Mwigulu Nchemba: Hakuna mwananchi atakayelipa mkopo, Serikali italipa

Mwigulu Nchemba: Hakuna mwananchi atakayelipa mkopo, Serikali italipa

Ama kweli hizi phd za mawaziri wetu naanza kukubaliana na wanaozitilia mashaka. Mchumi mzamivu kama anasema serikali ndiyo inalipa madeni na si wananchi hii inaleta ukakasi si kidogo. So kodi za wananchi zinaenda wapi? Tozo za wananchi zinaenda wapi? Masurufu ya wananchi yanaenda wapi? Serikali yenyewe hizo hela za kulipa inazichimba shimo gani? Hayo labda alikuwa anawaambia wanyaturu wenzie ws Kiomboi vijijini wasiojua hata kodi ni nini na kuwa labda serikali ni dudu linalotema hela.
 
Dah DR inakuwaje tena uchumi wa wapi huu mlipa deni ni mwananchi kupitia kodi za kila siku.
Zinatumika zaidi ya 800bil toka kwenye kodi yetu kulipa madeni sasa unasemaje kuwa mwananchi hatawajibika kulipa deni.
Uchumi wa wapi huu jamani?
Mkuu iamini serikali; hakuna mwananchi atakayeombwa fedha ya kulipa deni la taifa. Serikali italipa. Full stop.
 
Dah DR inakuwaje tena uchumi wa wapi huu mlipa deni ni mwananchi kupitia kodi za kila siku.
Zinatumika zaidi ya 800bil toka kwenye kodi yetu kulipa madeni sasa unasemaje kuwa mwananchi hatawajibika kulipa deni.
Uchumi wa wapi huu jamani?
Anamaanisha hakuna pesa ya ziada itakayowekwa kwa mwananchi kwa ajili ya kulipa mkopo zaidi ya makusanyo ya tozo na kodi zilizopo, misaada na michango. Kwa ufupi mapato ya serikali.
 
Wadau naomba kufahamu kama Tozo ni jambo la Muungano.
Kwani nimemskia Waziri wa Fedha Bw. Mwigulu Nchemba akidai kuwa kwa Mwezi wa Dec 2021. Zanzibar imepelekewa Bil. 161Tshs ili hali Bara Tshs Bil 91. Ina kuweje Pesa za Walipa kodi wa Bara ziende Zanzabar? Zanzibar ina watu wake wa kulipa Tozo. Inakuweje hii? Je ina maana kila mwezi Pesa za Bara zina pelekwa Zanzibar? Au ndio kujipendekeza bila kujali Sheria, taratibu na misingi ya Muungano pamoja na Sera za Fedha?
Zanzibar haina mapato ya kutosha kujiendesha kama nchi. Kwa kuwa sote tunajenga nchi moja, sio vibaya pesa kukamuliwa kutoka Tanganyika na kuwapelekea wazaznzibar ili nao wajikwamue kiuchumi. Nao ni wenzetu, tusiwatenge.
 
Zanzibar haina mapato ya kutosha kujiendesha kama nchi. Kwa kuwa sote tunajenga nchi moja, sio vibaya pesa kukamuliwa kutoka Tanganyika na kuwapelekea wazaznzibar ili nao wajikwamue kiuchumi. Nao ni wenzetu, tusiwatenge.
Kwa sheria ipi?
 
Anaposema serkali italipa anamaanisha nini?
1. Kwamba Tozo si za wananchi
2. Kuwa kodi ya mwananchi
3. Kwamba maliasili si za wananchi
Hivi Serkali ina mapato tofauti na wananchi na maliasili zao?

Huyu ni Phd holder
Shida ya mtu aliyetokea kijijini akachunga ng'ombe akasoma akapata cheo huwa anakuwa limbukeni wanajidai Sana Mana hakutegemea ni sawa mtu Aliye win jackpot atasumbua mtaa mzima tumjue.
Basi Kama vipi Kodi zetu zitufanye Mambo yetu ya kijamii afu tuone hiyo serikali watoe hela zao
 
Hawa ndio wasomi wetu na wanasiasa wachumia tumbo na PhD za kuunga unga. Wanafikiri sisi wote ni mazuzu. Hawajui kuwa wao ndio mazuzu. Wameacha kutumia ubongo kufikiri badala yake wanatumia matumbo....... Ni aibu na fedheha kubwa sana kuwa na wasomi wa aina hii.
Wamekariri tu madesa akatapika kwa exam akafaulu basi. Amefanya Nini Cha kusaidia Taifa lake ama Kijiji chake kuwa ni msomi
 
Kwa sheria ipi?
Rais mwenyewe ni SHERIA; lolote analoamua kwa manufaa ya nchi halipaswi kupingwa na mtu yeyote. Hata Mwendazake aliamua kujenga reli bila kumshirikisha mtu yeyote na hakuna aliyehoji. Sasa hivi watu wanahoji kwa kuwa wanamdharau Rais Samia kwa sababu ni mwanamke.
 
