Hayo ni mambo public, of course watu watataka kujionesha wana pain.
Kujua ukweli inabidi ukae nao private kama mimi nilivyokaa na Mama yangu.
Inawezekana kuna watu walikuwa wanakaripiwa kama watoto walikuwa hawapendi.
Magufuli alikuwa na hulka hiyo.
Kuna mtu kasema rais alikuwa Nyerere?!Yohana Paulo wa Pili alikuja Tanzania mwaka 1990 wakati Mwinyi akiwa Rais. Si Nyerere
Mwezi uliopita mmoja alipewa mic huko Njombe akaanza kuhamasisha waumini kutoa zakaNadhani huu uhuni wa kutumia mimbari za nyumba za Mungu kutoa matamko ya kisiasa tumeanza kuuona kwa JK,kwa Mwendazake ilizidi! Yaani akipewa Mic ilikuwa ni kufoka mpaka kukashifu Watumishi wa Mungu!
Hayati Magufuli alitumia kanisa kuwaunganisha Watanzania na sio kutugawa! Kama hofu ya Mwalimu Kutumia Dini ilikuwa kuwagawa Watanzania basi Magufuli aliitumia dini kutuunganisha!
Nenda kamsikilize Shekhe Kishki ambae alitokwa ma Machozi juu ya upendo wa Rais Magufuli kwa Waislamu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Uzuri sisi hatukuwa China.
Na inawezekana pia uzembe ukawa wa Rais mwenyewe.
Huyo wa tatu uliyemtaja mtoe anawaharibia sifa hao wengine.Ni pengo kubwa nyerere,mkapa na magufuli hawapo
Nchi imebaki kutafunwa
Ila wewe ni Kubwa JInga jinga hivi .Toka lini Amaan Karume akawa mdogo wa Rais wa Zamani Wa Zanzibar ? Ndugu zangu Watanzania ,hiki ndicho kizazi tulicho nacho sasa hivi ,maneno mengi lakini kichwani hamna kitu.Kizazi kilichopinda,kinachojifanya kinajua kila kitu lakini upuuzi mtupu.Ulizeni au fanyeni tafiti kabla ya kuandika siyo kukurupuka asubuhi asubuhi unaanza kuandika.Nilimsikiliza vyema Waziri Mkuu mstaafu Mzee Joseph Sinde Warioba pale alipopewa nafasi ya kuhutubia nyumbani kwa Mwalimu Nyerere pale Msasani kama sehemu ya sherehe ya kufikisha miaka 100 ya hayati Mwalimu.
Aliongea kwa lugha nzuri kama mwanasheria na mtu muungwana. Akamuelezea Mwalimu Nyerere jinsi alivyokuwa akimfahamu tangu alipokuwa kijana kabisa. Tukumbuke kuwa mwaka 1961 Mzee Warioba alikuwa ni mmoja wa vijana waliokuwepo pale uwanja wa Uhuru siku ya tarehe 9 mwezi Desemba. Hivyo anamfahamu vyema hayati Mwalimu.
Akiwa anaendelea kujenga hoja ya unyenyekevu(humility) wa hayati Baba wa Taifa akaongelea suala moja lililoniacha nikiwa nimezama katika fikra nyingi aple aliposema kuwa Mwalimu Nyerere hakuwahi hata mara moja kuhutubia kanisani.
Nikaona kamera ikizungushwa na akaonyeshwa Amani Karume mdogo wake na rais wa zamani wa Zanzibar, macho yake yakawa yanatazama juu hewani kama alikuwa na mawazo fulani yaliyomjia kichwani muda huo.
Kwamba Mwalimu Nyerere alipenda mno kujishusha na hakulewa na madaraka.Siku zote alikuwa tayari kujiweka katika nafasi ya mtu wa kawaida pasipo uwepo wa dalili wala viashiria vya makuu, ni kama Mzee Warioba aliamua kusisitiza kwa viongozi wa sasa waendelee kujishusha wawe ni watu wa kawaida wasiwe ni Miungu watu.
