My week end is super crazy

My week end is super crazy

Watazoea na wataacha kutapika.

Mpaka ifike november nyumba itakuwa haitamaniki.
Ngojea nione nitajaribu polepole.

Hlf vikiongea na mama yao wanasema wanampenda aunty hawataki kurudi nyumbani😁 kirohon nasema mtoto hata akukasirishe vipi ni ngumu kumchukia.Hata havijui kama vinanipa stress masikin na ninataman waondoke nipumur😁
 
Acha kulea watoto kimayai hao ma auncle ni damu yako huo mwezi mmoja unatosha kuwabadili mentality zao!

Wafundishe kitu tofauti kumbuka MTOTO UNAVYOMLEA...
Huko kwao ndo wamelelewa kimayai mkuu.
Halafu mi naona haisaidii kutumia nguvu kustrress wabadilike hlf baada ya wiki chache wanarudi kwao kudekezwa tena.

Wangekua wamehamia kwangu moja kwa moja lazima ningewabadilisha
 
Siwezi kuwarudisha hadi wazazi wao warudi,wamesafiri nje ya Tz na mimi mwenyewe ndo nilisema waletwe kwangu coz navipenda ila nimejua hawa inabidi mapenz ya mbalimbal,wakichukuliwa sitarudia tena kuvichukua
.
Pole sana. Hawa watakuwa watoto ambao wazazi wanalea kwa ule mfumo mpya wa 'gentle parent' mtoto haambiwi hapana, hafokewi, hachapwi.

Mtoto wangu wa kwanza tulilea kitaliban kama mimi nilivyokuzwa so far so good, mwanangu wa pili wamepishana miaka 5 nikasema hebu nifanye hiyo gentle parenting eh, heheheee..ananitoa jasho akianza kulia mtaa mzima unajua, na hapo sijatandika. Hizo tantrum sio za dunia hii. Mwanangu wa 3 sasa huyu sirudii kosa tunafanya vyote. Kuna namna nikimkata jicho anajua sichezi lakini huyu wa pili ananibully mpaka sasa 😂😂
 
Huo upuuzi kwangu hapana, mzazi wao angewatafutia kwa kwenda mapemaa
 
Pole sana. Hawa watakuwa watoto ambao wazazi wanalea kwa ule mfumo mpya wa 'gentle parent' mtoto haambiwi hapana, hafokewi, hachapwi.

Mtoto wangu wa kwanza tulilea kitaliban kama mimi nilivyokuzwa so far so good, mwanangu wa pili wamepishana miaka 5 nikasema hebu nifanye hiyo gentle parenting eh, heheheee..ananitoa jasho akianza kulia mtaa mzima unajua, na hapo sijatandika. Hizo tantrum sio za dunia hii. Mwanangu wa 3 sasa huyu sirudii kosa tunafanya vyote. Kuna namna nikimkata jicho anajua sichezi lakini huyu wa pili ananibully mpaka sasa 😂😂
Pole na hongera mkuu.


Halafu nahisi wakishadekezeka kuwakazia inakua ngumu
..

Yaani wewe ndo umenielewa hasa hapo kwenye kilio.Ni kama wanalia kukukomoa,😁 .
Mimi nikipata mtoto sitafanya kosa la kudekeza.

Pole kwa kuwa bullied na sec
born.😁 na wanavyojiamin sasa hata umtishie haisaidii.
 
Huo upuuzi kwangu hapana, mzazi wao angewatafutia kwa kwenda mapemaa
Nakuelewa dear ila wazazi wao wako nje na mim ndo nilijitolea kukaa nao mpaka warudi
 
Pole na hongera mkuu.


Halafu nahisi wakishadekezeka kuwakazia inakua ngumu
..

Yaani wewe ndo umenielewa hasa hapo kwenye kilio.Ni kama wanalia kukukomoa,😁 .
Mimi nikipata mtoto sitafanya kosa la kudekeza.

Pole kwa kuwa bullied na sec
born.😁 na wanavyojiamin sasa hata umtishie haisaidii.
Asante sana dear, bado napoa😂😂
 
Binafsi huwa sioni furaha ya kudekeza mtoto..
Ile ongea yao ya kimideko hasa likiwa la kiume huwa nakereka sana..

Napenda sana mtoto awe rafiki sio kuact kule kudekadeka hata huwezi kwenda nae mahali maana atakutia aibu.
 
Huo sasa mtihani, mpka warudi umepungua kilo.
Acha tu ndugu.
Nimetoka kupiga patrol vyumban kwao sasa hivi vimelala so peacefullly hadi nafsi inanisuta jinsi navisema huku JF😀.
Vinavutia sana vi min monster vyangu😀
 
Binafsi huwa sioni furaha ya kudekeza mtoto..
Ile ongea yao ya kimideko hasa likiwa la kiume huwa nakereka sana..

Napenda sana mtoto awe rafiki sio kuact kule kudekadeka hata huwezi kwenda nae mahali maana atakutia aibu.
Kabisa mkuu.
Inatia hasira.
Sema kuna wazazi wanaona kama ndo upendo eti
 
My week end is wacko.

