Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Nawashangaa wazazi kwa kutokufukuza. Miaka 24 unaishi kwa wazazi, hivi Africans tutatoboa lini.
Nipe namba za mzazi wako nimpe ushauri
 
Neno langu kwako ni hili,wa swahili husema "' Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu"'
kwa upande wangu naona mama yako anakuwazia mema anatamani akufunze njia ipasayo,ila ulimwengu unakutamani ukufundishe ndo maana unaona mtu aliyekubeba miezi tisa na kukutunza hadi leo una akili ya kumkosoa,unamuona anakupoteza.
Nimalizie kwa kusema mkataa pema pabaya panamngoja.
Ninachojua ni kwamba as long as bado unaishi kwake ni vyema ukamtii.
 
Ni sawa,kwa sababu ana wajibu wa kulea,mbona huulizi uhalali wa mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda shule ,kunywa dawa akiumwa,kula anapokataa kula?
 
ishu sio mimi kuamini au kutoamini, huo ni uamuzi wangu binafsi kwasababu nimeshazidi 18 na nina uwezo wa kupambanua.

ishu ipo kwenye uhuru wa kuabudu. Kwanini tulazimishane?
Kwani wewe ni jinsia gani?
maana kuna imani imeingia isiyohusisha kwenda kanisani wala msikitini
nayo si nyingine bali ni ushoga na usagaji,sasa ni heri umwambie mzazi wako kwamba umejiunga huko
akuondoe hapo nyumbani usiendelee kunajisi nyumba.
Ungekuwa kwangu ningekuwa nimeishakusend hayupo muda mrefu,sema mama yako ni mvumilivu sana.
 
Kwan we unaona ngapi
 
Mjinga Sana huyo
 
Kama alinizaa hata nizeekeje bado ni mtoto wake.
24 yrs bado upo nyumbani unafanya nini? Ndiyo maana mama yako alikuambia wazi kuwa kama unaishi kwake utafuata anachokitaka kwa lugha nyingine alikupa ujumbe wa kuhama kwake.
 
hatar kama ww n mama ajaye hii ni hatar sana ......npm namba za housgirl tafadhal sanaa🤕
 
Your ability to reason is below kindergatten

Una shida wewe binti na hukuwa na haja ya kuweka uzi kama umepanga kudharau watu wanaojitahidi kukushauri...

Kitu naona kwako, wewe ni mtu mwenye ubongo ambao upo enclosed kwenye dimension moja pekee...

Mtu anayeshindwa kutambua uwepo wa mamlaka ya kiroho, ni kama boksi tupu lisilo na mali yeyote ndani yake...
 
Sawa mkuu. So hata wazazi wakiamua nikafanyiwe FGM ni sawa tu kwakuwa ninaishi kwao.
As long as ulizaliwa nao ukuwakuta wanasali kanisan umekuwa bado wanasali kansan bas utaendelea hvyo hvyo had ujitegemee.
Ukiona sasa unataka jiondoa kwenye hayo, umekua mtu mzima, kajitegemee.
 
"Mimi na nyumba yangu nitamtumikia BWANA " .Kama hautaki kumtumikia ni vyema ukajiondoa katika nyumba hiyo ONLY THEN utakuwa na uhuru wa kuamua mambo yako.

Kwa sasa unapoishi home lazima uendane na a, b, c za hapo nyumbani.
 
Hongera! Umefanikiwa kutoka kwenye kundi la wapumbavu.... Sasa umeingia kwenye kundi la watu wenye akili timamu.
 
Kukutana na kusali pamoja ni ustaarabu ukiwa na umri wa kuchambua mema na mabaya unaweza kumuasi Mungu hiyo ni stage I stage II utagundua kwamba Mungu ni msaada Kwa Binadamu.
Ni kweli wapo wachungaji nk WANATUMIA Dini kujipatia KIPATO Kwa kutumia neno la Mungu Kwa MANUFAA binafsi lakini hiyo haimaanishi Kwamba Hakuna umuhimu wa kusali.
 
Sasa kila dini ina muumba wake, huku ni Allah asiyezaa wala kuzaliwa kule ni yesu aliyezaliwa huku ni Budha kule ni Krishna.
Na wote wanahusia vitu tofauti.
Huku anasema nguruwe usile, kule ni ruksa, Huku lazima ubatizwe kule lazima ushahadie.
Umepewa akili ya kuyajua yaliyo mema na mabaya
 
Uko sahihi, kulazimishana dini ni mambo ya zama za kale za giza ila ki Africa utapata tabu sana kuishi na wazazi vichwa vigumu kama hao na pia wao ndio wataonekana wako sahihi kwa sababu Africa dini zimekita mizizi kuliko hata huko zilipotoka.
Suluhisho ni kwenda kuishi kwako mwenyewe.
ishu sio mimi kuamini au kutoamini, huo ni uamuzi wangu binafsi kwasababu nimeshazidi 18 na nina uwezo wa kupambanua.

ishu ipo kwenye uhuru wa kuabudu. Kwanini tulazimishane?
 
Vipi kama angebadili dini awe Muislamu?
Bado ingekuwa ni halali yake kumshinikiza??
Ni halali yake kukushinikiza uende kusali atakako.
Unaishi kwake Kwa nini usifuate Sheria zake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…