Mzazi kumpa mtoto chochote anachokitaka ni sawa na kumharibu?

Mfundishe kuwa na kiasi, kwa umri wa miaka 4 atakuwa anaomba vyakula tu, kadiri anavyokuwa anaweza omba hata vitu ambavyo hata wewe huna.
 
wengi wanaosema mpe kila kitu bado hawana watoto, wengi wanaosema utamharibu ni wazazi tayari.
 
Mfundishe kuwa na kiasi, kwa umri wa miaka 4 atakuwa anaomba vyakula tu, kadiri anavyokuwa anaweza omba hata vitu ambavyo hata wewe huna.
Kwani unafikiri anakula bila kiasi?

Anakula kwa kiasi

Sema unaweza pika ugali akataka wali..au akataka chipsi .....kiazi fungu la jero anakaangiwa anakula anafurahi.

Anataka zaidi ya chakula hata baiskeli, mdoli....nk...akiomba nisivyoweza namjibu tu nitakununulia maisha yanasogea.
 
ukishindwa kumcontrol mtoto utotoni itakusumbua ukubwani. sio kila anachoomba unampa. kila siku atalilia chips na ww utampa. utaharibu afya yake.

we mnunulie mtoto wako ice cream kila mara halafu jiandae kupambana na kifua na mafua ya mtoto.
 
ukishindwa kumcontrol mtoto utotoni itakusumbua ukubwani. sio kila anachoomba unampa. kila siku atalilia chips na ww utampa. utaharibu afya yake.

we mnunulie mtoto wako ice cream kila mara halafu jiandae kupambana na kifua na mafua ya mtoto.

Sijasema nampa chipsi kila siku......nimesema akitaka. Kuna siku unaweza pika chipsi akataka ugali.

Mi nitampa kila atakacho ninachoweza ukubwani tutapambana tu...na nikiweza nampa vilevile.

Kwanini nimnyime rahaaa

Mbona sisi tukijisikia tunataka kitu fulani tunajipa.....mtu anakunywa bia kila siku ila mtoto akiomba kunywa soda mara moja moja tunasema tunamuharibu....... oooops

Umaskini tu unatusumbua
 
mimi kama mtoto sioni chochote kibaya na mbona sijaaribika? alafu mnaposema kuharibika mnakua mna maana ipi?
 
nitamnunulia akipendacho lakin iwe kwa kiasi, maana nikikomaa na misimamo ya kizaman mtoto ataend kupewa ivyo vitu na mabaharia ambao hawatomuacha salama
 
Marahaba, kama uwezo upo mtoto apewe tu akitakacho, maana usipompa atapewa na walimwengu.
Kwa mantiki hiyo wewe una mkataba na Muumba wako kuwa utakaa hapa duniani hadi huyo mtoto wako ajitegemee?? Ninyi ndo mnaowadekeza watoto hadi kumnunulia kitanda cha kuanzia maisha unampa na kochi kuubwa la kuanzia maisha. Mtoto huyo huyo analifanya ndio "Love nest" wa kike anaipatia hapo mimba yake ya kwanza kutoka kwa msela aso na chochote ila sound kubwa. Ila kama babako alikuachia urithi kula na wanao. Binafsi simpi chochote zaidi ya elimu. Akipenda kusoma nauza kila kitu asome afaulu vizuri aweze kubuni maisha yake mazuri
 
Mangatara haya ni maisha ya kikoloni, mtoto apewe elimu na kama uwezo unaruhusu ajengewe msingi wa kunyanyuka, hapa ndio wenzetu ngozi nyeupe wanatuzidi! Mr MO na manji wazazi wao wangesema wakue watafute vya kwao kisa wamepata elimu leo wasingetambulika kama mabilionea. Lkn wamekuwa hivyo sbb ya misingi iliyowekwa na wazazi, ngozi nyeusi tuache ubinafsi, tuishi kwa kuweka misingi ya vizazi vinavyokuja na misingi hiyo si elimu pekee.
 
well said@
 
wrong statement mkuu
 
wamekuwa hivyo sbb ya misingi iliyowekwa na wazazi, ngozi nyeusi tuache ubinafsi, tuishi kwa kuweka misingi ya vizazi vinavyokuja na misingi hiyo si elimu pekee.
Nimekuelewa sasa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…