Kuna watoto wazuri wa rafiki yangu watakaa na mimi mpaka katikati ya Nov. ila sijui nisemeje nisionekane wicked aunty ila wamekuja J nne na tayari niko super stressed na Nov. naiona mbali sana

Stress zilianzia kwa jinsi mtoto wangu hataki ku share Tv yake na wenzie sbb wenzie ni wadogo na vitu wanavyopenda kuangalia ni tofauti.

Nikatoa amri waangalie kwa kupokezana ila haikusaidia watoto coz bado hao madogo wageni mmoja wa kike wawili wa kiume.Vitu anavyopenda kuangalia wa kike hivi vijamaa viwili havipendi fulu kugombana.

Yaani ni mashitaka kila dakika.Huyu wa kwangu analalamika madogo wanaharibu vitu chumbani kwake na madogo wanalalamika kaka anawapiga na kuwafukuza chumbani kwake wasiangalie Tv.

Nikasema hizi stress zitaisha kila mtoto akiwa na tv chumbani kwake,nikatuma mtu akaninunulie Tv ndogo 4,zikaja zikafungwa kila mtu akafurahi nami nikasema nitapumua sasa ila nimejidanganya😃😃.eti baada ya kila mtu kupata Tv yake na interest ya kuangalia Tv ikaisha.Yaani madogo hawana muda na hizo Tv.Hela zangu zimepotea bure😭😭.

Hao wawili wa kiume ni mapacha wako very smart ila ni WATUNDU sana.Wamekaa siku mbili tu ila wameshaharibu vitu vingi halafu sasa vikiharibu kitu ukifoka unasikia “aunty you don’t look cute when you are angry” au “my daddy will buy you another one”

Leo asubuhi hivi vi twins vimefanya kitu cha hatari sana nikawatisha kuwa leo nawachapeni,nikaagiza niletewe fimbo mbili kubwa.Kumbe watoto wa watu hawajawaji kuchapwa wala kutishiwa fimbo.Kale ka kike kananiambia “aunty ukiwachapa baba yangu atakuchapa na wewe maana baba kasema mama akituchapa atamchapa na yeye” nikamwambia mimi simuogopi baba yako na fimbo zikija nawachapa kaka zako.

Fimbo zimefika ile watoto wanaziona tu waliteteeka hadi kamoja kakajikojolea na kengine kakatapika kwa panic.Nilishangaa sana maana mie wa kwngu keshakula sana mikwqju.Sasa nikajiuliza hata shule havichapwi hadi vitetemeke vile!

Ikabidi niache mkwara nianze kuvibembeleza na kutupa fimbo.Kale kakike kalivyoona nimetupq fimbo kakanimbia “usingenisikiliza baba yangu angekumaliza”

Huwezi kuamini hawa watoto eti kutishiwa fimbo tu wamelia zaidi ya masaa mawili.Na wanalia kwa kupokezana,huyu akinyamaza ukisema sasa wamenyamaza unashangaa mwengine kapokea .

Nimebembeleza nimechoka hadi na mim nikaingia chumbani kwangu kulia.Watoto hawa sijui baba yao uchumi ukiyumba itakuwaje coz wakitaka kitu lazima wapate la sivyo atalia siku nzima.Akitaka pizza kwa aman yako utahakikisha pizza imefika.Naona ajabu sbb mwanangu nikisema leo ni chai na kiporo cha ubwabwa kanakula.Mwanangu nikisema hata chai na ugali atakula with a smile on his face.Asubuhi ya kwanza the way vilitupelekesha ningekua na sukari ingepanda.Bodaboda walikua wanapishana getini kwetu coz kila tunachotumia sisi kwa breakfast walivikataa na kila kinacholetwa anakwambia sio hiyo ana favorite yake na lazima apate hiyo,unamrudisha boda ikija brand tofaut hali na hapo wako watatu na kila mmoja ana favorite yake.Ukisema uvikazie vitoto vya watu vitashinda njaa nafsi inakataa basi ni kuhangaika hadi kila mmoja apate anachotaka.

Hivi wazazi mnaodekeza watoto wenu faida ni ipi?

Mna upendo sana kushinda sisi wengine au?View attachment 3102518
Wewe ni winga wa kariakoo na ukome kupiga picha za TV kwenye maduka ya watu
 
My week end is wacko.

Kuna watoto wazuri wa rafiki yangu watakaa na mimi mpaka katikati ya Nov. ila sijui nisemeje nisionekane wicked aunty ila wamekuja J nne na tayari niko super stressed na Nov. naiona mbali sana

Stress zilianzia kwa jinsi mtoto wangu hataki ku share Tv yake na wenzie sbb wenzie ni wadogo na vitu wanavyopenda kuangalia ni tofauti.

Nikatoa amri waangalie kwa kupokezana ila haikusaidia watoto coz bado hao madogo wageni mmoja wa kike wawili wa kiume.Vitu anavyopenda kuangalia wa kike hivi vijamaa viwili havipendi fulu kugombana.

