Mwisho wa Kariakoo huu hapa: Serikali yapitisha gulio la Wachina Kurasini

Mwisho wa Kariakoo huu hapa: Serikali yapitisha gulio la Wachina Kurasini

Wachina unawajua au wawasikia?
Wale wanatakiwa waje Tz kujenga viwanda na si vinginevyo
Mkuu, kila kitu ni udhibiti, halafu hakuna mtu anakuja tu puup ajenge kiwanda, watakuja watauza watakapoona soko ni zuri kuna watakaoshawishika kujenga viwanda ila lazima wafanye biashara kwanza, watengeneze soko. Maendeleo ni hatua.

Mchina akileta bidhaa kutoka china akaziuza hapa kwa jumla ni nafuu kwa mfanyabiashara wa kitanzania kuliko akiufata mzigo china. Hata bei zitakuwa za kiushindani na kupelekea unafuu kwa mtumiaji wa mwisho. Hatuwezi jifungia watanganyika tu milele, lazima tufunguke halafu tuweke mifumo ya udhibiti. Kuna tofauti kubwa ya Dar na Moshi au Iringa sababu watu wa dar waliruhusu wageni, leo dar kila mtanganyika anataka kwenda.

Imagine bidhaa zinazohitaji vifungashio bora kama utavipata kiwepesi hapa badala ya kuviagiza China itakavyoboost wenye viwanda vidogo vidogo huko mikoani. Sasa hivi mmakonde kapambana kafungua kakiwanda kake ka kupaki unga kilo moja moja huko umakondeni vifungashio mpaka aagize China na hiyo exposure hana.
 
Kati ya vitu vya kijinga serikali inaenda kufanya kwa watu wake ni kuua soko la Kariakoo kwa kuruhusu gulio la Wachina Kurasini ili wauze bidhaa zao bila kodi na kodi ikusanywe pale tu bidhaa inapotoka.

Hizi akili itakuwa kazitoa Mwigulu lakini ikitokea hili limefanikiwa basi Kariakoo haitakua na watu tena. Wachina tunawajua wanauza mpaka miwa wale na bei yao hutaweza kushindana nao kwa sababu wanapewa backup kubwa na Serikali yao.

Tuwe tunafikiria kwa kutumia kichwa.
Itakuwa poa sana
 
Usikute hii hasara ya nchi ni katika lile dili la kumuokoa Ridhiwani asinyongwe China pale alipokamatwa na makontena ya madawa ya kulevya. Sitoshangai kama Kikwete alihusika hapa, Ridhiwani kalitia hili taifa hasara sana eti leo kawa naibu waziri?
Huko kwenye anako naibu watu wanalia kweli kweli; ardhi inoporwa TU.
 
Kati ya vitu vya kijinga serikali inaenda kufanya kwa watu wake ni kuua soko la Kariakoo kwa kuruhusu gulio la Wachina Kurasini ili wauze bidhaa zao bila kodi na kodi ikusanywe pale tu bidhaa inapotoka.

Hizi akili itakuwa kazitoa Mwigulu lakini ikitokea hili limefanikiwa basi Kariakoo haitakua na watu tena. Wachina tunawajua wanauza mpaka miwa wale na bei yao hutaweza kushindana nao kwa sababu wanapewa backup kubwa na Serikali yao.

Tuwe tunafikiria kwa kutumia kichwa.
Umekurupuka sana, najua umeitoa kwenye clip ya Bashe inayotrend ambayo aliitoa miaka karibu kumi imepita, Kurasini palitakiwa kujengwa Logisticts Center itakayounganishwa na Bandari ya DSM ili pawe duty free, baadae Serikali ikaja na mpango mpya wa kujenga Special Economic Zone ambayo itakuwa na viwanda pamoja na duty free shops. Hii ni fursa ya kila mfanyabiashara na fursa ya nchi yetu kuifanya DSM kuwa kitovu cha biashara Afrika Mashariki na Kati. Badala watu kukimbilia China waje hapa wanunue duty free products wapeleke nchini kwao wakalipe kodi huko.

Pale Ubungo ndio panajengwa hilo mnaita Gulio, ni mradi huru kwa kila mtu, hata wewe unaweza kununua space, ukaenda China ukaleta mzigo wako pale bila kodi ukauza alafu Mamlaka za forodha na mambo mengine nazo zitakuwa pale kuhakikisha kodi inalipwa baada ya mauzo kama ambavyo inafanyika kwenye show rooms za magari. Sasa ukija na mada siku nyingine chukua muda wako kujua namna mambo yanakwenda na sio kutujazia server tu.
 
Back
Top Bottom