Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Nawashangaa wazazi kwa kutokufukuza. Miaka 24 unaishi kwa wazazi, hivi Africans tutatoboa lini.
Nipe namba za mzazi wako nimpe ushauri
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Neno langu kwako ni hili,wa swahili husema "' Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu"'
kwa upande wangu naona mama yako anakuwazia mema anatamani akufunze njia ipasayo,ila ulimwengu unakutamani ukufundishe ndo maana unaona mtu aliyekubeba miezi tisa na kukutunza hadi leo una akili ya kumkosoa,unamuona anakupoteza.
Nimalizie kwa kusema mkataa pema pabaya panamngoja.
Ninachojua ni kwamba as long as bado unaishi kwake ni vyema ukamtii.
 
Ni sawa,kwa sababu ana wajibu wa kulea,mbona huulizi uhalali wa mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda shule ,kunywa dawa akiumwa,kula anapokataa kula?
 
ishu sio mimi kuamini au kutoamini, huo ni uamuzi wangu binafsi kwasababu nimeshazidi 18 na nina uwezo wa kupambanua.

ishu ipo kwenye uhuru wa kuabudu. Kwanini tulazimishane?
Kwani wewe ni jinsia gani?
maana kuna imani imeingia isiyohusisha kwenda kanisani wala msikitini
nayo si nyingine bali ni ushoga na usagaji,sasa ni heri umwambie mzazi wako kwamba umejiunga huko
akuondoe hapo nyumbani usiendelee kunajisi nyumba.
Ungekuwa kwangu ningekuwa nimeishakusend hayupo muda mrefu,sema mama yako ni mvumilivu sana.
 
Nani kakuambia sina uwezo wa kupambanua nipate chakula?
Hata kama basi tuseme sina, inamaana nikikosa huo uwezo basi automatically nakosa na uwezo wa kupambanua imani?
Mbona unalinganisha vitu ambavyo havilinganishiki?
Hivi dini imekula asilimia ngapi ya ubongo wako?
Kwan we unaona ngapi
 
Kwani wewe ni jinsia gani?
maana kuna imani imeingia isiyohusisha kwenda kanisani wala msikitini
nayo si nyingine bali ni ushoga na usagaji,sasa ni heri umwambie mzazi wako kwamba umejiunga huko
akuondoe hapo nyumbani usiendelee kunajisi nyumba.
Ungekuwa kwangu ningekuwa nimeishakusend hayupo muda mrefu,sema mama yako ni mvumilivu sana.
Mjinga Sana huyo
 
Kama alinizaa hata nizeekeje bado ni mtoto wake.
24 yrs bado upo nyumbani unafanya nini? Ndiyo maana mama yako alikuambia wazi kuwa kama unaishi kwake utafuata anachokitaka kwa lugha nyingine alikupa ujumbe wa kuhama kwake.
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
hatar kama ww n mama ajaye hii ni hatar sana ......npm namba za housgirl tafadhal sanaa🤕
 
Your ability to reason is below kindergatten

Una shida wewe binti na hukuwa na haja ya kuweka uzi kama umepanga kudharau watu wanaojitahidi kukushauri...

Kitu naona kwako, wewe ni mtu mwenye ubongo ambao upo enclosed kwenye dimension moja pekee...

Mtu anayeshindwa kutambua uwepo wa mamlaka ya kiroho, ni kama boksi tupu lisilo na mali yeyote ndani yake...
 
Sawa mkuu. So hata wazazi wakiamua nikafanyiwe FGM ni sawa tu kwakuwa ninaishi kwao.
As long as ulizaliwa nao ukuwakuta wanasali kanisan umekuwa bado wanasali kansan bas utaendelea hvyo hvyo had ujitegemee.
Ukiona sasa unataka jiondoa kwenye hayo, umekua mtu mzima, kajitegemee.
 
"Mimi na nyumba yangu nitamtumikia BWANA " .Kama hautaki kumtumikia ni vyema ukajiondoa katika nyumba hiyo ONLY THEN utakuwa na uhuru wa kuamua mambo yako.

Kwa sasa unapoishi home lazima uendane na a, b, c za hapo nyumbani.
 
Hongera! Umefanikiwa kutoka kwenye kundi la wapumbavu.... Sasa umeingia kwenye kundi la watu wenye akili timamu.
 
Kukutana na kusali pamoja ni ustaarabu ukiwa na umri wa kuchambua mema na mabaya unaweza kumuasi Mungu hiyo ni stage I stage II utagundua kwamba Mungu ni msaada Kwa Binadamu.
Ni kweli wapo wachungaji nk WANATUMIA Dini kujipatia KIPATO Kwa kutumia neno la Mungu Kwa MANUFAA binafsi lakini hiyo haimaanishi Kwamba Hakuna umuhimu wa kusali.
 
Sasa kila dini ina muumba wake, huku ni Allah asiyezaa wala kuzaliwa kule ni yesu aliyezaliwa huku ni Budha kule ni Krishna.
Na wote wanahusia vitu tofauti.
Huku anasema nguruwe usile, kule ni ruksa, Huku lazima ubatizwe kule lazima ushahadie.
Umepewa akili ya kuyajua yaliyo mema na mabaya
 
Uko sahihi, kulazimishana dini ni mambo ya zama za kale za giza ila ki Africa utapata tabu sana kuishi na wazazi vichwa vigumu kama hao na pia wao ndio wataonekana wako sahihi kwa sababu Africa dini zimekita mizizi kuliko hata huko zilipotoka.
Suluhisho ni kwenda kuishi kwako mwenyewe.
ishu sio mimi kuamini au kutoamini, huo ni uamuzi wangu binafsi kwasababu nimeshazidi 18 na nina uwezo wa kupambanua.

ishu ipo kwenye uhuru wa kuabudu. Kwanini tulazimishane?
 
Vipi kama angebadili dini awe Muislamu?
Bado ingekuwa ni halali yake kumshinikiza??
Ni halali yake kukushinikiza uende kusali atakako.
Unaishi kwake Kwa nini usifuate Sheria zake?
 
Back
Top Bottom