Na hii ndio maana halisi ya ule msemo wa kusema Mungu ni roho

Na hii ndio maana halisi ya ule msemo wa kusema Mungu ni roho

Thecoder

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2015
Posts
1,590
Reaction score
4,244
Kiuhalisia ni kwamba mara nyingi watu wamekua wakisema Mungu ni roho, namimi nakubaliana na hii kauli ya kwamba ni kweli Mungu ni roho, lakini tujiulize kidogo je, Mungu ni roho kwa namna gani? Kwa maana maandiko husema ya kwamba sisi tuliumbwa kwa mfano wake.

Kwahiyo kama sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu basi sisi ni kopi yake, na kama sisi ni kopi yake basi hakuna chochote kilicho kwetu kikawa hakipo kwake ingawa yawezekana yapo yaliyo kwake yakawa hayapo kwetu kwa maana kopi haiwezi kuwa sawasawa na ile halisi kwa asilimia mia moja ingawa kopi kimuonekano haiwezi kutofautiana na halisi.

Sasa hoja hii inaenda kupingana na ile hoja ya wale ambao wanaamini ya kwamba Mungu ni roho tupu isiyo na mwili kwa maana ukiachana na hii hoja lakini pia ukisoma maandiko katika kile kitabu cha mwanzo utagundua ya kwamba Mungu si roho tu pekee bali nayeye ni roho iliyo ndani ya nyama.

Maandiko yanasema hivi "roho yangu haitashindana na mwanadamu kamwe kwani yu nyama na yeye, Kwahiyo miaka yake itakua 120".

Hilo neno la kwani yu nyama na yeye inamaana ya kwamba Mungu angeweza kushindana na mwanadamu kama tu angekua na roho tupu ila kwakua mwanadamu anao upande wa kiroho na upande wa nyama kama vile Mungu alivyo basi inakua ngumu yeye Mungu kushindana nae.

Yu nyama na yeye inamaana ya kwamba na yeye ni nyama kama mimi.

Na andiko hilo hilo ukiendelea kulitafakari zaidi utagundua ya kwamba Mungu anaweza kumuendesha binadamu katika ule upande wa kiroho pekee ila unapokuja upande wa damu na nyama Mungu anakua hana uwezo wa kumuendesha mwanadamu.

Kwahiyo hii inamaanisha kwamba mambo yote yafanyikayo ndani ya mtu kupitia upande ule wa kiroho huwa Mungu anayajua moja kwa moja ila yale ambayo hufanyika katika upande ule wa kimwili huwa Mungu hayajui.

Na hii ndio sababu iliyopelekea Mungu amuhofie mwanadamu kwa maana ni ngumu kujua ya kwamba yale ayawazayo katika upande wa kiroho ndiyo ayawazayo katika ule upande wake wa kimwili kwa maana ya ule upande wa damu na nyama.

Kwa kulithibitisha hili kwenye maandiko ya kiimani kuna historia ya bwana mmoja anaitwa Ayubu, huyu mtu alikua ni mtu bora sana mbele za Mungu kwa maana upande wake wa kiroho haukua na shida yoyote hadi kufikia kiwango cha Mungu kujivunia yeye lakini licha ya kwamba Mungu alikua anajivunia yeye ila bado hakuwa na hakika na ile KWELI iliyo ndani yake kwa maana maandiko yanasema tumuabudu Mungu kwa ROHO na KWELI Sasa huyu bwana Ayubu ni kwamba kwenye upande wa ROHO alikua vizuri mbele za Mungu ila ile KWELI ndio ilikua inampa mashaka Mungu hadi kupelekea kumpa majaribu ya kimwili ili aone je yaliyopo rohoni mwake ni sawa na yale ambayo yapo mwilini mwake?

Lakini pia ukisoma maandiko hayo hayo kuna swali Yesu aliwauliza wanafunzi wake ya kwamba je, watu wanasema mimi ni nani?

Kikawaida ni kwamba kwa namna ya kiroho Yesu alijua vile watu wasemavyo kuhusu yeye ila kwa namna ya upande ule wa damu na nyama hakuwa anajua chochote na ndio maana alitaka apate uhakika ya kwamba je yale ya rohoni mwao ni sawa na yaliyopo katika ule upande wao wa kimwili?.

Kwa maana maandiko yanasema Mungu anataka kuabudiwa kwa ROHO na KWELI, kwa maana ni rahisi sana mtu kumuabudu Mungu kwa roho ila akashindwa kwenye kweli, kwa maana kumuabudu Mungu kwa roho ni kuwa mnyenyekevu mbele zake ila kwa kweli ni kuyaskia yale yote ya rohoni na kuyafuata kwenye upande wa mwili kwa maana ya kwamba ili uwe unamuabudu Mungu kwa roho na kweli nilazima uiruhusu roho yako iuongoze mwili, uiskie ile sauti ya ndani mwako na uifuate kama ambavyo inavyokuongoza na hapo ndipo utakapoweza kumuabudu Mungu kwa roho na kweli.

Kwa maana nyingine ni kwamba Mungu anataka akuongoze si wewe ujiongoze mwenyewe kwa kufuata yale maamuzi yatokayo katika upande wako wa damu na nyama.

Ni sawa na wewe hapo ukitengeneza robot lako hautataka lijiongoze lenyewe bali utataka uliongoze na ikitokea likaanza kujiongoza basi kuna namna hautajiskia vizuri.

Kwa hiyo Mungu ni kama rubani wa chini ila wewe yaani huo upande wako wa damu na nyama ni rubani wa ndani ya ndege kwa maana ili ndege iweze kwenda na kufika salama ni lazima rubani wa ndani ya ndege amskilize rubani wa chini kwa maana rubani wa chini ndiye anaejua mifumo yote ya anga pamoja na namna inavyokwenda Kwahiyo akisema shuka chini kidogo rubani wa ndani ya ndege anatakiwa ashushe ndege chini kwa kiwango alichoambiwa akisema aelekee mashariki basi anapaswa kufanya hivyo na kadhalika, Sasa ikitokea yule rubani wa ndani ya ndege akapuuzia sauti inayotoka kwa rubani wa chini basi moja kwa moja ndege inakuwa hatarini kwa maana rubani wa ndani ya ndege hajui mifumo ya anga Kwahiyo hali ya anga ikibadilika kidogo basi ndege itayumbishwa na itaanguka.

Lakini pia mawasiliano yakipotea baina ya rubani wa anga na rubani wa chini huwa ndege inapotea kwenye lada na ikipotea kwenye lada mifumo ya anga iliyopo chini huwa haiwezi kujua wapi hiyo ndege ilipo na ndio sawa sawa na mwanadamu pindi atakapoacha kuiskiliza sauti ya rohoni mwake na kuiskiliza sauti ya kimwili huwa ni rahisi sana kuishi maisha yaliyo nje ya hatima na ukiuacha mwili uiendeshe roho yaani mwili uifunze roho namna sahihi ya kuishi basi hapa mtu anakua amepotea katika ile mitetemo ya kimungu kwa maana yoote atakayo kuwa anayafanya kwa maana ya kimwili huwa hayaonekani katika mifumo ya Kimungu.

