Mzee Yusuph aamua kuachana na muziki na kumrudia Mungu wake

Zile mali alizozipata katika ushetani azirudishe
 
Hakuna kitu, huo ni unafiki au kuna hofu imemuingia maishani, nani aliwahi kumuona Mungu?
Hakuna aliyewahi kumuona ila tunasoma vitabu na kusikia na kuamini ndio maana tunatekeleza kile tulichosikia/kusoma na kuamini
 
Ampe Yesu MAISHA (ahokoke) hapo ndo atakuwa ameshinda la sivyo Hamna kitu
 
Hizi nyingine zinaitwa Paranoia na watu wengi wanaomwamini Mungu wa Saudi Arabia wana hii kitu. Ukiwasikiliza Sana waarabu utakufa masikini, yaani aache kupiga pesa kwasababu za kipuuzi. Subiri awe Shehe Ubwabwa wa Bungoni huko.
 
Ukiona hivyo muda wa mtu hujafika,muda ukifika kama kwa Mzee utaacha yote na utaongozwa na neema tuu,ingekua tunatumia nguvu kufanya mema wanadamu woote tungekuwa watakatifu ila ni NEEMA tu ikuvute
 
Aliyekuwa Mfalme na gwiji wa muziki wa taarabu Afrika mashariki MZEE YUSUF ameamua kuachana na mziki na kumrudia Allah.

Mzee Yusuf ametangaza Nia yake hiyo leo ijumaa tarehe 12-08-2016 Muda mfupi baada ya kumaliza kuswali swala ya ijumaa ktk msikiti wa ilala bungoni (Masjid Taqwa)

Alizungumza huku akibubujikwa na machozi mengi Mzee Yusuf amemuomba Allah amsamehe madhambi yake yote pamoja na kuwaomba waumini wote wamuombee msamaha kwa Allah. Kadhalika amewaomba wanamuziki wengine ambao ni waislamu kuachana na muziki na kuzitumia fani zao walizonazo ktk kutangaza na kusifia Shamaail za bwana mtume muhammad (s.a.w).

Gwiji huyo wa zamani wa taarabu amewaomba watu wote waliokuwa na Cd zake majumbani mwao kuacha kupiga nyimbo zake na wakikaidi wafahamu madhambi yote yatakuwa juu yao kwani yeye hivi sasa anafanya toba kwa Allah.

Pia amevitaka vituo vyote vya televisheni na redio kuacha kupiga nyimbo zake kwani yeye Hana dhimma hiyo Tena. Ikumbukwe hali kama hii ilishawahi kutokea kwa aliyekuwa msanii wa bongo fleva SUMA LEE kuamua kuachana na mziki na sasa ni mpenzi mkubwa wa mtume muhammad (s.a.w)

Yaa rabbi awape tawfiiq wanamuziki wote wa kiislamu waachane na muziki pamoja kutupa mwisho mwema wao pamoja nasi in shaa Allah.

Hakuweza kuendelea kuongea zaidi ya maneno hayo na kuangua kilio kilichomsababishia maneno kutoweza kutoka mdomoni mwake.


NB: ukitaka kujua ibliis huwa hapendi kuona watu wakiwa kwenye njia sahihi subiri comments hapa chini za ibilisi waliobaki ambao jambo hili limewakera na litawakera sana
 
Hizi dini zote mbili zimeanza kupoteza umaarufu kwenye bongo za binadamu wanaowaza kwa tafakuri, hivyo basi tukio kama hili la Mzee Yusuf ni moja ya wapanga mikakati wa hizi dini.

Mzee Yusuf kama alikuwa hajawa tajili basi sasa ndio utajili huo umemfikia yeye atatumika kama alama ya mtu maarufu aliyeamuwa kumcha Mungu.

Hii dunia ina mambo mengi nyuma ya panzia ambayo ni vigumu kuyagunduwa katika jicho la kawaida.
 
mi naona kastaafu, maana kashalamba vitamu vyote
 
Atakuwa anawaza na kujutia mambo ya akina Issa Kijoti, Sheba Juma n.k! Ha ha ha ha!
 
Hakuna comment
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…