TANZIA Mwili wa Ulomi, Mfanyabiashara aliyedaiwa kupotea wakutwa mochwari Mwananyamala

TANZIA Mwili wa Ulomi, Mfanyabiashara aliyedaiwa kupotea wakutwa mochwari Mwananyamala

Baada ya Assad kuangushwa Wananchi waliaamua kuingia kwenye Magereza ya Assad na kugundua ukatili mkubwa sana ulikuwa unafanywa kwa Wasyria.

Pengine hata Tanzania tuna sehemu kama hizo nyingi na kibaya ukute zinafanywa na watumishi wa ngazi za chini kwa umaskini tu.

Huyu Ulomi kwa hizi biashara zilizoandikwa hapo ni mtu wa kawaida sana na ninaweza kusema ni poor na si mtu wa kuwa tishio kiasi hicho.

Maoni yangu hawa vijana wa Vyombo vya ulinzi wanavimb sana kichwa na pengine wanavuka mipaka yao ya kazi na kuuanza kuwa waalifu, Serikali iliangalie hili kabla ya kuwa too late
 
Mfanyabiashara Daisle Simon Ulomi, aliyepotea tangu Desemba 11, 2024 amekutwa amekufa na mwili wake kukutwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam.
View attachment 3177965
Ulomi aliyekuwa akifanya biashara za fedha za mitandao ya simu maeneo yaa Sinza Kijiweni na Mwenge alipotea tangu 11 Desemba 2024.

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro zinaendelea, baada ya simu zake kuita bila kupokelewa.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, Desemba 16, 2024 baba mkwe wa Ulomi, Japhet Munisi amesema alipigiwa simu leo asubuhi na mke wa marehemu, akimjulisha kuwa amepata taarifa kuwa mwili wa mumewe uko hospitali.

Pia, Soma:

Mfanyabiashara Ulomi apotea, familia na Polis wanamtafuta
TRA: Hatuhusiki na kupotea kwa mfanyabiashara Daisle Simon Ulomi
Polisi waanza kumtafuta Ulomi anayedaiwa kupotea
Mwananyamala wao wamepokea mwili WA Marehemu kutoka kwa Nani?
 
Taarifa za awali wakati wa kupotea kwake zilisema alikuwa anaelekea kufuatilia mizigo yake (Kontena) bandarini, na TRA wakatoa ufafanuzi kuwa wao hawahusiki na kwamba marehemu alikuwa akimtumia wakala mwingine wa forodha (binafsi)

Kwa aina ya biashara zilizoorodheshwa hapa sijaona yoyote inayohusiana na masuala ya kufuatilia mizigo.

Marehemu ana biashara nyingine? Kufuatilia kwake mizigo yake kuna uhusiano wowote na kifo chake?

Maswali ni mengi, apumzike kwa amani.
 
Wakuu,

Mwili wa Mfanyabiashara Daisle Simon Ulomi aliyepotea tangu Desemba 11, 2024 umekutwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam akiwa amefariki Dunia.

Mwananchi Digital leo Jumatatu, Desemba 16, 2024 imeripoti kuwa baba mkwe wa Ulomi, Japhet Munisi amesema alipigiwa simu leo asubuhi na mke wa marehemu, akimjulisha kuwa amepata taarifa kuwa mwili wa mumewe uko hospitali.

Mnamo Desemba 14, 2024 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaanm SACP Muliro J Muliro alitoa taarifa kuwa Jeshi la Polisi lilipokea taarifa ya kupotea kwa Daisle Simon Ulomi, ambaye hakurudi nyumbani kwake toka alipoingia kazini kwake Disemba 11.

Muliro alisema kuwa siku hiyo Ulomi alionekana akitoka ofisini kwake Sinza Kijiweni majira ya saa 6:00 mchana kuelekea Mbagala, Bandari kavu alikodai anaenda kukagua ‘container’ la bidhaa zake baada yakuitwa na watu aliodai ndiyo waliokuwa wanashughulika na kutoa kontena hilo bandarini na alikuwa akitumia pikipiki namba MC 415 DQC aliyokuwa akiendesha mwenyewe.
 
Vifo vingine vinatokana na dhuruma nk. Sidhani kama kufikiria serekali ya fisiemu inauwa hawa watu wote ni sahihi
Huyu kaka hakuumwa lakini leo anakutwa amefariki.

Mnaotenda huu ukatili mtakosa amani ya moyo hata kama mnaishi kwenye mahekalu na kuendeshwa kwenye VX.

Hizi damu na masononeko lazima zitawawesesha kupita maelezo.
let be reasonable guys. Serekali haiwezi kuuwa watu hovyo ikuuwe ww nani!!?? Yani serekali ije ikuuwe ww tigopesa kuweni na heshima kidogo basi
 
Back
Top Bottom