Na ndio maana watu husema Mungu ni roho kwa maana ya kwamba uwezo wa Mungu kuyajua yote yakiyomo ndani ya mwanadamu huwa unaishia katika upande huo wa kiroho ila ukija kwenye upande wa kimwili hawezi kujua.

Mambo haya ni kama hii teknolojia ya AI, ni kwamba mtu anapotengeneza robot huwa analiwekea command ya kwamba liwe na uwezo wa kufanya moja mbili tatu, lakini ukiacha nafasi ndani ya robot na kulipa uwezo wa kuweza kuhifadhi na kujifunza mambo mengine mapya kutokana na mazingira huwa ni ngumu kwa mtu aliyelitengeneza kujua ni mambo mangapi robot hilo litakua limejifunza kutokana na mazingira ukiachana na yale ambayo yeye aliliwekea ndani yake wakati analitengeneza.

Na teknolojia hii kwa kadri inavyokua na ikija kufikia kwenye hatua ya kuweza kuyapa haya marobot uwezo wa kuamua kwa maana ya ule uwezo wa kujua mema na mabaya kama ambavyo mwanadamu alipewa huo uwezo pale bustanini na wale wana wa Mungu ambao walikuwepo pale basi hapo ndipo ugumu utakapokuwepo kwenye kuyaongoza haya marobot kwa maana yatakua na pande mbili yaani upande ule wa zile command yaani amri ambazo waliwekewa wakati yanatengenezwa lakini pia yatakua na ule upande wa kumbukumbu zao binafsi ambazo zinahifadhiwa ndani yao kutokana na mazingira waliyopo sasa wakiyafanya yale yaliyo ndani ya command itakua rahisi kujua hatua inayofuata baada ya hapo ila yakifanya yale mambo yaliyo nje ya zile command kwa maana yakifanya yale mambo ambayo yenyewe yamejifunza inakua ngumu kujua ni nini kinafuata baada ya hapo na ndio hapa ambapo watu husema kwamba linakua linabehave tofauti na vile ilivyo tarajiwa.

Kwahiyo hii teknoloji bado iko katika kiwango cha awali kabisa kwa sasa hapa duniani au ulimwenguni kwa ujumla ila kwa kadri siku zinavyokwenda itaendelea kukua na itafikia pahala dunia yote itakua inaiogopa hii teknoloji kwa maana vitu tutakavyo vizalisha vitatushinda kwenye kuviongoza kwa maana vitakua na uwezo wa kujiendesha venyewe na kuanza kuwa na maamuzi yake binafsi na hapa ndipo tutakapojua au kugundua kwamba tabu tutakazo zipata kupitia hizo robots ndizo ambazo waliyo tuumba wanazipata.

Kwakusema hayo naomba nihitimishe hili andiko langu kwa kusema hili neno la Mungu ni roho na si mwili linamaanisha kwamba uwezo wa Mungu kuyaona yaliyomo ndani ya mtu huishia kwenye ule upande wa kiroho ila ukija upande wa kimwili hana anachokijua.
 
Kiuhalisia ni kwamba mara nyingi watu wamekua wakisema Mungu ni roho, namimi nakubaliana na hii kauli ya kwamba ni kweli Mungu ni roho, lakini tujiulize kidogo je, Mungu ni roho kwa namna gani? Kwa maana maandiko husema ya kwamba sisi tuliumbwa kwa mfano wake.

Kwahiyo kama sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu basi sisi ni kopi yake, na kama sisi ni kopi yake basi hakuna chochote kilicho kwetu kikawa hakipo kwake ingawa yawezekana yapo yaliyo kwake yakawa hayapo kwetu kwa maana kopi haiwezi kuwa sawasawa na ile halisi kwa asilimia mia moja ingawa kopi kimuonekano haiwezi kutofautiana na halisi.

Sasa hoja hii inaenda kupingana na ile hoja ya wale ambao wanaamini ya kwamba Mungu ni roho tupu isiyo na mwili kwa maana ukiachana na hii hoja lakini pia ukisoma maandiko katika kile kitabu cha mwanzo utagundua ya kwamba Mungu si roho tu pekee bali nayeye ni roho iliyo ndani ya nyama.

Maandiko yanasema hivi "roho yangu haitashindana na mwanadamu kamwe kwani yu nyama na yeye, Kwahiyo miaka yake itakua 120".

Hilo neno la kwani yu nyama na yeye inamaana ya kwamba Mungu angeweza kushindana na mwanadamu kama tu angekua na roho tupu ila kwakua mwanadamu anao upande wa kiroho na upande wa nyama kama vile Mungu alivyo basi inakua ngumu yeye Mungu kushindana nae.

Yu nyama na yeye inamaana ya kwamba na yeye ni nyama kama mimi.

Na andiko hilo hilo ukiendelea kulitafakari zaidi utagundua ya kwamba Mungu anaweza kumuendesha binadamu katika ule upande wa kiroho pekee ila unapokuja upande wa damu na nyama Mungu anakua hana uwezo wa kumuendesha mwanadamu.

Kwahiyo hii inamaanisha kwamba mambo yote yafanyikayo ndani ya mtu kupitia upande ule wa kiroho huwa Mungu anayajua moja kwa moja ila yale ambayo hufanyika katika upande ule wa kimwili huwa Mungu hayajui.

Na hii ndio sababu iliyopelekea Mungu amuhofie mwanadamu kwa maana ni ngumu kujua ya kwamba yale ayawazayo katika upande wa kiroho ndiyo ayawazayo katika ule upande wake wa kimwili kwa maana ya ule upande wa damu na nyama.

Kwa kulithibitisha hili kwenye maandiko ya kiimani kuna historia ya bwana mmoja anaitwa Ayubu, huyu mtu alikua ni mtu bora sana mbele za Mungu kwa maana upande wake wa kiroho haukua na shida yoyote hadi kufikia kiwango cha Mungu kujivunia yeye lakini licha ya kwamba Mungu alikua anajivunia yeye ila bado hakuwa na hakika na ile KWELI iliyo ndani yake kwa maana maandiko yanasema tumuabudu Mungu kwa ROHO na KWELI Sasa huyu bwana Ayubu ni kwamba kwenye upande wa ROHO alikua vizuri mbele za Mungu ila ile KWELI ndio ilikua inampa mashaka Mungu hadi kupelekea kumpa majaribu ya kimwili ili aone je yaliyopo rohoni mwake ni sawa na yale ambayo yapo mwilini mwake?

Lakini pia ukisoma maandiko hayo hayo kuna swali Yesu aliwauliza wanafunzi wake ya kwamba je, watu wanasema mimi ni nani?

