Mwigulu Nchemba: Serikali imekusanya bilioni 48 kutoka kwenye Tozo za miamala ya simu kwa wiki nne

Mwigulu Nchemba: Serikali imekusanya bilioni 48 kutoka kwenye Tozo za miamala ya simu kwa wiki nne

$14.2bn over the next five years to construct a 2,561km
The Tanzanian Government intends to invest around $14.2bn over the next five years to construct a 2,561km standard-gauge railway network, which will connect its Indian Ocean port of Dar es Salaam to the other regions within the country. Source : Turkey's Yapi Merkezi wins $1.92bn Tanzania railway contract

UFUJAJI WA KODI ZA WANANCHI NA KUWAZIDISHIA MZIGO WA MADENI YA TAIFA
Serikali hii inapoteza fedha kwa miradi isiyo na maana. Mfano ujenzi wa SGR Reli ni upotevu wa fedha . Ilitakiwa waiimarishe reli ya kati na kurekebisha sehemu kadhaa korofi kwa kujenga madaraja au mahandaki siyo kutandika reli mpya ya SGR mwanzo-mwisho pamoja na stesheni za gharama zenye nakshi za kutafuta ufahari usiolingana na uwezo wa mradi huo kuendeshwa kiuchumi.

Mfano ikiwa reli ya kati inaweza kubeba mzigo wote huu kutoka DSM ukafika Malampaka mpaka Mwanza kunahaja gani ya ujenzi wa reli Mpya ya SGR ?

19 August 2021 Reli ya kati yahimili kubeba mzigo wote huu wa makatapili na malori

VIFAA VYA UJENZI WA SGR MWANZA ISAKA VYA WASILI


Huku ni kutafuta ufahari usiokuwa na maana wakati hakuna mizigo ya ndani ya nchi itakayosafirishwa kwa wingi pia nchi jirani siku zote wana mbadala wa wapi waipitishe mizigo hivyo kwa uchambuzi pembuzi yakinifu wa kawaida kabisa ujenzi wa reli ya SGR MPYA ni ufujaji na upotevu wa fedha za umma na kuitwisha nchi madeni ambayo yangeepukika kwa kuimarisha tu sehemu korofi za reli ya mkoloni au ujenzi wa madaraja imara na mahandaki badala ya kuwa na mradi wa matrilioni ya pesa wakati nchi uchumi wake hauwezi kuhimili dizaini ya mradi mzima wa reli mpya.

RELI YA KATI YA MKOLONI YABEBA TANI 900 ZA MIZIGO KWA MKUPUO MMOJA


Video zote Source : TRC RELI TV
 
Watanzania ni wavivu wa kuyatafakari mambo kwa kina ... Wengi ni wafuata mkumbo..

Naona kuna hata MATAGA yanapiga kelele.. Ila yalikuwa yakimshangilia Magufuli alivyoigeuza nchi yote ka pocket money yake...

Miradi yote kaanzisha yeye...pesa zote alikomba yeye...

Watu tuliishi ka madigidigi na bado alikuwa akitutukana...na kufilisi watu na kuwafungia biashara zao.

Wapumbavu na wavivu wa kufikiri wanafikiri Rais Samia kuna pesa yeyote kaikuta..

Tutafakafi mambo kwa kina na sii kusubiri kutafakariwa.

Hii miradi Mama ana uwezo wa kuisusa. Anaongozwa na Busara

Wapumbaavu wana CCM ambao mnajitoa akili makusudi kabisa dawa yenu inachemka.

Mama songa Mbele..

Una maadui wengi.
 
Hapa nimejifunza kitu kimoja kuwa kipanya ni mtu wa ndani anayejua mipango yote huko ndani ndio maana katuni zake zinafikirisha sana ila ziko wazi sana kutoa ujumbe sahihi.

Ona hiyo juu imetoka leo msela anasepa na maburungutu ya mapato ya serikali. Madelu kaja kuuthibitishia umma wa watanzania kuwa imekusanywa 48.4

Bilioni na wamepeleka 22Bilioni kwenye miradi hivyo 26.4Bililioni imeyeyuka ila kipanya katuonesha kuwa kuna kigogo kasepa nayo home.
 
Serikali hii inapoteza fedha kwa miradi isiyo na maana. Mfano ujenzi wa SGR Reli ni upotevu wa fedha . Ilitakiwa waiimarishe reli ya kati na kurekebisha sehemu kadhaa korofi kwa kujenga madaraja au mahandaki siyo kutandika reli mpya ya SGR mwanzo-mwisho...
Waambie MATAGA wanafikiri hiyo ni miradi ya Mama.
 
Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amesema katika kipindi cha wiki nne Serikali imekusanya Sh 48.4 bilioni kutokana na tozo za miamala ya simu, na zaidi ya Sh22 bilioni zimepelekwa katika vituo vya afya zaidi ya vituo 90...
Sawa, tupate na mrejesho wa hizo zahanati zikimalizwa
 
Mambo yote saivi tunamaliza sisi wa hali ya chini😖😖😭😭
 
Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amesema katika kipindi cha wiki nne Serikali imekusanya Sh 48.4 bilioni kutokana na tozo za miamala ya simu, na zaidi ya Sh22 bilioni zimepelekwa katika vituo vya afya zaidi ya vituo 90...
Lameck kadanganya Data. Kwa mahesabu yangu kwa siku wanakusanya 10 billion. Kwa iyo billion 300 kwa mwezi. Billion 248 zingine wanazoficha zinaenda wapi? Waache kutupotosha mara moja. Billion 48 kwa mwezi ni kidogo sana.

