Mwandishi maarufu JF aliteswa sana baada ya yale Maswali

Mwandishi maarufu JF aliteswa sana baada ya yale Maswali

Wafuasi wa Magu wanaweza kumbishia hata muhusika
Kwakuwa jamaa anapenda kuquote nyuzi zake za nyuma ngoja nimtag auweke ule uzi wake siku hiyo kapandisha uzi kwa kukosa usingizi.

Hao walinda legacy uchwara achana nao , japo Mayalla baada ya hili tukio niliacha kumchukulia serious maana alirudi nyuma sana na kuwa chawa kupitiliza .

Cc Pascal Mayalla
 
Hii habari imenisikitisha sana

Kuna mwanafamilia mmoja wa Mwandishi huyo alisoma nae Tambaza anasema Mwandishi huyo maarufu humu JF aliteswa sana baada ya yale maswali.

Ilifika mahali alitamani kurudi kijijini na kama sio uhusiano wake na Rais Mkapa mambo yangekuwa mengine

Hii ni kwenye mjadala wa Kitabu maarufu chenye siri za kutosha za utawala wa awamu ya Tano CH

Pole sana mkuu, you have my respect on...

Kuna watanzania huwa wanapitia magumu kimya kimya kiuhalisia ila tunaishia kuwabeza humu ..

Narudia tena, pole sana kiongozi, una heshima yangu ya kutosha .. ikikuoendeza utasema siku ikifika.
Mbona hueleweki ulichoongea? Umeanzia uzi katikati au.??!! Habari haina kichwa wala miguu.
 
Yes Tambaza, Ilboru, JKT, TSJ, RTD 1990-1995
DTV 1995-2000
TVT 2000-2005
UDSM LL.B (hons)2005-2009
Ubalozi Uingereza 2010-2014
PPR from 2015 to date!.
Nina wake 3, US, Canada na Bongo.
Nina watoto 9 wa nyumbani! Ni mtu anaependa kula vyakula vizuri Uliwahi kula vyakula gani kutoka sehemu mbalimbali Duniani ukafaidi?
P
Nimekusikiliza sana RTD miaka hiyo ya 90 mpaka 95 nami nikiwa shule ulikua kichwa sana aisee kwenye utangazaji wako na kuandaa vipindi pana mwimbo mmoja wa dada mmoja wa USA unaitwa 5 o'clock in the morning... ulikua unaupiga sana saa kumi na moja kabla ya vipindi kuanza mimi bhana sikudai kabisaa big up kwako..
 
Alichoulizwa na alichojibu ni hasi na chanya, hayo maswali hayajibiki lakini, lazima tukiri Pascal Mayalla ni Mwanahabari mahiri na mwenye upeo mkubwa wa akili.

Na baada ya hapa Pascal Mayalla hajawahi kuwa yule tena, aligeuka ndumilakuwili wa kung’ata na kupuliza hadi hii leo!
Hakika mkuu. Ndio maana nataka kukubaliana na kilichoandikwa alipigwa vitasa na kupewa maelekezo
 
Umeasi dhehebu la katoliki mpaka uwe na wake 3?
No, sijaasi Katoliki, mke wa kwanza ni wa kanisa Katoliki, ndie anaishi US na watoto wake, wa pili ni wa kimila yeye anaishi Canada, na wa tatu ni wa kiserikali ndie niko naye Dar, na nimekufa nimeoza,ila kula kula kuko pale pale!。

Nimefuatilia sana Bible kwa makini kabisa, hakuna nabii yeyote aliyekuwa na mke mmoja,hata wanawake waliokuwa wakimhudumia Bwana wetu Yesu Kristo ni watatu,Maria Magdalena,kuna Veronica na Salome!。 Nimesoma sana Bible, nikakuta hakuna popote issue ya mke mmoja, sio mpango wa Mungu,ni uongo wa wazungu kutokana na wao kutokuwa very active,ni damu baridi, uwezo wao ni kula mboga moja tuu hiyo hiyo, sisi Africa ni damu moto,huwezi kushiba mboga moja hiyo hiyo kila siku,lazima ubadili mboga!。 Nilimshauri hata Blaza "Pongezi Rais Magufuli Kuwa Mkweli Daima. Tuanzishe Church of Africa, Tuoe Wake Wengi, Tuzae Watoto Wengi?"
P
 
Alichoulizwa na alichojibu ni hasi na chanya, hayo maswali hayajibiki lakini, lazima tukiri Pascal Mayalla ni Mwanahabari mahiri na mwenye upeo mkubwa wa akili.

Na baada ya hapa Pascal Mayalla hajawahi kuwa yule tena, aligeuka ndumilakuwili wa kung’ata na kupuliza hadi hii leo!
Magu mtu wachuki na visasi..lazima alimtisha Pasco..na Pasco akaona isiwe tabu
 
Back
Top Bottom