Kikawaida ni kwamba kwa namna ya kiroho Yesu alijua vile watu wasemavyo kuhusu yeye ila kwa namna ya upande ule wa damu na nyama hakuwa anajua chochote na ndio maana alitaka apate uhakika ya kwamba je yale ya rohoni mwao ni sawa na yaliyopo katika ule upande wao wa kimwili?.

Kwa maana maandiko yanasema Mungu anataka kuabudiwa kwa ROHO na KWELI, kwa maana ni rahisi sana mtu kumuabudu Mungu kwa roho ila akashindwa kwenye kweli, kwa maana kumuabudu Mungu kwa roho ni kuwa mnyenyekevu mbele zake ila kwa kweli ni kuyaskia yale yote ya rohoni na kuyafuata kwenye upande wa mwili kwa maana ya kwamba ili uwe unamuabudu Mungu kwa roho na kweli nilazima uiruhusu roho yako iuongoze mwili, uiskie ile sauti ya ndani mwako na uifuate kama ambavyo inavyokuongoza na hapo ndipo utakapoweza kumuabudu Mungu kwa roho na kweli.

Kwa maana nyingine ni kwamba Mungu anataka akuongoze si wewe ujiongoze mwenyewe kwa kufuata yale maamuzi yatokayo katika upande wako wa damu na nyama.

Ni sawa na wewe hapo ukitengeneza robot lako hautataka lijiongoze lenyewe bali utataka uliongoze na ikitokea likaanza kujiongoza basi kuna namna hautajiskia vizuri.

Kwa hiyo Mungu ni kama rubani wa chini ila wewe yaani huo upande wako wa damu na nyama ni rubani wa ndani ya ndege kwa maana ili ndege iweze kwenda na kufika salama ni lazima rubani wa ndani ya ndege amskilize rubani wa chini kwa maana rubani wa chini ndiye anaejua mifumo yote ya anga pamoja na namna inavyokwenda Kwahiyo akisema shuka chini kidogo rubani wa ndani ya ndege anatakiwa ashushe ndege chini kwa kiwango alichoambiwa akisema aelekee mashariki basi anapaswa kufanya hivyo na kadhalika, Sasa ikitokea yule rubani wa ndani ya ndege akapuuzia sauti inayotoka kwa rubani wa chini basi moja kwa moja ndege inakuwa hatarini kwa maana rubani wa ndani ya ndege hajui mifumo ya anga Kwahiyo hali ya anga ikibadilika kidogo basi ndege itayumbishwa na itaanguka.

Lakini pia mawasiliano yakipotea baina ya rubani wa anga na rubani wa chini huwa ndege inapotea kwenye lada na ikipotea kwenye lada mifumo ya anga iliyopo chini huwa haiwezi kujua wapi hiyo ndege ilipo na ndio sawa sawa na mwanadamu pindi atakapoacha kuiskiliza sauti ya rohoni mwake na kuiskiliza sauti ya kimwili huwa ni rahisi sana kuishi maisha yaliyo nje ya hatima na ukiuacha mwili uiendeshe roho yaani mwili uifunze roho namna sahihi ya kuishi basi hapa mtu anakua amepotea katika ile mitetemo ya kimungu kwa maana yoote atakayo kuwa anayafanya kwa maana ya kimwili huwa hayaonekani katika mifumo ya Kimungu.

Na ndio maana watu husema Mungu ni roho kwa maana ya kwamba uwezo wa Mungu kuyajua yote yakiyomo ndani ya mwanadamu huwa unaishia katika upande huo wa kiroho ila ukija kwenye upande wa kimwili hawezi kujua.

Mambo haya ni kama hii teknolojia ya AI, ni kwamba mtu anapotengeneza robot huwa analiwekea command ya kwamba liwe na uwezo wa kufanya moja mbili tatu, lakini ukiacha nafasi ndani ya robot na kulipa uwezo wa kuweza kuhifadhi na kujifunza mambo mengine mapya kutokana na mazingira huwa ni ngumu kwa mtu aliyelitengeneza kujua ni mambo mangapi robot hilo litakua limejifunza kutokana na mazingira ukiachana na yale ambayo yeye aliliwekea ndani yake wakati analitengeneza.

Na teknolojia hii kwa kadri inavyokua na ikija kufikia kwenye hatua ya kuweza kuyapa haya marobot uwezo wa kuamua kwa maana ya ule uwezo wa kujua mema na mabaya kama ambavyo mwanadamu alipewa huo uwezo pale bustanini na wale wana wa Mungu ambao walikuwepo pale basi hapo ndipo ugumu utakapokuwepo kwenye kuyaongoza haya marobot kwa maana yatakua na pande mbili yaani upande ule wa zile command yaani amri ambazo waliwekewa wakati yanatengenezwa lakini pia yatakua na ule upande wa kumbukumbu zao binafsi ambazo zinahifadhiwa ndani yao kutokana na mazingira waliyopo sasa wakiyafanya yale yaliyo ndani ya command itakua rahisi kujua hatua inayofuata baada ya hapo ila yakifanya yale mambo yaliyo nje ya zile command kwa maana yakifanya yale mambo ambayo yenyewe yamejifunza inakua ngumu kujua ni nini kinafuata baada ya hapo na ndio hapa ambapo watu husema kwamba linakua linabehave tofauti na vile ilivyo tarajiwa.

Kwahiyo hii teknoloji bado iko katika kiwango cha awali kabisa kwa sasa hapa duniani au ulimwenguni kwa ujumla ila kwa kadri siku zinavyokwenda itaendelea kukua na itafikia pahala dunia yote itakua inaiogopa hii teknoloji kwa maana vitu tutakavyo vizalisha vitatushinda kwenye kuviongoza kwa maana vitakua na uwezo wa kujiendesha venyewe na kuanza kuwa na maamuzi yake binafsi na hapa ndipo tutakapojua au kugundua kwamba tabu tutakazo zipata kupitia hizo robots ndizo ambazo waliyo tuumba wanazipata.

Kwakusema hayo naomba nihitimishe hili andiko langu kwa kusema hili neno la Mungu ni roho na si mwili linamaanisha kwamba uwezo wa Mungu kuyaona yaliyomo ndani ya mtu huishia kwenye ule upande wa kiroho ila ukija upande wa kimwili hana anachokijua.
Basi huyo Mungu si mjuzi wa vyote na hajui yote.

Na kwa maana hiyo, Hawezi yote.
 
Ni kwa sababu viumbe vinakufa.

Fikiria viumbe visingekuwa vinakufa,leo hii kungekuwa hata na ardhi ya kutosheleza viumbe wote?
Maarifa yangeongezeka so kuna namna lile neno la kuutawala ulimwengu lingepata kukamilishwa... katika ulimwengu huu ni sayari moja tu ya dunia ndio ambayo mwanadamu anaishi ila ulimwengu si dunia tu pekee.
 
