Mzee Warioba na hoja fikirishi ya Mwalimu Nyerere kutohutubia Kanisani

Mzee Warioba na hoja fikirishi ya Mwalimu Nyerere kutohutubia Kanisani

Ukiamua kuelezea mazuri tu ya Iddi Amin basi naye anaweza kuwa malaika...kuna wakati nilikuwa na rafiki yangu kutoka Uganda, kila tukizungumzia siasa basi alikuwa akimsifia sana Iddi Amin..
Usemalo ni kweli kabisa, nilienda Uganda 2014, wenzetu wanamzunguzia Idd Amini very positive kuliko Militon Obotte
 
Nilimsikiliza vyema Waziri Mkuu mstaafu Mzee Joseph Sinde Warioba pale alipopewa nafasi ya kuhutubia nyumbani kwa Mwalimu Nyerere pale Msasani kama sehemu ya sherehe ya kufikisha miaka 100 ya hayati Mwalimu.

Aliongea kwa lugha nzuri kama mwanasheria na mtu muungwana. Akamuelezea Mwalimu Nyerere jinsi alivyokuwa akimfahamu tangu alipokuwa kijana kabisa. Tukumbuke kuwa mwaka 1961 Mzee Warioba alikuwa ni mmoja wa vijana waliokuwepo pale uwanja wa Uhuru siku ya tarehe 9 mwezi Desemba. Hivyo anamfahamu vyema hayati Mwalimu.

Akiwa anaendelea kujenga hoja ya unyenyekevu(humility) wa hayati Baba wa Taifa akaongelea suala moja lililoniacha nikiwa nimezama katika fikra nyingi aple aliposema kuwa Mwalimu Nyerere hakuwahi hata mara moja kuhutubia kanisani.

Nikaona kamera ikizungushwa na akaonyeshwa Amani Karume mdogo wake na rais wa zamani wa Zanzibar, macho yake yakawa yanatazama juu hewani kama alikuwa na mawazo fulani yaliyomjia kichwani muda huo.

Kwamba Mwalimu Nyerere alipenda mno kujishusha na hakulewa na madaraka.Siku zote alikuwa tayari kujiweka katika nafasi ya mtu wa kawaida pasipo uwepo wa dalili wala viashiria vya makuu, ni kama Mzee Warioba aliamua kusisitiza kwa viongozi wa sasa waendelee kujishusha wawe ni watu wa kawaida wasiwe ni Miungu watu.

Nikakumbuka miaka ile ya 1980 pale kanisani Saint Joseph Hayati Baba wa Taifa alikuwa siku moja moja akipenda kusali. Kilichokuwa kikituonyesha kwamba yeye ni rais ni kwamba kile kiti chake kirefu kilikuwa kikikaliwa na watu watatu tu. Yeye mwenyewe katikati kushoto mlinzi mmoja na kulia mlinzi mwingine. Hakuwa na mbwembwe za kutaka kupewa kipaza sauti wakati misa ikiwa inaendelea ili eti aanze kutoa maagizo mle mle kanisani.

Hoja kama hii ya Warioba ni nzito na pengine katika utu uzima wake alionao kwa sasa ni wakati muafaka kufikisha ujumbe kama ule ule aliousema Askofu Niwemugizi kwa Samia kule Kagera. Kwamba cheo chako kipo leo na kesho kinakwenda kwa mtu mwingine, hivyo tumia busara siku zote katika maamuzi yako.

Nakumbuka JK katika kumuongelea akasema kitu alichojifunza kwake ni kauli yake kwamba hoja hujibiwa kwa hoja na siku zote haipigwi bunduki. Kutoipiga bunduki hoja ni pamoja na kuwa na uwezo wa kujifanya wewe ni wa kawaida tu hata kama yanayosemwa dhidi yako yanaiumiza nafsi yako.

Pia ni kama ile picha maarufu ya Bilionea Bill Gates aliyoipiga akiwa kapanga foleni huko USA kavaa jeans yake kama vile ni mtu wa kawaida tu.

Anajishusha na kutojikweza siku zote, jaribu kumuweka Gates na pesa zake na ushawishi wake katika nafasi ya hawa matajiri wanaomiliki mabasi ya mikoani na vituo kadhaa vya kuuza petroli, namna wanavyotaka wanyenyekewe kama vile wao ndio wanaowapa binadamu wengine uhai na kuuondoa!.

Tutamkumbuka sana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alikuwa ni mtu wa kawaida mwenye ucheshi mwingi na busara nyingi. Lakini ndani kabisa ya nafsi yake akiwa mtu wa kawaida kabisa.

