Mzee Kikwete: Rais Samia ametuliza nchi na kuvutia Uwekezaji

Mzee Kikwete: Rais Samia ametuliza nchi na kuvutia Uwekezaji

Mzee amebarikiwa huyu. Kweli kama hukunji ndita muda wote unaishi... Mzee ananguvu huyu balaa. Alituletea magu, akatuletea makamu ambaye kwa sasa ni malkia. Halafu ndiye mshauri mkuu aliyebaki.
 
Wengi wa waachangiaji humu hatujui lolote kuhusu siasa, tunabwabwaja bwabwaja tu hatueleweki misimamo yetu.

Kikwete aliongoza nchi- hakuitawala.
 
Mambo murua kabisa.
iu
 
"Watu hawana wasiwasi, hawana wasiwasi kwamba nitakuwa salama au itakuwa salama, nitarudi nyumbani au sitarudi nyumbani. Kuna vipindi hivyo vilikuwa na mashaka.

Mazingira yale hayapo. Kuna wakati mazingira hayo yakiwepo kwa kiingereza wanasema people just take it for granted. Hata wafanyabiashara leo wakigongewa mlango hawana wasiwasi kwamba baada ya kufungua mlango kutakuwa na watu kama 10 hivi, mmoja atauliza hiki na mwingine atauliza kile.

Wafanyabiashara wanafanya shughuli zao kwa utulivu. Hili ni jambo kubwa sana. Kwenye mazingira ambayo ndani ya nchi kuna utulivu ndio mazingira yanachochea ukuaji wa uchumi, mazingira ya leo hapa hayamfanyi mtu kufikiria kuhamisha mtaji wake, shughuli zake au kutafuta nchi ya kwenda, hayo ni mambo makubwa yanayopambanua Urais wa @SuluhuSamia" Dkt. @jmkikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tumpe mama samia maua yake. Sijajua Jakaya alikua anamzungumzia nani lakini kusema za ukweli haya aliyoyasema kwa sasa yametulia sana.
 
Mwambie Kikwete sasa tutazame present, the past is over, sio kila siku tunaimba tu the past, vipi ya present tutayafanyia kazi lini?

Tunapigwa kila kona na mchwa dada yake anakiri hili na hajui afanye nini, yeye mwenyewe Kikwete anachangia kutuumiza kwa kuzunguka huko nje na dada yake kwa kutafuna kodi zetu bila huruma..
 
Mwambie Kikwete sasa tutazame present, the past is over, sio kila siku tunaimba tu the past, vipi ya present tutayafanyia kazi lini?
Ambiwe pia hiyo iwe katika katiba rasmi na kitaasisi, sio kutegemea aina ya mtu na fadhili za aliyeko magogoni.
 
"Watu hawana wasiwasi, hawana wasiwasi kwamba nitakuwa salama au itakuwa salama, nitarudi nyumbani au sitarudi nyumbani. Kuna vipindi hivyo vilikuwa na mashaka. Mazingira yale hayapo. Kuna wakati mazingira hayo yakiwepo kwa kiingereza wanasema people just take it for granted. Hata wafanyabiashara leo wakigongewa mlango hawana wasiwasi kwamba baada ya kufungua mlango kutakuwa na watu kama 10 hivi, mmoja atauliza hiki na mwingine atauliza kile. Wafanyabiashara wanafanya shughuli zao kwa utulivu. Hili ni jambo kubwa sana. Kwenye mazingira ambayo ndani ya nchi kuna utulivu ndio mazingira yanachochea ukuaji wa uchumi, mazingira ya leo hapa hayamfanyi mtu kufikiria kuhamisha mtaji wake, shughuli zake au kutafuta nchi ya kwenda, hayo ni mambo makubwa yanayopambanua Urais wa @SuluhuSamia" Dkt. @jmkikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tumpe mama samia maua yake. Sijajua Jakaya alikua anamzungumzia nani lakini kusema za ukweli haya aliyoyasema kwa sasa yametulia sana.
Wawakezaji wakubwa hawatazami mambo kwa kipindi kifupi cha miaka mitano tu, wanaangalia muda mrefu hata miaka 20 iliyopita na ijayo. Tanzania kuna udhaifu mkubwa sana katika kulinda property rights dhidi ya visasi vya watawala katika wakati wowote.
 
Ambiwe pia hiyo iwe katika katiba rasmi na kitaasisi, sio kutegemea aina ya mtu na fadhili za aliyeko magogoni.
..ameshasahau yaliyomkuta Dr. Ulimboka kule msitu wa Mwabepande, sasa anajiona mtakatifu kabisa.

Yeye ndie aliyeitupa ile Rasimu ya Warioba kwa kuchezea pesa za walipakodi, mwishowe akaja na Katiba Pendekezwa.
 
Tumetoka mbali toka mbali, ainuliwe Mungu juu, ni kwa neema tu ,, neema ,na rehema[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23], neema
Bado, hali inaweza kubadilika wakati wowote kutegemea na aliyeko ofisi namba au atakavyoamua siku na wakati atakaojisikia kufanya impendezavyo.
 
Back
Top Bottom