Kiuhalisia ni kwamba mara nyingi watu wamekua wakisema Mungu ni roho, namimi nakubaliana na hii kauli ya kwamba ni kweli Mungu ni roho, lakini tujiulize kidogo je, Mungu ni roho kwa namna gani? Kwa maana maandiko husema ya kwamba sisi tuliumbwa kwa mfano wake.

Kwahiyo kama sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu basi sisi ni kopi yake, na kama sisi ni kopi yake basi hakuna chochote kilicho kwetu kikawa hakipo kwake ingawa yawezekana yapo yaliyo kwake yakawa hayapo kwetu kwa maana kopi haiwezi kuwa sawasawa na ile halisi kwa asilimia mia moja ingawa kopi kimuonekano haiwezi kutofautiana na halisi.

Sasa hoja hii inaenda kupingana na ile hoja ya wale ambao wanaamini ya kwamba Mungu ni roho tupu isiyo na mwili kwa maana ukiachana na hii hoja lakini pia ukisoma maandiko katika kile kitabu cha mwanzo utagundua ya kwamba Mungu si roho tu pekee bali nayeye ni roho iliyo ndani ya nyama.

Maandiko yanasema hivi "roho yangu haitashindana na mwanadamu kamwe kwani yu nyama na yeye, Kwahiyo miaka yake itakua 120".

Hilo neno la kwani yu nyama na yeye inamaana ya kwamba Mungu angeweza kushindana na mwanadamu kama tu angekua na roho tupu ila kwakua mwanadamu anao upande wa kiroho na upande wa nyama kama vile Mungu alivyo basi inakua ngumu yeye Mungu kushindana nae.

Yu nyama na yeye inamaana ya kwamba na yeye ni nyama kama mimi.

Na andiko hilo hilo ukiendelea kulitafakari zaidi utagundua ya kwamba Mungu anaweza kumuendesha binadamu katika ule upande wa kiroho pekee ila unapokuja upande wa damu na nyama Mungu anakua hana uwezo wa kumuendesha mwanadamu.

Kwahiyo hii inamaanisha kwamba mambo yote yafanyikayo ndani ya mtu kupitia upande ule wa kiroho huwa Mungu anayajua moja kwa moja ila yale ambayo hufanyika katika upande ule wa kimwili huwa Mungu hayajui.

Na hii ndio sababu iliyopelekea Mungu amuhofie mwanadamu kwa maana ni ngumu kujua ya kwamba yale ayawazayo katika upande wa kiroho ndiyo ayawazayo katika ule upande wake wa kimwili kwa maana ya ule upande wa damu na nyama.

Kwa kulithibitisha hili kwenye maandiko ya kiimani kuna historia ya bwana mmoja anaitwa Ayubu, huyu mtu alikua ni mtu bora sana mbele za Mungu kwa maana upande wake wa kiroho haukua na shida yoyote hadi kufikia kiwango cha Mungu kujivunia yeye lakini licha ya kwamba Mungu alikua anajivunia yeye ila bado hakuwa na hakika na ile KWELI iliyo ndani yake kwa maana maandiko yanasema tumuabudu Mungu kwa ROHO na KWELI Sasa huyu bwana Ayubu ni kwamba kwenye upande wa ROHO alikua vizuri mbele za Mungu ila ile KWELI ndio ilikua inampa mashaka Mungu hadi kupelekea kumpa majaribu ya kimwili ili aone je yaliyopo rohoni mwake ni sawa na yale ambayo yapo mwilini mwake?

Lakini pia ukisoma maandiko hayo hayo kuna swali Yesu aliwauliza wanafunzi wake ya kwamba je, watu wanasema mimi ni nani?

Kikawaida ni kwamba kwa namna ya kiroho Yesu alijua vile watu wasemavyo kuhusu yeye ila kwa namna ya upande ule wa damu na nyama hakuwa anajua chochote na ndio maana alitaka apate uhakika ya kwamba je yale ya rohoni mwao ni sawa na yaliyopo katika ule upande wao wa kimwili?.

Kwa maana maandiko yanasema Mungu anataka kuabudiwa kwa ROHO na KWELI, kwa maana ni rahisi sana mtu kumuabudu Mungu kwa roho ila akashindwa kwenye kweli, kwa maana kumuabudu Mungu kwa roho ni kuwa mnyenyekevu mbele zake ila kwa kweli ni kuyaskia yale yote ya rohoni na kuyafuata kwenye upande wa mwili kwa maana ya kwamba ili uwe unamuabudu Mungu kwa roho na kweli nilazima uiruhusu roho yako iuongoze mwili, uiskie ile sauti ya ndani mwako na uifuate kama ambavyo inavyokuongoza na hapo ndipo utakapoweza kumuabudu Mungu kwa roho na kweli.

Kwa maana nyingine ni kwamba Mungu anataka akuongoze si wewe ujiongoze mwenyewe kwa kufuata yale maamuzi yatokayo katika upande wako wa damu na nyama.

Ni sawa na wewe hapo ukitengeneza robot lako hautataka lijiongoze lenyewe bali utataka uliongoze na ikitokea likaanza kujiongoza basi kuna namna hautajiskia vizuri.

Kwa hiyo Mungu ni kama rubani wa chini ila wewe yaani huo upande wako wa damu na nyama ni rubani wa ndani ya ndege kwa maana ili ndege iweze kwenda na kufika salama ni lazima rubani wa ndani ya ndege amskilize rubani wa chini kwa maana rubani wa chini ndiye anaejua mifumo yote ya anga pamoja na namna inavyokwenda Kwahiyo akisema shuka chini kidogo rubani wa ndani ya ndege anatakiwa ashushe ndege chini kwa kiwango alichoambiwa akisema aelekee mashariki basi anapaswa kufanya hivyo na kadhalika, Sasa ikitokea yule rubani wa ndani ya ndege akapuuzia sauti inayotoka kwa rubani wa chini basi moja kwa moja ndege inakuwa hatarini kwa maana rubani wa ndani ya ndege hajui mifumo ya anga Kwahiyo hali ya anga ikibadilika kidogo basi ndege itayumbishwa na itaanguka.

Lakini pia mawasiliano yakipotea baina ya rubani wa anga na rubani wa chini huwa ndege inapotea kwenye lada na ikipotea kwenye lada mifumo ya anga iliyopo chini huwa haiwezi kujua wapi hiyo ndege ilipo na ndio sawa sawa na mwanadamu pindi atakapoacha kuiskiliza sauti ya rohoni mwake na kuiskiliza sauti ya kimwili huwa ni rahisi sana kuishi maisha yaliyo nje ya hatima na ukiuacha mwili uiendeshe roho yaani mwili uifunze roho namna sahihi ya kuishi basi hapa mtu anakua amepotea katika ile mitetemo ya kimungu kwa maana yoote atakayo kuwa anayafanya kwa maana ya kimwili huwa hayaonekani katika mifumo ya Kimungu.

