Mzee Mwinyi alituachia PPF Tower, Mkapa katujengea National stadium, Kikwete kaacha Mwendokasi na UDOM, sasa twende na Rais Magufuli

Magufuli amekuja kufanya mambo mengi sana, Watanzania tutamkumbuka huyu Baba kwa uchapakazi na upendo wake kwa Nchi
Kama asipokuteua hata kuwa Mtendaji Kata utakuwa wa kwanza kumsahau na kumtukana matusi ya nguoni akiwa bado yuko madarakani. Wengi tutamkumbuka kwa matumizi mabaya ya kodi zetu katika miradi isiyokamilika kama vile SGR ikiwa bado iko Kibaha, JNPP ikiwa bonde la jangwa, Rwandair ikisafirisha minofu ya samaki, Chato International Airport ikiwa ni malisho ya swala toka Burigi National Park nk. Labda wakulima wa huko kwa kupungua ajali za mikokoteni ya punda kwa msaada wa taa za barabarani.
 
Una haki uiamini CCM Kwa sababu hatuna wapinzani tuna wapingaji
Miaka mitano ijayo ya Magufuli nchi yetu itapiga hatua kubwa sana maana hii mitano ya awali pamoja na ugeni wake kathubutu kufanya Mengi makubwa cha ajabu kwa pesa zetu za ndani. Mitano ijayo atakuwa mzoefu na anajua nani wa kufanya nae kazi tutegemee makubwa kwenye baraza lake la Mawaziri lijalo litakuwa ni moto wa kuotea mbali sidhani kama kutakuwa na Waziri asieendana na kasi yake natabiri makubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamba JK hakuacha mradi wa Ubungo na Tazara interchange? au JKN terminal III? kwa taarifa yako tu, the initial plan ya TAZARA ilikuwa more complex and attractive klk hii ya Sasa na bajeti ilikuwa tayari.

Daraja limeleta shida gani?
 
Katuletea siasa za ajabu ajabu za chuki ambazo hazijawahi kuwepo nchini kwetu, watu regardless itikadi zao walikuwa wanapendana, kampeni ni burudani tupu, kushindana kwa hoja majukwaani - sasa hivi watu wanawindana kwa mapanga na mashoka - hii si Tanzania tuliyoijua, hatuitaki.
 
Magufuli amekuja kufanya mambo mengi sana, Watanzania tutamkumbuka huyu Baba kwa uchapakazi na upendo wake kwa Nchi
Sema amekuja awamu ambayo miradi mingi ilikuwa imefikia hatua ya utekelezaji. Hakuwa na option, ilibidi itekelezwe tu.

Miradi yote unayoiona ni mipango ya muda mrefu hakuna jipya aliloibua
 
]Sema amekuja awamu ambayo miradi mingi ilikuwa imefikia hatua ya utekelezaji. Hakuwa na option, ilibidi itekelezwe tu.

Miradi yote unayoiona ni mipango ya muda mrefu hakuna jipya aliloibua
 
Unachokifanya hapa ni sawa na kuishukuru ATM kwa kukupa hela zako
 
Kafanya mengi sana ila kwenye ajira tyuu kabugi!nilisomeshwa kwa mkopo wa vikundi leo sina ajira ..nashindwa kulipa den nimeuza mpaka uwanja wa urithi ..anasema tujiajiri ikiwa yeye kaomba ajira kwa wanannchi!

Mkumbusheni ajira ..bwana
Asisingizie korona wakati bongo hatuna tena!
 
Hujui kitu bwana nenda zako. Kwanza nani kakuambia daraja la kigamboni ni la serikali.

Daraja la kigamboni na chuo cha udom ni vya nssf. Ukipita pale kigamboni wanaichaji hela ni wafanyakazi wa nssf.
usinifanye Nicheke aisee udom na Daraja ni vya nani?
 
Magufuli amekuja kufanya mambo mengi sana, Watanzania tutamkumbuka huyu Baba kwa uchapakazi na upendo wake kwa Nchi
Bila shaka huwa anakugonga wewe!!! Una ubwabwajo mwingi sana juu ya meko
 
KWA JAKAYA MRISHO KIKWETE,,kama umeminya hivi,,ila #Kuunga mikoa yote nchi nzima kwa Rami, # JAKAYA KIKWETE Heart Instute, # Maslahi BORA kwa wafanyakazi,
 
Mavi-Jana ya Tanzania ni mapunguani, yanafikri kukenga maflyover ndio maendeleo hayo! Hebu ulizeni raia walivyo chakali kwenye mifuko! Magu kafuta ajira serikalini raia wanalia!
 
Dah...kweli kuna vitu huvielewi......jiulize.....sasa kwanini mtu anapo oa anapongezwa?.....au anapofanya vizuri katika masomo yake anapongezwa? au Yanga anapomfunga Simba anapongezwa?? 🤣
 
Elewa mzee nimekuambia mradi ulisimama sababu ya buku mbili. Mradi ulianza kazi baada ya majaliwa chini ya jpmkuingilia kati na kuamua nauli iwe 600.

Fuatilia vizuri taarifa za huo mradi. Inawezekana we umeanza tu kupanda mwendokasi ili hujui nini kilikuwepo kabla mradi kuanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…