Nikakumbuka miaka ile ya 1980 pale kanisani Saint Joseph Hayati Baba wa Taifa alikuwa siku moja moja akipenda kusali. Kilichokuwa kikituonyesha kwamba yeye ni rais ni kwamba kile kiti chake kirefu kilikuwa kikikaliwa na watu watatu tu. Yeye mwenyewe katikati kushoto mlinzi mmoja na kulia mlinzi mwingine. Hakuwa na mbwembwe za kutaka kupewa kipaza sauti wakati misa ikiwa inaendelea ili eti aanze kutoa maagizo mle mle kanisani.
Hoja kama hii ya Warioba ni nzito na pengine katika utu uzima wake alionao kwa sasa ni wakati muafaka kufikisha ujumbe kama ule ule aliousema Askofu Niwemugizi kwa Samia kule Kagera. Kwamba cheo chako kipo leo na kesho kinakwenda kwa mtu mwingine, hivyo tumia busara siku zote katika maamuzi yako.
Nakumbuka JK katika kumuongelea akasema kitu alichojifunza kwake ni kauli yake kwamba hoja hujibiwa kwa hoja na siku zote haipigwi bunduki. Kutoipiga bunduki hoja ni pamoja na kuwa na uwezo wa kujifanya wewe ni wa kawaida tu hata kama yanayosemwa dhidi yako yanaiumiza nafsi yako.
Pia ni kama ile picha maarufu ya Bilionea Bill Gates aliyoipiga akiwa kapanga foleni huko USA kavaa jeans yake kama vile ni mtu wa kawaida tu.
Anajishusha na kutojikweza siku zote, jaribu kumuweka Gates na pesa zake na ushawishi wake katika nafasi ya hawa matajiri wanaomiliki mabasi ya mikoani na vituo kadhaa vya kuuza petroli, namna wanavyotaka wanyenyekewe kama vile wao ndio wanaowapa binadamu wengine uhai na kuuondoa!.
Tutamkumbuka sana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alikuwa ni mtu wa kawaida mwenye ucheshi mwingi na busara nyingi. Lakini ndani kabisa ya nafsi yake akiwa mtu wa kawaida kabisa.
Ukikutana nae pale ikulu katika zile koridoo karibu na yule Simba aliyekaushwa miaka ile anakuwekea mkono kichwani na kukuuliza hujambo mwanangu!?. Ni kama jana tu lakini inakaribia miaka 40 sasa.
Sikumbuki lini kumsikia akitoa maagizo st Peter au kanisani. Ikiwa aliongea katika maeneo ya dini ni katika hafla maalum kama sherehe. Nyerere alielewa maana ya kutenga dini na siasaNyerere alikuwa msomi wa falsafa, kamsoma John Stuart Mill Edinburgh Scotland na kumuandikia papers, anajua separation of church and state ni nini.
Ndiyo maana hakuhubiri kanisani.
Alijua namna ya kuishi na watu. Ukifuatilia hotuba zake Nyerere alionyesha kuijua nchi na watu wake. Alikuwa muungwana sanaKuhusu humility, kuna siku Mama yangu alivyokuwa anafanya kazi Ikulu, alikuwa anakata kona kwenye corridor moja ya Ikulu. Ikawa bado kidogo agongane na Nyerere uso kwa uso, kwa sababu hakumuona kwenye kona.
Basi Mama akawa ameogopa sana akaona atakaripiwa na Nyerere. Akaja kumkuta Nyerere mwenyewe ndiyo yuko so concerned kuhusu hali ya Mama, alimuona Mama kama kapanic hivi, Nyerere akawa anamtuliza anamuuliza kama yuko poa.
Nikasema, mtu mwenye cheo kikubwa anavyo ji conduct akiwa peke yake na staff wake inaonesha mambo mengi sana kuhusu integrity yake.
In this capacity, Nyerere was the consummate gentleman.