Na ndio maana watu husema Mungu ni roho kwa maana ya kwamba uwezo wa Mungu kuyajua yote yakiyomo ndani ya mwanadamu huwa unaishia katika upande huo wa kiroho ila ukija kwenye upande wa kimwili hawezi kujua.

Mambo haya ni kama hii teknolojia ya AI, ni kwamba mtu anapotengeneza robot huwa analiwekea command ya kwamba liwe na uwezo wa kufanya moja mbili tatu, lakini ukiacha nafasi ndani ya robot na kulipa uwezo wa kuweza kuhifadhi na kujifunza mambo mengine mapya kutokana na mazingira huwa ni ngumu kwa mtu aliyelitengeneza kujua ni mambo mangapi robot hilo litakua limejifunza kutokana na mazingira ukiachana na yale ambayo yeye aliliwekea ndani yake wakati analitengeneza.

Na teknolojia hii kwa kadri inavyokua na ikija kufikia kwenye hatua ya kuweza kuyapa haya marobot uwezo wa kuamua kwa maana ya ule uwezo wa kujua mema na mabaya kama ambavyo mwanadamu alipewa huo uwezo pale bustanini na wale wana wa Mungu ambao walikuwepo pale basi hapo ndipo ugumu utakapokuwepo kwenye kuyaongoza haya marobot kwa maana yatakua na pande mbili yaani upande ule wa zile command yaani amri ambazo waliwekewa wakati yanatengenezwa lakini pia yatakua na ule upande wa kumbukumbu zao binafsi ambazo zinahifadhiwa ndani yao kutokana na mazingira waliyopo sasa wakiyafanya yale yaliyo ndani ya command itakua rahisi kujua hatua inayofuata baada ya hapo ila yakifanya yale mambo yaliyo nje ya zile command kwa maana yakifanya yale mambo ambayo yenyewe yamejifunza inakua ngumu kujua ni nini kinafuata baada ya hapo na ndio hapa ambapo watu husema kwamba linakua linabehave tofauti na vile ilivyo tarajiwa.

Kwahiyo hii teknoloji bado iko katika kiwango cha awali kabisa kwa sasa hapa duniani au ulimwenguni kwa ujumla ila kwa kadri siku zinavyokwenda itaendelea kukua na itafikia pahala dunia yote itakua inaiogopa hii teknoloji kwa maana vitu tutakavyo vizalisha vitatushinda kwenye kuviongoza kwa maana vitakua na uwezo wa kujiendesha venyewe na kuanza kuwa na maamuzi yake binafsi na hapa ndipo tutakapojua au kugundua kwamba tabu tutakazo zipata kupitia hizo robots ndizo ambazo waliyo tuumba wanazipata.

Kwakusema hayo naomba nihitimishe hili andiko langu kwa kusema hili neno la Mungu ni roho na si mwili linamaanisha kwamba uwezo wa Mungu kuyaona yaliyomo ndani ya mtu huishia kwenye ule upande wa kiroho ila ukija upande wa kimwili hana anachokijua.
Thibitisha roho ipo.
 
Umejitahidi kutafakari Ila hujui mambo mengi sana na huiaujua uwezo wa Mungu! Endelea kujifunza na kusoma zaidi utakuja kuelewa ukiruhusu ufahamu wako kuelewa zaidi ya unavyoelewa Kwa sasa. Mungu ni Roho hana nyama kama unavyodhani. Tena akaamua kuuvaa mwili pale alipokuja duniani (Yesu Kristo) Kisha akaendelea Kwa mfumo huu (Roho Mtakatifu) anajua yote, ya rohoni na ya mwilini, ndiyo ameumba vinavyoonekana na visivyo onekana. Ameumba Dunia na mwili wa damu na nyama ameuumba ndiyo huu una asili ya Dunia hii. Haiwezekani aweze kuumba kitu asichokuwa na uwezo nacho. Yeye aliyeumba ni Mkuu kuliko kilichoumbwa, ni kama mfinyanzi na chombo cha udongo anachokifinyanga. Mungu ni Roho na mwanadamu ni roho ina nafsi inaishi ndani ya mwili wa damu na nyama. Mungu angekuwa na mwili wa nyama kusingeandikwa kwamba damu na nyama havitaurithi ufalme wa Mungu. Ila ipo miili ya kiroho, sasa usichanganye huu mwili wa kiroho na mwili wa damu na nyama mzee.
 
Halafu anaposema "Roho yangu haitashindana na mwanadamu Kwa kuwa na yeye ni nyama" hapa inamaana kwamba mwanadamu ni mungu siyo Mungu, tena ni kama viumbe wengine Kwa asili ya mwili wake hapa duniani maana yake anao ukomo wa kuishi maisha ya kimwili, na roho ndiyo inayotia uzima mwili pasipo roho hauna maisha. Tambua kwamba mtu ni roho na roho haifi inaishi milele, ndiyo maana Mungu aliye muumba mwanadamu ameamuru kupungua Kwa siku za mwanadamu na kuwa miaka 120 Kwa wakati ule, ukumbuke watu walikuwa wakiishi miaka mia tisa na zaidi. Baadaye huku unakutana na mtu mwingine anasema wazi wazi kuwa "siku zetu ni miaka 70 na ikiwa tuna nguvu ni miaka 80". Kwa hiyo Mungu yupo juu ya yote hakuna kiumbe cha kiroho pasipo mwili wala cha kiroho chenye mwili kinachoweza kushindana naye au kumficha kitu chochote asikijue
 
Umejitahidi kutafakari Ila hujui mambo mengi sana na huiaujua uwezo wa Mungu! Endelea kujifunza na kusoma zaidi utakuja kuelewa ukiruhusu ufahamu wako kuelewa zaidi ya unavyoelewa Kwa sasa. Mungu ni Roho hana nyama kama unavyodhani. Tena akaamua kuuvaa mwili pale alipokuja duniani (Yesu Kristo) Kisha akaendelea Kwa mfumo huu (Roho Mtakatifu) anajua yote, ya rohoni na ya mwilini, ndiyo ameumba vinavyoonekana na visivyo onekana. Ameumba Dunia na mwili wa damu na nyama ameuumba ndiyo huu una asili ya Dunia hii. Haiwezekani aweze kuumba kitu asichokuwa na uwezo nacho. Yeye aliyeumba ni Mkuu kuliko kilichoumbwa, ni kama mfinyanzi na chombo cha udongo anachokifinyanga. Mungu ni Roho na mwanadamu ni roho ina nafsi inaishi ndani ya mwili wa damu na nyama. Mungu angekuwa na mwili wa nyama kusingeandikwa kwamba damu na nyama havitaurithi ufalme wa Mungu. Ila ipo miili ya kiroho, sasa usichanganye huu mwili wa kiroho na mwili wa damu na nyama mzee.
Mungu ni roho iliyo ndani ya nyama ila yenye uwezo kuliko mwanadamu.

