Mzazi mwenzake hataki baba wa mtoto ampeleke mtoto kwa babu na bibi zake upande wa baba

...Labda SIO wake !...

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
 
Kama mtoto ni wake 100%, basi ajitahidi kujua Kwann huyo mwanamke hataki mtoto aende ukweni. Lazima patakuwa na sababu, sidhani kama amekataa from nowhere.

Maana kulingana na maelezo yako, pande zote mbili wanafahamiana.
Ishu ni kwamba wametengana na mtoto yupo kwa mama yake sasa je.? Ataruhusiwa kumchukua ili aende nae kwao na mama yake abaki kwasababu hataki kwenda
 
Bila shaka ni imani za kishirikina. Huyo dada atakuwa kaambiwa bibi au babu au wote wanga watamroga mwanae.
Nmeshuhudia vitu vya namna hii sana madada wanaamini haya mambo sana na huko makanisani wanawambia vitu kama hivi.
Hapo itabdi demokrasia ikishindikana atumie nguvu hakuna namna
 
Na ata yeye alimwambia jamaa kwamba eti je wakimfanya mtoto amsahau itakuaje ila sasa mimi nataka kujua kisheria ikoje hii iwapo jamaa atamchukua mtoto na kwenda nae akasalimie
 
Kugombaia mtoto ni utoto sana! Mtoto akikua ataanua cha kufanya. Huyo jamaa anashindwa kutafuta watoto wengine kwa mwanamke mwingine?! Kwani bila huyo mtoto kwenda kwa babu zake huyo Jamaa atakufa?! Ujinga ujinga tu.
Mtoto anauma sana anyway ushauri wako umepokelewa
 
Kama mtoto bado ni mdogo sana. Jamaa atulie tu kidogo. Soon atakuakua na ataweza kwenda.

Kama ni muhimu mno kwa hao ndugu kumjua mtoto basi waje kwa jamaa, kisha jamaa amchukue mtoto awajue ndugu zake.

Huyo binti anaweza kuwa na kinyongo tu, au anaweza kuwa na sababu sensitive kabisa.

Mfano: Mimi na bro wangu tuliepelekwa kijijini tukiwa na miaka 4 na 6, respectively. Jamaa hakurudi town, alifia kule kule na mie niliponea chupuchupu tu. Hivyo mwanangu hatakaa aende kijijini mpaka teenage labda.
 
Mtoto anauma sana anyway ushauri wako umepokelewa
Najua mtoto anauma, lakini the more you fight for ndivyo unavyozidi kuwa frustrated. Ni heri kupunguza tension nyingi kuliko upate kiharusi. Unazaa na mwanamke mwingine huku ukitengeneza pesa, mtoto akianza kupata ufahamu unamtupiatupia chochote kitu wakati akiwa masomoni huku akiendelea kukutambua. Shida iko wapi?
 
Nashukuru sana mkuu ili ni wazo zuri linaweza kupunguza misukosuko kabisa
 
Hivi hii hua inasababishwa na nini?🤔🤔.. I can relate
 
Hivi hii hua inasababishwa na nini?🤔🤔.. I can relate
Nadhani kubadilisha mazingira na kinga mwili dhaifu ya watoto vikiungana na huduma mbovu za afya maeneo ya vijijini hupelekea vifo vya watoto wengi japo watu huhusisha na ushirikina. Sh×t I don't buy.

My bro passed on kwa ajili ya yellow fever.
Siku hizi nikifikiria, naona kabisa tatizo lilikuwa ni huduma mbovu za afya ndo zilipelekea kumpoteza.
 
Sio kila Babu na Bibi ni wa kijijini wengine wapo mjini
 
Nimekupata vizuri kiongozi 👊👊
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…