Ukikutana nae pale ikulu katika zile koridoo karibu na yule Simba aliyekaushwa miaka ile anakuwekea mkono kichwani na kukuuliza hujambo mwanangu!?. Ni kama jana tu lakini inakaribia miaka 40 sasa.
Sasa hivi CCM yake imekuwa na wenyewe,ndani yake kumejaa waheshimiwa wa wizi wa kura na fedha pamoja na waporaji wa mali za umma.Mwl.alikuwa mnyenyekevu hadi umauti ulipomkuta akiwaita wananchi wenzake NDUGU.
Ndani ya chama dola na serikalini hakuna Mzalendo kama Mwalimu J.K.Nyerere,siyo hawa nyapara wa sasa wanaotulazimisha tuhamie Urundi.Yaani wakati sisi tukiambiwa twende huko tutakuwa tunapishana na Warundi wanaokimbilia kisiwa cha Amani!Maajabu hayaishi Tanganyika.
 
Warioba kwao anakotoka wengi wasabato wakiwemo ndugu zake
Wasabato huwa hawapendi siasa kanisani

Ndio maana kasema hivyo

Kakulia mazingira ya wasabato
 
Warioba kwao anakotoka wengi wasabato wakiwemo ndugu zake
Wasabato huwa hawapendi siasa kanisani

Ndio maana kasema hivyo

Kakulia mazingira ya wasabato
Ni suala la maadili tu bila ya kuingiza usabato wala upagani. Ni suala la unyenyekevu aliyojifunza kutoka kwa Mwalimu Nyerere aliyekuwa mkatoliki halisi.
 
Kifupi warioba kakulia kwenye eneo la usabato

Mkewe Evelyn Ojjiki ni msabato hasa

Wasabato na siasa kanisani mbali kabisa nje fanya sio kanisani .Mkewe ndie kam shape kwenye hilo

Apigiwe mkewe makofi ya hongera kwa kumshikisha adabu kuwa siasa fanya nje ya kanisa sio ndani ya kanisa

Hongera mama Evelyn Ojjiki kwa kazi umefanya credit zije kwako sio kwa warioba wala Nyerere
 
Si Mandela tu; hata rais wa Vatikano Yohana Paulo alipokuja ilikuwa hivyohivyo.
Papa alikuja 1990 Septemba kama sijakosea. Alipokelewa na Mwinyi aliyekuwa ni rais wa wakati ule, nadhani Mwalimu alikutana nae ikulu.

Nakumbuka jioni ile alipofika palikuwa na misa pale Saint Joseph jioni kama saa kumi na mbili hivi. Kesho yake tukaenda kwa maandamano kusali Jangwani misa aliongoza Papa mwenyewe.
 
Kifupi warioba kakulia kwenye eneo la usabato

Mkewe Evelyn Ojjiki ni msabato hasa

Wasabato na siasa kanisani mbali kabisa nje fanya sio kanisani .Mkewe ndie kam shape kwenye hilo

Apigiwe mkewe makofi ya hongera kwa kumshikisha adabu kuwa siasa fanya nje ya kanisa sio ndani ya kanisa

Hongera mama Evelyn Ojjiki kwa kazi umefanya credit zije kwako sio kwa warioba wala Nyerere
Unampa mtu sifa wakati hazistahili. Nyerere mwenyewe alikuwa mnyenyekevu mwenye akili timamu.

Hakulewa sifa za kijinga na alitanguliza tabia ya mijadala yenye tija. Alipenda kuusikia ushawishi wa hoja ya mtu na sio kupelekesha watu.
 
Labda wakati wanaoana miaka hiyo ndio alikuwa msabato. Yule mama mwaka 2001 nilikuwa nae katika mafungo ya karismatiki katoliki pale Mbagala kanisani na yalikuwa ni ya wiki moja.

Sidhani kama msabato anaweza kuhudhuria mafungo yale. Labda familia aliyotoka ni ya wasabato lakini baada ya kuolewa amekuwa ni mkatoliki.
 
Labda wakati wanaoana miaka hiyo ndio alikuwa msabato. Yule mama mwaka 2001 nilikuwa nae katika mafungo ya karismatiki katoliki pale Mbagala kanisani na yalikuwa ni ya wiki moja.

Sidhani kama msabato anaweza kuhudhuria mafungo yale. Labda familia aliyotoka ni ya wasabato lakini baada ya kuolewa amekuwa ni mkatoliki.
Atakuwa alibadili dini kufuata mwanaume enzi zao katoliki alikuwa hawaruhusiwi kuoa madhehebu mengine hadi mtu awe katoliki

Yule mama msabato kwao wote wasabato
 
Alifanikiwa kumzuia mmewe asihubiri siasa kanisani lakini akashindwa kimzuia kutumia whisky na sigara?! Hizo bidhaa kwetu wasabato marufuku.
Hakuweza kabisa ila kwenye hilo la marufuku siasa kanisani aliweza
 
Back
Top Bottom