wa Habari mwandamizi nchini, Ansbert Ngurumo amepata hadhi ya kupewa ulinzi nchini Finland, baada ya kudai amekimbia aliowaita "wauaji" wake.

Ngurumo ambaye amewahi kuwa mhariri wa magazeti kadhaa nchini; Mtanzania, Tanzania Daima na MwanaHalisi, ameiambia JamiiForums kuwa amekiepuka kifo kilichopangwa na wale aliowaita "wasiojulikana."

Akizungumza na JamiiForums, Ngurumo alisema ni kweli amekimbia Tanzania ili kuulinda uhai wake baada ya kuanza kuwindwa na watu wasiojulikana.

"Tangu mwaka jana nimekuwa nikipokea vitisho vingi na vyenye kuogofya kufuatia makala zangu kwenye gazeti la MwanaHalisi. Nimenusurika kuuawa mara kadhaa, lakini nashukuru Mungu hadi leo niko hai," anasema Ngurumo.

Anasema ili kunusuru uhai wake, alilazimika kujificha Mwanza tangu mwaka jana na baadaye kupata kwenda Kenya, kabla ya kwenda Sweden na sasa Finland, ambako amepewa hifadhi.

Ngurumo anasema hadhi aliyopewa Finland, siyo ya ukimbizini, bali ni "hifadhi ya kimataifa," kuunusuru uhai wa mtu ambaye yuko katika hatari ya kuuawa nchini mwake.

Vyombo vya Habari vya Finland na mitandao ya kijamii, imeandika habari ya Ngurumo kukimbia Tanzania kwa hofu ya kuuawa.

"Nimezungumzia mkasa wangu wa kunusurika kudakwa na watu wasiojulikana, ambao wamekuwa wakipanga kuniua na wamejaribu mara kadhaa bila mafanikio, sasa nikaona niwakimbie, kwani kufa kijinga ni dhambi kubwa," anaongeza Ngurumo.

JamiiForums inatambua kuwa Ngurumo alianza kuhofia maisha yake baada ya kudai kupokea vitisho kwa alichodai ni kufuatia kuandika makala kwenye gazeti la MwanaHalisi ikiwa na kichwa cha habari; “Tumuombee Rais Magufuli au Tundu Lissu?”
mi tangu nipo Mdogo nilifundishwa na mzee wangu Uhuru bila mipaka ni fujo,na sasa nakumbushwa kitu kitu kimoja "ukiona mtu alikuwa anapinga serikali ya jk na ya magufuli pia anapinga" mwangalie vizuri ni kuwa hayupo kwenye maslahi ya taifa
 
mi tangu nipo Mdogo nilifundishwa na mzee wangu Uhuru bila mipaka ni fujo,na sasa nakumbushwa kitu kitu kimoja "ukiona mtu alikuwa anapinga serikali ya jk na ya magufuli pia anapinga" mwangalie vizuri ni kuwa hayupo kwenye maslahi ya taifa
Mipaka ni ile iliyopo kwenye sheria na katiba sio matamko ya watu tu kila kukicha kutokana na uroho wa madaraka na hulka zao.
Kama mtu anavunja sheria au mipaka kama unavyoiita basi tumeweka mahakama ,apelekwe huko.
Ndio utawala bora.

Kila nchi ina watu wanaokiuka taratibu na sheria ila wanafikishwa mahakamani sio kuwaita wasaliti.
Ndio maana nchi za wenzetu hata wakubwa wanafikishwa mahakamani. Baadhi ya nchi hawataki mana wanajua wazi kuwa wanavunja sheria sana,na wakifikishwa huko watazeekea gerezani.
 
Je huyu Ngurumo alitekwa au alipotea, alijiteka au namna gani? Maana watu wametoa mapovu mpaka mishipa ya shingo mithili ya kupasuka kumbe mtu ana mambo yake na raha zake ili mradi Sera za CDM kuonesha ubaya wa uongozi uliopo
 
Back
Top Bottom