Huwezi kusema unakitengeneza kitu fulani kwa mfano wa kitu fulani halafu ukaacha kukiweka kwenye mfanano.

Angalia simu mnazoziita copy ni kwamba ukiiangalia ile simu halisi inakua haina tofauti na ile simu kopi kwa nje ila utofauti wake huwa unakua kwa ndani kwa maana ya uwezo wa kufanya kazi.

Robot kitu chenye umuhimu zaidi si umbo lake nje ila ni ile chipu iliyowekwa ndani yake kwa maana taarifa zote muhimu zipo humo.

Kwahiyo roho itakwenda na mwili utabaki.

Mungu alikua na uwezo na sisi kabla hatujapata kujitambua kwa maana ya kujua mema na mabaya ila baada ya sisi kupata huo uwezo Mungu aliamua kuighairisha ile project yake iliyokua inaendelea pale bustanini na mwenyewe alisema kwamba anaghairi na atafuta vyote alivyoviumba juu ya uso wa dunia kwa maana ule mradi ulikua unaenda kwa namna tofauti na vile ambavyo yeye alitaka uende.

Na walioharibu ule mradi ni wale wana wa Mungu pamoja na mwanadamu ambae alikuwepo pale bustanini kwa maana mwanzo ule mradi haukutakiwa kuwa changamani kwa maana kila jamii ilitakiwa iwe inaendeleza kizazi chake yenyewe kwa yenyewe pasipo kuingiliana baina ya jamii na jamii ila ilipotokea wale wana wa Mungu kuingiliana na mwanadamu hapo ndipo mambo yalipoharibika hadi kupelekea ule mradi kufutwa kwa gharika... nenda kasome biblia yako vizuri tena ukiwa katika hali ya utulivu wa akili hasa kile kitabu cha mwanzo.
 
Mungu ni roho iliyo ndani ya nyama ila yenye uwezo kuliko mwanadamu.

Huwezi kusema unakitengeneza kitu fulani kwa mfano wa kitu fulani halafu ukaacha kukiweka kwenye mfanano.

Angalia simu mnazoziita copy ni kwamba ukiiangalia ile simu halisi inakua haina tofauti na ile simu kopi kwa nje ila utofauti wake huwa unakua kwa ndani kwa maana ya uwezo wa kufanya kazi.

Robot kitu chenye umuhimu zaidi si umbo lake nje ila ni ile chipu iliyowekwa ndani yake kwa maana taarifa zote muhimu zipo humo.

Kwahiyo roho itakwenda na mwili utabaki.

Mungu alikua na uwezo na sisi kabla hatujapata kujitambua kwa maana ya kujua mema na mabaya ila baada ya sisi kupata huo uwezo Mungu aliamua kuighairisha ile project yake iliyokua inaendelea pale bustanini na mwenyewe alisema kwamba anaghairi na atafuta vyote alivyoviumba juu ya uso wa dunia kwa maana ule mradi ulikua unaenda kwa namna tofauti na vile ambavyo yeye alitaka uende.

Na walioharibu ule mradi ni wale wana wa Mungu pamoja na mwanadamu ambae alikuwepo pale bustanini kwa maana mwanzo ule mradi haukutakiwa kuwa changamani kwa maana kila jamii ilitakiwa iwe inaendeleza kizazi chake yenyewe kwa yenyewe pasipo kuingiliana baina ya jamii na jamii ila ilipotokea wale wana wa Mungu kuingiliana na mwanadamu hapo ndipo mambo yalipoharibika hadi kupelekea ule mradi kufutwa kwa gharika... nenda kasome biblia yako vizuri tena ukiwa katika hali ya utulivu wa akili hasa kile kitabu cha mwanzo.
Wana wa Mungu na wana wa wanadamu wameingiliana huku kipindi cha Nuhu, ujuzi wa kujua mema na mabaya umetokea kipindi Adamu na Hawa wakiwa bado ndani ya bustani ya Edeni wakiwa bado hawajazaa hata mtoto mmoja!
 
Wana wa Mungu na wana wa wanadamu wameingiliana huku kipindi cha Nuhu, ujuzi wa kujua mema na mabaya umetokea kipindi Adamu na Hawa wakiwa bado ndani ya bustani ya Edeni wakiwa bado hawajazaa hata mtoto mmoja!
Mwanzo sita ndio unayosemea wewe ila bado kuna code hujaifungua vizuri pale bustanini na kwa kukusaidia tu wacha nikupe hiki kipande usome.
Wana wa Mungu na wana wa wanadamu wameingiliana huku kipindi cha Nuhu, ujuzi wa kujua mema na mabaya umetokea kipindi Adamu na Hawa wakiwa bado ndani ya bustani ya Edeni wakiwa bado hawajazaa hata mtoto mmoja!
Sasa basi ni kwamba dunia ilitakiwa iwe sehemu yenye mchanganyiko wa viumbe walio na mfanano sawa na binadamu ila katika utofauti wa uwezo wao wa kufikiri na namna ya kukabiliana na mambo.

Mradi huu wa ulimwengu na jamii ya viumbe hivyo haukutakiwa kuwa changamani kwa maana ya kwamba kila jamii ilitakiwa iendeleze uzao wao wenyewe kwa wenyewe bila kuingiliana, yaani jamii hii kwenda kuzaa na jamii ile na kadhalika.

Sasa Mradi huu ulikuja kushindwa kwenda katika namna ile iliyotakiwa baada ya viumbe kuanza kuchangamana katika maswala ya uzazi, na waliofanya mradi huu ufe au usitishwe ni viumbe wa jamii mbili yaani kiumbe asilia na kile ambacho kilikua kopi ya kile kiumbe asilia.

Na stori hii imeelezewa vizuri sana ila katika mtindo wa mafumbo kwenye kile kitabu cha mwanzo katika biblia.

Basi namie nitatumia kitabu hiko hiko cha mwanzo ili kuelezea asili hii ya uumbaji katika ulimwengu pamoja na uwepo wa nguvu za asili za ulimwengu ambazo ndizo tutakazo kwenda kuzizungumzia kwa kiasi kikubwa katika maeneo mengi ya kitabu hiki.

Pia ningependa niliweke hili sawa, hiki kitabu hakifungamani na dini ya aina yoyote ile ila katika sehemu hii nitatumia aya kadhaa za maandiko ambazo nimezitoa kwenye kile kitabu cha Mwanzo na nimetumia biblia ila najua utofauti wa aya hizi katika biblia utakua ni mdogo sana katika vitabu vingine vya kiimani ambavyo ndani yake kitabu hiki cha Mwanzo kipo kwa mfano Quran.