Rais mwenyewe ni SHERIA; lolote analoamua kwa manufaa ya nchi halipaswi kupingwa na mtu yeyote. Hata Mwendazake aliamua kujenga reli bila kumshirikisha mtu yeyote na hakuna aliyehoji. Sasa hivi watu wanahoji kwa kuwa wanamdharau Rais Samia kwa sababu ni mwanamke.
Maana ya kuwa na Sera, sheria na Katiba ni ipi?
 
Wadau naomba kufahamu kama Tozo ni jambo la Muungano.
Kwani nimemskia Waziri wa Fedha Bw. Mwigulu Nchemba akidai kuwa kwa Mwezi wa Dec 2021. Zanzibar imepelekewa Bil. 161Tshs ili hali Bara Tshs Bil 91. Ina kuweje Pesa za Walipa kodi wa Bara ziende Zanzabar? Zanzibar ina watu wake wa kulipa Tozo. Inakuweje hii? Je ina maana kila mwezi Pesa za Bara zina pelekwa Zanzibar? Au ndio kujipendekeza bila kujali Sheria, taratibu na misingi ya Muungano pamoja na Sera za Fedha?
Huu muungano hutakuja kuitoa CCM madarakani au utaleta mpasuko. Maana naona mama yupo busy na zanzibar yake.

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
 
Waziri wa Fedha na Mipango Dr Mwigulu Lameck Nchemba (PhD) leo amewaondoa wasiwasi wananchi wanaolia kwa sababu ya ukubwa wa deni la taifa (Trilion 70+) kwamba hakuna mtanzania hata mmoja atakayegongewa mlango au kutakiwa kutoa mali zake binafsi ili kulipia deni la taifa. Amesema deni hilo litalipwa na serikali yenyewe kwa fedha zake bila mwananchi yeyote kutakiwa kutoa hata senti moja ili kulipia deni. Msikilize wewe mwenyewe kwenye klipu hii hapo chini 👇 👇 👇 👇 👇
View attachment 2068601
Dr Mwigulu alisema hayo wakati Rais Samia alipokuwa akihutubia Baraza la Mawaziri ikulu Jijini Dodoma ili kuweka mambo sawa baada ya Spika wa Bunge kuwa mbogo kuhusiana na ukubwa wa deni la taifa ambapo Spika alisema kuwa serikali ya Samia isipokuwa makini kwenye ukopaji, ipo siku nchi hii itauzwa kwa sababu ya ukubwa wa madeni.

MAONI YANGU
Nawaomba wananchi tutulie, tuache kupapalika bila sababu kwa kuwa sasa tumehakikishiwa kwamba hatutahusika hata chembe kwenye ulipaji wa deni la taifa. Nawashangaa sana watu wanaowapotosha wananchi kwa makusudi kuwa watahusika kwenye ulipaji wa deni la taifa huku wakijua fika kwamba serikali itajilipia yenyewe deni lake. Tuache upotoshaji ndugu watanzania. Kuna makundi ya watu wabaya wanaotumia na watu wasioitakia mema nchi hii kuifarakanisha serikali na wananchi wake. Tuwe makini! ✍️
Madeni yote ya Tanzania tunalipa sisi wananchi kupitia kodi. Mwigulu ni muongo anapaswa kushitakiwa kwa kupotosha. Waache kukusanya kodi basi kama wananchi hatulipi kodi.
 
Maana ya kuwa na Sera, sheria na Katiba ni ipi?
Rais akiona nchi haiendi anayo mamlaka ya kutupa sheria na sera pembeni na kutawala kwa sheria zake binafsi. Na kumbuka Rais ni kama Mungu; huwa hahojiwi na mtu yeyote. Mbona Mwendazake alikuwa anatawala kwa sheria zake binafsi mlikuwa hamseni? Kwanini sasa?
 
Ndugu yangu una akili kichwani kweli??? Madeni yote ya Tanzania tunalipa sisi wananchi kupitia kodi. Mwigulu ni muongo anapaswa kushitakiwa kwa kupotosha. Waache kukusanya kodi basi kama wananchi hatulipi kodi.
Haya sio maneno yangu mkuu; ni maneno ya Mwigulu Nchemba . Hebu msikilize kwenye klipu hapo juu.
 
Huu muungano hutakuja kuitoa CCM madarakani au utaleta mpasuko. Maana naona mama yupo busy na zanzibar yake.

Sent from my SM-J250F using JamiiForums mobile app
Kama anaipenda Zanzibar. Akawanie Urais Zanzibar. Mambo ya kuchukua pesa za Bara na kupeleka Zanzibar hatutaki! Watu mil 2 vs mil 60+
 
Rais akiona nchi haiendi anayo mamlaka ya kutupa sheria na sera pembeni na kutawala kwa sheria zake binafsi. Na kumbuka Rais ni kama Mungu; huwa hahojiwi na mtu yeyote. Mbona Mwendazake alikuwa anatawala kwa sheria zake binafsi mlikuwa hamseni? Kwanini sasa?
Una bwabwaja tu.
 
Back
Top Bottom