Nnaandika haya kwa uchungu kwasababu mimi ni mlipa kodi
 
Itabidi accounts za makusanyo za serikali Zia's decentralized kama serikali inataka kuaminika maana hapa inaonekana kuna mabilioni yanakwenda kwenye acc za mtu kwaajili ya kampeni 2025
 
17 August 2021
RELI YA MKOLONI YABEBA MAFUTA YA KWENDA UGANDA KWA UFANISI. MRADI WA RELI SGR MPYA NI UFUJAJI WA FEDHA ZA KODI ZA WANANCHI


Hakukuwa na haja ya serikali kujiingiza ktk mradi mkubwa wa ujenzi wa reli mpya ya SGR. Ilitakiwa waiimarishe reli ya kati ya mkoloni kwa kujenga madaraja na mahandaki sehemu korofi na kuimarisha reli nzima ya zamani. Mzigo huu wa mafuta unapelekwa Uganda kwa reli hii hii ya zamani huo ni uthibitisho tosha kulikuwa hakuna ulazima wa ujenzi wa reli Mpya ya SGR mwanzo mwisho ulio na makolombezo yote ya ufahari usio na ulazima wowote kiuchumi.
 
Kodi watu hawapingi,, shida ya nchi hili ni ubadhilifu, kesho na keshokutwa unasikia fedha zimechotwa, sijui nanii kapiga bilioni 2, halafu wanachekeana, lau kama wangekuwa serious(mafisadi wachukuliwe hatua, matumizi ya serikali yapunguzwe, wabunge mishahara ipunguzwe, walipe kama wengine, na kero ndogo ndogo) sio tu kodi, bali wananchi tungekuwa tuko radhi kuchangia mradi fulan.. Tuliweza kuwachangia watani(yanga) [emoji23][emoji23]ndio tushindwe vitu vya msingi kwa serikali yetu bwana.
Acha ujinga, nani kasema anataka kukatwa. Tunataka kukatwa kodi halali, siyo hii y kisenge
 
Wakuu,

Waziri wa Fedha, Dr Mwigulu Nchemba anazungumza na waandishi wa habari muda huu kuhusu miradi ya Serikali pamoja na Tozo za miamala ya simu pamoja na mafuta. Kuwa nami kukujuza yanayojiri

==========

Mwigulu Nchemba-Waziri wa Fedha na Mipango
=▷
Itakuwa aibu mtanzania yoyote alie hai, kuna mradi umekwama kwasababu tu viongozi waanzilishi labda hawapo duniani au hawapo kwenye madaraka, itakuwa aibu ya kila mtanzania alie hai leo.

=▷ Katika kipindi cha wiki nne Serikali imekusanya Sh 48.4 bilioni kutokana na tozo za miamala ya simu, na zaidi ya Sh22 bilioni zimepelekwa katika vituo vya afya zaidi ya vituo 90

=▷
Kipindi cha mwezi mmoja Serikali imekusanya Sh 24 bilioni, kutokana na tozo za mafuta ambazo ni mahususi kwa ajili ya kujenga barabara.

=▷ Kama serikali tutaendelea kupokea na kuyafanyia kazi maoni yote, na haijalishi mtoa maoni yuko Serikalini au la, kwetu maoni ni maoni muhimu maoni hao yanalenga kujenga nchi yetu





=▷ Tuliokuwepo hapa ni dhamana tu, la msingi hata yote tunayofanya ni yetu na ni njia ya kupangalia namna ya kuyafanya, ndio maana ndio maana kiongozi wetu mkuu alisikia sauti hizo na akaelekeza kwamba haya mambo yafanyike.

=▷ Imechukua muda, ni utaratibu tu za kiutekelezaji wa maelekezo na sababu nitazielezea mbele, huwa tunahusisha na makundi mengine ambayo yako nje yetu sisi.

=▷ Mheshimiwa Rais akishakuwa na malengo mazuri namna hii na kule vijijini kwenye maeneo yetu, yakishakuwa mazuri hivi tusigombane kuhusu malengo wala khusu utaratibu. Tushauriane tu namna ya kufanya vizuri kwa ufanisi mzuri zaidi.

=▷ Tunapata ufanisi zaidi tukifanya hivyo, watanzania wanaoishi vijijini na wanaoishi mjini wote wajione wako Tanzania.

=▷ Hii ndio itakayotuondlea pengo la walionacho na wasianacho, zamani ilikuwa inatokea wanafanya mtihani, kijiji kizima hatokei hata mtoto mmoja aliefaulu kwahiyo kuboresha hii miundombine, afya watanzania tukibebe kwa yowe kabisa kwa sababu ni chetu. Niwaombe watanzania kuendela kuwa watulivu na wavumilivu.
Ukimsikiliza Nchemba, unagundua kwamba tuna mawaziri wenye uwezo mdogo sana wa akili. Ni mtu hawezi hata kuzungumza na umma. Hawezi hata kuonesha kwamba ana digrii moja. Hata usoni haoneshi kama ana akili timamu. What a hell with this creature?
 
Back
Top Bottom