Na kabla sijaenda kwenye maandiko Kwanza nataka uelewe ya kwamba neno Adamu katika biblia huwa linatumika mara mbili, kwa maana ya kwamba neno hili kuna nyakati huwa linatumika kama kiwakilishi cha wale watu ambao waliumbwa mwanzo kabisa yaani mwanaume na mwanamke na pia kuna wakati huwa linatumika kumzungumzia mwanaume (ndio maana hapo juu kuna sehemu nimekua nikisema Adamu mwanamume au Adamu mwanamke)

Lakini yote kwa yote unatakiwa ujue ya kwamba matumizi sahihi ya neno hili yamefafanuliwa katika biblia ukisoma pale mwanzo 5 kuanzia mstari ule wa Kwanza hadi wa pili kwa maana ya 5:1-2.

Andiko hilo linaanza kwa kusema hivi " Hiki ndio kitabu cha vizazi vya Adamu. (Je, Adamu ni nani? Biblia inaendelea kukufafanulia zaidi kwa kuendelea kusema kwamba) Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya; mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa".

Sasa kutokana na hayo maandiko hapo juu utagundua kwamba neno Adamu ni jina ambalo walipewa mwanamume na mwanamke siku ile ambayo waliumbwa, kwa hiyo biblia kuna nyakati ikisema Adamu kuwa na hakika inamaanisha mtu mume na mtu mke ambao waliumbwa kwa mfano wa Mungu.

Maeneo yote ambayo neno Adamu limetumika kumzungumzia mwanamume huwa linafafanuliwa moja kwa moja na maeneo yote ambayo neno Adamu lilitumika bila kufafanuliwa jua linazungumzia huo muunganiko wa mwanamume na mwanamke waliyoumbwa kwanza na mara zote huwa linatajwa katika hali ya umoja kwa maana wawili hao ni wamoja katika mgawanyiko wa miili iliyopewa majukumu tofauti.

Jukumu la Adamu mwanamume lilikua ni kuendeleza kizazi cha viumbe kopi ambao walitengenezwa kwa mfano wa viumbe halisi na jukumu la Adamu mwanamke lilikua ni kuendeleza kizazi cha viumbe wanaotokana na Mungu yaani kiumbe halisi na wote waliokua wanazaliwa ndio wale ambao waliitwa wana wa Mungu.

Ni kwa namna gani hawa viumbe au wana wa Mungu walizaliwa basi turudi katika biblia pale kwenye injili ya Luka Mtakatifu sura ile ya kwanza na kuanzia mstari wake wa 31 hadi 35, kwa maana ya 1:31-35.

Andiko linaanza kwa kusema hivi " tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakua mkuu, ataitwa mwana wa aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele na ufalme wake utakua hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, litakuwaje neno hili maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako na nguvu zake aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwasababu hiyo hicho kitakachozaliwa kinaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu".

Kwa hiyo ukisoma hilo andiko utapata ufafanuzi ya namna ile ambayo wana wa Mungu huzaliwa, kwa hiyo Sasa yule Adamu mwanamke ilikua kila yakifika majira fulani katika mwaka anazaa watoto na watoto hawa walipewa mfano wa matunda ya ule mti unaotokana na ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Ukisoma biblia kitabu kile cha mwanzo utagundua kwamba Mungu baada ya kumuumba Adamu aliweza kumruhusu kula matunda ya miti yote ya pale bustanini ila alimkataza kula matunda ya ule mti wa katikati.

Sasa hili neno lina maana gani? Maana ya hili neno ni kwamba Mungu alimruhusu Adamu kushirikiana na kila kiumbe ambacho Mungu alikiumba pale bustanini isipokua haruhusiwi kushirikiana na wale wana wa Mungu ambao walikua wanazaliwa na yule Adamu mwanamke pale bustanini.

Neno linasema ya kwamba licha ya Mungu kuumba viumbe na wanyama wa kila aina pale bustanini ila bado katika jamii yote ile hakukuwa na kiumbe chochote chenye muunganiko wa moja kwa moja na Adamu na ndio maana akaamua kuwafanyia msaidizi ambae anafanana nao.

Na msaidizi huyu ni kopi ya Adamu kwa maana ya kwamba Adamu ni kopi ya Mungu na yule msaidizi ni kopi ya Adamu (hapa nasisitiza ili tuelewane) na msaidizi alikua ni mwanamke na hili ni jina ambalo alipewa na Adamu mwanamume na alifafanua pale Mwanzo 2:23.

Inasema " Adamu akasema Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume".

Sasa ukiangalia hiyo sentensi utagundua kwamba Adamu ambae alikua anayasema maneno hayo ni yule Adamu mwanamume na ndio maana unaona hapo mwisho amefafanua kwamba "kwa maana ametwaliwa katika mwanamume" kwa maana ya ile kopi ya yule mwanamke ilitolewa kwa yule Adamu mwanamume na yule mwanamke aliitwa Hawa.

Huyu Hawa yeye hakuwa na muunganiko wa moja kwa moja na Mungu kwa hiyo hata ile hali ya utii ndani yake ilikua ndogo sana na ndio maana lile neno la kula yale matunda liliingia kwa kupitia yeye.

Kwa mujibu wa biblia ni kwamba nyoka alipofika pale bustanini alianzia mbali sana kwa kuanza kumuuliza huyu mwanamke ya kwamba naskia mmekatazwa kula matunda ya bustanini? Kwa maana ya kwamba naskia mmekatazwa msishirikiane na viumbe wote wa hapa bustanini? Nae akajibu, hapana tumeruhusiwa kula matunda yote ya hapa bustanini isipokua yale matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kwa maana ya kwamba hapana tumeruhusiwa kushirikiana na viumbe wote wa hapa bustanini isipokua na wana wa Mungu pekee.

Kwa hiyo baada ya ule ushawishi kuendelea Hawa alijikuta anazini na mmoja ya wale wana wa Mungu na baadae akarudi kwa mumewe yaani Adamu mwanamume akamshawishi afanye hivyo nae akafanya na baada ya hapo zile nguvu za muunganiko wa kiroho zilizopo katika hao wana wa Mungu ziliweza kuwafunua na kuwapa ule muunganiko na dunia moja kwa moja.

Kumbuka lengo la huu mradi ni kutokuingiliana kati ya Adamu, Hawa na wale Wana wa Mungu ila wao wakaungana na katika kuangalia chanzo muanzilishi wa huu mradi akaona dawa ya hawa ni kuwatenga tu, na ndio pale akamtoa Adamu pamoja na Hawa pale bustanini na kuwaacha wale wana wa Mungu pamoja na jamii ya viumbe vingine.

Sasa ukisoma biblia utagundua ya kwamba Adamu mwanamume aliweza kupata uzao na Hawa na biblia inasema kabisa kwamba Adamu akamjua mkewe Hawa na wakapata mtoto ambae walimuita Kaini, halafu inaendelea kwa kusema kwamba baada ya kumjua Akaongeza tena na kumzaa ndugu yake Habili.