Yaani ni mashitaka kila dakika.Huyu wa kwangu analalamika madogo wanaharibu vitu chumbani kwake na madogo wanalalamika kaka anawapiga na kuwafukuza chumbani kwake wasiangalie Tv.

Nikasema hizi stress zitaisha kila mtoto akiwa na tv chumbani kwake,nikatuma mtu akaninunulie Tv ndogo 4,zikaja zikafungwa kila mtu akafurahi nami nikasema nitapumua sasa ila nimejidanganya😃😃.eti baada ya kila mtu kupata Tv yake na interest ya kuangalia Tv ikaisha.Yaani madogo hawana muda na hizo Tv.Hela zangu zimepotea bure😭😭.

Hao wawili wa kiume ni mapacha wako very smart ila ni WATUNDU sana.Wamekaa siku mbili tu ila wameshaharibu vitu vingi halafu sasa vikiharibu kitu ukifoka unasikia “aunty you don’t look cute when you are angry” au “my daddy will buy you another one”

Leo asubuhi hivi vi twins vimefanya kitu cha hatari sana nikawatisha kuwa leo nawachapeni,nikaagiza niletewe fimbo mbili kubwa.Kumbe watoto wa watu hawajawaji kuchapwa wala kutishiwa fimbo.Kale ka kike kananiambia “aunty ukiwachapa baba yangu atakuchapa na wewe maana baba kasema mama akituchapa atamchapa na yeye” nikamwambia mimi simuogopi baba yako na fimbo zikija nawachapa kaka zako.

Fimbo zimefika ile watoto wanaziona tu waliteteeka hadi kamoja kakajikojolea na kengine kakatapika kwa panic.Nilishangaa sana maana mie wa kwngu keshakula sana mikwqju.Sasa nikajiuliza hata shule havichapwi hadi vitetemeke vile!

Ikabidi niache mkwara nianze kuvibembeleza na kutupa fimbo.Kale kakike kalivyoona nimetupq fimbo kakanimbia “usingenisikiliza baba yangu angekumaliza”

Huwezi kuamini hawa watoto eti kutishiwa fimbo tu wamelia zaidi ya masaa mawili.Na wanalia kwa kupokezana,huyu akinyamaza ukisema sasa wamenyamaza unashangaa mwengine kapokea .

Nimebembeleza nimechoka hadi na mim nikaingia chumbani kwangu kulia.Watoto hawa sijui baba yao uchumi ukiyumba itakuwaje coz wakitaka kitu lazima wapate la sivyo atalia siku nzima.Akitaka pizza kwa aman yako utahakikisha pizza imefika.Naona ajabu sbb mwanangu nikisema leo ni chai na kiporo cha ubwabwa kanakula.Mwanangu nikisema hata chai na ugali atakula with a smile on his face.Asubuhi ya kwanza the way vilitupelekesha ningekua na sukari ingepanda.Bodaboda walikua wanapishana getini kwetu coz kila tunachotumia sisi kwa breakfast walivikataa na kila kinacholetwa anakwambia sio hiyo ana favorite yake na lazima apate hiyo,unamrudisha boda ikija brand tofaut hali na hapo wako watatu na kila mmoja ana favorite yake.Ukisema uvikazie vitoto vya watu vitashinda njaa nafsi inakataa basi ni kuhangaika hadi kila mmoja apate anachotaka.

Hivi wazazi mnaodekeza watoto wenu faida ni ipi?

Mna upendo sana kushinda sisi wengine au?View attachment 3102518
Pole Sana..yani Naelewa unachopitia sasa Mimi nashauli pia kuhusu suala la wazazi humu ndani tuzoeshe watoto wetu kwenda Shule kwa usafiri wa kawaida
Mimi ilishanikututa siku moja sitasahau na Siwezi msimulia mtu Anaenijua ni kwamba toka Mwanangu kazaliwa Alikuwa hajawahi
kupanda Dala dala mpaka Amefika Darasa la Tano
sasa Siku moja nikasema ngoja niende nae tu tupande Dala dala nilikuwa naenda kumnunulia vitu vya Shule Aisee ile tumepanda tukakuta nafasi zimejaa msongamano..jasho..kukanyagwa Aisee Alipiga kelele Dala dala nzima wananishangaa tu Sababu Alikuwa Anadai Ashuke mbona niliona Aibu Mimi toka hapo Asubuhi Alikuwa Anapelekwa na gari Shule Saa ya kuludi ni Dala dala na Nilimwambia kabisa Akae Akijua Labda tu Mvua Inyeshe Nahisi hichi kituko kuna hata wazazi kilishawatokea ila ni Aibu kusimulia kabisa.
 
Mwisho wa siku ndo wanakuomba kitu unawaambia hauna, Wanajiongeza halafu mnakuja kulalamika watoto wanalawtiwa sana sikuhizi.
 
Back
Top Bottom