Pre GE2025 Mwenezi akiwa Makonda, Chadema na Lissu walipoteana, Masikio ya Watanzania yalielekezwa Kwa Makonda, kwasasa Lissu anajipigia tu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Siasa sio uadui !
Hapo zamani ilikuwa haiwezekani kabisa kabisa mchezaji wa Yanga akahamia Simba au mchezaji wa Simba akahamia Yanga !
Lakini kwa sasa hiyo kitu ni ya kawaida sana !
Kama Kibu Denis kuhamia Yanga ! 😅🙏
Wakae wasameheane tu
 
Makonda nyota yake ipo CHADEMA ni yeye tu hajui.
 
mtu yeyote anayemfuatilia makonda huyo ni mfu kifikra. yaani sasa umfuatilie makonda ili usikie nn cha maana toka kwake? aliingia na punda, roli, mkokoteni hata punda. vitu hivi vina mahusiano gani na uenezi
 
Mmoja ajishushe tu
Labda makondo, Lissu aliemdindia mpaka Jiwe. Hawa watu wangepatana tungekua mbali sana leo. Ila ndo hivo Misimamo ya Lisu mara zote humwacha peke yake.
 
Mnara wa Babeli !
 
CHADEMA waliumia sana Makonda alipopewa Uenezi. Wakaungana na wahuni kujenga presha atolewe ili wapumue. Jamaa alijua kupiga home and away. Chama cha hoja act wazalendo nacho ndio ivyo Tena 😁 😁
Hivi kwa akili yako tu ya kuvukia barabara unaweza kuniambia bashite ana hoja gani za kuitetemesha chadema? Tatizo mmezoea kuishi kwa maigizo
 
Hahahaa.......Yaani Makonda amefikia hatu ya Kulinganishwa na Mwamba Lissu?

Mnamkuza sana
 
Inawezekana but tutaunda Nchi ya Kifashisti.

Lissu na Makonda ni Wafashisti (Watu wa Watu)
 
H Hili nyumbu la wapi tena?
 
Unaambiwa Kwa Sasa MTU Bora asile lakini aweke Bando afatilie Lissu kasema nini !!!.
🤣🤣🤣🤣
CCM ya Makala na Nchimbi, Iko wapi?? Mbona imepoteana .🤣🤣🤣🤣
 
Kwa kupanda mapunda?...Acha upumbavu kuwa mwerevu
 
Hivi kwa akili yako tu ya kuvukia barabara unaweza kuniambia bashite ana hoja gani za kuitetemesha chadema? Tatizo mmezoea kuishi kwa maigizo
Leo hii unaweza kumwambia Makalla aitishe mkutano wa hadhara na Makonda aitishe na utashangaa watu wamejaa mkutano wa Makonda bila hata kuambatana na wasanii.

Ni rahisi raia wa kawaida kwenda kwenye mkutano wa Makonda na sio mkutano wa Makalla au kumsikiliza.

Sasa kwenye siasa mtaji ni watu ambao hupiga Kura pia, unaweza kusema hao wanaompenda ni wajinga ukawa sawa lakini ndio kundi kubwa la wananchi na kundi hilo ndio linalochagua viongozi ukiweza kuteka hisia zao kisiasa unakua umeshinda.

Siasa zinataka idadi ya watu sio kingine kama utapata idadi kubwa ya watu uwezekano wa kupigiwa kura ni mkubwa Sana.

Ukiniuliza Makalla na Nchimbi wanaushawishi kwa siasa za sasa zenye kundi kubwa la vijana waliozaliwa miaka ya 90 mpaka 2000 jibu ni hapana.

Lissu anaweza kuligusa kundi la vijana vizuri na Makonda anaweza ila Nchimbi na Makalla hapana.

Ukiuliza Makonda amefanya nini itabidi tuulize Makalla amefanya nini? Kazi ya kukieneza chama inataka mtu mwenye ushawishi Sana.

Kuna mkoa alipita Makonda kama mwenezi viongozi wa chama hawakupata tabu ya kukusanya watu ilikua rahisi ni kutangaza tu Makonda anakuja watu wanajaa uwanjani lakini walipopita Nchimbi na Makalla ilibidi mpaka wasanii pia wawepo lasivyo ingekua shughuli pevu kupata watu uwanjani.

Siasa ni namba ya watu(wapiga Kura) haijalishi uelewa wao ni wa miwango gani.

Wananchi wanapata hisia kwamba Makonda anaweza kutatua shida zao hata kama hawezi hata kama ni maigizo ila wanaimani Sana na Makonda. Nadhani pia kuna watu wanatokea kupendwa tu bila hata sababu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…