Na uzao huu wa Adamu mwanamume na Hawa uliendelea ila biblia haijauweka huu uzazi katika kitabu cha vizazi vya Adamu kwa maana tuliona hapo juu ya kwamba Adamu ni muunganiko wa mtu mume na mtu mke ambao waliumbwa mwanzo kwa mfano wa Mungu na kizazi Chao watu hawa tunakiona pale mwanzo 5:3.

Andiko linasema " Adamu akaishi miaka Mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi".

Kwa hiyo utaona kwamba wakati Adamu mwanamume anazaa watoto na Hawa tuliambiwa kwamba alimjua, Lakini andiko hilo hapo juu linasema Adamu baada ya kuishi miaka mia na thelathini akazaa mwana kwa sura yake na kwa mfano wake, hii inamaanisha kwamba yule Adamu mwanamke na Adamu mwanamume kwa pamoja walifanikiwa kupata mtoto wao wakiwa na miaka 130 tangu kuumbwa kwao kwa mfano wa Mungu na baada ya hapa ndio tukapata neno mwanadamu kwa maana ya mwana wa Adamu.

Kwa hiyo mwanadamu anatokana na kizazi cha Adamu na wala si kile kizazi cha Hawa na Adamu mwanamume kwa maana hiyo basi kizazi cha mwanadamu kilianza pale tu Sethi alipozaliwa.

Ukiendelea kusoma biblia utagundua ya kwamba baada ya Mungu kuwatoa kina Adamu pale bustanini, wao waliendelea kuzaa na wakawa wanaishi maisha yao kama kawaida ila sasa ule muendelezo wa kuzaliana ukapelekea hadi wana wa kike wazaliane kwao na baada ya hawa wana wa kike kuzaliwa basi wale wana wa Mungu wakaanza tamaa za kuwatamani hawa wana wa kike wanaozaliwa katika uzao wa wanadamu na wao haraka wakasogea na wakaanza kujichagulia wake wanaowapenda huko na kuzaa nao na hili swala ndio likamchukiza sana muanzilishi wa huu mradi na kukili kwamba jambo analotaka kulianzisha haliwezekani kwa maana wana wa Mungu wako kwenye umbo la damu na nyama lakini pia na mwanadamu yupo kwenye umbo hilo hilo kwahiyo ni ngumu sana kuwafanya wasiingiliane.

Na kilichomfadhaisha zaidi ni watoto waliokua wanazaliwa kutokea kwenye huo muunganiko wa wana wa Adamu Na wana wa Mungu, walikua ni watu hatari sana kwa maana biblia inasema walikua ni watu hodari na ni watu wenye sifa. Mwanzo 6:4.

Na ukiendelea kusoma kwa umakini utagundua hiki kizazi kilikua kinataka kumpindua Mungu ama kuwa na sifa zote za Mungu kwa maana ukisoma hapo hapo mwanzo 6 kwenye ule mstari wa 5 unasema hivi " BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu siku zote". Ukiutafakari huu mstari utagundua kwamba walikua wanawaza mapinduzi kila uchwao na ndio maana muanzilishi wa huu mradi yaani Mungu akaamua aachane na mradi wenyewe kwa maana ya kughairi kuendelea nao kwakua alijua moto unaowaka kuna siku hatoweza kuuzima. Mwanzo 6:6 inazungumzia swala la BWANA kughairi.

Ukiendelea na hilo andiko utaona kwamba BWANA akaamua kuapa kwamba atafutilia mbali vile vyote alivyoviumba katika uso wa dunia hasa vile venye uhai na akaamua kwenda na mwanadamu ambae alitokea kwenye uzao wa Adamu kwa maana ya Nuhu na familia yake na hapo ndipo alipoiaangamiza dunia na kufuta vile vyote ambavyo aliviumba moja kwa moja na badala yake akaacha kizazi ambacho bila shaka alikiona ni chema na hakitakua na usumbufu wowote kwake.

Kumbuka Mungu kabla hajashusha gharika ulimwenguni ili aufute ule mradi ambao alikua anautengeneza pale bustanini, kaa ukijua ya kwamba kulikua na jamii nne ya viumbe venye umbo la mtu, ambavyo ni Adamu ambao ni kopi ya Mungu, Hawa ambae ni kopi ya Adamu mwanamume, wana wa Mungu na wanefili.

Na uweke hii kichwani mwako ya kwamba Adamu aliumbwa kwa lengo la kupokea na kuyatunza yale mawazo ya kimungu ambayo yanaingia ndani yake yakiwa yamebeba ajenda mbalimbali za ulimwengu, lakini pia wakati yeye anapokua na hilo wazo basi anahitaji kuwa na mtu ambae atamsaidia kulibeba na kusimamia kwenye utendaji wake hadi likamilike na huyu ndio yule Hawa sasa ambae yeye aliumbwa akiwa na nguvu kubwa ya usaidizi ndani yake.

Lakini pia tunawaona wale wana wa Mungu na hawa ndio viumbe ambao walikua wamejawa maarifa ya aina mbalimbali, ni viumbe ambao walikua na uwezo wa kutafsiri kila wazo limjialo Adamu kwaajiri ya ulimwengu na hawa walikua wakishalitafsiri wazo husika basi walikua wanawatumia wale wanefili ambao hawa wao walikua ni watu wakubwa watu ambao wana nguvu sana za kimwili na ndio ambao walikua wanatumika katika kufanya kazi mbalimbali ambazo zinahitaji nguvu.

Kwahiyo utaona hapo ambavyo Mungu alitaka ulimwengu ufanye kazi ila sasa baada ya uhasi ndio kama ambavyo nilikuambia ya kwamba Mungu aliamua kuzifuta nguvu mbili kwa maana ya ile nguvu ya maarifa pamoja na ile nguvu ya utendaji kazi na kumuacha mwanadamu pekee ambae wote tumeona hapo juu ya kwamba kiasili yeye huwa anakuja akiwa na nguvu mbili tu yaani ile ya maono au ya uwezo wa kutengeneza mawazo yenye tija na ile ya usaidizi kwahiyo nguvu mbili za msingi zilikosekana duniani kwa muda au nyakati fulani ila kutokana na uwezo mkubwa wa kupokea na kutengeneza mawazo ambao anao mwanadamu hii changamoto iliweza kupata ufumbuzi ambao ulipelekea mabadiliko makubwa katika mfumo wa maisha hapa duniani.
 
Where he resides matters when defining whether he has phyiscal body(flesh) or he is spiritual.

Mungu makazi yake ni mbiguni(true).Heaven is a spiritual world so heavenly figures will have spiritual body contrary to earthly figures(human beings,animals,...) who have both spiritual body and phyiscal body(flesh)
 
Back
Top Bottom