Ni ngumu sana kuamini!! Sidhani hao wasadizi wangeweza kusema tofauti..lakini wasaidizi wa Jpm wanasema alikuwa anapenda kula chakula na wasaidizi wake na kutaniana nao.
..pia wanasema Jpm alikuwa akiwahimiza wasaidizi wake kusali/kuswali. Zaidi aliwahimiza wasaidizi wake Waislamu kwenda hijja.
Kuwahimiza watu kusali/kuswali si kazi ya rais.Tena inaweza kuwa improper imposition of a president's beliefs on others...lakini wasaidizi wa Jpm wanasema alikuwa anapenda kula chakula na wasaidizi wake na kutaniana nao.
..pia wanasema Jpm alikuwa akiwahimiza wasaidizi wake kusali/kuswali. Zaidi aliwahimiza wasaidizi wake Waislamu kwenda hijja.
Taasisi ya urais ilikosea kutoweka vioo katika corridors za Ikulu ili watu wanapokata kona za corridors za Ikulu waweze kuona upande wa pili wa kona kuna mtu anakuja ama la.Rais ni taasisi hakoseai ,ππ
Magufuli alipoanza kuhutubia vijimambo kila alipoenda kusali, nilimtonya rafiki yangu mmoja nikamwambia , huyu jamaa hajui anafanya nini.Mwanasiasa anayepanda madhabahuni anakuwa karibu sana na anguko lake. Labda awe alishawahi kuwekwa wakfu.
Jamani hivi kweli mnamlinganisha Nyerere na JPM?!!Mada inamhusu nyerere hao wengine wa Nini? By the way kufa kwao hakumaanishi ndo nchi itafunwe, Kuna tofauti kubwa kipnd Cha utawala wa nyerere na Karne hii ya wasomi, mi naona mzee alikuwa Bora kwa kipindi kile, kwa namna Tanzania ilivyo kwa Sasa akitokea mtawala km nyerere watu watampinga hadharani, na hicho ndo kilichotokea kwa jpm
2014 unaongea na vijana wa waliozaliwa miaka ya tisini (1990s), unaulizia utawala ulioisha kabla hata hawajazaliwa!!Usemalo ni kweli kabisa, nilienda Uganda 2014, wenzetu wanamzunguzia Idd Amini very positive kuliko Militon Obotte
Mjinga ni wewe unayejifanya profesa wa chuo kikuu kumbe kidampa fulani tu. Lengo langu nimsema mdogo wake aliyekuwa Rais wa Zanzibar ambaye ni mtoto wa Karume mzee.Ila wewe ni Kubwa JInga jinga hivi .Toka lini Amaan Karume akawa mdogo wa Rais wa Zamani Wa Zanzibar ? Ndugu zangu Watanzania ,hiki ndicho kizazi tulicho nacho sasa hivi ,maneno mengi lakini kichwani hamna kitu.Kizazi kilichopinda,kinachojifanya kinajua kila kitu lakini upuuzi mtupu.Ulizeni au fanyeni tafiti kabla ya kuandika siyo kukurupuka asubuhi asubuhi unaanza kuandika.
Kila Jumapili panafanyika mageuzi ya sakramenti, yale ni mambo mazito na jicho la kibinadamu huwezi kuona kitu lakini katika hali ya kiroho panatisha pale mahali.Magufuli alipoanza kuhutubia vijimambo kila alipoenda kusali, nilimtonya rafiki yangu mmoja nikamwambia , huyu jamaa hajui anafanya nini.
Na nilijisemea tu kuwa madhabahu itamwadhibu, pale si mahali pa mizaha.
Mtu asiye na roho wa Mungu huwa haelewi kuwa madhabahu zinawekwa wakfu na ni mahali pa waliowekwa wakfu vile vile.
Ila weye mkuu una mambo sana.πππVidole vyangu vina allergy na hewa chafu ya baadhi ya watu humu.
Ukiona hivyo karibu nitaondoka.
Nimekusawazishia usihitaji algorithms za Claude Shannon kunisoma.